Mkutano wa Kikatiba tu ndiyo utaandika Katiba Mpya

Mkutano wa Kikatiba tu ndiyo utaandika Katiba Mpya

Tujiandae kuupinga muswada wa Katiba

ban_tahariri.jpg

amka2.gif
TUKIWEKA mbele masilahi ya taifa, tunaungana na Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), kuelezea kushtushwa kwetu na maudhui ya muswada wa sheria ya mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2011 (The Constitutional Review Act 2011) uliochapwa katika gazeti la serikali toleo No. 1 Vol. 92 la tarehe 11 Machi 2011, mwaka huu.
Baada ya kupitia kwa umakini uchambuzi uliofanywa na Mnyika pamoja na muswada wenyewe unaokusudiwa kuwasilishwa bungeni katika Bunge la mwezi Aprili kama alivyoahidi Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, tumejiridhisha pasipo shaka yoyote ile kuwa Rais Jakaya Kikwete, serikali yake na chama chake (CCM), hawana nia ya kweli ya kuhakikisha wananchi wanashiriki vizuri na kuwa na nguvu ya mwisho ya kuamua aina ya katiba wanayoitaka pamoja na maudhui yake.
Kikubwa kinachosikitisha katika muswada huo ni kupendekeza kuwa rais apewe mamlaka ya kuunda tume ya kuongoza mchakato mzima wa katiba bila kuhusisha Bunge ama wadau wengine wa msingi.
Katika hilo, imependekezwa kuwa rais awe na mamlaka ya kuteua wajumbe wa tume husika bila kushauriana na mtu yeyote isipokuwa Rais wa Zanzibar; na muswada unaelekeza kuwa katika kuteua wajumbe rais atazingatia uwakilishi wa makundi ya kijamii, lakini makundi husika hayatajwi hata kwa ujumla wake, hali itakayoacha mamlaka yote ya kuamua uwakilishi kubaki kwa rais.
Izingatiwe kuwa muswada huo unataka kumpa rais mamlaka ya kutengeneza hadidu rejea za tume, jambo ambalo lilipaswa kufanywa na Bunge kwa kuwa sehemu ya sheria husika ama kufanywa na mkutano mkuu wa kikatiba.
Itiliwe maanani kuwa kwa kutoa mamlaka ya kuunda hadidu rejea kwa rais mwanya umetolewa kwa mtu mmoja kuweka mipaka ya nini kinastahili kufanywa na tume wakati wa mchakato wa katiba mpya na hivyo kuminya wigo wa mabadiliko.
Muswada unataka tume iwasilishe ripoti yake kwa rais ambaye atampa nakala Rais wa Zanzibar na baadaye kumwelekeza waziri mwenye dhamana kupeleka bungeni yale atakayoamua yeye rais ndiyo yapelekwe, hivyo utaendeleza yaleyale yaliyofanywa na marais waliopita kuhusu ripoti na mapendekezo ya tume nyingine, hivyo kukwamisha mabadiliko ya kweli yanayotakiwa na Watanzania wengi.
Wakati wadau wengi wakiwamo wale walioshiriki kongamano la kwanza la katiba mpya katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakiwa wamependekeza kuwa ni muhimu kuitishwa kwa Mkutano Mkuu wa Katiba, muswada huo unataka kutoa mamlaka kwa tume itakayoundwa kuitisha jukwaa (fora) ambalo litaundwa kwa ajili ya kupata maoni pekee, huku uwakilishi katika jukwaa hilo ukiwa umetajwa tu kuwa ni wa kijografia na kimakundi bila kuweka bayana mnyumbuliko wa uwakilishi.
Wakati wadau wengi wakitaka kuona uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2014, na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 unafanyika katika mazingira ya haki yatakayoihakikishia nchi usalama, muswada huo kwa ujumla haujaeleza muda wa mchakato wa katiba na vipindi vitakavyotumiwa na vyombo mbalimbali katika hatua mbalimbali za mchakato wa katiba; ama kutoa mamlaka ya kuwekwa kwa muda huo kwa chombo chenye uwakilishi mpana wa umma kama mkutano wa katiba au Bunge na hivyo kutoa mwanya kwa mchakato mzima kucheleweshwa.
Wakati kongamano la pili la wadau kuhusu katiba mpya likitarajiwa kufanyika keshokutwa (Jumamosi) katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, tunatoa rai yetu kwa washiriki wa kongamano hilo na Watanzania wote kwa ujumla kuielewa nia mbaya na ya makusudi ya serikali ya kutaka kuhakikisha kuwa katiba tunayoitaka inachelewa na itakayopatikana si tunayoitaka. Watanzania wote wake kwa waume, vijana kwa wazee bila kujali dini, kabila na vyama vyetu vya siasa, tuujue, tuujadili na kuupinga kwa nguvu muswada huo, kwani haulitakii mema taifa hili.
 
‘Kero za Muungano ni kikwazo'


na Andrew Chale


amka2.gif
NAIBU Waziri wa Ushirikino wa Afrika Mashariki, Dk. Abdallah Abdallah, amesema kuwa Muungano wa Tanzania Bara na Zanzibar una kero nyingi ambazo zikishughulikiwa mapema zitaiwezesha Zanzibar kunufaika na changamoto za Muungano wa Afrika Mashariki.
Aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam muda mfupi baada ya kuhutubia mkutano wa wadau wakuu kuhusu rasimu ya Sera ya Utawala Bora ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, uliofanyika katika ukumbi wa DICC.
Alizitaja kero hizo ambazo alisema ni changamoto kubwa kwa visiwa hivyo kuwa ni tatizo la bandari, hali ya kisiasa, mabadiliko ya Katiba na nyingine nyingi.
Alisema kwa sasa Jumuiya ya Afrika Mashariki imeweza kuiwezesha Zanzibar kuwa kwenye ukanda maalumu wa kiuchumi ambao utasaidia kuinua maendeleo mbalimbali ndani ya visiwa hivyo.
Dk. Abdallah alisema Jumuiya hiyo inakabiriwa na majukumu mbalimbali ambayo yapo mbioni kufanyiwa mchakato ikiwemo vikwanzo vya kiforodha ambavyo vitashughulikiwa ili kupunguza malalamiko, ikiwamo ushuru wa mipakani kwa magari yanayosafirisha bidhaa kutoka nchi moja hadi nyingine.
Katika mkutano huo, wadau hao walijadili mambo mbalimbali ikiwemo maeneo makuu ya rasimu hiyo, yakiwemo uendelezaji wa demokrasia, utawala wa sheria na upatikanaji wa haki, ulinzi wa haki za binadamu na mapambano dhidi ya rushwa na ujenzi wa maadili na utu.
 
Wasomi: Serikali isithubutu kutuingilia


na Betty Kangonga


amka2.gif
WANATAALUMA wa vyuo vikuu wameeleza kusikitishwa kwao na hatua ya serikali kutaka kuingilia uhuru wao, jambo ambalo linaweza kusababisha mvurugano.
Wakizungumza na Tanzania Daima wanataaluma hao walisema kuwa wao si walimu wa vyuo vikuu pekee bali ni wa dunia nzima, ndiyo maana wana uwezo wa kutoa mawazo yao bila kuingiliwa na chombo chochote.
Akichangia zaidi, Mhadhiri wa Chuo Kikuu sehemu ya Mlimani jijini Dar es Salaam, Sengondo Mvungi, alisema kuwa ni kitendo cha ajabu iwapo serikali itaingia madarasani na kusikiliza kile ambacho tunakifundisha.
Alisema kitendo hicho kinaweza kusababisha kutoelewana na hata kuvifanya vyuo vikuu kuwa kama shule za msingi kama wataingilia uhuru wa wanataaluma hao.
Mvungi alisema kuwa wahadhiri wanapofundisha hawapangiwi wafundishe kitu gani na hata ikitokea wanafunzi wakauliza swali wanapaswa wapewe majibu ya kutosheleza.
"Leo mwanafunzi ananiuliza swali hata kama linahusiana na Chama Cha NCCR- Mageuzi ninapaswa kuwajibu yale ambayo yanajitosheleza bila kumung'unya kitu chochote na majibu yawe yana maana," alisema.
Alisema serikali isijaribu wala kuthubutu kuingia wakati anafundisha kwani kitendo hicho ni kinyume cha sheria na inaweza kumfanya akachukua hatua isiyofaa.
Naye Profesa Joseph Mbele katika maoni yake alisema kuwa aliiona taarifa hiyo ya serikali hivyo alitumia wadhifa wake kama mwanataaluma na mzoefu wa kufundisha au kutoa mihadhara vyuo vikuu sehemu mbalimbali za dunia kuchangia hoja hiyo.
Alisema si kazi ya serikali kuingia darasani chuo kikuu ili kuchunguza mwalimu anafundisha nini au anafundishaje.
Hii ni kazi ya wanataaluma na wahadhiri, kufuatana na taratibu zinazotambulika katika jumuia ya wanataaluma.
Taratibu hizo ni za kulinda, kutathmini, kuratibu na kuboresha viwango vya utafiti, ufundishaji na taaluma kwa ujumla.
Profesa Mbele alisema serikali inapaswa kutambua kuwa dhana ya chuo kikuu duniani pote, inaendana na haitengeki na uhuru wa kitaaluma. Walimu wa vyuo vikuu si tu wana wajibu, bali uhuru wa kufukuzia taaluma bila vipingamizi, kwa mujibu wa vigezo vya taaluma hizo vinavyotambulika miongoni mwa wanataaluma kimataifa.
"Kama kuna walakini katika utendaji kazi wa mwalimu wa chuo kikuu, kama vile kutofundisha somo inavyotegemewa, wanaowajibika kuchunguza ni wanataaluma wenzake, si serikali," alisema.
Aliongeza kuwa serikali haitegemewi wala kuruhusiwa kuingilia uhuru wa walimu na watafiti chuo kikuu katika kufanya utafiti, ufundishaji, uandishi na kwa misingi na viwango vinavyotambuliwa kitaaluma.
Alieleza jambo jingine la msingi kuwa chuo kikuu ni mahala pa tafakari na malumbano kuhusu masuala mbali mbali, kwa kiwango cha juu kabisa. Ni sehemu ambapo fikra za kila aina na hoja za kila aina zinapaswa kusikika na kuchambuliwa.
"Chuo kikuu cha kweli, chenye hadhi ya chuo kikuu, ni maskani ya wachochezi wa fikra na hoja, katika taaluma mbali mbali, ikiwemo siasa. Huwezi kumwambia mtafiti au mhadhiri asiiponde serikali iliyoko madarakani iwapo utafiti na tafakari yake inampeleka huko," alifafanua.
Alisema dhana ya kwamba kuna wanaoeneza siasa za chuki miongoni mwa wanafunzi wa chuo kikuu ni dhana ya kusikitisha.
Inamaanisha kuwa hao wanafunzi ni wajinga au ni wavivu ambao hawana uwezo au dhamira ya kujibidisha katika kusoma na kutafakari mambo ili waweze kugundua mapungufu ya hoja wanazosikia, na kupambana kwa hoja.
Alieleza kuwa inamaanisha hao ni wanafunzi mbumbumbu, wasio na akili au wasiotumia akili. Kitendawili ni je, walifikaje hapo chuoni, kama si kwa njia za panya?
Profesa Mbele alisema wanafunzi wa chuo kikuu wanawajibika kuwa tayari na makini katika kupambana kwa hoja na wanafunzi wenzao na pia na walimu wao. Ni fedheha iwapo wanafunzi hao kiwango chao ni duni kiasi cha kuweza kupotoshwa na walimu wao.
Alisema hao hawastahili kuitwa wanafunzi wa chuo kikuu, na hicho chuo chenyewe hakistahili kuitwa chuo kikuu. Na ni fedheha kama tumefikia mahali ambapo serikali inaona ije darasani kuwanusuru hao wanafunzi feki.
Mwishoni mwa wiki iliyopita serikali kupitia Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, alisema kuwa inawachunguza wahadhiri wa vyuo vikuu nchini wanaotumia muda mrefu madarasani kuzungumzia siasa badala ya kufanya kazi zinazohusu taaluma.
"Tunaendelea na uchunguzi wa kuwabaini baadhi ya wahadhiri wanaojihusisha na siasa kwa kuingia madarasani na kuzungumzia siasa kwa dakika kumi kabla ya kuanza kufundisha," alisema Mulugo.
Alisema lengo la wahadhiri hao ni kuwafanya wanafunzi kuchochea migomo na maandamano na kupandikiza chuki baina ya serikali na wanafunzi.
 
ULAGHAI WA KIKWETE KUHUSU KUUNDWA KWA KATIBA YENYE WANANCHI KWENYE STERINGI SASA TUNASEMA BASI: TUNATAKA SERIKALI YA MPITO KUSHUGHULIKIA KATIBA NCHINI NA KUKAMILISHA KILA KITU 2014

CHADEMA,Asasi za Kiraia nchini, Vyuo Vikuu na Nchi Wahisani tunaomba mtuelewe kwamba sasa uzalendo umetushinda na huu utani wote na kiburi ya Mhe Kikwete - tunataka serikali mpya ya mpito sasa hivi kushughulikia katiba!!!

Wananchi; kila mmoja mahala ulipo wakati umefika wa kuachana na mchezo katika mambo ya msingi ambayo tumejaribu kutafuta kiungwana ndio hivo imeshindikana. Hakuna haja kuendelea kubisha mlango usiofunguliwa bali hapa ni kutafuta njia njingine kabisa kwa uwezo wa Nguvu ya Umma.

Cha msingi sasa sisi wenyewe tena vijana, kwa njia zetu zile, TUNAIPA SERIKALI YA Mhe Kikwete hadi April 08, 2011 iwe imewashirikisha wadau wote na mawazo yetu, katika hatua zote za ushiriki, usimamizi na uendeshaji wa mambo ya katiba kwa kuzingatia matakwa ya wananchi na wala si kutulazimiza na matakwa ya watawala ambao ndio haswa tunaowalalamikia kwa unyanyasaji.

Vijana tuliowengi nchini tusimame kutetea haki zetu kwani haki hapewi mtu hata siku moja. Endpo serikali haitotii hayo maoni yetu basi Vijana kote nchini pamoja na taasisi marafiki wa UTAWALA WA KIDEMOKRASIA NA USHIRIKISHWAJI WA WANANCHI MOJA KWA MOJA tujiweke tayari kwa maandamano ya amani kote nchini mpaka matakwa haya yatimizwe au serikali inaposhindwa basi ikatupishe njia haraka!!

Tunasema katika huu mzaha wa serikali kuhusu tume HURU YA BUNGE kugeuzwa kuwa TUME TEGEMEZI YA RAIS ikibarikiwa na Bunge; Vijana tumefika Tamati tena hadi hapa!!!

Kumbe Kupatikana kwa Katiba Mpya chini ya Uongozi wa CCM haiwezikani bila serikali kututwisha MADALALI kwenye mambo ya kuundwa kwa Katiba Mpya nchini.

CHADEMA tusikilizeni, tunahitaji kwana SERIKALI YA MPITO kumbe yenye jukumu moja tu kushughulikia Katiba kwa MUJIBU WA MATAKWA WA WANANCHI katika hatua zote za usimamizi na maamuzi.

BAVICHA na matawi yetu yote ya CHADEMA nchini tueleweni kwamba wananchi sasa tunasema baaasi na Serikali ya CCM iondoke madarakani sasa hivi. Sote tunao uwezo wa kubadilisha haya mambo yote kabla hatujaingizwa porini zaidi.

Mwenye kupata ujumbe huu na akawajulishe vijana wengine 10 juu ya ulaghai uliotangazwa na serikali majuzi kutupora haki ya kusimamia kuundwa kwa katiba mpya bila kuingiliwa na dola.

Lengo lao likiwa ni kuleta katiba waitakayo MAFISADI nchini, kuchelewesha muda tuingie uchaguzi 2015 bila katiba mpya, na vile vile kukiundia CHADEMA mikesi ya kuchonga kisiasa ili baadhi ya wale tunaowapenda wasigombee.

SASA TUNASEMA KATIBA MPYA NA TUME HURU YA UCHAGUZI BARA NA VISIWANI YOTE YAWEZEKANA BILA CCM, TUPISHENI NJIA!!!
 
Mnyika ashtukia mudawa wa mabadiliko ya katiba


Na Rabia Bakari

MBUNGE wa Jimbo la Ubungo (CHADEMA), Bw. John Mnyika amedai kushtushwa na maudhui ya muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa
mwaka 2011 uliochapwa katika Gazeti la Serikali toleo No. 1 Vol. 92 la Machi 11, mwaka huu, akidai kuwa hauna nia ya dhati ya kuleta mabadiliko ya katiba.

Bw. Mnyika alisema jana kuwa kilichomshtua zaidi ni mamlaka makubwa aliyonayo rais katika muswada huo, ambapo maudhui yamedhihirisha tahadhari aliyotoa mara kadhaa kwamba serikali haina dhamira ya kweli ya kuhakikisha panakuwepo na mchakato mzuri wa kuwa na katiba mpya.

Alisema kuwa muswada huo umelenga kuhalalisha yote ambayo yalitangazwa kufanywa na rais kuhusu mchakato wa katiba mpya na kupingwa na wadau mbalimbali, ambapo sasa yanataka kupewa uhalali kwa sheria inayotaka kutungwa na bunge kupitia muswada huo.

"Muswada huo unataka kumpa mamlaka rais ya kuunda tume ya kuongoza mchakato mzima wa katiba bila kuhusisha bunge ama wadau wengine wa msingi. Muswada huo pia utaka kumpa rais mamlaka ya kuteua wajumbe wa tume husika bila kushauriana na mtu yoyote isipokuwa Rais wa Zanzibar.

Muswada huo unaelekeza kuwa katika kuteua wajumbe, rais atazingatia uwakilishi wa makundi ya kijamii, lakini makundi husika hayatajwi hata kwa ujumla wake na hivyo kuacha mamlaka yote ya kuamua uwakilishi kubaki kwa rais," aliongeza.

Mambo mengine yaliyomo kwenye muswada huo, Bw. Mnyika aliyataja kuwa ni pamoja na kumpa rais mamlaka ya kutengeneza hadidu rejea za tume jambo ambalo lilipaswa kufanywa na bunge kwa kuwa sehemu ya sheria husika ama kufanywa na Mkutano Mkuu wa Kikatiba.

Aliongeza kuwa kwa kutoa mamlaka ya kuunda hadidu rejea kwa rais mwanya umetolewa kwa mtu mmoja kuweka mipaka ya nini kinastahili kufanywa na tume wakati wa mchakato wa katiba mpya na hivyo kuminya wigo wa mabadiliko.

"Muswada huo unataka tume iwasilishe ripoti yake kwa rais ambaye atampa nakala Rais wa Zanzibar na baadaye kumwelekeza waziri mwenye dhamana kupeleka bungeni yale atayoamua rais. Muswada huu kwa kuwa na kifungu hiki utaendeleza yaliyofanywa na marais waliopita kuhusu ripoti na mapendekezo ya tume zingine na hivyo kukwamisha mabadiliko ya kweli," alisema Bw. Mnyika.

Pamoja na hayo, aliongeza kuwa muswada huo unataka kutoa mamlaka finyu kwa jukwaa linalohusiana na mambo ya katiba tofauti na mkutano mkuu wa kikatiba ambao ungekuwa na mamlaka zaidi katika mchakato husika.

Aidha kwa mujibu wa Bw. Mnyika pia, muswada huo unataka kutoa mamlakama kubwa kwa rais kuteua wawakilishi wa chombo kikuu zaidi katika mchakato wa katiba bila kushauriana na kundi lolote ama wananchi kuhusika katika uteuzi ama kuwa na wawakilishi walioteuliwa na makundi yenyewe, mathalani vyama vya siasa, asasi za kiraia, taasisi za dini, vyama wa wakulima, vyama vya wanafunzi, vyama wa wafanyakazi na wengineo.

Alisema muswada huo unataka Rais ashauriane na Rais wa Zanzibar na Mwanasheria Mkuu wa Serikali pekee ambapo pia unatoa mamlaka makubwa zaidi ya rais kuamua hata kufanya bunge la kawaida kuwa ndilo bunge la katiba, jambo ambalo linaweza kurejesha udhaifu uliofanywa katika mchakato wa katiba inayotumika sasa ambapo umma uliporwa wajibu na mamlaka yake ya kushiriki moja kwa moja katika kupitisha katiba.

"Muswada kwa ujumla haujaeleza muda wa mchakato wa katiba na vipindi vitavyotumiwa na vyombo mbalimbali katika hatua mbalimbali za mchakato wa katiba; ama kutoa mamlaka ya kuwekwa kwa muda huo kwa chombo chenye uwakilishi mpana wa umma kama mkutano wa katiba au bunge na hivyo kutoa mwanya kwa mchakato mzima kucheleweshwa," alisema.

Bw. Mnyika alikumbusha kuwa mnamo Februari 9 mwaka huu, alitoa tamko kuwa alipokea kwa tahadhari uamuzi wa Serikali kupitia kwa Rais Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kubadili misimamo ya awali kuhusu mchakato wa katiba mpya na kuamua kukubaliana na mwito wa kutaka mchakato husika uanzie bungeni kupitia kutungwa kwa sheria ya bunge ya kuratibu na kusimamia mchakato husika kama alivyokuwa akitoa mwito kwa nyakati mbalimbali.



6 Maoni:

blank.gif

GÖttingen said... Halafu mbona unasomeka marekebisho ya Katiba (review) badala ya Mchakato wa kutengeneza katiba mpya?

Tunaomba Serikali isipuuze maoni yetu wananchi. Kwanini haitaki kukubaliana nasi?

Imefata Mawazo ya Jaji Werema ambaye alishatamka kuwa hakuna hitaji la Katiba Mpya.
March 30, 2011 10:32 PM
blank.gif

Anonymous said... Tatizo la watawala ni kwamba kila wanapobanwa na hoja fulani huamua kuzifuta kiaina. Issue ya katiba mpya si ya mjadala lakini imegeuzwa na kuwa marekebisho ya katiba? Katiba imerekebishwa mara ngapi? Serikali inajua kuunda katiba mpya ni mwanzo wa mwisho wao wa utawala. Watanzania lazima tuamke tusikubali kuburuzwa, nchi ni yetu sote si watawala pekee.
March 30, 2011 10:50 PM
blank.gif

Anonymous said... ni assumption yangu kuwa Rais na waziri mkuu wanasoma au kupitia watu wao maoni haya huyapata.
NAOMBA NIWASHAURI MHE. KIKWETE NA MHE.PINDA MALIZENI KAZI VIZURI KWA KUWATENDEA HAKI WATANZANIA HUSUSA NI KWENYE SUALA LA KATIBA MPYA. WATANZANIA WANAISUBIRI KWA HAMU. TANZANIA YA LEO SI YA JANA. MAPINDUZI YATALETWA NA VIJANA WENGINE SIO HAO UVCCM (WATOTO WA MANYANG'AU NA MAFISADI)
March 30, 2011 10:52 PM
blank.gif

Anonymous said... Ni dikteta tu ndiye anayeweza kufanya kila kitu peke bila kushirikisha wengine. Sipendi kuamini kama Tanzania inaoongozwa kinamna hiyo. Lakini dalili ya mvua ni mawingu. Nashawishika kusema kuwa kwa namna hii ilivyo, huenda tunaongozwa kidikteta bila kujua, maana demokrasia inazidi kuminywa siku hadi siku. Tusikubali hali hii.
March 31, 2011 12:24 AM
matogolo said... mbona mswada ulikuwa ni katiba mpya sasa inakuwaje kuwa ni marekebisho?si katiba hii ilikwisha fanyiwa marekebisho zaidi ya mara mbili, hatuwezi kuendelea na mfumo uliopitwa na wakati
March 31, 2011 2:22 AM
blank.gif

Anonymous said... tunataka Katiba Mpya na si Marekebisho.
March 31, 2011 2:25 AM
 
NCCR yauponda muswada wa marejeo ya Katiba Send to a friend Saturday, 02 April 2011 09:27

Fidelis Butahe
CHAMA cha NCCR-Mageuzi kimeuponda muswada wa marejesho ya Katiba ya Tanzania wa mwaka 2011 kwa kuwa unampa mamlaka makubwa Rais, yakiwamo mamlaka ya kuunda Tume ya Kutunga Katiba. Pia chama hicho kimesema muswada huo ambao utajadiliwa Bungeni Juni mwaka huu, hauna lolote kwa kuwa umenakiliwa ‘neno kwa neno' kutoka Sheria ya Kenya ya Marejeo ya Katiba namba 9 ya mwaka 2008.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia alisema maudhui ya muswada huo yanaonyesha wazi serikali imekamia kuunda Tume ya kutunga katiba ambayo itateuliwa na Rais. "Pendekezo hilo linamaanisha kuwa Rais ndiye mdau katika mchakato wa kutunga katiba mpya, vifungu vya 5,6(1) na (2) katika muswada huu, vinampa mamlaka makubwa Rais.

"Viko vifungu vingi vinavyompa mamlaka rais ni kifungu cha 8(1), 13(2), 13(4), 14(2), 16(2), 16(3), 21(1), 21(3), 23(3), 23(4) na 25(2)," ,"alisema Mbatia. Mbatia alisema kazi ya kutungwa kwa katiba lazima liwashirikishe Watanzania kwa kuwa katiba ni kauli ya umma kuhusu utawala wa nchi na jinsi wanavyotaka kuishi.
"Rais ni mtumishi namba moja wa taifa lake, hana nafasi au mamlaka ya kulitungia taifa lake katiba,"alisema Mbatia. Alisema rais anapaswa kuviachia vyombo huru vya umma ili vianze mchakato wa kutunga katiba mpya.

"Kwa kuwa hatuko katika nafasi sifuri, yaani bila taifa wala dola, ni vyema kiutaratibu kupeleka bungeni muswada wa marekebisho ya ibara ya 98 ili iruhusu bunge kutunga sheria ya baraza la kutunga katiba na sheria ya kura za maoni,"alisema Mbatia.
Alisema hatua ya pili ni kupelekwa bungeni muswada wa sheria ya baraza la kutunga katiba na sheria ya kura za maoni na kusisitiza kuwa mambo hayo mawili yanaweza kufanywa wakati mmoja katika kikao kijacho cha bunge. Baraza la kutunga Katiba

Mbatia alifafanua itungwe sheria ya baraza la kutunga katiba na wabunge wa bunge la Jamhuri wawe wajumbe wa baraza hilo huku likiwa na wajumbe wengine.
"Wajumbe wengine wawe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Muungano na la Serikali ya Zanzibar, mwakilishi wa chama cha wafanyakazi kilichosajiliwa, mwakilishi wa asasi ya kitaifa ya kijamii, makamu wakuu wa vyuo vikuu, wawakilishi wa vyama vya siasa.

"Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano na Jaji Mkuu wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, majaji wa mahakama za rufani, marais wastaafu, mawaziri wakuu, wawakilishi wa madhehebu ya dini, watu 10 mashuhuri watakaopendekezwa na bunge pamoja na wakuu wa vituo vya sheria," alisema. Alisema baraza hilo linapaswa kuwa na mamlaka ya kuteua Tume ya Kutunga Katiba.

Serikali imenakili sheria ya Kenya

Mbatia alisema muswada wa marejeo ya katiba wa mwaka 2011 umenakiliwa kutoka sheria ya Kenya ya Marejeo ya Katiba namba 9 ya mwaka 2008 na kufafanua kuwa sheria hiyo iliridhiwa na Rais wa Kenya, Desemba 11, 2008 na kuanza kutumika, Desemba 22, 2008.
"Kuiga au kunakili moja wa moja sheria ya nchi nyingine si jambo la ajabu, lakini lazima ujihadhari na mambo ambayo hayaihusu nchi yako na hasa hatari ya kuiga sheria isiyoandamana na mila, desturi, siasa, utamaduni na mahitaji ya wakati huo," alisema Mbatia.

Alisema kama mazingira ya Kenya yalihitaji marejeo ya Katiba, mazingira ya Tanzania hayahitaji suluhisho kama hilo bali yanahitaji katiba mpya na kuhoji kwamba iweje muswada huo unakiliwe neno kwa neno wakati Tanzania kuna wataalamu wengi wa masuala ya katiba na sheria.
"Kenya ni nchi yenye muundo rahisi kikatiba ‘simple state', wakati Tanzania ni nchi yenye muundo mgumu ‘complex state' , Tanzania ni Jamhuri ya Muungano, Kenya wao ni Jamhuri tu, sasa wapi na wapi," alisema Mbatia.

Naye Mkuu wa Idara ya Katiba na Sheria wa chama hicho, Dk Sengondo Mvungi alifafanua kwamba hawana lengo la kufungua kesi mahakamani kupinga muswada huo bali watawatumia wabunge wa chama hicho kuomba mabadiliko ya muswada huo bungeni.
"Inawezekana kabisa wataalamu wa Rais wakawa wamempotosha kuhusu hili la muswada, Rais hasipelekwe kabisa katika hili, maana hapa kwetu Zanzibar tayari nchi, Tanganyika je, ni mkoa au, wananchi wanatakiwa kulitambua hili," alihoji Mvungi.
 
PHP:
 "Kwa kuwa hatuko katika nafasi sifuri, yaani bila taifa  wala dola, ni  vyema kiutaratibu kupeleka bungeni muswada wa marekebisho  ya ibara ya  98 ili iruhusu bunge kutunga sheria  ya baraza la kutunga  katiba na  sheria ya kura za maoni,"alisema Mbatia.  
Alisema hatua  ya pili ni kupelekwa bungeni muswada wa sheria ya baraza  la kutunga  katiba na sheria ya kura za maoni na kusisitiza kuwa  mambo  hayo mawili  yanaweza kufanywa wakati mmoja katika kikao kijacho cha  bunge.  Baraza  la kutunga Katiba

Jk is not a genui9ne reformer....that is what we need to appreciate in full...........................he is anti-reformer in chief..............
 
PHP:
Mbatia alifafanua itungwe sheria ya baraza la  kutunga katiba na wabunge   wa bunge la Jamhuri wawe wajumbe wa baraza  hilo huku likiwa na  wajumbe wengine. 
 "Wajumbe wengine wawe wa  Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Baraza la  Mawaziri la Jamhuri ya  Muungano na la Serikali ya Zanzibar, mwakilishi  wa chama cha wafanyakazi  kilichosajiliwa, mwakilishi wa asasi ya  kitaifa ya kijamii, makamu  wakuu wa vyuo vikuu, wawakilishi wa vyama  vya siasa.

"Jaji Mkuu  wa Jamhuri ya Muungano na Jaji Mkuu wa Mahakama Kuu ya  Zanzibar, majaji  wa mahakama za rufani, marais wastaafu, mawaziri  wakuu, wawakilishi wa  madhehebu ya dini, watu 10 mashuhuri  watakaopendekezwa na bunge pamoja  na  wakuu wa vituo vya sheria,"  alisema.  Alisema baraza hilo linapaswa  kuwa na  mamlaka ya kuteua Tume  ya Kutunga Katiba.

Mbatia is yet to learn that in Kenyan experience the parliament was a problem but not the solution..........................members of judiciary too have no role in constitutional making process.........unless, of course we want a status quo constitution

Mkutano wa Kikatiba ni lazima uchaguliwe na wananchi moja kwa moja.............................Kenya did it through BOMA but MPs illegalized the whole process................................................................


Tukumbuke ya kuwa Raisi ndiye anayewateua Majaji mfumo ambao una dosari kubwa......kwa sababu hautoi fursa sawa kwa watanzania wote wenye sifa.................................na katiba hii muundo wa uandishi wake ni lazima utoe fursa sawa kwa wote.....................Hiyo TUME watu wenye sifa waombe hizo nafasi na Bunge lifanye kazi ya kuwasaili kupitia kamati husika ya mambo ya kikatiba................................................................................vinginevyo it is not yet UHURU.......................
 
Serikali yadaiwa kunakili Katiba ya Kenya


na Efracia Massawe


amka2.gif
MWENYEKITI wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia, amesema Katiba iliyoandaliwa na serikali inayotarajiwa kufikishwa bungeni kwa ajili ya kujadiliwa imenakiliwa kutoka Katiba ya Kenya.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kwa niaba ya wanachama wake, mwenyekiti wa chama hicho alisema muswada wa Katiba unaotarajiwa kuletwa na serikali ni marejeo ya Katiba namba tisa ya mwaka 2008.
Alisema kilichofanyika katika Katiba mpya iliyoandaliwa ni uigaji na hata kunakili moja kwa moja sheria ya nchi nyingine, hali mbayo itasababisha hatari ya kuigiza sheria isiyoandamana na mila, desturi, siasa na hata utamaduni wa wananchi.
Kadhalika chama hicho kimelitaka Bunge la Jamuhuri litumike kama wajumbe katika baraza hilo lakini lijumuishe wajumbe wengine kutoka Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar.
"Chama kinataka wajumbe kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Muungano na Baraza la Mawaziri la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Jaji Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano na Jaji Mkuu wa Mahakama Kuu ya Zanzibar.
Hata hivyo wanahitaji wawakilishwe majaji wa Mahakama ya Rufaa, marais wastaafu wa Jamhuri ya Tanzania, na serikali ya Zanzibar wakiwemo mawaziri wake wastaafu, viongozi wa dini, wawakilishi wa kila chama cha wafanyakazi kilichosajiliwa, bara na visiwani.
Vile vile wawepo wawakilishi wa kila chama kikuu cha ushirika kilichosajiriwa bara na visiwani, kutoka asasi za kitaifa na kijamii, wakuu wa vyuo vikuu na tume ya vyuo vikuu vya Tanzania, mwakilishi wa kila chama cha siasa chenye usajili wa kudumu pamoja na Watanzania 10 mashuhuri watakaopendekezwa na Bunge la Jamuhuri kutokana na uelewa wao wa kitaalamu katika utoaji wa huduma za kijamii.
Alieleza lengo la kuwashirikisha watu hao ni kuwa miongoni mwa Baraza la Tanzania la Kutunga Katiba mpya (Constitutional Assembly).
 
Jaji ataka Katiba imtambue Mungu

Imeandikwa na Anastazia Anyimike; Tarehe: 2nd April 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 102; Jumla ya maoni: 0








JAJI mstaafu Barnabas Samatta ameshauri Katiba mpya kumtaja Mungu kwa maana ya kumtambua, imtenganishe Rais asiwe sehemu ya Bunge, impunguzie madaraka na pia liundwe Baraza la kumshauri.

Akizungumza katika ufunguzi wa kongamano la pili la Katiba lililoandaliwa na Jumuia ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA), Samatta alisema pamoja na kuwa serikali haina dini, ni vema ikamtaja Mungu.

Alisema wimbo wa taifa unamtaja Mungu mara nyingi, lakini Katiba haimtaji Mungu hata mara moja, kuna nchi kadhaa zikiwemo za Afrika Mashariki, Kenya na Uganda ambazo zimefanya hivyo na kuongeza kuwa pamoja na kwamba serikali haina dini, ni vyema katiba ikamtaja Mungu.

Akizungumzia huru wa raia katika kutoa maoni, Jaji Samatta alisema Katiba inatakiwa kuwa na utashi wa wananchi na pia kutoa nafasi kwa wafungwa na mahabusu katika kutoa maoni.

"Watu washirikishwe katika mchakato wa kutengeneza Katiba kuliko ilivyo sasa kwenye muswada na pia ni vyema Rais akaondolewa kuwa sehemu ya Bunge ili kutoa uhuru zaidi kwa wabunge na pia liundwe baraza la kumshauri rais ambalo litajumuisha watu waliopitia masuala ya sheria na wengine na wengineo," alisema.

Akiainisha juu ya Katiba mpya kutoe nafasi kwa wananchi kuwa juu ya Bunge ikiwa ni tofauti na ilivyo sasa, Samatta alisema; "Kuna wakati mwananchi mmoja(Mchungaji Christopher Mtikila) alifungua kesi ya kutaka kuwapo mgombea binafsi na hukumu ikatolewa kwa upande wake, lakini suala hilo likapelekwa bungeni ambao walilipinga na kuja na kitu kingine kilichoiondolea nguvu mahakama".

Pia alitaka suala la itikadi katika Katiba liainishwe kama litakuwa moja au kila chama kitakacho kuwa madarakani kuwa na itikadi yake.

Aidha, katika mjadala huo wajumbe walikosoa baadhi ya vipengele vya muswada huo na kudai kama vitaachwa kama vilivyo vitapelekea kupatikana kwa Katiba ambayo haitakidhai matakwa ya wananchi na ustawi wa nchi.

Mabere Marando akiwakilisha Chadema alikosoa muswada huo na kudai kuwa kifungu cha 20 cha muswada huo ambacho kinakataza kwa mtu yeyote kwenda kuhoji mchakato wa Tume mahakamani na kwa kufanya hivyo mtu huyo atakuwa ametenda kosa la jinai ambalo litamfanya alipe faini isiyozidi milioni tano au kifungo kisichozidi miezi 12.

Pia Marando alihoji kipengele cha 28, ambacho kinaelezea kuwa kampeni ya Katiba mpya inatakiwa kusimamiwa na kuendeshwa na tume na vyama vya siasa au taasisi havitahusika kufanya hivyo na atakayeendesha kampeni za katiba nje ya utaratibu huo atahukumiwa
kifungo cha miaka miwili jela bila kutozwa faini.

Dk Sengondo Mvungi wa NCCR-Mageuzi alipendekeza kuundwa kwa baraza la kutunga katiba ambalo linaweza kuundwa na uwakilishi wa kila jimbo na tume itakayoundwa kusimamia mchakato huo kuwajibika kwenye Baraza ikiwa ni toafuati na muswada ambao unataka tume
kuwajibika kwa Rais aliyeiteua.

"Nimesikitishwa sana na huu muswada, kwani umetengenezwa si katika kuhakikisha tunakuwa na Ktiba iliyo nzuri, hivyo ni lazima tuungane katika kuupinga kabla hata haujafika bungeni hiyo Aprili 7," alisema.

Pamoja na kupendekeza viongozi wa vyama vya siasa na wanachi kuwa katika mkao wa kiharakati kutokana na kutokubaliana na muswada huo, Naibu Katibu Mkuu (Tanzania Bara) wa Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro alisema wamesisitiza suala la kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi ambayo itaundwa na makundi mbalimbali ya kijamii na suala la kuruhusiwa kwa mgombea binafsi.

Naye Profesa Issa Shivji alisema kuwa katika muswada huo kumekuwapo na vipengele ambavyo vinakinzana na kutolea mfano wa kifungu cha 16 ambacho kinaeleza kuwa baada ya tume kukamalisha ripoti ambayo haitakiwi kuhojiwa, ina wajibu wa kupelekwa kwa Rais ambaye anajadiliana na Rais wa Zanzibar na hivyo kupingana na kifungu cha 17 ambacho kinasema tume inaweza kupeleka katiba hiyo kujadiliwa na wananchi kwa usimamisi wa viongozi wa serikali za mitaa, vijiji na tarafa.

Mwenyekiti wa UDP, John Cheyo aliwataka vijana na wananchi wa Tanzania kuendesha mchakato wa Katiba kwa amani na kuwa wao kama wabunge watakuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha muswada huo unakuwa mzuri kabla ya kupitishwa.

Mwenyekiti wa Chama cha wanasheria Wanawake(TAWLA), Maria Kashunda alihoji kifungu cha 6 ambacho kinaelezea wajumbe wa tume wasiozidi 30 wataundwa kwa idadi sawa ya Tanzania Bara na Zanzibar na kuwa hakitakuwa na uwiano wa uwakilishi.

"Hiki kipengele kina matatizo, Tanzania Bara ina wananchi zaidi ya milioni 42, Zanzibar ina watu milioni moja sasa kama utakuwa na uwiano sawa sijui kama kutakuwa na uwakilishi, na pia kama Zanzibar yenye watu milioni moja wakikataa katiba na bara kuikubali inamaana katiba itapita tu, na pia muswada ulitakiwa kubainisha uwakilishi wa jinsia."

Profesa Chris Maina alipendekeza katiba na muswada huo kuandikwa kwa lugha ya Kiswahili ili kutoa nafasi kwa Watanzania wote kuelewa na kuchangia na kuwa kinyume cha hivyo sasa ambao umewalenga wachache wanaojua lugha ya Kiingereza.

Mjadala wa Katiba uliibuliwa wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 na baadaye Rais Jakaya Kikwete aliridhia kuanza kwa mchakato wa kuandaliwa kwa katiba itakayokwenda sambamba na wakati uliopo.
 
J Sunday Apr 03, 2011
04_11_egm33y.jpg
A participant at debate forum on the envisaged new constitution, Prof. Issa Shivji, presents his views.The debate was held at Nkrumah Hall at the University of Dar es Salaam on Saturday. (Photo by Fadhili Akida)
 
Sunday April 03, 2011 Local News
Samata calls for cut-back on presidential powers





By PIUS RUGONZIBWA, 2nd April 2011 @ 15:00, Total Comments: 0, Hits: 98

RETIRED Chief Justice Mr Barnabas Samata has advised that the President should not be part of the Parliament of Tanzania if the doctrine of separation of powers should have much sense.

He has also advised for a new Act to re-check the current constitutional powers vested in two-thirds of all Members of the Parliament to approve changes in the constitution.

He was participating in a public debate on the government proposed bill on the Constitutional Review Act of 2011 to be tabled in the Parliament in Dodoma next week.

Justice Samata also called for the Bill to include the public outcry which calls for an independent candidate and review the current restriction that prevents presidential election results from being challenged in a court of law.

"We also want the constitution to limit the size of the cabinet to be in line with other countries such as Ghana where their constitution stipulates on the number of Cabinet members. Our new constitution should not remain silent on that," he said.

Meanwhile, the stakeholders who attended the Conference expressed their dismay over the government's decision to table before the Parliament next week the Bill on the Constitutional Review Act, instead of writing a new constitution as proposed before.

Debating the new Bill at the University of Dar es Salaam on Saturday, various speakers including university students, academicians, politicians, lawyers, activists and the general public said the Bill was prepared contrary to the people's recommendations, therefore it has to be re-drafted and thoroughly discussed by the majority of members of the public.

Another concern raised by the participants was on the timeframe given by the government to discuss the Bill.

They further said that the time was not enough for most citizens to contribute their views conveniently on the drafting of the new constitution.

The Executive Director of the Legal and Human Right Centre, Mr Francis Kiwanga, and Justice Samata advised on the fresh Bill to be published in media outlets for more public debate instead of rushing it to Parliament.

"The government has to respect people's basic rights of expressing their views, freely and fairly. I propose that all people be given enough time to contribute towards the new constitution because this one has been so abrupt and confusing," he said.

On his part, besides the government preparing the Bill which doesn't incorporate people's views, Mr Kiwanga said the Bill should be written in Kiswahili language so that many stakeholders with different capacities of understanding and knowledge may contribute their views.

He said for the new peoples' constitution to be available four things must be accomplished. These are a free constitution commission, a constituency assembly, a referendum and the National Assembly which were not considered in the Bill to be tabled before the April meeting in Dodoma.

A representative of the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM), Prince Bagenda, said his party has agreed to have the constitution reviewed.

"CCM has agreed to accommodate public views on the agenda but has insisted that all stakeholders including politicians have the rights to participate -- not only specialists as proposed here. We also want a specific timeframe for the agenda to reach to an end," he said.

He was followed by CHADEMA representative Mr Mabere Marando who said the proposed Act aimed at preventing opposition parties from participating in the campaign process for the proposed constitution and leave the task in hands of CCM local leaders and Shehas in Zanzibar.

Representative from NCCR-Mageuzi Dr Sengondo Mvungi said the Bill has proposed for the National Parliament to act as a National Constitutional Assembly which is unacceptable.
"It appears those who prepared this bill are not Tanzanians!

Why have they neglected views of the majority! It is high time now activists prepared schedule of amendments to be presented in Dodoma the same day this bill will be presented," he suggested.

But John Cheyo of UDP asked for peace to prevail for the whole process to become successful and counselled all who want to instigate chaos especially using the youths to stop their plans.

That was before the CHADEMA Chairman, Mr Freeman Mbowe, had called for the application of what has been usual party's motto in recent days calling for people's power to have the new bill as opposed to the proposed one.

According to the notice signed by the Permanent Secretary, Mr Phillemon Luhanjo, the Constitutional Review Act of 2011 shall if passed in the Parliament become operational on the first day of June this year and shall apply to the Mainland Tanzania as well as Tanzania Zanzibar.
 
Diwani aanzisha somo la Katiba


na Rodrick Mushi, Moshi


amka2.gif
KUTOKANA na wananchi wengi kutoifahamu Katiba ya Tanzania, Diwani wa Kata ya Njoro, Manispaa ya Moshi Jomba Khoi (CHADEMA), ameanza kutoa elimu kwa wananchi kwa kuweka utaratibu wa wananchi kuisoma Katiba iliyopo ili kutambua udhaifu uliopo.
Alisema ameamua kufanya utaratibu wa wananchi kufika katika ofisi za Chama cha CHADEMA iliyopo katika kata hiyo, ambapo watapata fursa ya kujisomea katiba inayotumiwa hivi sasa ili kufahamu haki zao.
Khoi aliyasema hayo wakati akiwashukuru wananchi wa kata hiyo kwa kumchagua katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Railway na kusikiliza changamoto mbalimbali za wanachi wa kata hiyo.
Alisema kuwa ameamua kuwa mstari wa mbele katika suala hilo la katiba kutokana na katiba kubeba maisha ya Watanzania, ambapo pia alisema kuwa wananchi wakiisoma Katiba iliyopo na kuilewa itarahisisha katika kutoa maoni kuwa wanahitaji katiba ya namna gani.
Kutokana na utaratibu huo wa usomaji wa katiba ndani ya Kata hiyo ya Njoro, diwani alisema muda wa kujisomea katiba hiyo itakuwa inapatikana muda wote na kutakuwepo na Katiba iliyoandikwa mwaka 1977 ambayo ndiyo inayotumiwa hivi sasa.
Diwani huyo alisema zoezi hilo ambalo amelianzisha litakuwa endelevu ili kutoa fursa kwa wananchi kutoa maoni yao pindi tume ya kukusanya maoni itakapoanza kazi ya kukusanya maoni kwa wananchi.
 
Majukumu ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
ban.sheria.jpg


Allan Kajembe​

amka2.gif
TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ni mojawapo ya tume iliyopewa majukumu makubwa na muhimu, katika utekelezaji na usimamizi wa utawala bora na haki za binadamu hapa nchii.
Ni tume iliyoanzishwa na sheria yake mahususi, ambayo ni sura namba 39 ya marejeo ya sheria ya mwaka 2002 ya seria za Tanzania.
Sheria hiyo imeipa mamlaka tume hiyo kufanya kazi katika pande zote za Tanzania yaani Tanzania Bara na visiwani kama ambavyo kifungu cha 3 cha sheria hiyo kinavyosema.
Kitu kingine cha muhimu katika sheria hiyo ni matumizi ya sheria hiyo yanavyokwenda sambamba na Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 (kama ilivyofanyiwa marekebisho mara kwa mara), kwa mujibu wa kifungu cha 2 cha sheria hiyo.
Tume hiyo imepewa majukumu mengi na ya muhimu katika kusimamia utawala bora na haki za binadamu ambazo ni pamoja na kuinua na kulinda haki za binadamu kama ambavyo zinaelekezwa na katiba yetu, pia kufanya uchunguzi kuhusu mambo yote yanayohusisha uvunjifu wa haki za binadamu hapa nchini.
Tume hiyo pia ina majukumu ya kufanya utafiti juu ya haki za binadamu na utawala bora na pia kuielimisha jamii kuhusiana na mambo hayo.
Majukumu mengine yaliyopewa kwa tume hiyo ni jukumu linalopatikana chini ya kifungu cha 6(1) kifungu kidogo cha (e) ambacho kinaipa tume mamlaka ya kumfungulia mtu, watu au idara yoyote ile, kesi mahakamani, kama itajiridhisha kulikuwa na uvunjaji wa haki za binadamu na kwamba tume itakuwa inaomba fidia kwa ajili ya mwathirika wa uvunjaji huo wa haki za binadamu.
Ina majukumu ya kuhakikisha mikataba yote ya kimataifa ambayo Tanzania inaingia kuhusiana na haki za binadamu inaridhiwa na kufuatilia utekelezaji wa mikataba hiyo hapa nchini.
Jukumu jingine linaloendana na hilo ni kushirikiana na serikali, tume imeagizwa kushirikiana na idara na vyombo vya Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika, Jumuiya ya Madola na vyombo kadhaa vitakavyoanzishwa kwa makubaliano ya nchi mbili au zaidi, na hata kushirikiana na taasisi za hapa nchi au za nchi nyingine katika kuhakikisha kuna ulinzi na kuinua haki za binadamu na utawala bora hapa nchini.
Tume hiyo pia ina majukumu ya kusaidia upatanishi na maridhiano baina ya pande mbili zilizo katika mgogoro ambao wameenda kupata ufumbuzi katika tume.
Tume hiyo pia inaweza kutembelea maeneo au watu walioathirika na uvunjifu wa haki za binadamu kama vile vizuizini au panapofanana na hivyo ambapo chini ya kifungu cha 6(1),(h) ya sheria hiyo, tume baada ya kufika eneo au kwa mtu huyo itafanya makadirio na uchunguzi kwa mtu/watu hao na mwisho kutoa mapendekezo yake kuhusu njia gani za kuwalipa fidia wahanga wa uvujnifu wa haki za binadamu kwa kuzingatia mahitaji ya sheria hiyo.
Pamoja na kuwa na majukumu mengi ndani ya sheria, tume imepewa mamlaka ya kutoa maoni yake kuhusiana na sheria, kanuni au miongozo yoyote iliyopo ili kuhakikisha kwamba viwango vya haki za binadamu pamoja na kanuni za utawala bora zinafikiwa na kutekelezwa.
Jukumu hili linakwenda sambamba na kutoa ushauri kwa serikali na taasisi zingine za umma kuhusiana na masuala yahusuyo haki za binadamu na utawala bora hapa nchini.
Ndugu msoamaji, majukumu ya tume hiyo ni mengi na yoye yanahusu haki za binadamu na utawala bora, aidha kama haki hizo zimevunjwa au kuna nia ya kuzivunja basi tume hiyo uhusika moja kwa moja kuchukua hatua itakayoona inafaa.
Uongozi wa tume hiyo umewekwa chini ya Mwenyekiti wa tume, ambaye kwa mujibu wa kifungu cha 7, anapaswa kuwa jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania au ya Zanzibar, au Jaji wa Mahakama ya Rufaa ya Tanzania.
Pia tume ina Makamu Mweneyekiti ambaye kimajukumu anapaswa kutoka upande mwingine wa Jamhuri ya Muungano dhidi ya ule wa Mwenyekiti, kwa maana ya kwamba kama mwenyekiti atatoka Tanzania Bara basi Makamu wake atapaswa kutoka Tanzania visiwani, kwa mujibu wa kifungu cha 7(1), (b) cha sheria hii.
Pamoja na kuwa na mwenyekiti na makamu mwneykiti, tume hii pia itakuwa na wajumbe wasiozidi watano ambao wanajulikna kama makamishna, ambao uteuzi wanaopaswa kuzingatia vigezo vya kuwa watu wenye elimu na uelewa, uzoefu kuhusiana na mambo yanayohusu haki za binadamu, sheria, masuala ya kiserikali, siasa na masuala ya kijamii.
Makamishna hawa watasaidiwa na makamishna wasaidizi na wote hawa huteuliwa na rais baada ya kupata maoni kutoka kwa kamati ya uteuzi.
Hata hivyo mtu yeyote atakayeteuliwa kuwa Kamishna, Naibu Kamishna au Mweneyekiti wa tume hiyo, chini ya vifungu vya 8 na 9 watatakiwa kuacha kazi kama wanafanya kazi katika ofisi kama mbunge, mwakilishi (kwa Zanzibar), Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Spika wa Baraza la wawakilishi.
Kwa mujibu wa kifungu hicho atatakiwa pia kuacha kazi ikiwa atakuwa jaji au ofisa yeyote wa mahakama, ofisi yoyote ya umma, ofisa wa tume ya uchaguzi, au ofisa wa serikali za mitaa au ofisi yoyote ya umma.
Hata hivyo mweneykiti anaweza kutolewa katika nafasi yake kama atatangazwa mufilisi au kama atastaafu au kufariki dunia.
Kifungu hiki cha sheria hii kinaendana sambamba na matumizi ya ibara ya 129(6) ya Katiba ya Muungano.
Kamishna ambaye ataacha ofisi/kazi katika mojawapo ya ofisi zilizoainishwa kifungu cha 9(1), yaani tulivyoviona hapo juu, atarudishwa katika nafasi hiyo baada ya kumaliza muda wake kama kamishna.
Haya ni mahitaji ya sheria hii chini ya kifungu cha 9(2) cha sheria hii.
Kwa maelekezo ya kifngu cha 10 cha sheria hii, kamishna ataondolewa kuwa kamishna kama atakuwa anashindwa kutimiza majukumu yake kutokana na ugonjwa, tabia mbaya/utovu wa nidhamu kinyume na maadili ya viongozi wa umma, au kwa sababu nyingine yoyote itakayoonekana inafaa.
Tume hiyo pia itakuwa na katibu mkuu ambaye pia atateuliwa na rais baada ya kushauriana na tume, miongoni mwa watu wanaoongoza au waliowahi kuongoza nafasi za juu serikalini.
Katibu huyu ni lazima awe na shahada ya sheria kutoka katika chuo kikuu kinachotambuliwa na serikali na ana uzoefu wa miaka mitano ya uongozi katika taasisi za umma, au amefanya kazi za sheria kwa maana ya uwakili, kufanya tafiti au kufundisha sheria, kwa kipindi kisichopungua miaka mitano.
Tume hii inaweza kufanya uchunguzi kwa kuamua yenyewe au baada ya kupokea malalamiko kwa mujibu wa sheria hii toka kwa mtu aliyeathirika na uvunjaji wa haki zake za kibinadamu ambapo tume itafanya uchunguzi kwa niaba ya mtu huyo, pia inaweza kupokea malalamiko kutoka katika kikundi cha watu au jumuiya.
Hata hivyo mamlaka ya tume hii katika kufanya uchunguzi imewekewa mipaka kwa kutumia Ibara za 46 ya Katiba ya Jamhuri na ibara ya 36 ya Katiba ya Zanzibar, haitakuwa na uwezo wala mamlaka ya kumchunguza Rais wa Jamhuri ya Muungano na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Pia tume imewekewa mipaka ya kutochunguza shauri lililopo mahakamani au katika baraza lolote lenye mamlaka ya kimahakama, kuhusu masuala yanayohusu kazi kati ya serikali ya Tanzania na serikali za nje au kampuni au shirikisho lolote la nje, au kuchunguza suala lolote linalohusiana na msamaha wa rais.
Katika mambo hayo, tume haitakuwa na mamlaka ya kuchunguza kitu chochote isipokuwa kama rais ataelekeza vinginevyo, kama ambavyo kifungu cha 16(3) cha sheria hii kinavyoelekeza.
Malalamiko yanaweza kupelekwa katika tume hii kwa njia ya mdomo au kwa maandishi na yatatakiwa kujazwa katika fomu maalumu zinazopatikana katika tume hiyo.
Inapotokea kama malalamiko yatapelekwa na mtu aliyeko chini ya ulinzi kama jela au mahabusu au kama ni mgonjwa aliyeko hospitali, basi malalamiko yatapelekwa haraka na mtu atakaye pewa na mtu huyo.
Malalamiko hayo yanaweza kupelekwa na mtu binafsi au na kampuni, iwe imesajiliwa au la.
Mtu anayepeleka malalamiko yake katika tume, anaweza kuwakilishwa na wakili katika malalalmiko yake, na kwamba baada ya kupokea malalamiko hayo, tume itamuita mlalamikiwa au mtu yeyote aliyekaribu naye na kwamba tume itatoa muda na nafasi ya kutosha kwa kila upande unaohusika na malalamiko hayo.
Tume hii pia ina uwezo wa kumwamrisha mtu kwenda kwa njia ya samansi kumhoji mtu akiwa chini ya kiapo kwa malalamiko yaliyopo mbele yake na pia kutoa amri ya muda mfupi ikisubiriwa kumalizika kwa shauri zima
 
Wazo Langu

Katiba mpya izingatie masuala muhimu kwa jamii


Imeandikwa na Mayrose Majinge; Tarehe: 2nd April 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 46; Jumla ya maoni: 0


04_11_1pnkk3.jpg








TANZANIA imo katika mchakato wa kuandika Katiba mpya ambapo Watanzania watapewa fursa ya kuchangia kikamilifu katika kuhakikisha wanakuja na Katiba wanayoitaka wao wenyewe, ili kuondokana na malalamiko kuwa Katiba inatoka juu na kushushwa chini.

Mimi ni mmoja wa Watanzania wenye haki ya kutoa maoni yao kuhusu suala hili la uandaaji wa Katiba mpya, ingawa inanisikitisha kwamba Taifa linakabiliwa na roho ya kunyoosheana vidole na kulaumiana, kuliko kutoa mchango chanya katika kukabiliana na changamoto zinazotukabili zikiwamo mtambuka za njaa, magonjwa na ujinga.

Katika kulitakia heri na fanaka Taifa letu la leo na kesho, lazima tujiwekee misingi ya kuzingatia wakati wote tunapoandaa Katiba mpya, ambayo ndiyo sheria mama ya nchi.

Vinginevyo ama tutatumia muda mrefu kuikamilisha au kujikuta tunaandaa Katiba kipindi hiki na baada ya muda tukaona haitufai.

Madhumuni makuu ya Katiba mpya inafaa yawe ni haki kwa wote kwa maana ya kila Mtanzania kupata haki anayostahili kama mwanadamu na kama mwananchi anayejivunia nchi yake na uhuru kamili, kwa maana ya Katiba kulenga kumfanya Mtanzania awe huru katika mambo yake ya msingi, ikiwa ni pamoja na Taifa kujitawala lenyewe kisiasa, kiuchumi na kimaadili.

Katika kuhakikisha kwamba Katiba inalenga mambo hayo mawili ya msingi, ni lazima kuzingatia kwamba Katiba inatakiwa kuwa mtetezi na mlinzi wa haki na uhuru wa kila Mtanzania na pia kuwa kichocheo cha heshima ya nchi.

Katika kuwa mtetezi wa haki na uhuru wa Mtanzania, maana yake ni kuhakikisha kwamba haki inapatikana kwa kila Mtanzania, lakini pia haki haiwezi kuzungumzwa bila kuzingatia pia wajibu; kila mtu atakapotimiza wajibu wake haki kamwe haitapotea.

Watanzania wengi wameacha kuangalia na kutimiza majukumu yao ya kazi na kuendekeza uzembe na rushwa, wakati huo pia wakisimama kidete kudai haki. Haki itatoka wapi huku uzembe na rushwa vimekithiri? Tusijichanganye hapo.

Ni muhimu sana wakati wote wa kuandaa Katiba tuzingatie namna gani kila Mtanzania ataweza kubanwa na Katiba ili atimize wajibu wake.

Katiba inapaswa kuwa kichocheo cha heshima ya nchi yetu kwa kuhakikisha inalinda na kudumisha heshima ya Taifa letu. Mtu huwezi kuwa mtumwa au mfungwa ukasema una heshima, haiwezekani mfungwa au mtumwa akaheshimika.

Mambo muhimu ambayo ni nyenzo mbadala za kuleta uhuru wa kweli katika Taifa letu ni nidhamu ya kazi, chuki dhidi ya ujinga, kuchochea uwezo wa kitaifa na heshima kwa kila Mtanzania.

Hakuna asiyejua kuwa nidhamu ya kazi katika nchi yetu inatia shaka. Uhuru bila kazi itatoka wapi? Kaulimbiu ya Uhuru ni Kazi itiliwe mkazo ili tuishi vizuri.

Watanzania wengi hatuishi tunavyostahili kuishi. Wakati tunajua kazi ni kipimo cha utu na ni uhai. Sasa utu wetu uko wapi? Uhai wetu uko wapi? Nidhamu ya kazi ni muhimu katika mustakabali wa maisha ya kila Mtanzania.

Watanzania takriban asilimia 95 bado hawajachukia vya kutosha adui ujinga na ndiyo maana wengi utawasikia wakisubiri kulipwa posho, ndipo wahudhurie semina au mijadala! Mtu anakupa chakula cha akili bado unataka akulipe! Umasikini wetu uko katika vichwa vyetu.

Katiba mpya ihakikishe inachochea watu kuchukia ujinga, kwani ni adui mbaya kuliko adui wote duniani. Kuna kitabu kinasema: "Mkiijua kweli itawaweka huru."

Kuchochea uwezo wa kitaifa ni jambo muhimu sana katika maendeleo ya kila Mtanzania, kwani Taifa lisilo na uwezo ni balaa. Ni vema kujua silaha ya uwezo wa kitaifa ni ipi.

Silaha hiyo ni namna ya kutoa vipaumbele kwa raslimali za Taifa letu hasa lugha ya Taifa na vipaji vya Watanzania - haya hayajatumika ipasavyo kujikomboa.

Baraza la Kiswahili la Taifa (Basata) litumike kuhakikisha masuala yote ya kitaifa yanatafsiriwa kwa Kiswahili-mikataba, miswada, sheria. Na wageni wachochewe kujifunza lugha yetu.

Vipaji vya Watanzania vitambuliwe, viwe msaada kwao, kwani vinaonesha uwezo asili wa mtu.
Kuhusu heshima kwa kila Mtanzania, hilo halina mjadala, lakini tujue heshima pia ina mipaka, kuna madaraja kati ya wakubwa na wadogo.

Mtu akipewa madaraka au ukuu kidemokrasia aheshimiwe, kwani ana uwezo, ndiyo sababu kapewa madaraka aachiwe mamlaka ya ulinzi na usalama wake, vinginevyo mambo hayatakwenda.

Ukuu anaopewa mtu una meno yake na nyenzo zake. Ukuu ni nguvu na uwezo wa kimamlaka juu ya wanaoongozwa. Bila mamlaka hakuna ukuu. Kuna mambo ambayo Rais lazima yampe ahueni au ulinzi wa kimaadili.

*Mwandishi wa Wazo hili ni Mwenyekiti Mtendaji wa Shirika la Huduma za Maendeleo ya Jamii.
 
Mswada wa Katiba wazidisha nguvu za rais


Na Tumaini Makene

WAKATI kilio cha muda mrefu cha wanaharakati na wasiasa wakitaka madaraka ya rais yapunguzwe hakijamalizika, Muswada wa Sheria ya mabadiliko ya
Katiba umezidisha mamlaka hayo kuanzia maandalizi yake, huyo ukizuia kujadili suala la urais na muungano.

Muswada huo juzi ulitawala kongamano la katiba lililoandalwia na wanataaluma wa chuo kikuu cha Dar es Salaam ambapo wachangia wengi walitoa wito kwa watanzania kuukataa kila njia.

Kifungu cha tano cha muswada huo, katika sehemu ya tatu, pamoja na masuala mengine kinazungumzia mamlaka ya Rais wa Muungano kwa kushauriana na Rais wa Zanzibar, kuteua tume itakayoratibu mchakato wa utungwaji wa katiba mpya.

Kifungu cha 6 (1), kinazungumzia wajumbe wa tume hiyo ambao nao watateuliwa na rais, kwa kuzingatia uwiano sawa wa uwakilishi kati ya Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar.

Pia katika uteuzi huo, rais atazingatia sifa zingine kama uzoefu na kiwango cha taaluma, umri, jinsia kwa makundi mbalimbali, mgawanyiko wa nchi nzima ya Tanzania, maslahi ya taifa na sifa zingine ambazo rais ataona zinafaa.

Kifungu cha 16 (1) katika sehemu hiyo ya tatu, kinasema kuwa baada ya tume kumaliza kukusanya maoni, itakabidhi ripoti yake kwa rais, ambaye atatoa nakala kwa Rais wa Zanzibar, kisha atamwelekeza waziri kuwasilisha muswada katika Bunge la Katiba.

Pia kifungu cha 21 katika sehemu ya tano ya muswada, kinazungumzia mamlaka ya rais kuunda Bunge la Katiba, kutangaza katika Gazeti la Serikali, baada ya 'kuligeuza; bunge la sasa kuwa bunge la katiba. Pia atakuwa na mamlaka ya kuteua majina ya wabunge watakaounda Bunge la Katiba.

Hoja zinazopinga vifungu hivi vinavyotoa mamlaka makubwa kwa rais kuanzisha, kusimamia hata kuamua mchakato wa katiba ni pamoja na kuwa rais mwenyewe kama kiongozi wa moja ya mihimili ya serikali, ni zao la katiba. Hivyo hawezi kutengeneza katiba kisha akawapatia wananchi waifuate.

Suala hilo la kuhamisha mamlaka kutoka kwa wananchi ambao ndiyo 'wenye' katiba na kuyaweka mikononi mwa mtu mmoja, wadau wengi, wakiwemo wataalam wa sheria wanasema kuwa, litasababisha katiba itakayopatikana kukosa uhalali.

Kwa mujibu wa wataalam wa sheria, katiba ya sasa haina mwafaka wa kisheria wala kisiasa kwa sababu taratibu za msingi, hasa katika kuwashirikisha watu katika mchakato mzima na namna ya kupata bunge la katiba, hazikufuatwa, kitu ambacho kinaonekana kutaka kujirudia tena sasa.

Mathalani, Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) katika mada yake katika Kongamano la Maudhui ya Msingi ya Katiba Mpya, mwishoni mwa wiki, Chuo Kikuu Dar es Salaam, alisema kuwa utaratibu huo wa kumpatia rais mamlaka makubwa ni kupora mamlaka ya wananchi.

Imeelezwa kuwa kulifanya bunge la sasa kuwa bunge la katiba si sahihi, ndiyo mfumo uliotumika kwa katiba ya sasa, ambayo inalalamikiwa kwa ukosefu wa uhalali.

"Rais ni zao la katiba, rais hawezi kutengeneza katiba na kuwapa wananchi waifuate, hii itapelekea katiba hiyo kuwa na lack of legitimacy (kutokuwa halali) tatizo ambalo linadhihirika sana katika katiba ya sasa. Wananchi wameporwa mamlaka kwa kumfanya rais kama chombo cha utengenezaji katiba".

"Kazi ya kutengeneza katiba ni ya wananchi, katiba ni ya wananchi, kwa manufaa ya wananchi," anasema Bw. Kiwanga katika mada yake aliyoitoa kwenye kongamano juzi.

Sifa na muundo wa tume 'mungu mtu'

Kifungu cha 6(1) kinazungumzia wajumbe wa tume watakaoteuliwa na rais na namna muundo wake utakavyokuwa kama ilivyoelezwa hapo juu. Hiki kinaibua hoja ya uhuru wa tume hiyo, huku ikihojiwa kuwa kwa nini wajumbe hao wasiteuliwe na wananchi, kupitia kamati ya bunge ikishirikiana na rais.

Hadidu za rejea, ambazo tume itatumia kufanyia kazi ya kukusanya maoni, zimezungumziwa katika kifungu cha 8(1), ambapo imesemwa kuwa rais ndiye atatoa hadidu hizo kwa tume, kisha ataipatia muda wa kufanya kazi hiyo na kukabidhi ripoti.

Hili nalo linapingwa, huku wadau wakitaka hadidu za rejea ziwekwe bayana katika sheria ikayotungwa na bunge, kwani tume hiyo inapaswa kuwa ya wananchi si ya rais. Wanatolea mfano wa Tume ya Jaji Kisanga ya White Paper (1998) ambapo ilipewa hadidu za rejea na rais, baadaye 'akafoka' kuwa wamefanya nje ya majukumu aliyowaagiza.

Lakini pia kwa mujibu wa katiba ya sasa, rais hawajibiki kusikiliza ushauri wa mtu yeyote anapokuwa akitimiza majukumu yake, hivyo wadau wanasema kuwa kifungu hicho kinaweza kutumika kuweka kapuni baadhi ya maoni ya tume ya kukusanya maoni, kisha akapitisha yale tu, anayoona yeye yanafaa.

Kifungu cha 20 katika sehemu ya nne ambayo inazungumzia utaratibu wa tume ya kukusanya maoni, pamoja mambo mengine, kinasema kuwa tume hiyo haitashtakiwa katika mahakama yoyote ile, wala mahakama hazina nguvu ya kuhoji mamlaka ya tume, kitu kinachodaiwa 'kuifanya tume mungu mtu'.

Ni katika sehemu hiyo ambapo inaelezwa kuwa mtu yeyote atakayeonekana kupinga, kuingilia au kuzuia utendaji kazi wa mjumbe wa tume au sekretarieti (au vyombo hivyo), atakuwa amefanya kosa la jinai, ambalo adhabu yake ni faini ya sh. milioni 5 au kifungo kisichozidi miezi 12 gerezani.

Profesa Chriss Maina anaona hakuna umuhimu wa kufanya makosa kama hayo ya jinai, huku wengine wakisema imewekwa kwa nia ya kutaka kuwatisha watu, hasa wale watakaoonekana kutoa maoni kinzani na mwenendo wa tume.

Pia kinapingwa kuwa watendaji wa vijiji na kata ambao watatumika katika mchakato huo wa kukusanya maoni, kuwa wengi ni makada wa CCM, pia wamekuwa ni 'majaji' katika masuala mengi huko vijijini, hivyo kuna uwezekano wakatumia mwanya katika kifungu hiki kuwakamata wote watakaoonekana kutoa hoja kinzani.

Pia kifungu hiki kinazungumzia mikutano ya kijiji itakayoitishwa na watendaji wa vijiji, kutoka sehemu moja mpaka nyingine, kukutana, kujadili, kutoa maoni yao kwa tume kisha kuondoka, bila kuwa na mamlaka yoyote ya kuhakikisha walichojadili kinafanyiwa kazi.

Kifungu hiki kinaelezwa kuwa kimekwepa hatua ya muhimu ya kuwepo kwa Jumuiko la Kitaifa la Katiba, ambalo Dkt. Willibrod Slaa anasema kuwa ni mkutano rasmi wenye mamlaka ya kuyadili maoni hayo na rasimu ya katiba, kipengele kwa kipengele.

Bw. Kiwanga anasema kuwa Jumuiko la Kitaifa la Katiba lina uwakilishi mpana wa mikoa au kanda, jumuiya za dini, vyama vya siasa, vijana, wanawake, watoto na wenye mahitaji maalum, kuwa litajadili, kurekebisha na kupitisha pendekezo la katiba mpya.

Ushirikiswaji wa wananchi ni muhimu

"Kupitisha pendekezo la sheria kama mswada ulivyo hivi sasa tutaruhusu utaratibu unaonyang'anya mamlaka ya wananchi. Nia nzuri ya kutunga katiba ionekane kwa wenzetu wenye mamlaka na dhamana ya uongozi kwa kuweka taratibu nzuri.

"Tanzania ni yetu, hatma ya taifa hili iko mikononi mwetu, tuwajibike, tuache woga, tujadili, tufikie mwafaka wa kitaifa. Katiba mpya ni jibu. Jibu la kurudisha maadili ya taifa na kulinda rasilimali za taifa. Tuchukue hatua," anasema Bw. Kiwanga.

Suala la kura ya maoni

Sehemu ya sita ya muswada huo, kifungu cha 28, kinazungumzia upigaji wa kura ya maoni ya siri, kuikubali au kuikataa rasimu ya katiba mpya kwa kusema 'ndiyo' au 'hapana', huku kikizuia vyama vya siasa au asasi zingine za kiraia kupiga kampeni kuhamasisha wananchi.

Kifungu hicho kimefanya kosa hilo kuwa la jinai kwa mtu yeyote, chama cha siasa au asasi yoyote kufanya kampeni kuhamasisha wananchi kupiga kura hiyo, adhabu yake ni kifungo cha miaka miwili gerezani bila faini. Kazi hiyo itafanywa na tume ya uchaguzi pekee na si vinginevyo.

Hapa napo kumezua mjadala mkali, kwani vyama vya siasa na asasi ndizo zenye wafuasi wengi na ni haki yao kuhamasisha na kuwapatia elimu wananchi, hali ambayo, Profesa Issa Shivji anasema 'kura ya maoni bila kempeni ni hatari sana', kwani ni muhimu elimu ya uraia kutolewa wakati huo.

Vitu visivyohojiwa

Kifungu cha 9(2) katika sehemu ya tatu ya muswada kinapiga marufuku kuzungumzia masuala kadhaa wakati tume itakapokuwa ikifanya kazi yake, nayo ni; suala la muungano wa Tanganyika na Zanzibar, mihimili ya serikali yaani dola, bunge na mahakama.

Mengine yasiyohojika ni; Serikali ya Mapiduzi ya Zanzibar, Umoja, mshikamano na amani ya Tanzania, mfumo wa uchaguzi unaotoa haki kwa wote, ukuzaji na ulinzi wa haki za binadamu, haki sawa mbele ya sheria, utu wa binadamu, serikali kutokuwa na dini na uhuru wa mahakama.

Hapa inashauriwa kuwa wakati wa mchakato wa utungwaji katiba si sahihi kupiga marufuku kuhoji baadhi ya mambo, bali wakati wa utungwaji wa katiba mambo hayo yanaweza kuwekwa, mathalani itapigwa marufuku kuhoji serikali kuwa na dini.

Pia marufuku hiyo izingatie historia ya taifa la Tanzania, kama vile suala la muungano, tunu za taifa, uhuru, umoja na maadili, Azimio la Taifa, Ripoti ya Jaji Kisanga, Misingi ya Haki za Binadamu na Demokrasia.

Katika mada yake, Bw. Kiwanga alimalizia kwa kusema "hatuhitaji kujenga watu au viongozi madhubuti, tunahitaji kujenga mifumo madhubutini itakayodumu na kulinda maslahi ya taifa na kulinda rasilimali za taifa kwa faida ya vizazi vya sasa na miaka mingi ijayo".
 
Moto wa Katiba kuwaka Bungeni Send to a friend Sunday, 03 April 2011 20:46

Habel Chidawali, Dodoma
BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kuanza vikao vyake kesho mjini Dodoma, huku macho na masikio ya Watanzania yakielekezwa katika muswada maalumu wa kuunda Tume ya kukusanya maoni na kupendekeza muundo wa Katiba mpya.

Mbali ya Katiba, wabunge watapokea ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ambayo Rais Jakaya Kikwete aliagiza ipelekwe bungeni.
Akijibu moja ya maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu katika mkutano wa pili wa Bunge hilo, Pinda alisema kuwa suala la Katiba litapelekwa katika huu wa tatu wa akiwataka wabunge kusubiri kwani watapata uwanja mpana wa kuogelea.

Kwa mujibu wa maelezo ya Pinda, hakukuwa na sababu ya kujibu swali lililohusiana na Katiba akisema tayari Rais alishapanga muswada huo uwasilishwe mapema bungeni na wabunge wapate nafasi ya kuujadili kabla ya kutoa mapendekezo ya namna mchakato wake utakavyoendeshwa.

Suala la Katiba ndilo linalogonga vichwa vya watu huku wengi wakiwa na wasiwasi kuwa likipelekwa bungeni hakutakuwa na haki kwani kwa sehemu kubwa itakuwa ‘ndiyo' kutokana na wingi wa wabunge wa CCM katika ya uwakilishi huo.

Juzi, katika kongamano la kujadili Katiba lililoandaliwa na Jumuiya ya Wanataaluma ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam baadhi ya wasomi na wanazuoni walionyesha wasiwasi wao kuhusu muswada huo kuwasilishwa bungeni wakisema kuwa unaweza kubebwa na upande mmoja kwa ajili ya maslahi ya chama kilichopo madarakani.

Katika Mkutano huo ambao wabunge watakaa kwa muda wa wiki mbili mjini hapa, CAG atawasilisha ripoti yake April 12 ikihusu ukaguzi wa hesabu za Serikali za Mitaa, Serikali Kuu na Mashirika ya Umma na ukaguzi wa ufanisi wa mwaka 2009/2010.

Kwa mujibu wa Kanuni za Bunge, Waziri wa Fedha kwa niaba ya Waziri Mkuu, atawasilisha ripoti hiyo mbele ya kikao cha Bunge kwa niaba ya Waziri Mkuu ambaye aliagizwa na Rais kupeleka Hesabu hizo bungeni ili watunga sheria hao wakazisome na kutoa michango yao pale inapobidi.

Taarifa ya CAG inaonyesha kuwa bado kuna upungufu na changamoto nyingi zinazohitaji kufanyiwa marekebisho makubwa. Ametoa mapendekezo yanayolenga kudhibiti matumizi ya fedha na rasilimali za nchi, mapendekezo ambayo Rais ameyaafiki.

Kwa upande mwingine Spika wa Bunge atakuwa na kazi ya kumalizia viporo vya maswali mengi ambayo yalibaki katika Mkutano wa Pili ambayo yalikuwa ndani ya ratiba lakini hayakuulizwa kutokana na muda.

Katika maswali ya papo kwa hapo ambayo huulizwa Waziri Mkuu kila Alhamisi Bunge linapokuwapo, huenda akakutana na swali kuhusu tiba ya Loliondo kwa babu kwani licha ya Serikali kutoa ufafanuzi juu ya tiba hiyo kutokuwa na madhara kwa binadamu, huenda wabunge wakataka kujua uchunguzi wa Serikali umebaini inatibu magonjwa yapi.
 
Wabunge wasikubali mswaada huu wa marekebisho ya Katiba Waheshimiwa wabunge, MUSWAADA wa marekebisho ya katiba ya JMT iliyopo nimeuchukulia kama mzaha au utani mkubwa toka kwa wale waliouandaa ambao wanatia mashaka kama ni Watanzania wenye uchungu na jinsi nchi yetu inavyoendeshwa kwa udhaifu na mapungufu makubbwa na kama kweli wanakitakia mema na bora kizazi chetu kijacho. Baada ya kuzungumza na wazee wawili watatu waliokuwa wameshika nyadhifa za juu katika masuala ya sheria nchini nikafunguliwa macho na masikio na kugundua kwamba muswada huo ni hila makusudi ya CCM katika kujinunulia muda na kurefusha mchakato wa katiba bila kujali gharama inazozidi kuwabebesha wananchi ikiwemo zile za Richmond, Dowans, Ufisadi Benki Kuu, IPTL, leseni za madini na mikatba mingine bomu kama hiyo. Rais na chama chake imedaiwa kwamba wana malengo mawili. Lengo hilo ni kuwa kwa kuleta muswaada mbovu bungeni na kuwatumia watu wasio wataalamu kuuandaa waliamini kuwa wanasheria na vyama vya upinzani watakwenda mahakamani. Na watu walio ndani kabisa ya chama tawala na serikali wanasema hayo ndiyo yaliyokuwa matarajio yao. Kwa bahati mbaya, wanakongamano na wanasheria wote kwa ujumla walio na mapenzi ya nchi na watu wake na siyo mapenzi na chama fulaani cha kisiasa wakagutukia hili. Wamekataa kwenda mahakamani. Na wanatafuta njia mbadala ambazo mchakato pamoja na kuchelewa kidogo lakini utaendelea kuliko kusimamishwa kabisa. Lingine ambalo CCM na kiongozi wake wanaomba litokee kwa kupeleka muswaada mbovu bungeni ni kuwa wabunge na wanaharakati wanaoipenda nchi yao na wanaotaka haki ya wananchi kuwa na katiba waliyoshiriki kuiandaa wataukataa nayo itapata sababu ya kuurejesha ulikotoka na hivyo kuendelea kupata nafasi ya kupumua na kuuchelewesha muswaada huo ili katiba mpya isipatikane kabla ya uchaguzi mkuu. CCM ina uhakika kuwa katiba iliyopo hivi leo ndio katiba tu itakayoweza kuwasaidia kuiba kura tena mwaka 2015 na kurejea tena madarakani na kwamba katiba hiyo ikikatishwa muda wake kabla ya mwaka 2015 CCM haitakuwa na muda wa kujijenga upya na kurejesha kuaminiwa na kukubalika kwake nchini kama baadhi ya vyama vya upinzani vinavyoaminiwa na kukubalika sasa bila hata ya kwenda kwa babu! CCM imeshindwa kuamini kwamba matatizo ya nchi hii hayaruhusu wao kulazimisha kubaki madarakani na kama watafanya hivyo na huku chama hicho kikianza kutafuta msaada wa dini fulani nchini tayari watakuwa wamepanda mbegu ya kuleta vilio na misiba Tanzania mwaka 2015 kwani haitakuwa rahisi kwa watu na vyama vyao na wagombea kukubali kuibiwa kura kwa mara nyingine tena. Ni mzaha kwa hiyo viongozi wa CCM wanapoongelea amani na umoja nchini humu na huku wanawatumia viongozi wa dini fulani kuwaunga mkono; wanachezea mchakato wa katiba na ujio wa sheria mpya; wanagombana wenyewe kwa wenyewe; wanaifilisi hazina; wanawatumia watu wasio hata na elimu ya sekondari kuwashauri; wanabagua watu, wilaya na mikoa na uongozi umeanza kugeuka wa kibabe kwa kukaripia na kuwakosoa watumishi wa umma hadharani kudhani kuwa chama hicho kweli kinataka amani na umoja uendelee kuwepo hapa Tanzania na kama chama hicho kitaondoka bila kufanya vituko, fujo na ghasia endapo kitashindwa katika uchaguzi mkuu ujao. Ielweke kwa wapenda amani wote Tanzania kwamba CCM kwa kuleta muswaada kama huu bungeni imetangaza kwamba ni ADUIA WA AMANI NA UMOJA WA WATANZANIA! Pia nilishiriki katika kongamano lililofanyika UDSM chini ya UDASA na kwa kweli nimefurahishwa na uzalendo wa wote waliohudhuria pale, pamoja na kuonekana dhahiri kwamba CCM imepuuza kongamano hilo na imemtuma mamluki ambaye kazi yake ni kuhama toka kusiko na maslahi na kwenda kwenye maslahi. Kuwepo kwa wataalamu na wasomi hawa lakini kukosekana kwa CCM kunadhihirisha kitu kimoja tu. Nacho sio kingine lakini namna ambayo serikali yake ilivyowadharau na kupuuza kutumia ushauri wa wataalamu na badala yake kuwa mtumiaji mkubwa wa ushauri wa watoto wa mjini au wakaa vijiweni. Inaelekea kazi ya kuandaa muswaada huu ilifanywa na watu wa karibu na Ikulu ambao kwa kuwa wananufaisha uongozi uliopo na chama tawala kwa namna moja au nyingine walipewa kazi hii. Na pamoja na kulipwa mapesa mengi kilichofanyika ni 'kucopy na kupaste' na kama Profesa Shivji angelipewa nafasi katika kongamano la pili la katiba pale mlimani alikuwa na mengi tu ya kukosoa. Haikuwa hivyo. Lakini kilichodhirika hatima ya yote ni kwamba muswaada huo ni mbovu na haufai kukubaliwa na bunge la wabunge wanaowajali na kuwatetea watanzania hata kama watahongwa mabilioni ya fedha kwa maana watakuwa wameichimbia misingi ya maangamizi na upotevu nchi yao na vizazi vyake vyote vijavyo. Wabunge ukataeni muswaada huu. Ikumbukwe Kenya ilichukua miaka mingi kupita kiasi kutokana na ubishi wa viongozi wa chama tawala. CCM ijue basi kuwa kama inavyowabebesha Watanzania gharama haramu za IPTL, ndege ya rais, ukarabati wa majengo ya wakubwa, kuingilia TANESCO na mashirika mengine katika kazi zao, safari za nje za viongozi wake, Dowans, Ufisadi benki kuu ndivyo pia inavyotaka kuwabebesha Watanzania gharama zisizo na sababu kwa kufanya madudu katika uandaaji wa muswaada wa katiba. Na nia ya chama tawala ni dhahiri: 'inataka kama ikiwezekana katiba mpya wasiwepo na iendelee kuwatawala Watanzania kwa katiba ya viraka milele na milele!' Hayumkiniki, kama CCM ina nia ya kweli ya kuwapa Watanzania katiba mpya. Maana kinachozungumzwa humo ni marekebisho ya Katiba. Ingawa tunashangaa uungwana wa mheshimiwa Mwenyekiti wa CCM ulipoishia maana alishawaahidi mengi Watanzania kuhusiana na katiba lakini kaishia pungufu kwa asilimia 75 katika kauli zake na kututia Watanzania wapenda haki na amani wasiwasi mkubwa. Hili ni pamoja na ule ukweli kwamba katika mfumo wa vyama vingi, uwazi na ukweli hatuna budi kusema kwamba mheshimiwa rais kadiriki KUPORA madaraka ya wananchi kwa kupendekeza kuteua tume ya uchaguzi badala ya kuwaachia wananchi katika makundi yao ya kimaslahi kuchagua baraza la Katiba la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 20111 kwa utashi na ridhaa yao wenyewe bila kuingiliwa na mkuu yoyote wala chama chochote. Kwa heshima na taadhima, tunamuomba rais awarudishie Watanzania kilicho chao, yaani, mamlaka juu ya uundaji wa Katiba mbadala ya JMT, na yeye abakie na chake, yaani, Chama cha Mapinduzi na serikali iliyoko madarakani. BARAZA LA KATIBA LA JMT 2011 ambalo litaundwa kwa kuhakikisha kila mkoa, kila kundi la maslahi, watumishi wa serikali, vyama vya kisiasa, viongozi wa dini, wabunge waliopo, wakulima, wafanyakazi, wazee, wanawake, watoto, vijana wote wanapata fursa ya kuwawakilisha wenzao barazani ndilo linalostahili kuunda Tume ya Katiba Mpya ya Tanzania kwa kuchagua miongoni mwa wananchama wake na nje ya baraza hilo watu wa kuiwezesha tume hiyo kufanya kazi hiyo bila upendeleo, kwa haki, ukweli, uwazi, kitaalamu na kiufundi. Kuna kila sababu ya CCM kuogopa ujio wa Katiba Mpya. Hili linaeleweka. Lakini ni dhambi isiyosameheka kwa wabunge, wawe wa upinzani au wa chama tawala kutosa matarajio, matazamio, mustakabali, maslahi na amani ya watoto wao, wajukuu zao na vizazi vyao eti kwa kuikoa CCM na hatari iliyoko mbele yake. Katika suala hili, ni dhahiri tutatambua ni nani anaiwakilisha CCM bungeni na ni nani anawakilisha wananchi wake bungeni. Ni dhahiri, ikiwa mbunge ni mtu mwenye kufaa na manufaa kwa watu wake haijalishi anatokea chama gani. Na hili kwalo sasa Watanzania wameanza kuamka baada ya kugundua wabunge toka upinzani pia wanaweza kufanya makubwa kama serikali na CCM isipowachezea shere katika maamuzi na mipango ya majimbo yao. CCM ingelikuwa na akili, kwanza ingelijizaa upya na kujipanga kufuatana na katiba maridhawa ambayo pengine itakuwa bora kuliko ile ya Kenya kama sio ile ya Marekani tayari kwa ajili ya Tanzania mpya ambayo mafiga yake yatakuwa demokrasia, haki na usawa na amani na umoja. Ni makosa kwa hiyo pia kuwa na kifungu chochote katika muswaada huo ambacho kinawatisha wananchi ambao ndio mabwana na waajiri wa serikali na rais kwa lolote lile. Hii itakuwa ni sawa na kumwibia mwananchi haki yake na kisha kumtisha kumtia ndani endapo atalalamika kwamba ameibiwa na anaendelea kuibiwa. Wananchi kama mabwana na matajiri wa watawala (serikali na rais) kimsingi ndiyo wenye haki ya kuamua juu ya vipi wale wanaotaka kuwatawala watatakiwa kuwatawala, nguvu zao na mipaka yao. Mambo yakienda kinyume cha hivyo ni kuwa waajiriwa (rais na serikali) wameamua wao wenyewe kumwambia tajiri yao watafanya kazi gani, hawafanyi nini na watajilipa kwa uamuzi wao wenyewe mishahara kiasi gani. Hiki ni kichekesho cha mwaka. Tanzania nchi iliyotangulia kukubali demokrasia haistahili kabisa kuwa kichekesho cha nchi nyingine za Kiafrika zilizokuwa za mwisho kabisa kukubali demokrasia na mfumo wa vyama vingi. Ni baraza la katiba tu linaloweza kufanya kazi hii bila kuingiliwa na rais au mtu yeyote. Maana unapozungumzia kuwa katiba isomwe, ieleweke na itafsiriwe na watu wengi kadri iwezekanavyo kiungo cha kuwaunganisha wananchi na wale watakaowasaidia kuunda sheria zinazotoka kwenye mawazo na mapendekezo yao ni baraza ambalo lina mizizi yake ndani ya vikundi mbalimbali vya kimaslahi, kimaeneo na kijamii. Bila baraza hatutakuwa na uwakilishi mzuri baina ya makundi yafuatayo: watawala dhidi ya watawaliwa; vya kidini na visivyo vya kidini; kisiasa na visivyo vya kisiasa; mjini dhidi ya vijiini; wanasiasa dhidi ya wasio wanasiasa; wakulima dhidi ya wafanyakazi na wafanyabiashara; raia dhidi ya polisi na jeshi; matajiri dhidi ya maskini; Watanzania walioko nchini na walioko nchi za nje; Washauri toka vijiweni na washauri toka vyuo vikuu; walimu dhidi ya wanafunzi; wagonjwa (waliopo na watarajiwa) dhidi ya madaktari na manesi; wanaonufaika na fedha za hifadhi ya jamii dhidi ya wazee na wastaafu wasionufaika sana na mifuko ya jamii; wachezaji mpira na viongozi wa mpira; wenye nyumba na wasiokuwa na nyumba; wanaonufaika na mfumo uliiopo na wasionufaika na mfumo uliopo; wafungwa na raia huru; wazalshaji dhidi ya walaji; wanawake dhidi ya wanaume; watoto dhidi ya watu wazima; vijana dhidi ya wazee; wafugaji na wasio wafugaji; wawindaji na wasio wawindaji; wachimba madini na wasiochimba madini; wavuvi na wasio wavuvi; wakulima na wasio wakulima; viongozi wa kuteuliwa dhidi ya viongozi wa kuchaguliwa; mikoa yenye vyuo vikuu na mikoa isiyo na vyuo vikuu; mikoa yenye redio na televisheni na mikoa isiyo na redio na televisheni; mikoa yenye benki kata na benki za kijamii na mikoa isiyokuwa benki kata na benki za kijamii; mikoa yenye maji ya uhakika na mikoa isiyo na maji kabisa; makabila makubwa kwa makabila madogo; makabila yanayofaa kuwa rais na makabila yasiyokubaliwa kutoa rais; mikoa dhidi ya nchi (Zanzibar); wenye dini na wasio na dini; mikoa yenye barabara na mikoa isiyo na barabara wala madaraja; na kadhalika. Kwa haraka haraka, haiwezekani kamwe Tume ya Katiba kufikia makundi yote haya wala kuwa na uwakilishi wa makundi yote haya. IT IS IMPOSSIBLE. Turudi kwenye ya msingi (back to basics) mheshimiwa akubali kashauriwa vibaya na kinachohitajika sio tume na wala yeye hastahili kuunda tume hiyo na akubali kwamba WATANZANIA WANA HAKI YA KUCHAGUA BARAZA LA KATIBA 2011 litakalochagua tume na kufanya kazi ya kuiwezesha nchi hii kuwa na katiba mpya, na taasisi zote zikiwa na wataalamu na wasio wataalamu kama wajumbe na ambazo hazitaweza kuingiliwa na rais au mwanasiasa yoyote au chama chochote cha kisiasa au kundi lolote la kidini katika kazi yake. Eti inasemekana kwamba CCM inapeleka muswaada huu bungeni ulioandaliwa na watoto wa mtaani kwa sababu ilihofia kuwapa wataalamu ambao wengi wao wanatoka dini moja na hivyo kuhatarisha maslahi ya chama tawala ambacho kimeanza kulalia upande fulani kwa makusudi huku kikihubiri hadharani kinyume cha yale inayoyafanya. MASHARTI YA KUWEZESHA KUPATIKANA KATIBA MPYA BORA, SAFI NA NZURI DUNIANI: 1. Wananchi waitwae haki yao ya kuunda Baraza la Katiba la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; 2. Rais na chama chake tawala, CCM, lazima wakubali kuwa ni wadau katika uundwaji wa katiba ijayo; 3. Rais na chama chake tawala, CCM na serikali yao lazima kisalimishe haki ya mchakato wa katiba kwa wananchi wakitambua kwamba wananchi ndio bwana na wao ni watumishi wa wananchi; 4. Baraza la Katiba 2011 liundwe kutokana na makundi ya kimaeneo, kijamii, kimaslahi na kiajira au kikazi; 5. Baraza liwe na angalau mwakilishi mmoja wa kimaeneo kutoka kila wilaya Tanzania, hawa wawe wanajua hofu, matatizo na matarajio ya wilaya zao; kisha kuwe na uwakilishi wa vikundi au vyama vya kisiasa na wanaharakati; kisha kuwe na uwakilishi wa vikundi vya kiimani au kidini; kisha kuwe na makundi ya uwakilishi wa wazalishaji, mathalani, kilimo, ufugaji, uvuvi, uchimbaji madini, viwanda na kadhalika; kisha kuwe na uwakilishaji wa walimu/wahadhiri, madaktari, manesi, wahandisi, wanateknolojia, watumishi wa umma, watumishi wa sekta binafsi, wafanyabiashara na makundi mbalimbali ya kikazi na kijamii; bila kusahau kuwepo kwa vikundi vingine vyovyote vitakavyochangia ukamilifu na utilimilifu wa katiba tarajiwa; 6. Tume iundwe na Baraza la Katiba kwa kuwachagua baadhi ya wajumbe wake na wajumbe toka nje ya Baraza ili mradi tume iweze kuwa na sura pana, ya kina na ya mitazamo na mielekeo tofauti ili kuweza kuleta changamoto tarajiwa katika mchakato mzima wa kuzaliwa upya kwa katiba tarajiwa; 7. Kila panapopwaya Tume iwe huru kuunda kamati mbalimbali zitakazokidhi matakwa na matarajio yake kwa wakati ili kuhakikisha katiba mpya inapatikana ndani ya miaka 2-3; 7. Uwe wajibu wa baraza na tume kuandaa mikakati ya uelimishaji, ufahamu, uhamasishaji na ushirikishwaji wananchi katika kutoa maoni kwa kufuata utaratibu mzuri wa statistiki wa sampling na uteuzi wa watu wa kuhojiwa ili kitakachopatikana kiwe kinawakilisha kwa kiasi kikubwa mtazamo wa wadau walio wengi; 8. Matokeo ya awali au rasimu itakayoandaliwa na tume itarudishwa barazani kujadiliwa, kuboreshwa au kurejeshwa kwa tume kwa masahihisho au nyongeza au utoaji maudhui zisizostahiki na tume inaweza kuwashirikisha wadau fulani fulani ionapo upo umuhimu wa kufanya hivyo ili kupata kilicho bora zaidi; 9. Wadau wote na ikiwezekana wananchi wote wapate rasimu hiyo kupitia gazeti la bure litakalochapwa na kusambazwa nchi nzima. Baraza na Tume pia ifanye mipango na mikakati itakayowezesha watu majumbani kwao kuizungumzia rasmi hiyo wakishirikiana na redio, televisheni na njia zingine za mawasiliano ikiwemo simu za mkononi; 10. Baraza na Tume liunde wavuti na kuihimiza serikali kuanzisha vituo vya muda vya kijamii katika maeneo mbalimbali nchini ambako kompyuta na mtandao utapatikana kwa watu kuchangia maoni au mawazo yao na kuisoma rasimu kabla haijapelekwa mbele zaidi; 11. Baraza litakaporidhika rasimu hiyo ifanywe muswaada rasmi wa kupelekwa bungeni kujadiliwa na kupitishwa kama sheria halali iliyo. Baraza litafanya hivyo kwa kupigia kura muswaada huo huku ikiwa kiwango cha kukubalika kimeshaamuliwa kabla; 12. Wananchi na wajumbe wa Baraza na Tume wawe huru kumjadili yeyote na kujadili chochote kwa maslahi makubwa ya nchi hii na watu wake na hasa kama kweli tuna nia ya kuwa na katiba mpya itakayokidhi mahitaji ya Watanzania kwa miaka 50 au zaidi ijayo; 13. Huu ni wakati wa kutumia rasilimali watu na rasilimali zetu nyingine kikamilifu tukijua kwamba kazi tunayoifanya siyo ya miaka 2-3 bali kazi inayohitaji kutufaa sisi na kizazi kijacho hata kwa miaka 100 au zaidi kama The Declaration of Independence ya Marekani linavyoifaa nchi hiyo miaka 240 toka kuandikwa na kutamkwa hadharani. 14. Ionekane na ikubalike kwamba ni dhambi isiyo na mfano kwa kiongozi au mwananchi yeyote kuchukulia suala la kuundwa kwa katiba mpya kama utani au mzaha kwani suala hili linahusu uhai, usalama na ustawi wa taifa letu na watu wake. 15. Watanzania bila kujali vyama vyao vya siasa wasikubali kabisa hatima ya watoto, wajukuu na vizazi vyao vijavyo kuchezewa na watu wachache wasioitakia nchi hii na watu wake katiba safi, bora, nzuri na inayofaa kuwalinda wananchi wa nchi hii kwa miaka 100 au zaidi! CCM inajua fika kutokana na sera zake mbovu kisiasa, kiuchumi, kijamii, kiteknolojia na kiutamaduni hivi leo asilimia 70 ya Watanzania ni wajinga. Kutokana na ujinga wa asilimia hii 70 pamoja na kujua kwamba wanaharakati na vyama vya upinzani vikipewa fursa ndani ya miezi michache vinaweza kuwatoa wananchi kwenye ujinga waliomo inataka bado kuendelea na dhamira yake ya kuutumia ujinga wa Watanzania hao ili kutia katiba iliyopo viraka na kuendelea kutawala kwa kuwadanganya, kuwadhihaki, kuwakejeli, kuwaonea, kuwapuuza, kuwanyanyasa, kuwadhalilisha na kuwachimbia kwenye umaskini zaidi baada ya chama hicho kula fedha zote za MKUKUTA chenyewe na vibarakala wake na sasa vinataka kutapanya pia kile kitakachotolewa kama ruzuku na misaada kwa ajili ya MKUKUTA2. Chama hicho kingelikuwa na nia njema na hatima ya Tanzania kingewalitumia wasomi, wataalamu wa sheria na wananchi wengine waliofunguka macho kuwa ndio kiini cha kuwafungua macho na kuwaelimisha raia wengine ili mwisho wa siku kila MTANZANIA BAADA YA MIAKA MIWILI MITATU AWE KATIKA NAFASI YA KUJIVUNA KWAMBA NA MIMI NILISHIRIKI KUUNDA KATIBA MPYA YA TANZNAIA TUNAYOITUMIA LEO. KATIBA AMBAYO ITANG'ARA AFRIKA NZIMA NA IKIWEZEKANA DUNIANI KOTE NA SIO KATIBA ITAKYOTUFANYA TUCHEKWE, TUKEJELIWE NA KUDHIHAKIWA NA DUNIA NZIMA! Binafsi, nitashangaa na ninaamini Watanzania wenzangu watashangaa pia kama safari hii Watanzania na wabunge wao watafanywa na uongozi uliopo madarakani kuwa wajinga waliwao na mabwege wa mwisho kabisa duniani. Hata kama ni asilimia 40 tu ya Watanzania wanaosikiliza redio na ni asilimia 15 tu ya Watanzania wanaoona televisheni na asilimia 3 tu ya Watanzania wanaosoma magazeti kila siku bado wanaharakati, wabunge wetu na wananchi wote waliofunguka macho wanaweza kabisa kuwaambia wananchi nini kinachoendelea kuhusiana na katiba hii. Hakika Bwana Reginald Mengi na kituo chake cha Televisheni (ITV) na redio yake ya Radio One wanastahili heshima na shukrani za kipekee kwa kuwa Mtanzania pekee anayewatakia mazuri na mema Watanzania wenzakae na vizazi vyetu vijavyo. Mungu ampe afya na maisha marefu katika kutenda mema na mazuri kwa Watanzania. Wabunge wetu waheshimiwa, ninaomba kutoa hoja: 'KATAENI MSWAADA HUO, BUNGE LISIMAME KWA MUDA, KUSIWE NA KIKAO CHA BAJETI HADI BARAZA LA KATIBA 2011 LIMEUNDWA NA MCHAKATO WA KATIBA MPYA UMEANZA!' Mungu ibariki Tanzania na wape rehema, huruma na neema zako wale wote wanaoututakia mema Watanzania wa leo na wa kesho na walaani na uwaingize motoni wale wote wanaoitakia mabaya na hasara na gharama kubwa wananchi wa Tanzania kwa kuleta mzaha na kurefusha kazi inayotakiwa kufanywa siku moja ikachukua mwezi, wiki moja ikachukua mwaka, mwezi mmoja ikachukua miaka 10 na mwaka mmoja kuchukua karne! Walaani na watupe katika kaburi la sahau la historia ya nchi yetu na watu wake!
 
Kikwete kitanzini
• Muswada wa Katiba wapondwa pondwa

na Mwandishi wetu


amka2.gif
RAIS Jakaya Kikwete anakabiliwa na wakati mgumu wa kuuendeleza mchakato wa uandaaji wa Katiba mpya, hasa baada ya wadau kuukataa kwa madai una upungufu mkubwa.
Wadau hao wamewaonya wabunge kutoupitisha muswada huo unaotarajiwa kuwasilishwa bungeni katika vikao vya Bunge vinavyotarajiwa kuanza kesho kutwa mjini Dodoma.
Huo utakuwa ni mtihani mwingine mgumu kwa Rais Kikwete ambaye hivi sasa anakabiliwa na jukumu zito la kukisafisha chama chake kinachodaiwa kuwabeba makada waliokifanya kipoteze baadhi ya majimbo kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 30, mwaka jana.
Wakizungumza katika kongamano lililoandaliwa na Umoja wa Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA) lililofanyika jana jijini Dar es Salaam, wadau hao walisema muswada huo hautoi haki kwa wananchi wote kama ilivyotarajiwa.
Wasomi, wanaharakati na viongozi wa vyama vya siasa walisema serikali ichukue maamuzi magumu, hasa kwa kukubali maoni na marekebisho yanayofanywa na wadau badala ya kuendelea kumrundikia madaraka makubwa Rais Jakaya Kikwete.
Akifungua kongamano hilo, Jaji Mkuu mstaafu wa Tanzania, Barnabas Samatta, alisema muswada huo umepotoshwa na umelenga zaidi kutogusa vyombo muhimu katika mabadiliko ya sasa ya Katiba mpya.
Alisema kitendo cha mwandishi wa muswada huo kutaka kutoguswa wala kujadiliwa mamlaka ya Rais na Mahakama ni kwenda kinyume cha mahitaji na matakwa ya Watanzania wa sasa.
Jaji Samatta alisema Katiba mpya inatakiwa kutoa uhuru hata wa kitaaluma na sanaa na kueleza endapo mtu akienda kinyume cha kufafanua haki zake ndani ya Katiba mpya.
"Kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yake, neno maoni yake ni muhimu kuzingatiwa, mwandishi wa muswada huu amepotosha, kuna nini hadi hataki watu wajadili mamlaka ya rais katika Katiba mpya, kwa umuhimu huu, je, kama ikitamkwa kuwa kiongozi wa juu hatakiwi kuwa na chama nani atawajibika? Hapa ndipo tunapoona umuhimu wa muswada huu kuachiwa wananchi kwa maamuzi sahihi.
"Rais kutokuwa sehemu ya Bunge ni muhimu katika mabadiliko ya Katiba mpya, lakini sasa iko haja ya Katiba kutamka Naibu Spika kutoka chama cha upinzani ili kwenda sambamba na ukuaji wa demokrasia nchini," alisema.
Aliongeza kuwa kama mabadiliko yanayozungumzwa kwenye muswada huo hayatazingatia wadau na viongozi wa vyama vya siasa, watu watarajie hukumu nyingi za magereza ya nchini kujaa wafungwa wa kisiasa.
Alibainisha kuwa ili kuepusha hali hiyo serikali ikubali maoni ya wadau na hata kuufanyia mabadiliko muswada wa Katiba kabla ya kupelekwa bungeni.
Alisema ili kwenda sambamba na ujenzi wa Tanzania mpya, mabadiliko hayo ya Katiba ni muhimu kugusa katika kila ibara na haitakiwi rais kuwa sehemu ya Bunge kama ilivyo katika Katiba ya sasa.
Profesa Issa Shivji
Akichangia mjadala huo, Mwenyekiti huyo wa kigoda cha taaluma cha Mwalimu Julius Nyerere, alisema muswada ulioandaliwa kwa ajili ya kupelekwa bungeni umejaa makosa mengi, hasa ya lugha, kimuundo na kikanuni.
Alisema ni lazima serikali ichukue maamuzi magumu, hasa kwa kukubali maoni na marekebisho yanayofanywa na wadau katika mabadiliko hayo ya Katiba mpya ya nchini.
Alisema kwa kutambua hilo, Tanzania inatakiwa kujua haki na wajibu wa mwananchi wa kawaida na si kumfumba mdomo kupitia Katiba mpya.
Dk. Slaa
Akichangia katika kongamano hilo, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), alisema umefika wakati kwa wanasiasa kutoa dira kwa taifa kuhusu mabadiliko ya Katiba mpya.
Alisema kifungu cha 20, kifungu kidogo cha pili katika mabadiliko ya sasa kilikuwepo katika White Paper mwaka 2008, ambapo iliwapa mamlaka watendaji wa vijiji kusimamia maoni hayo na hata kupelekea wananchi wengi kutishwa na hata kukamatwa kutokana na kifungu hicho.
"Kifungu hiki kimewapa mamlaka makubwa watendaji wa vijiji, hali hii tutawashuhudia wananchi wengi wakikamatwa na hata kuogopa kutoa maoni yao katika kuhoji kifungu fulani cha mabadiliko haya ya Katiba mpya.
"Huenda mpaka kufikia mwaka 2020 isipatikane Katiba mpya nchini lakini ni lazima serikali itambue suala la Katiba mpya ni uhai wa Mtanzania na si jambo la kufanyia mzaha kwa kipindi hiki na Tanzania ya leo," alisema Dk. Slaa.
Dk. Slaa alisema ipo haja kwa wabunge kuacha tofauti zao za vyama na kuungana na kuwa kitu kimoja ili kuukataa muswada huo kwa kauli moja.
Alisema wabunge watakaoupinga muswada huo watapata uungwaji mkono na wananchi ambao ndiyo walengwa wa mabadiliko ya Katiba mpya.
Alisema kama Katiba mpya haitajali maslahi ya makundi ya wananachi wa kawaida ipo siku nchi inaweza kuingia katika hali tete, iwapo mwananchi hatashirikishwa kwa hatua zaidi.
Francis Kiwanga
Mkurugenzi huyo wa Kituo cha Haki za Binadamu nchini alisema mabadiliko ya Katiba ni msingi muhimu nchini.
Kiwanga, alisema kutokana na utungwaji wa muswada ambao unaotarajiwa kuwasilishwa kuwa wa kiwango cha chini, ipo haja ya kufanya makongamano mengi zaidi ili kupata mawazo ya watu wengi.
"Katika hili ni muhimu tupate maoni ya watu wengi na tunasema wote kwa umaskini wetu tutatembea kwa miguu hadi Dodoma ili kwenda kupinga kwa nguvu zetu zote na katu katika hili tunasema wanaharakati kupitia jukwaa la katiba katu hatutarudi nyuma katika madai ya Katiba mpya itakayokuwa na misingi ya haki na demokrasia imara ya nchi," alisema Kiwanga.
Julius Mtatiro
Naibu Katibu Mkuu wa CUF Bara, Julius Mtatiro, alisema kitendo cha serikali kuandaa muswada wa Katiba bila kupata maoni ya wadau hasa vyama vya siasa ni kitendo kinachoashiria kutokuwa tayari kwa mabadiliko ya Katiba mpya.
Alisema upungufu wa makosa hasa katika maandalizi ya muswada huo umefanywa na mtu mmoja akiwa na lengo mahususi la kulinda masilahi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na si kuzingatia haki za mwananchi wa kawaida.
Prince Bagenda
Alikuwa akikiwakilisha Chama Cha Mapinduzi (CCM). Prince Bagenda, alipata wakati mgumu wa kuendelea kutoa maoni baada ya watu kuzomea na kupiga makofi ili asisikie kile alichokuwa akikisema.
Kabla ya watu kufikia hatua hiyo, Bagenda, alisema hoja ya kujadili Katiba mpya ni ya msingi na serikali inayoongozwa na chama chake imekubali, hivyo ni vema Watanzania waitumie fursa hiyo adhimu.
John Cheyo
Huyu ni Mwenyekiti wa UDP, ambaye alikumbana na zomea zomea kama iliyomkuta mwakilishi wa CCM baada ya kusema kuwa muswada huo si sheria, hivyo ni vema wale wasioridhishwa nao wakapinga kwa amani na utulivu.
Mabere Marando na Sengondo Mvungi
Mshauri wa Sheria wa Chama cha NCCR-Mageuzi Dk. Sengondo Mvungi na Mabere Marando (CHADEMA) wameupinga muswada huo kwa madai hauna manufaa kwa taifa na badala yake umejaa vitisho.
Walisema muswada huo umeonyesha hauna nia njema kwa Watanzania na una kipengele kinachokataza mtu yoyote au kiongozi wa chama cha siasa kufanya kampeni juu ya Katiba mpya kwa madai suala hilo ni jukumu la tume itakayoundwa.
Katika kongamano hilo wachangiaji wengi walionekana wazi kuupinga muswada huo wa Katiba ulioandaliwa na serikali.
Kutoka Zanzibar, Mwandishi Wetu anaripoti kuwa baadhi ya wanasheria na wanaharakati wamelalamikia kuwepo serikali kubwa ya Zanzibar ambayo ni matokeo ya madaraka makubwa aliyopewa rais na katiba iliyopo ya 1984.
Walisema tangu Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein, kutangaza baraza lake lenye mawaziri 19, wakiwemo watatu wasiokuwa na wizara maalumu, kumekuwa na malalamiko mengi ya ukubwa wa serikali, wakati Zanzibar ikikabiliwa na uchumi duni.
Akiwasilisha mada katika mjadala uliofanyika jana na kuandaliwa na taasisi tatu zisizokuwa za kiserikali, mwanaharakati, Salma Maulid, alisema Katiba ya Zanzibar imempa mamlaka makubwa rais na ndiyo maana kunaweza kuwepo mawaziri wasiokuwa na wizara maalumu."Rais amepewa madaraka makubwa kikatiba, kuna haja gani Zanzibar kuwepo mawaziri wasiokuwa na wizara maalumu?" alihoji.
Aidha, alisema kwamba wananchi wanahitaji kuiangalia kwa umakini Katiba ya Zanzibar kwa vile kuna vifungu vinampa mamlaka makubwa rais, ikiwemo uwezo wa kulivunja Baraza la Wawakilishi, uwezo wa kuzuia kufanyika uchaguzi mkuu na uwezo wa kusamehe mtu yeyote aliyehukumiwa kufungwa.
Salma alisema sura ya nne hadi 38 kuhusu mamlaka ya rais imetoa uwezo mkubwa kwa rais na kutoa mfano wa Baraza la Wawakilishi, limepewa uwezo kumjadili rais, lakini kutokana na uwezo aliopewa anaweza kulivunja Baraza hilo hata kabla halijamjadili.
Naye, mwanasheria Ali Ali Hassan alisema rais amepewa uwezo wa kuzuia kufanyika uchaguzi mkuu kama kutatokea hali ya vita, lakini katiba hiyo haijaeleza ni vita ya aina gani.
Alisema kwamba, rais amepewa uwezo wa kuteua nafasi mbalimbali nyeti kwa mtu yoyote atakayeona anafaa na katiba hiyo hiyo imempa uwezo wa kumfukuza mtu aliyemteua; awe waziri, katibu mkuu au naibu.
Mwanasheria huyo alisema mjadala huo wa katiba una umuhimu mkubwa kwa wananchi kuifahamu katiba na kuainisha vifungu vyenye kasoro na hivyo kutumia fursa hiyo kupata katiba yenye masilahi.
Aliongeza kuwa suala la uteuzi wa nafasi za uongozi Zanzibar bado lina kasoro, kwa vile baadhi ya watu huteuliwa bila ya kuangaliwa sifa kwa aliyeomba na wakati mwingine hukosekana uwazi na usaili kutofanyika, kama ulivyopangwa.
Taarifa hii imeandaliwa na Bakari Kimwanga (Dar) na Hassan Shaaban (Z'bar).
 
Wabunge tumieni busara, hekima kupitisha Katiba mpya
ban.tafakuri.jpg


Deogratius Temba​

amka2.gif
MUSWADA maalumu unaopendekeza kutungwa kwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa mwaka 2011, kwa ajili kuunda tume itakayosimamia mchakato huo upo tayari kwa ajili ya kupitishwa na Bunge na kutiwa saini na rais.
Muswada huu unakuja kwa udharura na utasomwa bungeni mara moja, kujadiliwa na baadae kupitishwa kama wabunge watauridhia, hofu ni kwamba unaweza usikidhi kiu na hamu ya kupata katiba mpya iliyopo katika mioyo ya wananchi hivi sasa.
Tukumbuke muswada wa sheria ya gharama za uchaguzi ulivyopelekwa Bungeni Februari 2010, wabunge kwa kukosa umakini hawakuusoma, wakaupitisha na makosa yake na kusababisha Rais kusaini sheria yenye mapungufu.
Binadamu au kiumbe chochote chenye uhai kinapodai au kulalamika kuwa na kiu ya kunywa maji, haitokwisha hadi maji yapatikane, hivi ndivyo ilivyo kwenye suala hili la Katiba mpya. Hii ni kiu kubwa kwa Watanzania.
Watanzania masikini wanaume, wanawake, vijana na watoto wanalilia katiba mpya. Wanataka mabadiliko. Umasikini unaowanyonga unatokana na mfumo mbovu wa kiuongozi katika Taifa hili, maradhi na ujinga imepigwa vita kwa zaidi ya miaka 50 haviondoki kwasababu katiba haioneshi namna ya kuviondoa kabisa.
Mkombozi Mkuu ni Katiba mpya ya wananchi iliyoshirikishi. Wasiwasi wangu na hata wadau mbalimbali wanaotetea demokrasia, haki na usawa wa kijinsia nchini unatokana na muswada huu kubeba hotuba na maelekezo ya mkuu wa nchi, yaani Rais Jakaya Kikwete.
Mfano maelekezo ya yaliyopo katika hotuba ya rais ya mwisho wa mwaka aliyoitoa Desemba 31, 2010 yanaonekana ndiyo yamechukuliwa kama kiongozi cha kuandaa muswada na hii itaminya uhuru, usawa na ushirikishwaji wa jamii katika kundaa Katiba mpya.
Serikali na wawakilishi wa wananchi (Wabunge) wasipokuwa makini, hili suala litaua kiu na matarajio ya wengi, wananchi watakata tamaa, na watashindwa kuelewa kama tunakwenda kupoteza muda na fedha nyingi za wapiga kura kwaajili ya kutengeneza katiba ya nani?
Nani ni mdau halisi wa katiba? Je, ni serikali iliyoko madarakani? Je, ni chama tawala? Je, ni wafanya biashara wakubwa? Au ni wanasiasa wa vyama mbalimbali?
Baadhi ya kasoro zinazojenga hofu ni mamlaka makubwa anayopewa rais ikiwemo kuunda tume bila kushirikisha Bunge au wadau wengine, kutengeneza hadidu za rejea na tume hiyo kuwasilisha taarifa yake kwake.
Muswada huu umetoka mwishoni mwa mwezi uliopita watu hawajausoma na unakimbizwa bungeni mwezi huu ili upitishwe. Mapungufu yake ni mengi tunahitaji kuyatafakari.
Mapungufu makubwa yanaanza kuonekana katika sura ya tatu inayoelezea kuanzishwa kwa tume, kifungu (5), (6)-(i-ii). Rais anaunda tume ya kutengeneza chombo cha wananchi kwa kushauriana na Rais wa Zanzibar bila kuwashirikisha wananchi.
Makundi mengine ambayo yameanishwa katika muswada kuwa yatashirikishwa katika tume hayakutajwa kwa majina wala kuaanishwa ni makundi kutoka wapi au ya kijamii au ya wafanyakazi.
Muswada huo pia unataka kumpa rais mamlaka ya kuteua wajumbe wa tume husika bila kushauriana na mtu yoyote isipokuwa Rais wa Zanzibar. Hii imegeuka kuwa ni suala la Ikulu na dola badala ya kulirudisha kwa wananchi.
Muswada huo unaelekeza kuwa katika kuteua wajumbe rais atazingatia uwakilishi wa makundi ya kijamii, lakini makundi husika hayatajwi hata kwa ujumla wake na hivyo kuacha mamlaka yote ya kuamua uwakilishi kubaki kwa Rais.
Kwa wiki kadhaa katika safu hii sasa nimeandika kuwa Watanzania wanadai Katiba mpya iandikwe si mapambo au kuiga wenzetu wa Kenya bali taifa linahitaji Katiba mpya.
Katiba mpya inahitajika kwa haraka kwasababu tumechelewa kuibadilisha na tuko nyuma ya wakati na tusipofanya hivyo kuna hatari.
Kama wabunge watakaa na kukubali kuupitisha muswada huu ambao unalenga kumpa rais mamlaka ya kisheria ya kuunda tume ya kuongoza mchakato mzima wa katiba bila kuhusisha Bunge ama wadau wengine wa msingi watakuwa wamewasaliti Watanzania.
Lengo la Watanzania kudai maabadiliko ya Katiba ni kutaka mabadiliko ya kimfumo, kisiasa na hata kiuchumi, taifa lisonge mbele badala ya kurudi nyuma.
Wasiwasi wetu ni kwamba kama mamlaka ya kuunda hadidu za rejea itaachwa mikononi mwa Rais itakuwa imempa mwanya wa kutoa maagizo kuwa kazi ifanyike jinsi yeye atakavyotaka au chama chake kinavyotaka.
Kasoro nyingine iliyopo kwenye muswada huo ni ile ya tume kuwasilisha ripoti yake kwa Rais ambaye atampa nakala Rais wa Zanzibar na baadaye kumwelekeza waziri mwenye dhamana kupeleka bungeni yale atakayoamua rais.
Kifungu hicho kitakwamisha mabadiliko ya kweli ya Katiba kwa kuwa hakina tofauti na tume zilizofanywa na marais waliopita.
Aidha, uwakilishi katika jukwaa hilo umetajwa tu kuwa ni wa kijografia na kimakundi bila kuweka bayana mnyumbuliko wa uwakilishi. Muswada huo unataka kutoa mamlaka finyu kwa jukwaa hilo kuwa ni kutoa ushauri kuhusiana na muswada; tofauti na mkutano mkuu wa kikatiba ambao ungekuwa na mamlaka zaidi katika mchakato husika.
Kama kweli tumedhamiria kwa dhati kuingia katika mabadiliko, mchakato wa katiba uwe kianzio cha kuonyesha ukomavu wetu kidemokrasia.
Haitakuwa demokrasia au kuwa na Katiba huru kama Rais atateua wawakilishi wa chombo kikuu zaidi katika mchakato wa katiba bila kushauriana na kundi lolote ama wananchi kuhusika katika uteuzi ama kuwa na wawakilishi walioteuliwa na makundi yenyewe, mathalani vyama vya siasa, asasi za kiraia, taasisi za dini, vyama wa wakulima, vyama vya wanafunzi na vyama vya wafanyakazi.
 
Back
Top Bottom