Pre GE2025 Mkutano wa Tundu Lissu na waandishi wa habari februari 12, 2025 umehairishwa

Pre GE2025 Mkutano wa Tundu Lissu na waandishi wa habari februari 12, 2025 umehairishwa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Source #1
View Source #1
JAMII CHECK_LISSU_POTOSHI_12FEB25.jpg
 
Tunachokijua
Tundu Lissu ni mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA ambaye alichaguliwa kutumikia nafasi hiyo mnamo Januari 21, 2025 amkimshinda Freeman Mbowe ambaye alikuwa akitetea nafasi hiyo baada ya kuongoza chama hicho kwa miaka 20.

Mara nyingi kumekuwapo na taarifa za upotoshaji ambazo zimekuwa zikimuhusisha Lissu juu ya masuala mbalimbali ya kisiasa ndani na nje ya chama chake. Rejea hapa, hapa, hapa na hapa.

Mnamo tarehe 10 mwezi februari 2025 CHADEMA ilitoa taarifa kwamba mwenyekiti wa Chama hicho Taifa Tundu Lissu atalihutubia Taifa siku ya Jumatano Februari 12, 2025, saa kumi jioni, ikitarajiwa kufanyika Makao Makuu ya Chama Mikocheni Dar es salaam

Kupitia mtandao wa X kumeibuka chapisho linalosambazwa katika mtandao huo kwamba mkutano huo wa Lissu umehairishwa.


Je, ni upi uhalisia wa chapisho hilo?

Ufuatiliaji wa kimtandao uliofanywa na JamiiCheck ulibaini kuwa chapisho hilo si la kweli na halijachapishwa na kurasa rasmi za mitandao ya kijamii ya CHADEMA.

Aidha hakuna taarifa rasmi iliyotolewa na Chama hicho kuhusu kuhairishwa kwa mkutano huo wa mwenyekiti na waandishi wa habari bali unatarajiwa kufanyika kama ulivyopangwa Jumatano tarehe 12, 2025 saa kumi jioni kama ambavyo taarifa rasmi ya chama hicho ilivyoeleza.

Hata hivyo mkutano huo unatarajiwa kuanyika katika makao makuu ya chama hicho na si Ubungo Plaza kama ilivyoelezwa katika chapisho hilo linalopotosha.​

Attachments

  • Gjkp5kMa4AAZ8ya.jpg
    Gjkp5kMa4AAZ8ya.jpg
    126.6 KB · Views: 4
Back
Top Bottom