Mkutano wa Wanachama wa Simba wapigwa STOP na Polisi

M

Nikiwa shabiki wa Simba kindakindaki namuunga mkono Mangungu mpaka Mwamed atuonyeshe B20 kaweka kwenye akaunti gani.
Mangungu na MO wote hawafai...

Maana kilichotokea, kipindi Mo anadanganya kuweka b20 hakuna kiongozi wa Simba aliyeongea...

Kwanini leo wanaonekana kupingana?

Ni kwasababu hana uhakika na maslahi yake kwasasa, na sio kwamba anaipenda Simba...

Tunashauri Mangungu aondoke na viongozi wengine wote wa wanachama ili tutafute viongozi watakaokaa upya na mwekezaji atuoneshe b20 yetu...

Kama hajawahi kuweka tudili naye kisheria.
 
Mbona hapo mkuu hekima imetumika. Kwa tension ya sasa iliyopo ndani ya Simba, ni hatari sana kuruhusu makusanyiko ndani ya Simba.
 
Wanasimba poleni, naona kufanya vibaya kumewatia upofu mpaka hamuoni mnaelekea wapi!

Mchakato wa mabadiliko haujakamilika, MO anakiwa mpigiwa kura wakati huo huo msimamizi WA kura!
Vipi haki itatendeka?

Hamuoni huu mpango ni harakati za Mo kuweka watu watuifu kwake ili wapitishe matakwa yake?
 
Kikao hakina baraka ya Uongozi mzee.
 
Nadhani kuna kitu cha kujifunza kuhusu uwekezaji kwenye timu, (sports club), ni tofauti na biashara ya kuuza bidhaa ya vitu ama huduma. Timu za mpira kubwa, zinaitwa kubwa kwanza kutokana na idadi ya mashibiki na kiwango cha uwekezaji, ukishirikisha watu kuwa wanachama inamaanisha unabadilisha fikra za watu kuanza kuifikiria hiyo timu kwa Hali na Mali, (kwa moyo), ni sawa na msemo wa kipendacho roho hula nyama mbichi nije kwenye hoja ya msingi mimi napinga muwekezaji kuwa na asilimia kubwa ya umiliki, (uwekezaji), naona timu inakuwa km ya kwake wanao umia mashabiki inaposhindwa kufanya vizuri swali fikirishi je huyo mfadhili akiahirisha kufikiri ama muda wake ukifika kuondoka dunian,i si Ndiyo mtaanza upyaaaaa! Hapo itakuwa kulia na kusaga meno
 
jamani eh, hyo b20 mnayopigia kelele kila siku mo alishasema mpaka chai ya ofisi anagharamia yeye na ni sehemu ya hyo b20. kimsingi mo akiweka daftari la matumizi mezan kwa sasa mnamdai tsh 672.80 tu

tumeelewana.
Asante Kwa taarifa, hauko mbali na nilicho andika hapo juu
 
Samahani Mkuu, unaweza kutueleza japo kwa ufupi madudu ya Mheshimiwa Murtaza Mangungu?
 
Ndio maana ili uweze kufanikiwa katika suala unalopanga, kuna Kipengele kinaitwa Uzoefu kutoka katika Taasisi zingine zilizofanikiwa katika suala hilo unalopanga kulitekeleza. Uzoefu unaupata kwa kwenda kujifunza namna walivyopitia hatua mbalimbali za utekelezaji wa suala hilo. Baada ya kujifunza ndio unaandaa suala ulilolipanga kwa kuchota uzoefu wa wenzio na kuujumuisha na baadaye kuweka vile unavyotaka wewe. Sasa je hili suala la uzoefu lilifanywa na Simba wakati wa kufanya mabadiliko ya uendeshaji kutoka kuwa Timu ya Wanachama kwenda kuwa Timu inayomilikiwa na Wanachama pamoja na Mwekezaji?
 
Mangungu oyeeee,,,,Mlikuwa mnadhani mangungu Ile confidence anatoa wapi? Serikali Ina watu wake pale wanaoangalia usalama wa hivi vilabu, aiwezekani mhindi aje kupora Mali ya wanachama kwa njia za panya na aachwe tu, atoweza akumbuke kilichomkuta manji wakati anataka kuikodisha yanga, Mo kayakanyaga ni Bora izo pesa zake anazotumia kuwaonga wanachama wamtoe mangungu azitumie kufanyia kazi nyingine atapata hasara ya bure serikali ndiyo iliyoshika mpini na sio mangungu Kama anavyodhani!
 
Bado Wana nafasi ya kujirekebisha mimi nionavyoona kinacho hitajika ni pesa kwanza, lakini hizo pesa zikipatika uongozi huu utakuwa nazo makini? ,Kwakuwa bado wanavutana, nadhani Simba wajipange upya hata kwakuchelewa kidogo, kuhusu muwekezaji naona kaiweka Simba kwenye kiganja Kwa maana usajili wa dirisha kubwa uko mlangoni na unahitaji pesa za kutosha je wanachama wanaweza changa hizo pesa Kwa muda mfupi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…