Mkuu wa chuo DIT unatambua huu unyanyasaji?

Mkuu wa chuo DIT unatambua huu unyanyasaji?

Uchumikati

Member
Joined
Dec 8, 2020
Posts
82
Reaction score
97
Pamekuwepo kilio cha mda mrefu sana ambacho hakijawahi tafutiwa ufumbuzi juu ya waalimu wa part-time kunyanyaswa kwenye malipo na si mara moja au mbili malamalamiko yalisharipotiwa.

Tunasema ni manyanyaso kwa sababu kila semester yanajirudia. Licha ya kujaza claim kila mwezi lakini bado malipo hayafanyiki,yaani mtu anajaza claim analipwa baada ya miezi 6 au 7 bila sababu yoyote.

Hapa ninaandika leo ni mwezi wa 9 lakini kuna waalimu hawajalipwa tangu mwezi wa 3. Hii ni sawa? Kila siku wanaambiwa malipo yanashughulikiwa, hivi kweli nini kinashughulikiwa tangu mwezi wa 3?

Wakati huohuo external examiners wakija wanalipwa ndani ya wiki moja. Hivi mnadhani hii hali waalimu wanaifurahia? Wafanyakazi wengine wote claims zao zinalipwa bila shida yoyote ndani ya muda mfupi.

Kwanini ubabaishaji hauishi licha ya malalamiko ya kila siku? Hamuitambui kazi inayofanyika kwa wanafunzi? Au mnataka waalimu wakale kwa wanafunzi?

Tunaamini wewe mkuu wa chuo ni mtu msikivu licha ya kutokua msikivu mara zote huko nyuma,bado tunaamini utarekebisha kasoro na kuwawajibisha watendaji wako wanaokuhujumu na tunaomba waalimu ambao hawajalipwa tangu mwanzo wa semester mwezi March walipwe na ubabaishaji usiwepo tena.
 
Mkuu wa Chuo cha DIT na huku kwenye Jukwa wapi na wapi! Si umeandikie yeye au uende ukamuone ofisini kwake ili mvue gloves na kuzichapa kavu kavu?
 
Serikali inapuuza kutoa ajira hasa baada ya kupunguza watu kipindi cha magu, wanaishia kutoa ajira za polisi ili wajihakikishie ulinzi wao waendelee kukumbatia madaraka......haingii akilini hamuwezi kuajiri watu, wanaojitolea mnawazungusha kuwalipa posho zao.....mambo kama haya hayawezi kuvumilika.
 
Hapa nawaza jinsi serkal inavyochezea elimu

Elimu n suala nyeti Sana mwlimu Kama huyu anaweza kupata vishawish kuvujisha mitihan ili apate kujikimu

Pole Sana mwalimu imewah nitokea hii miaka fulan napiga temple vyuo vya mafunzo ya uvuvi FETA

Nusu nivujishe paper kwa kukosa pesa
 
Wao wanalipana kila siku posho kwa mafungu ya ndani, external examiners wakija wiki hiyohiyo wanalipwa. Na hii ndio inaumiza zaidi
Mafungu ya ndani nafikiri una maana ya lile fungu wanalopenda kuliita 'Own Source' kama ni hivyo hilo fungu linalipa baadhi ya madai siyo madai yote.
 
Back
Top Bottom