Mkuu wa mkoa kuwaamuru Jamii moja kuondoka mkoani haijakaa sawa

Mkuu wa mkoa kuwaamuru Jamii moja kuondoka mkoani haijakaa sawa

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Leo asubuhi kwenye taarifa nimesikia ya kuwa Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Talak amewapa siku mbili Wafugaji walioingia mkoani hapo kuondoka.

Kwa upande wangu sioni kama hii imekaa sawa, anachopaswa kujiuliza Kiongozi huyu ambaye ni Muwakilishi wa Raisi wa nchi hapo Mkoani kwake ni "waende wapi ambako ndiko wanahitaji hilo tatizo analoona wamepeleka hapo Mkoani kwake?".

Kama ambavyo ni wajibu wa Raisi tuliyempa madaraka na usimamizi wa ardhi yetu basi na Wasaidizi wake Muwajibike kuangalia namna bora ya kuwafanya Wananchi wote bila kubagua Jamii yoyote wanaishi na kuifurahia ardhi yao.

Sikatai kwamba ujio au uwepo wao unaleta adha kwa wengine haswa wale wanaojishughulisha na Kilimo lakini hilo haliondoi ukweli kuwa bado ni wajibu wa mamlaka kuangalia watu wanaelimika na kufuata taratibu za nchi na si kufukuziwa kwingine.

Kwa hiyo mnawafukuza Watu wa nchi yako ile ile waende sehemu nyingine ndani ya nchi ile ile? hivi kesho na kesho kutwa mkikosa Nyama ndio mtawaita tena?.

Labda tu kama taarifa niliyoisikia ni kwa kifupi sana lakini ni aibu kwa taifa kuwa na viongoi wanaokimbia wajibu wao kwa kutoa tu amri za kutumia nguvu ili tu tatizo lihamie kwa wengine, na vipi kama huko mnapowafukuzia nako watafukuzwa?.

Ifike mahali kama Kiongozi unadhani jambo linakuzidi nguvu basi unyooshe tu mikono juu na kuwaachia waoweza.
 
Naona kalewa madaraka..hao wafugaji waende wapi??wakati mkonwa lindi robo tatu ni mapori yasiyo na kazi..hizo ng'ombe wanazipenda tu zikiwa buchani na kwenye mabakuli yao wakila nyama na supu.

Wafugaji wa nchi hii wanaonewa sawa ndani ya nchi yao.

#MaendeleoHayanaChama
 
Hivi kwa nini wafungaji wasiwe wananunua maeneo yao wenyewe ya kuchungia kama mkulima anavyofanya..
Maana wao kazi ni kupeleka kwenye maeneo ya wezao wakati ,kila mtu ardhi kanunua hajapata bure.
Wanatakiwa wawajibike na kazi zao,hapo ndo watapata mapato makubwa kwenye mazao yao.
Tusiendelee kuendekeza huu ujinga.
 
Naona kalewa madaraka..hao wafugaji waende wapi??wakati mkonwa lindi robo tatu ni mapori yasiyo na kazi..hizo ng'ombe wanazipenda tu zikiwa buchani na kwenye mabakuli yao wakila nyama na supu.

Wafugaji wa nchi hii wanaonewa sawa ndani ya nchi yao.

#MaendeleoHayanaChama
Hapo ndio tatizo linapoanzia mapori yasio na kazi wakati ni maeneo ya watu uingize tu mifugo bila ruhusa ya muhusika
 
Hayo mawazo ya kijamaa ,kwa nini wasinunue tu hata ekari mia wafuge wao wenyewe mpaka wakachukue maeneo ya wengine..
Wauze ngombe wanunue ardhi .sio kuinhia maeneo ya watu.
Ng'ombe zaidi ya maelfu utawafuga eneo la heka 100.

Hapo bado maji malisho wakati wa kiangazi..sio mchezo.

Mimi nashauri mkoa wa lindi uwe mkoa wa wafugaji.

#MaendeleoHayanaChama
 
Mkoa wa lindi kuna maeneo ni mapoli wala hayana mwenyewe hayalimwi yapo tu.

#MaendeleoHayanaChama
Hawa walisha pewa maeneo huko kilwa, sasa kule Nachimgwea wanako uwa wenyeji, kwa kugombea kulisha mifugo mashamba ya watu, wanastahili kuindolewa.

Nachimgwea Rwangwa ndizo zinazolisha Lindi na Mtwara, ukihamishia wafugaji umewauwa.
 
Sasa kama nimuunganiko wawafugaji wengi wanashindwa kwel hata ,kila mmoja akinunua alfu wakashare.hata ekari 5000 hadi 10000 wanaweza .
Wanatakiwa wakatazwe kabisa kupeleka maeneo ambayo siyo yao.wabebe mzigo wao wauze nusu ya ngombe zao wanunue ardhi si watazaana tena..
Hiyo njia ufugaji wa kutembea na ngombe ni wakijima sana.wao utapanuka na kukua sana ..maana zitakuwa kama private ranch.
Watabaki kuwa masikini wakisipo badilika.
Ng'ombe zaidi ya maelfu utawafuga eneo la heka 100.

Hapo bado maji malisho wakati wa kiangazi..sio mchezo.

Mimi nashauri mkoa wa lindi uwe mkoa wa wafugaji.

#MaendeleoHayanaChama
 
Hawa walisha pewa maeneo huko kilwa, sasa kule Nachimgwea wanako uwa wenyeji, kwa kugombea kulisha mifugo mashamba ya watu, wanastahili kuindolewa.

Nachimgwea Rwangwa ndizo zinazolisha Lindi na Mtwara, ukihamishia wafugaji umewauwa.
Wafugaji wa nchi hii hawana amani ndani ya nchi yao kila mahala wanafukuzwa.

#MaendeleoHayanaChama
 
Rais kasema kuzunguka kwa mifugo kusimamishwe maana kunasababisha fujo na mapigano
Maisha ya wafugaji ndivyo yalivyo huwezi kaa sehemu moja una ngombe wengi..sa100 hakuji hata kufuga kuku atajuaje kuhusu mifugo kama ng'ombe na mbuzi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Leo asubuhi kwenye taarifa nimesikia ya kuwa Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Talak amewapa siku mbili Wafugaji walioingia mkoani hapo kuondoka.

Kwa upande wangu sioni kama hii imekaa sawa, anachopaswa kujiuliza Kiongozi huyu ambaye ni Muwakilishi wa Raisi wa nchi hapo Mkoani kwake ni "waende wapi ambako ndiko wanahitaji hilo tatizo analoona wamepeleka hapo Mkoani kwake?".

Kama ambavyo ni wajibu wa Raisi tuliyempa madaraka na usimamizi wa ardhi yetu basi na Wasaidizi wake Muwajibike kuangalia namna bora ya kuwafanya Wananchi wote bila kubagua Jamii yoyote wanaishi na kuifurahia ardhi yao.

Sikatai kwamba ujio au uwepo wao unaleta adha kwa wengine haswa wale wanaojishughulisha na Kilimo lakini hilo haliondoi ukweli kuwa bado ni wajibu wa mamlaka kuangalia watu wanaelimika na kufuata taratibu za nchi na si kufukuziwa kwingine.

Kwa hiyo mnawafukuza Watu wa nchi yako ile ile waende sehemu nyingine ndani ya nchi ile ile? hivi kesho na kesho kutwa mkikosa Nyama ndio mtawaita tena?.

Labda tu kama taarifa niliyoisikia ni kwa kifupi sana lakini ni aibu kwa taifa kuwa na viongoi wanaokimbia wajibu wao kwa kutoa tu amri za kutumia nguvu ili tu tatizo lihamie kwa wengine, na vipi kama huko mnapowafukuzia nako watafukuzwa?.

Ifike mahali kama Kiongozi unadhani jambo linakuzidi nguvu basi unyooshe tu mikono juu na kuwaachia waoweza.
Ahsante kwa kutujuza, lakini habari ngumu kama hizi ni bora zikawa na maelezo ya kutosha na sio kurukia rukia tu.
Wafugaji wa lindi eneo gani walioambiwa watoke? Au lindi yote?

Kwa sababu zipi?!!! Au hakuna sababu amekurupuka tu mkuu wa mkoa?!!

Uamuzi huo umechukuliwa baada ya muda gani wa kuisikilizia amri (km ipo) iliyotolewa na setikali?!!! Au hakukuwa na vikao na makubaliano ya kabla ambayo pengine yamekuwa violated ndo maana imekuja amri hii?!!!!

N.k
 
Ifikie wakati haya makabila mawili ya Wasukuma na Wamasai yabadilishe mifumo yao ya ufugaji! Nomadic livestock kwenye karne hii ya 21 ni upuuzi.

Aina hii ya ufugaji inasababisha uharibifu mkubwa wa mazingira, ukame, na pia migogoro ya ardhi. Watafute maeneo, watulie! Waanzishe ufugaji wa kisasa.
 
Hii awamu ipite tu haraka na mambo yake.

Kila siku drama tu kama watoto wadogo vile.

Hakuna maamuzi yanayofanyika kwa kuangalia mapana yake.
 
Sasa mtu unafuga ng'ombe 500 wa nini
Wafugaji wafunge mifugo kiasi ikikomaa anakuwa anavuna anapata pesa
Kuzurula na mifugo karne hii haiko sawa
Wapewe mafunzo na mbegu bora wafuge kisasa
Ukiwa na ng'ombe 10 tu wa kisasa unakuwa tajiri tu bila hii migogoro
 
Back
Top Bottom