Leonel Ateba Mbinda
JF-Expert Member
- Feb 20, 2023
- 644
- 2,695
Umeongea kwa mamlaka dhidi ya wafanyabiashara, na umenikuna sana kiongozi. Umeonyesha ujasiri mkubwa kwa wananchi unaowaongoza Dar es Salaam. Umenigusa sana pale uliposema kama nchi inapeleka jeshi kupigana Congo, vipi ishindwe kulinda Kariakoo.
Dawa yao hao wafanyabiashara wanaotumwa na wanasiasa na kudhani wanamkomoa Rais ni kuhakikisha waliofunga maduka leo wasiyafungue hadi madai yao yatakaposikilizwa ili tuone wanamkomoa nani.
Ulinifurahisha zaidi uliposema serikali haishindwi jambo. Naamu, kabisa kabisa! Yaani wafanyabiashara muishinde serikali? Nyie wafanyabiashara Kariakoo mnaona serikali ni jambo dogo sana?
Halafu, najiuliza kwa nini ujinga huu hawakumletea Hayati Magufuli?
Nani yuko nyuma yao? Hivi mnataka Rais aweke pembeni 4R turudi enzi za Magufuli?
Kuna watu wanasubiri tu mama aweke pembeni 4R ili turudi tulikotoka maana mnafanya mchezo sana nyie wafanyabiashara.
Ni kweli RC Chalamila, wafanyabiashara wa Kariakoo wakwepa kodi wamekithiri, hawataki kukaguliwa. Serikali ikiamua kufanya uchunguzi, watakaobaki salama hawazidi 20 pale Kariakoo.
Kuna uhujumu uchumi mkubwa unafanywa na wafanyabiashara pale Kariakoo. Mfano mzuri, wanaotoa risiti pale Kariakoo hawazidi hata 100 kati ya watu milioni 3 wanaokwenda kupata mahitaji. Serikali inawavumilia sana, lakini leo mnataka kuichezea sharubu.
RC Chalamila, hotuba zako ni za kimamlaka, na hao waliogoma wanataka kuhatarisha usalama wa mkoa.
Ushauri kwa vyombo vya usalama: fuatilieni kwa kina mambo haya ya migomo pale Kariakoo. Nani anaanzisha movement hizi?
Anzeni na wale waliokuwa wakitoa kero kwa DC juzi, wale ndio wa kuanza nao. Wale mkiwapa kesi za uhujumu uchumi, hamtasikia tena upumbavu wa namna hii.
Asante, Mkuu wa Mkoa.
PIA SOMA
- Mgomo wa Wafanyabiashara ambapo Biashara zilifungwa Kariakoo leo Juni 24, 2024.
- Chalamila kuwasili Kariakoo katika jitihada za kutatua mgogoro
- Baada ya Chalamila kuondoka Kariakoo, bado Wafanyabishara waliendeleza mgomo wa kufunga maduka.
Dawa yao hao wafanyabiashara wanaotumwa na wanasiasa na kudhani wanamkomoa Rais ni kuhakikisha waliofunga maduka leo wasiyafungue hadi madai yao yatakaposikilizwa ili tuone wanamkomoa nani.
Ulinifurahisha zaidi uliposema serikali haishindwi jambo. Naamu, kabisa kabisa! Yaani wafanyabiashara muishinde serikali? Nyie wafanyabiashara Kariakoo mnaona serikali ni jambo dogo sana?
Halafu, najiuliza kwa nini ujinga huu hawakumletea Hayati Magufuli?
Nani yuko nyuma yao? Hivi mnataka Rais aweke pembeni 4R turudi enzi za Magufuli?
Kuna watu wanasubiri tu mama aweke pembeni 4R ili turudi tulikotoka maana mnafanya mchezo sana nyie wafanyabiashara.
Ni kweli RC Chalamila, wafanyabiashara wa Kariakoo wakwepa kodi wamekithiri, hawataki kukaguliwa. Serikali ikiamua kufanya uchunguzi, watakaobaki salama hawazidi 20 pale Kariakoo.
Kuna uhujumu uchumi mkubwa unafanywa na wafanyabiashara pale Kariakoo. Mfano mzuri, wanaotoa risiti pale Kariakoo hawazidi hata 100 kati ya watu milioni 3 wanaokwenda kupata mahitaji. Serikali inawavumilia sana, lakini leo mnataka kuichezea sharubu.
RC Chalamila, hotuba zako ni za kimamlaka, na hao waliogoma wanataka kuhatarisha usalama wa mkoa.
Ushauri kwa vyombo vya usalama: fuatilieni kwa kina mambo haya ya migomo pale Kariakoo. Nani anaanzisha movement hizi?
Anzeni na wale waliokuwa wakitoa kero kwa DC juzi, wale ndio wa kuanza nao. Wale mkiwapa kesi za uhujumu uchumi, hamtasikia tena upumbavu wa namna hii.
Asante, Mkuu wa Mkoa.
PIA SOMA
- Mgomo wa Wafanyabiashara ambapo Biashara zilifungwa Kariakoo leo Juni 24, 2024.
- Chalamila kuwasili Kariakoo katika jitihada za kutatua mgogoro
- Baada ya Chalamila kuondoka Kariakoo, bado Wafanyabishara waliendeleza mgomo wa kufunga maduka.