Mkuu wa Wilaya Monduli, Frank Mwaisumbe aliyepopolewa Mawe na wananchi afunguka, ampiga chini Mwenyekiti wa kijiji

Kamata hao wahalifu wakatiwe adabu kuchekea upuuzi kama huu haikubaliki..

Polisi wawasake wote waliohusika.
Kwa mwendo huu ongezeni kasi ya kujenga mahabusu, magereza na bajeti ya kuwalisha wa tz.

Huishi huko, huwezi hukumu kwa stori ya mtu mmoja

Kama wazili alibebewa bango akatoa ufafanuzi, yawezekana tatizo sio wanainchi

Utambue hata viongozi hukosea
 
Mkuu wa wilaya ana mamlaka ya kumsimamisha kazi mwenyekiti wa kijiji?
Hana kwani mwenyekiti wa Kijiji kachaguliwa na wananchi hivyo ni mkutano mkuu wa Kijiji tuu ndiyo wenye uwezo wa kuazimia kwamba hawamtaki na sababu za kumkataa.
 
Hii hatari sana, mwenyekiti amechaguliwa na wananchi, mkuu wa wilaya ni mteule wa rais kuna shida sehemu
Labda Atakuwa amemsimamisha kuhudumu masuala ya ulinzi na usalama nje kijiji chake! Maana DC ndiye mwenye zamana wa jambo hilo wilayani.
 
Walikupiga mawe baada ya kuona unamtetea mwenyekiti wa wilaya.

Alafu baada ya kupigwa mawe ukaja kumsimamisha mwenyekiti wa kijiji.

======

Kuna kitu hakiko sawa mahali.
 
Wananchi sio wapumbavu, kuna kitu hakijaenda sawa inavyotakiwa na bado mtakula sana mawe.
 
Kuna imbalance mahali hapo wakubwa wamchunguze mkubwa kwanza
 
Hii hatari sana, mwenyekiti amechaguliwa na wananchi, mkuu wa wilaya ni mteule wa rais kuna shida sehemu
Na mimi nimejiuliza hiyo power ya kutengua mwakilishi wa wananchi kaitoa wapi? Labda atakuwa Mtendaji wa Kijijiji na siyo Mwenyekiti wa kijiji!

La sivyo kuna mahali pana loophole kubwa sana kwenye uongozi wa nchi!!
 
Habari inatoka upande mmoja tu wa huyo DC
Huyo mwenyekiti wa kijiji na wananchi hakuna maoni kutoka kwao
 
Mkuu wa wilaya ana mamlaka ya kumsimamisha kazi mwenyekiti wa kijiji?

Hana mamlaka hayo , Huyo DC itakuwa hajitambui na haelewi mipaka yao.
Ndio tabu ya kuteua hovyohovyo unapata maviongozi ya hovyo kama hilo li Dc, ni lipumbavu sana
 
Ni wazi Dc anashida apa afu kama anatumia nguvu nyingi kumkandamiza mwenyekiti wa kijiji
Mwenyekiti anakulaje 150m z ujenzi wa madarasa[emoji23][emoji23][emoji23] huu ni uongo mkubwa bora angetwambia Ded wake kala
 
Yaani wamasai wa siku hizi wamechakachuliwa kabisaaa.... Haiwezekani Mmasai kukosa shabaha hadi mawe yamkose mkuu wa wilaya
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hana mamlaka hayo , Huyo DC itakuwa hajitambui na haelewi mipaka yao.
Ndio tabu ya kuteua hovyohovyo unapata maviongozi ya hovyo kama hilo li Dc, ni lipumbavu sana
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hii habari ina walakini,kama chanzo cha yeye kuchukiwa na wananchi ni kuhisiwa kwamba anamtetea mwekezaji bwana Paulo Narida,iweje tena mtu huyo aungane na wagomvi wake ambao ni wananchi kumpopoa mawe?

Yaani watu waliokata mabomba kwenye mashamba yake ndio hao ashirikiane nao pamoja na mwenyekiti kufanya vurugu? Sasa watakuwa wanataka nini hasa?
 
Wenyeviti walipitishwa kimabavu na wabunge,wapambane na hali zao
 
Halafu hii hoja ya maswala ya mapato na matumizi ya kijiji yameletwa wakati tayari kuna mgogoro mkuu wa ardhi. Mgogoro wa ardhi uishe kwanza. Inakuwaje mkuu wa wilaya hajui maswala ya mgongano wa maslahi?
 
Kingine cha muhimu ni wananchi kama umma wanapaswa kusikilizwa dhidi ya mtu mmoja anayetumia nguvu ya pesa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…