Tetesi: Mkuu wa Wilaya Mpya wa Kisarawe ni "Mtoto" wa Rais Magufuli

Tetesi: Mkuu wa Wilaya Mpya wa Kisarawe ni "Mtoto" wa Rais Magufuli

Poor arguement. Conflict of interest haiangalii sifa ya mhusika huangalia tu mazingira yaani kuna mazingira ambayo yanaweza kuwa yametoa upendeleo kutokana na mhusika kuwa na maslahi na mhusika.

Sifa ulizozitaja inawezekana kweli anazo lakini je hizo sifa ni yeye tu aliye nazo? Hakuna wengine walio na sifa kama yeye au kumzidi. Ni nini kilichomtofautisha yeye na hao wengine? Kwa kuwa hatujui, ndiyo maana kimaadili haitarajiwi kumpa kitu chochote chenye manufaa mtu ambaye wewe una maslhai naye kwa kupitia nafasi uliyopewa na umma. Hapa uteuzi huu unafanana kabisa na angalizo alilolitoa Mwalimu kuhusiana na corruption. Mwalimu alisema, 'corruption ipo katika mataifa mengi lakini mbaya zaidi ipo Africa. Asia mtoto wa Rais au mjomba wake atapewa tenda ya kutengeneza barabara, na barabara itatengenezwa, tena kwa viwango sahihi. Corruption ya Africa, tenda ya barabara atapewa mtoto au mjomba wa Rais, hela italipwa na barabara hamtaiona, lakini zote ni corruption.' Kama huyu mteule ana uwezo na sifa, kazi itafanyika lakini haitafuta ukweli kuwa kuna ukosefu wa maadili.

First, I don't see any competing professional or personal interest that can make it difficult for Magufuli to fulfill his duties impartially. PERIOD. Pili, uhusiano wa JPM na Happy ni tetesi tu there is no factual or empirical evidences to support this claim. Baloney.
 
Isitoshe sio baba yake wa kumzaa shida iko wapi hapo?. Tatizo tunalolikataa wananchi ni kubeba mtu asiyebebeka...huyo dada anayo elimu nzuri tu...
Mkuu, kuwa na elimu pekee sio kigezo. Kinachotakiwa ni uwezo wa kufanya shughuri hiyo. Mbona Jerry Muro (msemaji MKUU wa klabu ya Yanga) ana elimu "nzuri!" lakini kila analolizungumza kwenye media ni kichefuchefu?
 
Unajua huyo Mwanasheria Mkuu wa Marekani anavyopatikana? Ukijua hutakuja kamwe na mfano huo.

Angalia sasa umehamisha goli. Marekani unauliza unajuwa taratibu za kumpata Mwanasheria Mkuu Marekani. Hili ni suala lingine fungua uzi mwingine tuongelee hili suala. Definition ya conflict of interest haibadiliki kwa Marekani. Marekani wana taratibu zao kutokana na mazingira yao nasi tuna taratibu zetu kutokana na mazingira yetu.

BTW, ukitaka kuongelea conflict of interest CHADEMA kuna case study nyingi sana, labda tuanzie huko
 
Happy amesoma na mdogo wangu wa kike UDOM....mimi huwa nadhani ni mwanae kabisa JPM,kumbe ni wa kumlea tu!!ana elimu nzuri japo sina hakika na uwezo wake wa kiungozi
Hapo (bolded) ndo pa kupaangalia mkuu, isiwe ni mtu wa kupewa maagizo tu.
 
Hongera sana kwa huyo mh. mkuu wa wilaya ya kisarawe ana juhudi sana na hakati tamaa mapema ndo maana alipokosa viti maalum bado alikuwa anapambana hvyo hvy

Nae Kippi Warioba mtasemaje nae kalelewa na Sinde Warioba na yeye sasa DC wa Moshi!!! Kama wanavigezo wateuliwe tu sio kama mkweree aliwateua ndugu zake wakina Maneno wa darasa la nne na kuwapa UDC kule Kigoma!!!
 
majungu tu,kosa likö wap kama vigezo anavyo?mnataka kusema ukizaliwa kwenye familia ya kiongozi au uwe na undugu nae basi usahau kupata cheo kwasababu itaonekana umependelewa?yaan kuwa na undugu na kiongozi isiwe tena ni furaha kwenye familia bali majanga?
 
Mara baada ya uteuzi wa wakuu wa Wilaya uliofanyika na kutangzwa leo, jamii imeanza kuwachambua na kujuwa historia zao na ushiriki wao katika kumasaidia kazi Mh Rais.

Wananchi wamekuwa na shauku ya kumfahamu na kuelewa historia ya Mkuu wao mpya wa Wilaya Mh. Happynes Senenda William. Kabla ya kuwa DC wa Kisarawe tunaambiwa dada huyu alikuwa Manager wa HR wa TANROADS Mkoa wa Tanga, ni mdada mdogo mwenye elimu ya Masters. Mwaka 2010 aligombea ubunge viti maalumu kupitia mkoa wa Geita lakini hakufanikiwa, mwaka 2015 alipumzika ili kuzunguka na baba kumtafutia kura

Habari zinazidi kupenyeza kuwa Mh.Happyness William ni mtoto wa kulelewa na Rais JPM, amesomeshwa na Rais na amekuwa akiishi na JPM kwa maisha yake mpaka alipopata kazi. Kifupi Mh.Happyness ni "mtoto" wa JPM na kwa sasa ni DC wa Kisarawe

Ama hakika huu ni msimu wa vijana...Vijana mjiibidishe ili muonekane na mpate Wilaya au Mkoa.


Hivi, mh. Mkapa alikulia kwa nani vile..
 
Mnashangaa nini hii ndiyo Tanzania, Ila kwa Afrika sitashangaa kabisa. Rais nanihii kamteu mwanaue kuwa Vice President, Museven kamteua mke kuwa --- , kamteua mtoto kuwa --- yaani ni mwendo wa ---- tu.
 
safi sana binti ulibebwa na ukabebeka, wangapi wa kusaidiwa wamefanya madudu kibao.. watu wamepoteza pesa zao..tena namjua mmoja wa kiume alisaidiwa coz mzazi wake hakuwa na uwezo.. form alipata division one ya point 10, form six division one ya point 7 kufika chuo starehe na mademu ndio mpango mzima, alikuja kudisco mwaka wa tatu semester ya mwisho... fungu la kukosa. nampongeza sana huyo dada...
 
Na pia kama Raisi Magufuli kulingana na maneno yako hana tofauti na Raisi Museveni pia hana tofauti na JF Kennedy Raisi wa 35 wa USA ambaye alimteua kaka yake Robert kuwa Mwanasheria Mkuu wa USA (Attorney General), hivyo usiishie kutoa mifano ya nchi masikini tu kutaka kuthibistiha unachokiamini tolea mifano pia na Wazungu wenu!
Akili zingine za ajabu sana, wewe unadhani mfumo wa US ni kama huu wenu ambao bwana mkubwa hata amteue chizi hakuna wa kuhoji bali ni kupiga makofi na kushangilia kama mfanyavyo hapa?
Wenzetu nafasi hizo Rais anateua lakini kuna vyombo kama sikosei seneti anaenda kuhojiwa na kuidhinishwa au kukataliwa. Kwa hiyo huyo Kennedy kama uteuzi wake ulipita basi hao wengi waliomhoji waliona anafaa.
Huku tunaweza kuona mzee akaamka asubuhi na kumuondoa Ndalichako na kumuweka mamaa Janet akisema ni mwalimu mzoefu ataiweza wizara hiyo na hakuna wa kuhoji nanyi vuvuzela mkaja hapa na nyimbo na mapambio kusifia uteuzi huo.
 
Mara baada ya uteuzi wa wakuu wa Wilaya uliofanyika na kutangzwa leo, jamii imeanza kuwachambua na kujuwa historia zao na ushiriki wao katika kumasaidia kazi Mh Rais.

Wananchi wamekuwa na shauku ya kumfahamu na kuelewa historia ya Mkuu wao mpya wa Wilaya Mh. Happynes Senenda William. Kabla ya kuwa DC wa Kisarawe tunaambiwa dada huyu alikuwa Manager wa HR wa TANROADS Mkoa wa Tanga, ni mdada mdogo mwenye elimu ya Masters. Mwaka 2010 aligombea ubunge viti maalumu kupitia mkoa wa Geita lakini hakufanikiwa, mwaka 2015 alipumzika ili kuzunguka na baba kumtafutia kura

Habari zinazidi kupenyeza kuwa Mh.Happyness William ni mtoto wa kulelewa na Rais JPM, amesomeshwa na Rais na amekuwa akiishi na JPM kwa maisha yake mpaka alipopata kazi. Kifupi Mh.Happyness ni "mtoto" wa JPM na kwa sasa ni DC wa Kisarawe

Ama hakika huu ni msimu wa vijana...Vijana mjiibidishe ili muonekane na mpate Wilaya au Mkoa.

generally speaking, na kama hii stori ya kweli, then kumteua huyu linaweza lisiwe ni tatizo.

tatizo liko hapa....

1. ni JPM - ambaye kwa mtizamo uliopo sasa hapaswi kuwa linked na any wrongdoing, aka "above reproach"
2. na kwa uzito uleule wa (1) hapo juu, kutoku-declare hiyo "interest" kabla ya uteuzi
 
Akili zingine za ajabu sana, wewe unadhani mfumo wa US ni kama huu wenu ambao bwana mkubwa hata amteue chizi hakuna wa kuhoji bali ni kupiga makofi na kushangilia kama mfanyavyo hapa?
Wenzetu nafasi hizo Rais anateua lakini kuna vyombo kama sikosei seneti anaenda kuhojiwa na kuidhinishwa au kukataliwa. Kwa hiyo huyo Kennedy kama uteuzi wake ulipita basi hao wengi waliomhoji waliona anafaa.
Huku tunaweza kuona mzee akaamka asubuhi na kumuondoa Ndalichako na kumuweka mamaa Janet akisema ni mwalimu mzoefu ataiweza wizara hiyo na hakuna wa kuhoji nanyi vuvuzela mkaja hapa na nyimbo na mapambio kusifia uteuzi huo.


Blah blah blah blah! Akifanya Mzungu ni sawa na unatafuta sababu za kuhalalisha kwamba inakubalika, ila jambo hilo hilo likifanywa na Mwafrika siyo sawa!
Amka kijana nepotism ni nepotism tu na haijalishi inafanywa na nani, na ndiyo maana kuna hili neno nepotism kwa Wazungu na kwetu Waafrika vile vile!

Haya Kiongozi Mkuu wa Singapore Kuan Lee Yew alimuachia mtoto Uongozi ambaye mpka leo ndiyo Kiongozi Mkuu wa nchi tajiri ya Singapore, hapo napo utatetea vipi?
 
Kwahio kama amemlea na anazo sifa za kuteuliwa basi aachwe?
Sasa anyamaze kutukana wenziwe na kujifanya ni msafi hiyo si conflict of interest anavyochonga sana kujidai watu wanajaza ndugu kumbe na yeye ni wale wale waafrika bwana ndivyo tulivyo
 
Blah blah blah blah! Akifanya Mzungu ni sawa na unatafuta sababu za kuhalalisha kwamba inakubalika, ila jambo hilo hilo likifanywa na Mwafrika siyo sawa!
Amka kijana nepotism ni nepotism tu na haijalishi inafanywa na nani, na ndiyo maana kuna hili neno nepotism kwa Wazungu na kwetu Waafrika vile vile!
Haya Kiongozi Mkuu wa Singapore Kuan Lee Yew alimuachia mtoto Uongozi ambaye mpka leo ndiyo Kiongozi Mkuu wa nchi tajiri ya Singapore, hapo napo utatete vipi?
Hakuna cha Mzungu wala nani msipotoshe hapa. Wenzetu hata Kenya katiba yao ishaachana na mambo hayo ya utawala wa kijima na sasa nafasi nyingi Rais akiteua lazima bunge limjadili na kumpitisha aliyeteuliwa.
Hayo mambo ya Kimuseveni yashapitwa na wakati
 
Hii ni dalili mbaya sana ufalme unarejea polepole ngoja tusubiri huyu naona anaweza hata kug'ang'ania hapo..
 
Hata nabii musa as alimpigia pande nguguye haruni as Ili naye awe nabii.
Nalog off
 
Ndio, kwani uteuzi unapata uwanja mpana. Na kama mtu hastahili hapitishwi hata kama kalelewa na nani?


Ingekuwa hivyo unavyosema ni kweli basi leo Kenya kusingekuwa na crisis, kuna ishu kubwa kwamba watu wanapendelewa kwenye uongozi!
 
Usikurupuke, amemwelezea vema kuhusu alipotokea hadi alipo na akahitmisha kwa kuwapa changamoto vjana.
 
Back
Top Bottom