Heshima kwenu wakuu,
Nimekua shahidi wa michango mizuri humu inavyo fika sehemu husika na kusaidia watu mbalimbali.
Niende moja kwa moja kwenye mada.
Nina mzee wangu amestaafu kazi serikalini Takribani Miaka kadhaa iliyopita
(Zaidi ya kumi)
Alikua Mkuu wa Wilaya (Wilaya tofauti tofauti kwa Takribani Miaka 16)
Kisha wizara ya Maendeleo ya Jamii hadi kustaafu kwa mujibu wa sheria.
Kinachosikitisha Ni Mafao kiduchu aliyolipwa (Tsh Milion mbili tu)
Baada ya kufatilia sana ilifika akaambiwa ajisaidie ili asaidiwe (yani ili asaidiwe akubali kugawana Mafao yake na hao watakao msaidia)
Kilichofanya nilete jukwaani hapa ni michango yenu na ushauri wenu ili kilio chake kiweze fika mahala husika
Ikiwezekana kuonana na Mhe Rais ,
Kwani amekua akisumbuka kwa zaidi ya Miaka 10 kufatilia bila mafanikio na kwasasa Ni mgonjwa anaelekea kupata ganzi mwilini bila kupata haki zake.
Amekua mtiifu nakusumbuka bila mafanikio.
Documents zote Original anazo endapo zitahitajika mahala husika.
Na kwasasa yupo Temeke anapoishi.
NB ;amepita ngazi husika kwa zaidi ya Miaka 10 bila mafanikio.
Natanguliza Shukrani.
Sent using
Jamii Forums mobile app