TANZIA Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Wakili Avod Mmanda afariki Dunia. Atazikwa Mtwara na Serikali na wahudhuriaji wasiozidi 10

TANZIA Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Wakili Avod Mmanda afariki Dunia. Atazikwa Mtwara na Serikali na wahudhuriaji wasiozidi 10

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
images (1).jpeg
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Advocate Evord Herman Mmanda, afariki Dunia alfajiri ya leo.

Aliwahi kulazwa Muhimbili miezi 4 iliyopita kwa presha akaruhusiwa.

Mauti imemkuta akiwa kalazwa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Mtwara Ligula, akisumbuliwa na maradhi ya Moyo.

002FE3AB-5616-4BA3-892E-F8F4037B2E8C.jpeg

Mmanda aliteuliwa kuwa mkuu wa Wilaya ya Mtwara na rais Magufuli 19 Dec 2016 akichukua nafasi ya Dkt. Khatib M Kazungu ambaye alihamishiwa Wizara ya Fedha.

Wakili Msomi Mmanda aliyekua pia mjumbe wa Bunge la Katiba. Katika Bunge hilo, aliteuliwa na MWENYEKITI wa Muda wa vikao vya Bunge Maalumu la Katiba, Pandu Ameir Kificho, kama mmoja ya wajumbe 20 Watakaomshauri ili kuboresha utendaji.

2015 alitangaza nia ya kugombea Ubunge jimbo la Rombo kupitia CCM.
1587974185555.png
Stay tuned...

UPDATE

SERIKALI KUSIMAMIA MAZISHI YAKE

“Tumekubaliana na familia kwamba sisi Serikali ndiyo tutakaosimamia mazishi yake…na hakutakuwa na kusafirisha mwili…atazikwa hapa Mtwara…na hatazikwa na zaidi ya watu kumi,” Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa akielezea taratibu za mazishi ya liyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Evod Mmanda aliyefariki dunia Aprili 26, 2020 katika Hospitali ya Rufaa Ligula alipokuwa akipatiwa matibabu.
 
Nilimuona juzi Kati kwenye luninga.
RIP wakili msomi
Nimekuwa perplexed huyu mtu nilimsikia wapi! Ulipoandika kuwa ni wakili, nikakumbuka alikuwa na vipindi kwenye TV vya sheria. Kumbe alishakuwa DC! Ni CCM kumbe, and if that is the case kama kawaida ya CCM amewaonea watu wengi! tangulia kwenye hukumu ya haki! Huko kila mmoja atabeba mzigo wake bila Jiwe!
 
Eti bila jiwe. Daah. Ila jiwe katuweza sana. Hana plan yoyote na anapenda kujitange sana .wanadai chato kuna ventilator imetoka Mwanza/ bugando
Yaani jamaa kwa plan zinazomuhusu yeye yuko vema sana

Nimekuwa perplexed huyu mtu nilimsikia wapi! Ulipoandika kuwa ni wakili, nikakumbuka alikuwa na vipindi kwenye TV vya sheria. Kumbe alishakuwa DC! Ni CCM kumbe, and if that is the case kama kawaida ya CCM amewaonea watu wengi! tangulia kwenye hukumu ya haki! Huko kila mmoja atabeba mzigo wake bila Jiwe!
 
Back
Top Bottom