Mkwezi tungi kalitia maji lakini kaachwa

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Kaja mpitanjia kafanya kama mkwezi kaliwa kichwa..! Maisha bila connection usijiamini sana.. Ama inategemea connection yako ina nguvu kiasi gani.

Mdomo koma! Tumefunzwa kukaa kimya ama kufungua kinywa kwa tahadhari kubwa..! Maneno ni ni kama risasi.. Hakuna rivasi Umemaliza weekend salama unajiandaa kesho ukaendee na majukumu yako.. Mara paap! Unaropoka ya kuropoka.. Chaap kwa haraka kabisa unaliwa kichwa.

Mojawapo ya waraka wa ufumbuzi mfupi kuliko yote! Huyu sidhani kama watamuacha salama.. Katika nyakati hizi halafu mtu anatoa boko kama lile..😂 shetani akikukataa utaongea yote na bila kujua kama yalikutokaje!

Zamani tukisikia kuna mchawi anakaribia kukata moto tulikuwa tunawahi eneo la tukio kupata uhondo..maana mchawi hakati roho mpaka aongee maovu yake yote

Aliroga wangapi
Majina yao ni nani
Aliuwa wangapi na majina yao ni akina nani nknk

Chama chawala kiko mahututi hizi kauli za makada wake kuhusu maovu waliyowahi kufanya kwenye chaguzi mbalimbali ni sawa na mchawi anayekaribia kukata moto

Huu ni mwanzo tuu bado hawajasema wote.. Hawajasema yote..!

Alamsiki Tanganyika!
 
Kwani alisemaje
 
Dalili za mwisho kabisa kukaribia kwenye 'Kuanguka kwa Mnara wa Babeli.'
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…