Mlio jirani na Rais mshaurini; ni sawa kutoa zawadi lakini kutapanya pesa nyingi kiasi hiki hapana!

Mlio jirani na Rais mshaurini; ni sawa kutoa zawadi lakini kutapanya pesa nyingi kiasi hiki hapana!

Juzi hapo eti Rais akitoa mil. 500 Kwa Taifa Stars kuingia Afcon, Leo tena eti anatoa mil. 92 Kwa Ndondo Cup.

Hata Kama ni Kuunga mkono Michezo,kutapanya pesa za Walipakodi Kwa wingi huu Haikubaliki.

Matokeo yake badala ya watu kufurahia inatuma ujumbe wa Moja kwa Moja kwamba anatumia pesa za Umma vibaya.

Kwa mda mfupi kutoa mil. 592 kwa Ajili ya zawadi sioni kama Ina Tija. Zawadi zitolewe ila sio Kwa wingi huu maana Kuna maelfu ya mahitaji ya watu.

Sijui washauri wa Rais wanafanya nini,kama ni mambo ya kutafuta uungwaji mkono Kisiasa ni mara mia akiwa kwenye ziara au kwenye makongamano huko watu wanakoelezea Changamoto zao akawapa hizo hela itamsaidia kuliko hii ya sasa.

Mfano uko ziarani Wananchi wamechangia majengo Yao Nguvu ikaisha hapo ndio ukichangia hata mil.100 watafutahi Kwa kutatua shida Yao.Binafsi sijafurahishwa na hili kabisa it is too much.

---
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ametimiza ahadi yake ya kuiunga mkono Ndondo Cup kwa kuchangia Tsh. mil Tsh. 92 milioni kwa Washindi wa Ligi hiyo.

Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa leo katika Studio za @CloudsFMTZ Mikocheni amekabidhi zawadi kwa Washindi wa Ndondo Cup ambapo mgawanyiko wa zawadi kwa Timu zilizoshiriki Ndondo Cup 2023 msimu huu kuanzia hatua ya makundi jumla yake ni Tsh. 92 milioni.

Msigwa amekabidhi fedha hizo kwenye kipindi cha #SportsXra kwa niaba ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Ndondo Cup ni Mashindano ya mpira wa miguu yaliyoasisiwa na Clouds Media Group chini ya Mtangazaji Shaffih Dauda ambayo hufanyika kila mwaka na kuvipa nafasi vipaji vya Wakali wa soka kuanzia ngazi ya mtaa.



View: https://www.instagram.com/p/CxJT8G2RJ5X/?igshid=MTc4MmM1YmI2Ng==

Jambo nzuri sana mm kama aongeze pesa kwenye budget ya michezo angalau huko kunaoneka impact yake kwa urahisi..
Viwanja vya michezo viboreshwe wavutie wawekezaji wengi kwenye michezo..
Itasaidia kutangaza nchi sana..
 
Hii ndio point. Rais hawezi kuamka tu na kusema ananunua kila goli million kadhaa au anatoa kiasi kadhaa kwa watu fulani.

Unless hizo hela ziwe anatoa kwenye mshahara wake. Watu wanalia na ugumu wa maisha lakini vitendo vinavyofanywa na watawala ni vyakinyama kabisa.

Wizara ya Michezo haikuwa na budget kwaajili ya timu ya taifa?
Ofisi ya Rais Hadi DC Huwa Ina pesa za mambo hayo ila Sasa kuwe na regulations isiwe kadiri tuu Kiongozi anavyojiskia
 
Kuna Clip moja nilimsikia late Magufuri akisema" Laiti Samia asingekuwa mwanamke basi Makamo wake angekuwa Husein Mwinyi" sasa hivi tusingekuwa na haya mashaka.
Hata huyo Magufuli nae alikuwa anatapanya sana pesa Kwa kugawa hovyo Kwenye ziara zake kutafuta umaarufu.
 
Hii ndio point. Rais hawezi kuamka tu na kusema ananunua kila goli million kadhaa au anatoa kiasi kadhaa kwa watu fulani.

Unless hizo hela ziwe anatoa kwenye mshahara wake. Watu wanalia na ugumu wa maisha lakini vitendo vinavyofanywa na watawala ni vyakinyama kabisa.

Wizara ya Michezo haikuwa na budget kwaajili ya timu ya taifa?
Kuna fedha za mfuko wa rais, hizo hata CAG haruhusiwi kuzikagua. Hizo ndio fedha zinazotumika kufanya chochote atakacho rais ili kujibrand, ikiwemo vikundi vya kumpamba, na hata ikibidi kuwa na kundi la watu wasiojulikana. Lengo la fedha hizi ni kumtakatisha rais hata awe anachemsha vipi.

Mara nyingi sheria ya fedha za aina hii hupendekezwa na kupitishwa na washauri wa serikali zilizopoteza ushawishi kwa umma.
 
Jambo nzuri sana mm kama aongeze pesa kwenye budget ya michezo angalau huko kunaoneka impact yake kwa urahisi..
Viwanja vya michezo viboreshwe wavutie wawekezaji wengi kwenye michezo..
Itasaidia kutangaza nchi sana..
Sasa Bajeti ya michezo iongezwe kwenye Wizara sio kutoa toa hela bila utaratibu
 
Kuna fedha za mfuko wa rais, hizo hata CAG haruhusiwi kuzikagua. Hizo ndio fedha zinazotumika kufanya chochote atakacho rais ili kujibrand, ikiwemo vikundi vya kumpamba, na hata ikibidi kuwa na kundi la watu wasiojulikana. Lengo la fedha hizi ni kumtakatisha rais hata awe anachemsha vipi.

Mara nyingi sheria ya fedha za aina hii hupendekezwa na kupitishwa na washauri wa serikali zilizopoteza ushawishi kwa umma.
Hela zote ziwe na utaratibu wa matumizi hata kama CAG haruhusiwi kukagua.

CAG mwenyewe anazifikia taasisi chini ya 40%
 
Ofisi ya Rais Hadi DC Huwa Ina pesa za mambo hayo ila Sasa kuwe na regulations isiwe kadiri tuu Kiongozi anavyojiskia
Haya ndio madhara ya kupoteza ushawishi kwa umma. Unafanya chochote ili kujustfy kuwa bado unakubalika na umma. Hii naifananisha na yule mwanaume anayehonga sana na kuishia kuchunwa ili kulazimisha penzi.
 
Haya ndio madhara ya kupoteza ushawishi kwa umma. Unafanya chochote ili kujustfy kuwa bado unakubalika na umma. Hii naifananisha na yule mwanaume anayehonga sana na kuishia kuchunwa ili kulazimisha penzi.
Hizo pesa zipo sio lazima kwamba zitumike ku justify kukubalika, viongozi mara nyingi wanaalikwa na taasisi mbalimbali hizo taasisi zinaomba michango , unadhani Kiongozi atatoa mfukoni mwake Kwa kipato binafsi ataweza?

Ndio maana unaona hata wabunge wamewekewa mfuko wa Jimbo kwa kazi hizo hizo ila walauo wao ziko regulated.
 
Kuna mtu ameomba historia ya kweli ya mtu mweusi hamjampatia mpaka sasa
 
Uchumi wetu umekuwa imara acha atapanye au kwakuwa haumo kwenye mgao??!!! Kila siku mnatuhubiria uchumi umeimaraka sasa kuna tatizo gani kutapanya hayo mamilioni?? Bado kuna mabilioni ya kufundisha wananchi katiba yapo njiani. CCM hoyeee!!
 
Kukuza mpira peleka pesa kwenye Taasisi husika / Grassroot ili wadau wajue wapi wazipeleke na wapi panahitaji; Hayo mengine kama ni zake binafsi hata akiamua azipeperushe watu waziokote ni sawa lakini kama ni hizi zetu (our hard earned cash) haitakiwi atumie hata senti tano bila consultation kutoka kwetu...;

Its not only about the Cash bali its a matter of Principle...
 
Juzi hapo eti Rais akitoa mil. 500 Kwa Taifa Stars kuingia Afcon, Leo tena eti anatoa mil. 92 Kwa Ndondo Cup.

Hata Kama ni Kuunga mkono Michezo,kutapanya pesa za Walipakodi Kwa wingi huu Haikubaliki.

Matokeo yake badala ya watu kufurahia inatuma ujumbe wa Moja kwa Moja kwamba anatumia pesa za Umma vibaya.

Kwa mda mfupi kutoa mil. 592 kwa Ajili ya zawadi sioni kama Ina Tija. Zawadi zitolewe ila sio Kwa wingi huu maana Kuna maelfu ya mahitaji ya watu.

Sijui washauri wa Rais wanafanya nini,kama ni mambo ya kutafuta uungwaji mkono Kisiasa ni mara mia akiwa kwenye ziara au kwenye makongamano huko watu wanakoelezea Changamoto zao akawapa hizo hela itamsaidia kuliko hii ya sasa.

Mfano uko ziarani Wananchi wamechangia majengo Yao Nguvu ikaisha hapo ndio ukichangia hata mil.100 watafutahi Kwa kutatua shida Yao.Binafsi sijafurahishwa na hili kabisa it is too much.

---
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ametimiza ahadi yake ya kuiunga mkono Ndondo Cup kwa kuchangia Tsh. mil Tsh. 92 milioni kwa Washindi wa Ligi hiyo.

Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa leo katika Studio za @CloudsFMTZ Mikocheni amekabidhi zawadi kwa Washindi wa Ndondo Cup ambapo mgawanyiko wa zawadi kwa Timu zilizoshiriki Ndondo Cup 2023 msimu huu kuanzia hatua ya makundi jumla yake ni Tsh. 92 milioni.

Msigwa amekabidhi fedha hizo kwenye kipindi cha #SportsXra kwa niaba ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Ndondo Cup ni Mashindano ya mpira wa miguu yaliyoasisiwa na Clouds Media Group chini ya Mtangazaji Shaffih Dauda ambayo hufanyika kila mwaka na kuvipa nafasi vipaji vya Wakali wa soka kuanzia ngazi ya mtaa.



View: https://www.instagram.com/p/CxJT8G2RJ5X/?igshid=MTc4MmM1YmI2Ng==


Ungejua zinazotoka bila taarifa, ungejikalia kimya.
 
Mh Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania amekuwa ndani ya utumishi wa umma kwa muda mrefu sana, amefanya kazi maeneo mbalimbali,amekuwa mbunge kwa miaka mingi, amekuwa waziri,Amekuwa makamu wa Rais na sasa Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania.Hivyo kipato chake cha halali tu kinachotokana na mishahara yake hawezi kushindwa kutoa kiasi hicho cha fedha. Kiasi hicho hakimshindi hata kidogo kutoa na kuchangia kwa ajili ya kuwapa hamasa wachezaji wetu.

Lakini pia hatoi tu katika michezo bali amekuwa akichangia katika maeneo mbalimbali na kwa watu mbalimbali,hivi majuzi majuzi tu tuliona akimjengea nyumba mtoto mmoja hivi na kumpatia Tabasamu na matumaini.Rais samia kiasili ni mtoaji kwa kile akipatacho.

Rais samia ni kiongozi na Rais wa wote,ndio maana ukienda katika kila eneo lazima uone alama zake,lazima ukute mafanikio yake ,lazima ukute Tabasamu na matumaini yanayotokana na mikono ya Rais samia.kila kitu kina nafasi yake na umuhimu wake. Leo hii nchi kama Uingereza au Spain inapata mapato makubwa sana kupitia michezo,imelitambulisha Taifa lake kupitia uwekezaji mkubwa katika michezo, na ina kusanya na kuboresha miundombinu yake kupitia mapato ya michezo.

Michezo itatupatia na kuitangaza nchi yetu,itatuletea wawekezaji wakubwa,itatuletea watalii,itazalisha ajira kwa vijana Embu fikiria mtu kama Sadio mane Namna alivyo saidia nchini kwake hasa kijijini kwake kwa kujenga vituo vya afya,angalia mtu kama christiano Ronaldo namna alivyotoa heshima nchi yake ,leo hii mpaka anasaidia waganga wa tetemeko kule Morocco,.amefika hapo alipo kwa kuwa Taifa lake lilimpa hamasa ya kukuza kipaji chake. Angalia watu kama akina David Beckam.

Tusimkatishe Tamaa mh Rais ,tumpe moyo na kumuunga mkono. Kwani akichangia katika michezo, kwamba vituo vya afya vimesimama kujengwa? Shule zimesimama kujengwa, barabara zimesimama kujengwa? Hivyo vyote si vinaendelea? Si vinafanyika? Unakumbuka nchi ya Rwanda iliyoa kias gani cha fedha kwa club kutoka Uingereza kwa ajili ya kutangaza nchi yao? Vipi ingekuwa kwetu? Si tungepigaa Makele? Tuacheni nongwa kwa mh Rais ndugu zangu. Katika hili sioni kosa la mh Rais wetu
 
Juzi hapo eti Rais akitoa mil. 500 Kwa Taifa Stars kuingia Afcon, Leo tena eti anatoa mil. 92 Kwa Ndondo Cup.

Hata Kama ni Kuunga mkono Michezo,kutapanya pesa za Walipakodi Kwa wingi huu Haikubaliki.

Matokeo yake badala ya watu kufurahia inatuma ujumbe wa Moja kwa Moja kwamba anatumia pesa za Umma vibaya.

Kwa mda mfupi kutoa mil. 592 kwa Ajili ya zawadi sioni kama Ina Tija. Zawadi zitolewe ila sio Kwa wingi huu maana Kuna maelfu ya mahitaji ya watu.

Sijui washauri wa Rais wanafanya nini,kama ni mambo ya kutafuta uungwaji mkono Kisiasa ni mara mia akiwa kwenye ziara au kwenye makongamano huko watu wanakoelezea Changamoto zao akawapa hizo hela itamsaidia kuliko hii ya sasa.

Mfano uko ziarani Wananchi wamechangia majengo Yao Nguvu ikaisha hapo ndio ukichangia hata mil.100 watafutahi Kwa kutatua shida Yao.Binafsi sijafurahishwa na hili kabisa it is too much.

---
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ametimiza ahadi yake ya kuiunga mkono Ndondo Cup kwa kuchangia Tsh. mil Tsh. 92 milioni kwa Washindi wa Ligi hiyo.

Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa leo katika Studio za @CloudsFMTZ Mikocheni amekabidhi zawadi kwa Washindi wa Ndondo Cup ambapo mgawanyiko wa zawadi kwa Timu zilizoshiriki Ndondo Cup 2023 msimu huu kuanzia hatua ya makundi jumla yake ni Tsh. 92 milioni.

Msigwa amekabidhi fedha hizo kwenye kipindi cha #SportsXra kwa niaba ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Ndondo Cup ni Mashindano ya mpira wa miguu yaliyoasisiwa na Clouds Media Group chini ya Mtangazaji Shaffih Dauda ambayo hufanyika kila mwaka na kuvipa nafasi vipaji vya Wakali wa soka kuanzia ngazi ya mtaa.


View attachment 2748701View attachment 2748702View attachment 2748703
Acha chokochoko, mama anaupiga mwingi!!
 
Back
Top Bottom