Mlio karibu na hawa wasanii waambieni fani ya uchekeshaji hawaiwezi

jamani hakuna kazi ngumu kama kumfanya mtu mwenyestress zake kucheka, katika sanaa zote ya uchekeshaji ndio ngumu, na ndio maana unaona haina wachekeshaji, yaani kiujumla wachekeshaji waliopo Tanzania wanahesabika
 
Ukitaka kujua mtu ana talanta hiyo,kwanza kabla ya kuchekesha ukimcheki tu usoni we mwenyewe unaanza kucheka.mf.majuto,mtanga,senga,makilegan,mpoki,kingwendu,pembe,mkwere,sumaku.
 

Without the QUANTITY we can't talk about the QUALITY ebu waache waendelee kuwemo kuwemo
 
Kuna kademu kana act kama kafanya kazi ka ndani kanaitwa EVA aisee yule demu yupo siriaz kwenye igizo unaweza hisi kweli
 
Ungeweka na picha zao ingependeza zaidi wengine hatuwajui huyo black pussy ni wa kike?
 
Braza K nifuniko lao kwa sasa Bongo,basi tu hajui kujipromote.alikuwepo na mwingine mchombe wa kulichombe alipopotelea anajua mwenyewe.Kiufupi wachekeshaji wazuri hawajitambui ila wabahatishaji wanajua kujipromote
 
Ila wakali wa vichekesho bongo kuna joti,majuto,braza K,Senga,pembe,bambo,mtanga,Kingwendu.....mpoki kwa mbaaliii na wakuvanga.
1 Joti
2 Majuto
3 Mpoki
4 Mkwere
5 Masanja


Hao kwa upande wangu naamini wana vipaji vya uchekeshaji,hawatumii nguvu nyingi tofauti na hao wengine,mtu kama Joti ukimwona tuu lzm ucheke yaan
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…