Mliofanikiwa kimaisha kwa kutumia kanuni ya 'Ubahili' mliwezaje, mbona mie nashindwa kabisa?

Mliofanikiwa kimaisha kwa kutumia kanuni ya 'Ubahili' mliwezaje, mbona mie nashindwa kabisa?

Mkuu nina ndugu yangu mmoja hivi kwa mfano, kwa bahati mbaya kila nikijaribu kumshika mkono mambo yanakuwa yanenda ndivyo sivyo. Biashara hazifanikiwa yaani kila kinachoguswa hakiendi. Nilidhani ni uzembe nikafanya alaysis nikagundua yapo mambo mengine huenda ni nje ya uwezo.
Uongo huo.wewe kumbatia ujinga..!kwanini usimtafutie kibarua afanye apate ridhiki?final ishi mbali na family yako!jijenge.saidia wazazi tuh
 
Watu hawana shukran mkuu, watu hawana kumbukumbu mkuu, fanya mambo yako
 
Tumia mbinu chache tu, na matunda utayaona!

1) Ishi mbali kabisa na familia. Yaani ishi Mkoa wa mbali kidogo kutoka kwa hao ndugu zako. Na uhakikishe wanakubatiza jina jipya la SINA HELA! Yaani wakikupigia simu kwa ajili ya kukupiga mzinga, jibu lako liwe fupi tu; mimi SINA HELA! Watakusema weeeh! Baadaye watazoea.

2) Hakikisha huwaambii mipango yako ya maendeleo/wasifahamu mali unazo miliki/ ulizonunua. Yaani kwao iwe suprise tu, siku wakija kwenye matukio.

3) Jitahidi uwe na nidhamu ya fedha. Yaani tumia 1/3 ya kipato chako. Na ili ufanikiwe katika hili; ingia benki, vuta mkopo chefu chefu! Fanyia malengo. Kinacho bakia, ndiyo upambane nacho mpaka akili ikukae sawa.
 
Tumia mbinu chache tu, na matunda utayaona!

1) Ishi mbali kabisa na familia. Yaani ishi Mkoa wa mbali kidogo kutoka kwa hao ndugu zako. Na uhakikishe wanakubatiza jina jipya la SINA HELA! Yaani wakikupigia simu kwa ajili ya kukupiga mzinga, jibu lako liwe fupi tu; mimi SINA HELA! Watakusema weeeh! Baadaye watazoea.

2) Hakikisha huwaambii mipango yako ya maendeleo/wasifahamu mali unazo miliki/ ulizonunua. Yaani kwao iwe suprise tu, siku wakija kwenye matukio.

3) Jitahidi uwe na nidhamu ya fedha. Yaani tumia 1/3 ya kipato chako. Na ili ufanikiwe katika hili; ingia benki, vuta mkopo chefu chefu! Fanyia malengo. Kinacho bakia, ndiyo upambane nacho mpaka akili ikukae sawa.
Akitekeleza hivyo vyote,mafanikio lazima yawepo
 
Kama unafanyia kazi karibu na ndugu au ukoo wako hama nenda mikoa ya mbali na usi disclose/usitoe taarifa zako za kipato kwa ndugu maana ndg wengine hawajishughurishi akipata shida kidogo kwa furani
wakati ni sasa tumia kipato chako vizuri
Watu wa kuwasaidia ni wazazi wako tu hao wengine wapambane na khari zao binadamu hawana wema haohao unaowasaidia watakuja kukucheka
Jibu zuri hili. Fanyia kazi. Nilifanya hivi mimi. I was in the same situation kama mleta maada. Ila nikahama mji.
 
Unawezaje Mkuu. Assume brother ako hana kabisa hata pesa ya msosi. Kumbuka ni kaka yako wa damu. Tupeane mbinu. Huenda na mie nikabadili strategies.
Jana mtoto wa kaka kupitia Shem ex wife wa brother kaomba hela ya viatu na michango ya mtoto ..

Usku brother mwenyewe kanipiga rungu kuwa yupo shmbn na amekwama na hela ya chakula..40k imenitoka...Kuna muda najiona dalili za kufilisika nje nje ..

Hapo nawasomeshea watoto wao ..wenyewe wanavitambi Mimi nasinyaa kukomaa Biashara isife..
 
Jana mtoto wa kaka kupitia Shem ex wife wa brother kaomba hela ya viatu na michango ya mtoto ..

Usku brother mwenyewe kanipiga rungu kuwa yupo shmbn na amekwama na hela ya chakula..40k imenitoka...Kuna muda najiona dalili za kufilisika nje nje ..

Hapo nawasomeshea watoto wao ..wenyewe wanavitambi Mimi nasinyaa kukomaa Biashara isife..
Mkuu, wahenga walinena kutoa ni moyo. We endelea tu kutoa huenda ndio njia nyako ya mafanikio. Usijejikuta unafilisika kabisa utakapoacha kutoa. Maisha ya hapa Duniani ni complex phenomenon ambayo si rahisi kuielezea. Ila katika hali ya kawaida kibinadamu, kadri unavyotoa ndio unavyoishiwa akiba na kuishia kuwa mtu wa kawaida tu. Watu wengi wanaotoboa ni mabahili sana. Unaona hii complexity?
 
Kusaidia ni jambo jema, lakini kila jambo hata liwe zuri kiasi gani lifanyike kwa KIASI. Kumbuka pia mtiririko wako wa mapato hauwezi kusalia hivyohivyo miaka yote, kuna wakati utapanda au utashuka! Usijilegeze kupita kiasi, umewahi kuwapa hao watu wako msaada hadi ukabaki bila chakula, hela ya kodi ya nyumba, umeme, maji, simu nk?! Kama jibu ni ndiyo, wewe siyo mzima kichwani! Kama jibu ni hapana, haujayapa kipaumbele mambo kama kujenga, kujiimarisha kiuchumi nk. Kwa sababu ukiyapa kipaumbele kama ilivyo kwa chakula, simu, kodi ya nyumba nk utapata njia/namna ya kuyatekeleza.
 
Wasaidie wazazi wako tu hao wengine ni mbwembwe zako tu
Wewe sio charity wa kutoa kwa kila anaekuomba

Huo sio ubahili bali ndio maisha yanataka yawe hivyo

Siku ukiwa na watoto ndio utajua halafu huna lolote kisa ulikuwa unasaidia watu
Je utawaambia kuwa ulikuwa unawasaidia fulani na Fulani nao waende wakasaidiwe huko?

Kusaidia ni vizuri don’t get me wrong ila kwa utaratibu sio eti kila mwisho wa mwezi unasubiri nani wa kumsaidia
Sasa wewe hujui hizo nguvu za kazi siku moja zitaisha?
Au unafikiri nao watoto wao watakulea?

Amka na uwaze kuwa na biashara ambazo utawaajiri hao unaowapa kutwa Samaki badala ya Ndoano

Dunia haiendi hivyo baba pambana na hali yako
Unafikiri majengo na makampuni unayoyaona yameota kama uyoga?
 
Nawashukuru sana Wakuu kwa michango yenu. Kwakweli imenisidia sana tena sana. Nadhani sasa nitabadilika. Nataka kila mwezi niwape kiupaumbele wazazi tu. Kisha nitenge kiasi kidogo sana kama 50K kwa ajili ya misaada kwa wahitaji kila mwezi. Ikiisha hiyo pesa jibu ni kuwa sina pesa. Nadhani hii inaweza kunisaidia.
 
Inamahana hao ndugu zako kila mwenzi wanakuwa nashida?
Ndio mkuu. Siyo kwamba wanajirudia walewale. Kutokana na wingi wa watu unajikuta kila mwezi hawakosekani. Si unajua sisi familia maskini tuliotoka vijijini bado tuna ule mfumo wa extended family? Mfano unakuta kuna mtoto wa Mjomba, Dada, Kaka, Shangazi, Ba Mkubwa anahitaji msaada kidogo wa mahitaji ya shule n.k.
 
Financial Discipline = Ubahili

Msome taikon wa Fasihi neno kwa neno,, kuna jambo utajifunza

 
Jilipe Kwanza wewe mzee, kwenye mshahara unaopata jilipe 10% yake..eeh afu ivo utatajirika
 
Unawezaje Mkuu. Assume brother ako hana kabisa hata pesa ya msosi. Kumbuka ni kaka yako wa damu. Tupeane mbinu. Huenda na mie nikabadili strategies.
Endelea kuwa na Moyo WA kutoa Saudia pale unapoona panafaa kusaidia ukiiendekeza ndugu utalia na hutafsnya maendeleo yoyote kwenye life lako
 
Back
Top Bottom