Mlioko kwenye ndoa zaidi ya miaka 5

Hongera niah, 30yrs ndani ya kizungumkuti cha ndoa sio lelemama.
To be frank tangu nimeolewa, siwezi lalamika namshukuru mme wangu kwa kunipenda na kulea watoto wetu mpaka wameoa sasa wengine. Shida ni extended family usipoangalia ndiyo inavunja ndoa. Ndugu zetu ukiolewa wanafikiri na wenyewe wameolewa na wewe. Wawe wanaume au wanawake wanafikiri mme wako kawaoa wote! Nimebeba hiyo mizigo na mme wangu sasa nadhani tunakaribia kuitua.
 
Ndoa zilizoanza kwa misingi ya kishirikina hazijawahi kudumu.

Mmoja akitumia ndago kumshawishi au kumvuta mwenzie kimapenzi hadi mkaoana....ndago ziki-expire ndio mwisho wa mapenzi na mwanzo wa aliyevutwa kwa ndago kumchukia mwenzie.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi mkongwe ila ndoa mwanaume ni kichwa mke ni shingo, sijawahi kulalamikiwa na ndugu wa mke kuhusu ndoa, wife yuko very smart and matured hana papara hata likitokea jambo tunalimaliza kwa mjdala kunako bed
Ooh,hongereni sana mko vizuri,nimependa inaonesha unamkubali sana mkeo. Na je mlikua hivo tangu uchumba?, ama kuna vitu mmerekebishana? Hasa kwenye kutokua na papara na kumaliza mambo kwa majadiliano?, nataka kujua kama inawezekana mtu akabadilika(+ve way)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maisha ya uchumba na ya ndoa yanautofauti sana, usibebe akili za uchumba ukapeleka kwenye ndoa utakufa kwa presha ndoa inahitaji akili na maridhiano sana, ndo maana mabinti wengi wakiolewa wanataka Yale maisha ya uchumba yaendelee katika ndoa hilo huwa halitokei, ukiolewa ujue wewe ni mama wa familia kazi yako ni kulea mume wako na watu wote unaoishi nao outing zisikuumize kichwa, achana na marafiki starehe au wale wanaklokuchokonoa kuhusu maisha yako, ishi kama mumeo anavyotaka
 
hahaa....mkikaza kipindi hicho basi ndio hamuachani tena. Hapo ndio kila mmoja anaonyesha tabia zake halisi,ni mwendo wa kuvutana tu.
1. Mmoja lzm awe low kuweka mambo sawa,kuwa mvumilivu
2. Achana na simu yake
3.Usifuatie sana mienendo yake
4. Fanya majukumu yako
5. Usilalamike sana
6.
7.
8.
Kimsingi mambo ni mengi kikubwa ni kuvumiliana,pia tuliyofanya mpk kutoboa miaka 10 sio lzm nawe uyafanye sababu nyie sio sisi. Mungu awabariki sana
 
Nina miaka 9. Nina uelewa kidogo.. kuna changamoto nyingi nafahamu. Ila cha msingi ni kuwa.. mkijifanya wote wajuaji hamuwezi kufika. Niliwahi kuambia na mtu mmoja, ukiona marafiki wawili ujue kuna mmoja aneamua kujifanya bwege, ili mambo yaende.
.
.
Ni lazima mmoja akubali kutupa pembeni interest zake ili kufanya ndoa iende.. na pia kukubali kwamba lazima kuwe kuna kusikikizana.. ukitaka mambo yawe 50& 50 kama tunavyoambiwa na ma motivator, haiwezi ku work out.
.
.
Mkiamua kujoin kuishi pamoja, kuna vitu lazima ukubali kula hasara..



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Fact. Nina miaka saba kasoro ya ndoa. Hatujawahi gombana ugomvi mkubwa, ila kuvumiliana na kuchukuliana poa kwenye mapungufu ya kibinadamu hudumisha ndoa. Kikubwa kubali kuwa mwenzako sio malaika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…