Mliokutana na mauzauza katika ujenzi wa nyumba, naomba msaada wa hatua mlizochukua

Mliokutana na mauzauza katika ujenzi wa nyumba, naomba msaada wa hatua mlizochukua

Ndugu yangu mleta uzi

Usipoteze muda wako wala pesa zako kwa kwenda sijui kwa wazee wa hilo eneo wala kwenda kwa waganga.

Usimtegee binadamu hata kidogo ndg yangu watakuongezea matatizo na wataishia kukugombanisha na majirani utawachukia watu kwa sababu ya maneno watakayokwambia. Maana utaanza kuambiwa mara fulani mchawi

Ishi peace na majirani zako

Ukiona chochote kwenye nyumba yako cha kishirikina kichome moto

Mtegemee Mungu tu

Watafanya mauzauza yao yote baadaye watachoka
 
Mwenye hicho kiwanja yaani yule alomuuziq dogo ndo anakufanyia ujinga.

Yeye alimuuzia dogo kiwanja kwa bei rahisi na wewe dogo akakuuzia kwa bei kubwa hapo ndo tatizo lilianzia.

Kujua shida ni nini ni simple sana kama wewe sio bahili, tembelea huo mtaa anģalia mtu mzima ambae kaishi hapo muda mrefu hasa mwanaume. Fanya research huyo mtu asiwe wale wazee wasiojielewa wanashida kwenye pombe.

Basi nenda kwake mwambie ukweli wote na muombe akupelelezee chanzo cha hayo mauzauza. Wakati unaondoka mwachie hata efu 30 au 50 mwambie hiyo ni ya vocha tuwasiliane. Usubiri majibu kwa muda.
Ok noted luckyline
 
Ndugu yangu mleta uzi

Usipoteze muda wako wala pesa zako kwa kwenda sijui kwa wazee wa hilo eneo wala kwenda kwa waganga.

Usimtegee binadamu hata kidogo ndg yangu watakuongezea matatizo na wataishia kukugombanisha na majirani utawachukia watu kwa sababu ya maneno watakayokwambia. Maana utaanza kuambiwa mara fulani mchawi

Ishi peace na majirani zako

Ukiona chochote kwenye nyumba yako cha kishirikina kichome moto

Mtegemee Mungu tu

Watafanya mauzauza yao yote baadaye watachoka
Asante
 
Tanzania kuna vituko sana unaweza kununua kiwanja eneo fulani halafu utasikia watu/mtu anakwambia hili eneo kuna watu wanawafanya wenzao wawe wazito kujenga

Wanaweza hata kuanza kukuonyesha viwanja vingine ukaambiwa huyu mwaka wa kumi huu hata kusafisha eneo lake hakumbuki

Utasikia huyu naye kaleta tofali hizi mwaka wa tatu hata chumba kimemshinda

🤣🤣🤣
 
Ukipuuzia hakuna baya lolote utapata, ukiwaza na kuchukuliwa serious tegemea mabalaa mbele. Uchawi dawa yake ni kupuuzia. Ndio maana unashauriwa ukisikia usiku wachawi wanawanga au kucheza juu ya bati, toka nje kaa jifanye huna habari tena vuta na kiti kabisa chukua simu peruzi mtandaoni.

Wachawi wanapenda kutiliwa maanani, ukiwapuuzia hawana tena issue
Mkuu ushawahi kufanya hivyo?
 
Vip hao mbwa usiku uliwaachia nje
Ni lazima kuwaachia, kwenye mji wangu ukiingia bila kufuata protocol kuanzia saa 4 usiku mpaka saa 12 hakuna rangi utaacha ona. Hata hao walozi watafanya mambo yao nje ya gate la himaya yangu na sio ndani.
 
Wadau niombe msaada kihusu mada tajwa hapo juu. Nimekuwa napambana na ujenzi wa kibanda changu cha ndoto yangu kwa kipindi cha miaka mitano hivi.

Ilivyofika mwaka jana wakati wanapiga plasta nilikuta kitu kisichocha kawaida katika mchanga, nilimkuta sungura aliyechinjwa akiwa amefukiwa kwenye mchanga.

Tukio hilo nililipuzia nikamtupa huyo sungura kwa kumfukia kwenye shimo.

Mwezi huu tena baada kusimama ujenzi kwa muda mrefu nilianza kujenga fensi cha kushangaza kwenye msingi uliochimbwa tulikuta ngozi ya kondoo ikiwa imefukiwa napo nilipuzia

Kilichosababisha kuandika thread hii ni tukio la leo tumekuta kisu kilicho na damu pamoja na manyoya ya ndege kisu kikiwa na damu.

Niombe wadau walioexperience changamoto hiyo mlifanyeje. Lakini nini maana ya mauzauza hayo? Nini kinatafutwa

Kuhusu kiwanja niliuziwa na kijana mmoja ambaye naye alinunua kwa mmiliki, ambapo huyo kijana naye anaishi karibu na jengo langu ingawa miye sijahamia
Okoka ili Yesu awe Bwana na Mwokozi wako. Hayo yote yatakwisha
 
Wanakutisha tu hao wapuuzi,chukua CHUMVI ya mawe nyingi kiasi ifunge kwenye nguo nyeusi izike kwenye kona zote na katikati ya eneo,kabla ujaanza kujenga,CHUMVI hiyo utaisomea zaburi ya 91 Mara 9,kabla ya kuweka.
 
Tangia nianze kujenga hadi namaliza sijawai kukutana na upuuzi wa aina yeyote ,niliwaambia mafundi hapa hata wafukie kichwa cha mtu nitajenga hadi mwisho ,ukiona nimesimama basi ujue sina pesa ya kujenga lakini nikiwa nayo wachawi hata wafukie ngombe mzima nitajenga.
 
Ujenzi umechukua muda mrefu mpaka wachawi wameshahamia ivyo wanakutishia.

Dogo wako naye ameshaingia tamaa ukimbie umwachie mji.

Ulivyopata hiyo hela unajua mwenyewe, kama kuna maruweruwe upatikanaji wake uza tu ujipange upya
 
Wadau niombe msaada kihusu mada tajwa hapo juu. Nimekuwa napambana na ujenzi wa kibanda changu cha ndoto yangu kwa kipindi cha miaka mitano hivi.

Ilivyofika mwaka jana wakati wanapiga plasta nilikuta kitu kisichocha kawaida katika mchanga, nilimkuta sungura aliyechinjwa akiwa amefukiwa kwenye mchanga.

Tukio hilo nililipuzia nikamtupa huyo sungura kwa kumfukia kwenye shimo.

Mwezi huu tena baada kusimama ujenzi kwa muda mrefu nilianza kujenga fensi cha kushangaza kwenye msingi uliochimbwa tulikuta ngozi ya kondoo ikiwa imefukiwa napo nilipuzia

Kilichosababisha kuandika thread hii ni tukio la leo tumekuta kisu kilicho na damu pamoja na manyoya ya ndege kisu kikiwa na damu.

Niombe wadau walioexperience changamoto hiyo mlifanyeje. Lakini nini maana ya mauzauza hayo? Nini kinatafutwa

Kuhusu kiwanja niliuziwa na kijana mmoja ambaye naye alinunua kwa mmiliki, ambapo huyo kijana naye anaishi karibu na jengo langu ingawa miye sijahamia
Hapo hamna kitu, ni mapicha picha tu hayo. Tafuta na wewe style yako ya mapicha picha ufanye hapo kwenye eneo lako la ujenzi uone kama kuna jirani yoyote atarudi tena hapo kufanya mauzauza. Tafuta mmbwa koko mmoja mweusi, mpulizie rangi nyekundu upande mmoja, mvalishe shanga nyingi sana alafu mfungie chini ya mti hapo kwenye kiwanja kwa wiki moja alafu baada ya hapo mfungulie azurure hapo mtaani. Hapo utakua umemaliza kazi.
 
Wadau niombe msaada kihusu mada tajwa hapo juu. Nimekuwa napambana na ujenzi wa kibanda changu cha ndoto yangu kwa kipindi cha miaka mitano hivi.

Ilivyofika mwaka jana wakati wanapiga plasta nilikuta kitu kisichocha kawaida katika mchanga, nilimkuta sungura aliyechinjwa akiwa amefukiwa kwenye mchanga.

Tukio hilo nililipuzia nikamtupa huyo sungura kwa kumfukia kwenye shimo.

Mwezi huu tena baada kusimama ujenzi kwa muda mrefu nilianza kujenga fensi cha kushangaza kwenye msingi uliochimbwa tulikuta ngozi ya kondoo ikiwa imefukiwa napo nilipuzia

Kilichosababisha kuandika thread hii ni tukio la leo tumekuta kisu kilicho na damu pamoja na manyoya ya ndege kisu kikiwa na damu.

Niombe wadau walioexperience changamoto hiyo mlifanyeje. Lakini nini maana ya mauzauza hayo? Nini kinatafutwa

Kuhusu kiwanja niliuziwa na kijana mmoja ambaye naye alinunua kwa mmiliki, ambapo huyo kijana naye anaishi karibu na jengo langu ingawa miye sijahamia
Usishangae sana wala usiumize kichwa, ipo siku utakuta hata kondom, mizoga ya mbwa n.k.. hii ni kwa sababu hujahamia bado ni pagale.
 
Back
Top Bottom