Mliowahi kukopa benki na badae kuachana na mikopo na kubaki na mitaji yenu tupeane ujuzi nasi tujikwamue

Mliowahi kukopa benki na badae kuachana na mikopo na kubaki na mitaji yenu tupeane ujuzi nasi tujikwamue

Mkopo ni kama some sort of addiction, mtu akishaanza kuacha kazi sana. Matajiri wengi almost 90% wana run biashara kwa mikopo tena mikubwa sana ambayo sometimes hailipiki. 2004 mzee wangu akiwa nazo alikuwa na marafiki kma kina gachuma, lameck airo,patel na wengine nilijifunza wengi huendesha biashara kwa mikopo.

The difference ni kwamba wenzetu cjui wanafanyeje kuishi na madeni miaka yote mpk wanakufa na vizazi vinaendeleza madeni. Mpk leo i dont what went wrong mzee alikuwa na mtaji wa 800 milion back 2000 ilikuwa pesa kubwa tu kufikia 2005,alikuwa n 500 milioni fixed Account crdb,mpk benki ikamzawadia land cruiser mpya coz alikuwa akiweka pesa hatoi!

Wakawa wanamfuata mzee kukopa yaani anabembelezwa kabisa kukopa, hapo ndipo tatizo lilipoanza. To make the story short cjui kilitokea nn kufikia 2009 ,mzee alifilisiwa vibaya sana hawana hata chembe ya huruma walifilisi hadi kijiko. Infact tulitolewa kwenye nyumba na nguo zetu tu mpk leo mzee hayuko sawa,ana presha, kisukari ,magonjwa ya moyo yaani utadhani yeye ni benki ya magonjwa ! Hao watu watamu ukiwa unalipa ukiyumba utajuta kuzaliwa, i learned sitakuja nikope hata mia benki better litle with peace of mind
Duh! Mkuu pole sana.. Very interesting story ingawa hukusema alikopa kiasi gani..
Kwa ujumla mikopo ina kanuni zake.
Kwanza, usikope for biashara mpya unless ni long term.
Pili, usikope kwa kushawishiwa, kopa kama biashara inahitaji hvyo, tena kiasi sahihi, na kuna hesabu zake.
Unaeza kuta mtu ana biashara ya mtaji wa kama m30, biashara inahitaji jeki (working capital) ya 4m, anaenda kuchukua 15m. Maana yake 11m itakuwa idle au itatumiwa kwny mambo tofauti. Deni kama hilo halilipiki kamwe.
Pia, deni ya muda mfupi ikizidi 20% ya mtaji inakuwa kama kamari.
Kingine, usithubutu kuweka dhamana nyumba unayoishi, tumia kiwanja, shamba au nyumba ya ziada. Hii itakuepusha na ugonjwa wa moyo.
Kumbuka pia, kama umeamua kujilipua na mkopo, ni afadhali benki (au Saccos za jumuia kwa mikopo midogo) kuliko ki-microfinance cha mtu.. wanasema kwny hizi micro, mkopeshaji akipenda dhamana uliyoweka ataichukua tu.. Na pia usisahau kuelewa na kujiridhisha na masharti yote ya mkopo kabla ya kujifunga kwny mkataba
 
Habari za mda huu wanajamvi!

Sina shaka maana na jua kwa rehema za MUNGU mmeamka salama na baadhi tiari mpo makazini kuijenga nchi yetu.

Kwa wale ambao hawapo poa kiafya na kiakili Mungu awatie nguvu na afya mpate kurejea mapema vitani

Kama kichwa cha thread kinavyosema, mliowai kukopa mikopo mikubwa bank na baadae kuirejesha na kutokukopa tena mlitumia mbinu gani?

Binafsi ni mhanga wa hili janga kwa zaidi ya miaka5.
Nilikopa ili kuupa nguvu mtaji wangu uliokua mdogo mwanzoni sikupata tabu kurejesha..tatizo ni kwamba kila mwaka najikuta nashawishika kuongeza ukubwa wa mkopo

Na kwakua dhamana yangu inaruhusu basi ata jamaa wa bank huongeza ushawishi wa kukuongezea
Shida ni kwamba tangu mwaka jana nimeanza kula msoto usiowakawaida.

Mkopo nliokua nao nilirejesha kwa tabu sana,nliapa nikimaliza sintakopa tena,kumbe nlikua najidanganya tu.

Yaan baada ya kumaliza nilikaa bila mkopo kwa miezi miwili tu nikarudi tena kujisalimisha waniokoe.

Hapa nilipo nipo kwenye tabu na mateso ya marejesho yani biashara inavyokua ngumu ndio kabisa naiona siku ya rejesho kama siku ya ukumu.
Imebidi nisimamishe shughuli zingine ili niweze kuinusuru dhamana yangu.

Ukweli ni kwamba mpaka sasa sijakutana na mtu binafsi aliejingiza kwenye mikopo akatoka huko salama,nimeona matajiri wengi wenye mitaji mikubwa lakini mtego wa kujinasua kwenye banio la mabenk limewashinda.

Wengi wao hadi mauti yanawakuta na kuacha benk ikiwadai tena madeni yasiolipika kiraisi.

Vijana wengi wameaga mashindano baada ya kushindwa kurejesha mikopo na dhamana zao kupigwa mnada.

Je wewe uliefanikiwa uliwezaje?
Na nini kinachofanya sisi tushindwe?

Hapa hatuwaongelei wale wanaokopa kwa kutumia salaryslip zao.

Onyo: Wale mliozoea kutoa povu kavulieni nguo hapa sio mahala pake.

Karibuni.

Uzuri ni kwamba sijawah kukosa bank..Ila nilijiunga manager saccoss ambapo miez miwili ilopita nilikopa milion10.7 kwa ajili ya shughuli zangu..nakatwa taratibu kwenye mshahara kwa miaka3 wala sitaabiki...na bado shares zangu zinazidi kuongezeka.
Nakushauri hamia Saccoss
 
Uzuri ni kwamba sijawah kukosa bank..Ila nilijiunga manager saccoss ambapo miez miwili ilopita nilikopa milion10.7 kwa ajili ya shughuli zangu..nakatwa taratibu kwenye mshahara kwa miaka3 wala sitaabiki...na bado shares zangu zinazidi kuongezeka.
Nakushauri hamia Saccoss
Ongera sana mkuu.

Ila hapa nazungumzia wale risktaker kama sisi
 
Duh! Mkuu pole sana.. Very interesting story ingawa hukusema alikopa kiasi gani..
Kwa ujumla mikopo ina kanuni zake.
Kwanza, usikope for biashara mpya unless ni long term.
Pili, usikope kwa kushawishiwa, kopa kama biashara inahitaji hvyo, tena kiasi sahihi, na kuna hesabu zake.
Unaeza kuta mtu ana biashara ya mtaji wa kama m30, biashara inahitaji jeki (working capital) ya 4m, anaenda kuchukua 15m. Maana yake 11m itakuwa idle au itatumiwa kwny mambo tofauti. Deni kama hilo halilipiki kamwe.
Pia, deni ya muda mfupi ikizidi 20% ya mtaji inakuwa kama kamari.
Kingine, usithubutu kuweka dhamana nyumba unayoishi, tumia kiwanja, shamba au nyumba ya ziada. Hii itakuepusha na ugonjwa wa moyo.
Kumbuka pia, kama umeamua kujilipua na mkopo, ni afadhali benki (au Saccos za jumuia kwa mikopo midogo) kuliko ki-microfinance cha mtu.. wanasema kwny hizi micro, mkopeshaji akipenda dhamana uliyoweka ataichukua tu.. Na pia usisahau kuelewa na kujiridhisha na masharti yote ya mkopo kabla ya kujifunga kwny mkataba
Mkuu mm sio kwamba nipo kwenye danger zone kivile!

Ila nataka kupata namna ya kujinasua yaan niachane na mikopo kabisa na nibaki salama bila kuyumba.
 
Habari za mda huu wanajamvi!

Sina shaka maana na jua kwa rehema za MUNGU mmeamka salama na baadhi tiari mpo makazini kuijenga nchi yetu.

Kwa wale ambao hawapo poa kiafya na kiakili Mungu awatie nguvu na afya mpate kurejea mapema vitani

Kama kichwa cha thread kinavyosema, mliowai kukopa mikopo mikubwa bank na baadae kuirejesha na kutokukopa tena mlitumia mbinu gani?

Binafsi ni mhanga wa hili janga kwa zaidi ya miaka5.
Nilikopa ili kuupa nguvu mtaji wangu uliokua mdogo mwanzoni sikupata tabu kurejesha..tatizo ni kwamba kila mwaka najikuta nashawishika kuongeza ukubwa wa mkopo

Na kwakua dhamana yangu inaruhusu basi ata jamaa wa bank huongeza ushawishi wa kukuongezea
Shida ni kwamba tangu mwaka jana nimeanza kula msoto usiowakawaida.

Mkopo nliokua nao nilirejesha kwa tabu sana,nliapa nikimaliza sintakopa tena,kumbe nlikua najidanganya tu.

Yaan baada ya kumaliza nilikaa bila mkopo kwa miezi miwili tu nikarudi tena kujisalimisha waniokoe.

Hapa nilipo nipo kwenye tabu na mateso ya marejesho yani biashara inavyokua ngumu ndio kabisa naiona siku ya rejesho kama siku ya ukumu.
Imebidi nisimamishe shughuli zingine ili niweze kuinusuru dhamana yangu.

Ukweli ni kwamba mpaka sasa sijakutana na mtu binafsi aliejingiza kwenye mikopo akatoka huko salama,nimeona matajiri wengi wenye mitaji mikubwa lakini mtego wa kujinasua kwenye banio la mabenk limewashinda.

Wengi wao hadi mauti yanawakuta na kuacha benk ikiwadai tena madeni yasiolipika kiraisi.

Vijana wengi wameaga mashindano baada ya kushindwa kurejesha mikopo na dhamana zao kupigwa mnada.

Je wewe uliefanikiwa uliwezaje?
Na nini kinachofanya sisi tushindwe?

Hapa hatuwaongelei wale wanaokopa kwa kutumia salaryslip zao.

Onyo: Wale mliozoea kutoa povu kavulieni nguo hapa sio mahala pake.

Karibuni.
Unaweza kujinasua Kwa kupunguza kiasi cha mkopo kila unapokopa mpaka ukaja kuacha. Kama nimekuelewa vizuri wewe unaongeza kiasi cha mkopo au unarenew same loan amount kwa hiyo unajikuta in the same vicious cycle
 
Mkopo ni kama some sort of addiction, mtu akishaanza kuacha kazi sana. Matajiri wengi almost 90% wana run biashara kwa mikopo tena mikubwa sana ambayo sometimes hailipiki. 2004 mzee wangu akiwa nazo alikuwa na marafiki kma kina gachuma, lameck airo,patel na wengine nilijifunza wengi huendesha biashara kwa mikopo.

The difference ni kwamba wenzetu cjui wanafanyeje kuishi na madeni miaka yote mpk wanakufa na vizazi vinaendeleza madeni. Mpk leo i dont what went wrong mzee alikuwa na mtaji wa 800 milion back 2000 ilikuwa pesa kubwa tu kufikia 2005,alikuwa n 500 milioni fixed Account crdb,mpk benki ikamzawadia land cruiser mpya coz alikuwa akiweka pesa hatoi!

Wakawa wanamfuata mzee kukopa yaani anabembelezwa kabisa kukopa, hapo ndipo tatizo lilipoanza. To make the story short cjui kilitokea nn kufikia 2009 ,mzee alifilisiwa vibaya sana hawana hata chembe ya huruma walifilisi hadi kijiko. Infact tulitolewa kwenye nyumba na nguo zetu tu mpk leo mzee hayuko sawa,ana presha, kisukari ,magonjwa ya moyo yaani utadhani yeye ni benki ya magonjwa ! Hao watu watamu ukiwa unalipa ukiyumba utajuta kuzaliwa, i learned sitakuja nikope hata mia benki better litle with peace of mind
Unachosema ni kweli mkuu... Mi nmefanya sana kazi bank, moja ya vitu ni kwamba benki haipendi kukopesha watu wanaoenda kuomba mkopo bali watu ambao benki inawafuata kuwaomba wakope. Na hao mara nyingi wanakua hawajaplan juu ya mkopo vizuri na inaweza kuwa mwanzo wa kuanguka kama ilivyokua kwa mzee wako
 
Nashukuru mkuu!
Ni kweli biashara na mkopo sio maadui ila tatizo ni ugumu wa kujitoa kwenye mkopo ili ubaki na mtaji wako

Mfano una ml10 ukaenda kopa ml5 baada ya rejesho kuisha ni ngumu kutorudia kukopa...yani ipo kama kamari jinzi unavyokula unataka kula zaidi

Mwisho wasiku wengi wameliwa adi kile kilichokua kwao
Shida nafikiria sio kutorudia shida ni nini unataka je baada ya mkopo kuisha mtaji wako umekua? Kama ndio ni kwa kiwango inachotaka? Kama ndio then naamin hautokopa tena.
Shida ni kwamba hatujui ukomo wetu
 
Hili suala la mkopo ni balaa nmemaliza mkopo wangu wa benki mwezi July tu nlikopa stanbic then mkopo nkauza NBC mwaka 2014. Nimeapa sitokopa tena Bank kwa sasa nmebakiza mkopo wa kazini nao unaisha January.
 
Hili suala la mkopo ni balaa nmemaliza mkopo wangu wa benki mwezi July tu nlikopa stanbic then mkopo nkauza NBC mwaka 2014. Nimeapa sitokopa tena Bank kwa sasa nmebakiza mkopo wa kazini nao unaisha January.
Mikopo ni zaidi ya adui wa maisha
 
Shida nafikiria sio kutorudia shida ni nini unataka je baada ya mkopo kuisha mtaji wako umekua? Kama ndio ni kwa kiwango inachotaka? Kama ndio then naamin hautokopa tena.
Shida ni kwamba hatujui ukomo wetu
Mkuu ukitaka mtaji ukue basi usifanye swala lolote la kimaendeleo.

Wengi tunakopa ili tuweze kupata tulivyoshindwa kuvipata kabla.
 
Unachosema ni kweli mkuu... Mi nmefanya sana kazi bank, moja ya vitu ni kwamba benki haipendi kukopesha watu wanaoenda kuomba mkopo bali watu ambao benki inawafuata kuwaomba wakope. Na hao mara nyingi wanakua hawajaplan juu ya mkopo vizuri na inaweza kuwa mwanzo wa kuanguka kama ilivyokua kwa mzee wako
Point!
 
Mkopo ni kama some sort of addiction, mtu akishaanza kuacha kazi sana. Matajiri wengi almost 90% wana run biashara kwa mikopo tena mikubwa sana ambayo sometimes hailipiki. 2004 mzee wangu akiwa nazo alikuwa na marafiki kma kina gachuma, lameck airo,patel na wengine nilijifunza wengi huendesha biashara kwa mikopo.

The difference ni kwamba wenzetu cjui wanafanyeje kuishi na madeni miaka yote mpk wanakufa na vizazi vinaendeleza madeni. Mpk leo i dont what went wrong mzee alikuwa na mtaji wa 800 milion back 2000 ilikuwa pesa kubwa tu kufikia 2005,alikuwa n 500 milioni fixed Account crdb,mpk benki ikamzawadia land cruiser mpya coz alikuwa akiweka pesa hatoi!

Wakawa wanamfuata mzee kukopa yaani anabembelezwa kabisa kukopa, hapo ndipo tatizo lilipoanza. To make the story short cjui kilitokea nn kufikia 2009 ,mzee alifilisiwa vibaya sana hawana hata chembe ya huruma walifilisi hadi kijiko. Infact tulitolewa kwenye nyumba na nguo zetu tu mpk leo mzee hayuko sawa,ana presha, kisukari ,magonjwa ya moyo yaani utadhani yeye ni benki ya magonjwa ! Hao watu watamu ukiwa unalipa ukiyumba utajuta kuzaliwa, i learned sitakuja nikope hata mia benki better litle with peace of mind

Huyu Mzee kama namfahamu hivi,Sio Bwana Getano kweli huyu?

Back in 2005 hii story ya kuzawadiwa na CRDB ilitrend sana kule home Lake Zone n I think ni Getano ndo alipewa hiyo zawadi

Nina washkaji zangu huyu Getano ni Uncle yao n I know them deep down sema sikuwahi kujua kama Yule mzee alifilisika back then
 
Kuna mtu aliniambia siku ile unapeleka hati ya nyumba yako benki kama dhamana, ndiyo mwisho wa kuiona hiyo hati huwa haitoki benki .
Hakuna hata tajiri mmoja aliyeweza kutoa hati yake benki na kuirudisha nyumbani . Unakopa kuongeza mtaji lkni mwishowe hata mtaji wako uliokuwa nao utapotea.
Cha muhimu ukiona unaomba kufanyiwa topup ujue biashara yako imeisha ni kusubiria mnanda.
 
Aisrr
Kuna mtu aliniambia siku ile unapeleka hati ya nyumba yako benki kama dhamana, ndiyo mwisho wa kuiona hiyo hati huwa haitoki benki .
Hakuna hata tajiri mmoja aliyeweza kutoa hati yake benki na kuirudisha nyumbani . Unakopa kuongeza mtaji lkni mwishowe hata mtaji wako uliokuwa nao utapotea.
Cha muhimu ukiona unaomba kufanyiwa topup ujue biashara yako imeisha ni kusubiria mnanda.
aisee mbona hatari sana.
 
Shida nyingine ni aina ya uwekezaji tunao ufanya Mara nyingi tunawekeza kimazoea

Mfano una biashara yako imesimama vizuri unakopa na kulipa bila shida yoyote kosa kubwa unapo anza kuongeza miradi afu teamwork yako unachukua sijui binam mara mdogo wako kisa hana kazi unawaweka pale wao wanakuona umefanikkiwa tayari hivyo umewaleta pale na wao watoke kimaisha lkn kumbe wewe umekopa pesa hizo
Hapo kwa binamu&ndugu umenigusa
 
Aisrr aisee mbona hatari sana.
Kuna mtu aliniambia siku ile unapeleka hati ya nyumba yako benki kama dhamana, ndiyo mwisho wa kuiona hiyo hati huwa haitoki benki .
Hakuna hata tajiri mmoja aliyeweza kutoa hati yake benki na kuirudisha nyumbani . Unakopa kuongeza mtaji lkni mwishowe hata mtaji wako uliokuwa nao utapotea.
Cha muhimu ukiona unaomba kufanyiwa topup ujue biashara yako imeisha ni kusubiria mnanda.
Huu ni ukweli mchungu kabisa
 
Naomba mnipe ufafanuzi zaidi wajuzi,,, nimekopa benk flani nimelipa mkopo wangu kwa asilimia 70% Biashara imeyumba kidogo na nimewandikia barua kuwa mzunguko umekuwa mdogo je hili linaweza kuniletea shida? Kama kuuza dhamani nk?
 
Back
Top Bottom