Mkuu ukitaka mtaji ukue basi usifanye swala lolote la kimaendeleo.
Wengi tunakopa ili tuweze kupata tulivyoshindwa kuvipata kabla.
Hilo ni kweli mkuu,
Nakumbuka back in 2008 naanza ujasiliamali.
Biashara inaenda vizur, basi nkaingiwa na wazo LA kukopa niongeze mtaji.
Nakumbuka,
Nlkopa 3mil pale crdb, dhamana ilkua ni shamba LA miti LA mama yangu.
Nkaingiza kama laki 9 kwenye finishing ya nyumba, mil 1.2 nkanunua pikipiki ya kutembelea, Afu laki 9 nikanunua mzigo
Siwezi kusahau,
Baada ya miez 6 tu nilianza kuonja joto LA jiwe kwenye marejesho benki.
Aisee,
Nilifikia hatua ya kuuza kitanda, TV, na kabati LA vyombo ili kulipa deni LA benki.
Pikipiki yenyewe niliuza kwa hasara( laki 5) ili nisiadhirike.
Nakumbuka
jins mama alivoangua kilio usiku kucha aliposikia jina langu lipo kwenye wadaiwa Sugu wa CRdb ambao baada ya siku 90 Mali zilizowekwa dhamana zitapigwa mnada.
Ila namshukuru mungu,
Nilipambana mpaka nikamaliza deni lao.
TOKEA HAPO NMEKUA MAKINI NA PESA ZA MIKOPO.
KIUHALISIA KUPITIA HAPO NLIJIFUNZA KUA NA NIDHAMU NA PESA YA MKOPO.
NA BILA MKOPO, NI NGUMU SANA KUENDELEA KIMAISHA.
CHA MUHIMU,
NI KUKOPA KWA LENGO MAALUM, NA PESA YA MKOPO IELEKEZWE KWENYE LENGO MAALUM.
NB:
Nilikopa, Ninakopa na Nitaendelea kukopa.
Mchawi wetu ni nidhamu ya pesa