Mliowahi kukopa benki na badae kuachana na mikopo na kubaki na mitaji yenu tupeane ujuzi nasi tujikwamue

Mkuu... Unaweza ukatupa hizo kanuni za mikopo? Just briefly.
 
Watu Wauchumi wanasema Hivi. Mikopo siyo Njia Sahihi ya Kujikwamua Kimaisha...

Kama Una akili Fikiria Hili. Mie huwa nakwepa sana Mikopo
Vipi kama ni mkopo usio na riba kabisa?
 
Wana jf asanteni kwa Mawazo mapana juu ya mikopo,nimejifunza mengi,be blessed all
 
Kama huna mikosi benki ni mkombozi ukicheza kwa mahesabu makali . Miradi mikubwa mara nyingi ni mikopo na watu wanatoka .
 
Nilishaachana na mikopo nikiapa kuwa, mtu akimiona nakopa tena, anichinje kwa msumeno ila sasa nahisi kuitamani, tamani!
 
Yaan Leo nimetoka kupiga passport tayar Kwa kuelekea NMB kukopa, nimesoma comments za wadau Kwa makini saana.Nimejifunza ifuatavyo;-
1. Kopa Kwa lengo maalum.
2. Kopa Kwa lengo la kibiashara ili uweze kulipa P+I na hatamaye kubak na faida.
3. Hata Kama unauwezo wa kukopa kiasi kikubwa benk lakin kopa kiasi kile tu unachohitaji.
Kutokana na hayo itabid Kwanza kesho nihairishe kwenda benk Hadi hapo nitakapojika amri nyingine.πŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒ
 
Kwanza kabisa kukopa si kubaya=ni sawa na kuchukua pesa za watu na kufanyia kazi so ni kitu kizuri.Ukitoka kwenye mkopo maana yake kiwango chako cha kukua na kuzalisha ni kibaya.Kuna aina nyingi ya mikopo ikiwamo overdraft ambao ndio mkopo mzuri kwani huu unatumia na kulipia kile kiasi unachotaka.Kwa kawaida mfanya biashara anatakwa akikopa mkopo mkubwa ambao sio fixed basi uende kwenye asset au capita expenditure na akikopa mkopo wa operational basi uwe overdraft.Sasa ndugu yangu mkopo wako umeenda kwenye asset purchase ama umeenda kwenye operations?Ukinijibu hilo nitakupa njia ya kujinasua
 
Baba unavosema operational unamaanisha nin? Nafiriki nianzie Kwanza hapo kabla sijakujibi tayar Kwa kupata mawazo toka kwako.
 
Naomba mnipe ufafanuzi zaidi wajuzi,,, nimekopa benk flani nimelipa mkopo wangu kwa asilimia 70% Biashara imeyumba kidogo na nimewandikia barua kuwa mzunguko umekuwa mdogo je hili linaweza kuniletea shida? Kama kuuza dhamani nk?
kama unaona utayumba sana omba wakufanyie restructure ya mkopo rejesho lipungue Ingawa utalipa hela nyingi ila itakuwa ni afadhali kuliko kuhatarisha dhamana. Ni benki gani hiyo
 
Ongezea na kujua aina ya mkopo unaotaka kuchukua,kuna mtu alichukua overdraft akaitumia kama term loan , deni linamsumbua tu,
 
A
Narudia tena, wote manolalamika kuwa Awamu hii hakuna pesa, mlikuwa wapiga deal, pesa zimerudi kwa watu waliokuwa wanazipata kihalali, ridhika na hicho unachopata, ndicho kilitakiwa kuwa halali yako tangu Awamu zilizotangulia.
Acha kujitoa ufahamu wewe.
 
Mkuu ukisema operation unamanisha nn
 
Iyo mikopo tuna ngangania tu, ila Mwenyezi Mungu kayakataza hayo...(riba) Familia nyingi leo zinapitia wakati mgumu sana. Wazungu watatuletea mengi sana...
Mkuu mbona ata barabara unayotumia ni ya mkopo?

Ata uwe nani maisha bila mkopo ni uongo! labda uwe umevikuta au umeamua kufa maskini kitu ambacho ata MUNGU mwenyewe hapendi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…