Hapo ndipo utapoona umuhimu wa kuratibu uagizwaji, utunzajwi na usafirishaji wa kemikali hatari na milipuko zinazoweza kutishia usalama wa maisha, mazingira na mali .
Kwa Tanzania mamlaka kama OSHA
Occupational Safety and Health Authority Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania
KAZI ZETU | TAEC , Idara ya Customs / TRA, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na TPDF zinatakiwa kufanya kazi za ukaguzi na kwa ukaribu na wananchi ili kuona miongozo ya usalama inazingatiwa na wote pia kuratibu bidhaa zenye uwezekano wa kulipuka, kuumiza kama sumu au kemikali n.k
Mlipuko huu wa Beirut Lebanon ni somo kwetu wote kutochukulia kwa wepesi usalama wetu iwe kemikali za mercury, sulphuric acid, mbolea za kemikali, baruti , ma cylinder ya gas za majumbani na viwandani, oxygen cylinder , gesi za kuchomelea vyuma n.k
Siku zote tunapotumia bidhaa za hatari tushirikishe taasisi na mamlaka zinazohusika ili zitushauri namna bora ya kutumia, wingi wa kuhifadhi, maeneo salama ya kuhifadhi na usafirishaji wake.