Mmejitahidi sana kuipamba na kuinogesha harusi ya leo, ila hata haijafikia 25% ya iliyokuwa Harusi ya Mtoto wa Mzee Rupia

Mmejitahidi sana kuipamba na kuinogesha harusi ya leo, ila hata haijafikia 25% ya iliyokuwa Harusi ya Mtoto wa Mzee Rupia

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
Wengi wenu hapa JamiiForums bahati mbaya miaka hiyo ya mwishoni ya 90 bado mlikuwa katika Zipu za Baba zenu ila kwa Wakongwe tulikuwepo na mpaka hii leo sijaona bado Harusi ya Kuizidi hiyo.

Ilikuwa ni Harusi ya Mtoto wa Mzee Rupia ( Tajiri wa Kihistoria Tanzania ) na Binti yake Mzee Mramba ( aliyekuwa Waziri wa Fedha ) ambapo Harusi yao ilifanyika ndani ya Meli, Watu tulikunywa na kula Wiki Mbili na kila Kitu kilikuja na Meli kutoka huko ilikotoka na baada ya Harusi ikaondoka.

Cha Kusikitisha zaidi pamoja na Mbwembwe zote hizi ( hizo ) Harusi hii ilidumu kwa Wiki Mbili tu sababu kubwa ni Mke ( Bibi Harusi ) kukataa Kutekeleza Majukumu yake kwa Mumewe ( siyo Kufanya Ngono ) na kutaka kila Kitu kifanywe na Beki Tatu / Dada wa Kazi na hatimaye wakashindwana.

Ulikuwa ukienda Posta kwa Shughuli zako ukisikia tu hamu ya Gambe ( Bia ) basi unaelekea ilipo Meli na Kuchukua zinazokutosha kisha unaendelea na Ratiba zako za Kimaisha. Na Watu wengi walijifunzia Kulewa katika hizi Bia za Bure za iliyokuwa Harusi ya Mtoto wa Mzee Rupia na Binti wa Mzee Mramba.

Nasikia Mlimani City Bia za Uchoyo!!!!!
 
Hii harusi ya leo kali sana acha majungu

Harusi kuwa nzuri sababu sio chakula wala vinywaji. Bali Ni jinsi inavyo touch other peoples feelings, hasa maharusi wenyewe jinsi wanavyoendana. Na Jinsi wavyopendwa na jamii hasa watoto.

Unajua leo kanisani watoto waliokuwa kwenye mafundisho wa kipaimara walitoroka darasani kwao sababu kwenda kuwaona maharusi tu wanavyoingia kanisani na kwenye ibada watoto wakazama wakasahau kurudi darasani kwenye mafundisho yao.

Pia watumishi wa kanisa walivyokuwa wanawapokea.. wapo makini sana maana yake wanajua harusi kubwa hii.

Kwa sisi wakristo wa KKKT ukiona harusi jumamosi inatenganishwa na za wengine ujue harusi yako ni ya kibabe.. harusi ya nandy na billnass imefungwa saa 5 asubuhi wakati saa 9 ndio ulikuwa muda wa harusi zingine zote za kanisa hilo hilo la usharika wa mbezi beach katika tarehe hiyo. Maana walijua nandy na bill nass wakiwaingiza saa tisa pamoja na maharusi wa kawaida. Watawafunika maharusi wenzao kwa attention wajisikie vibaya.
 
Utakuwa na safari ndefu sana ya kutoboa kimaisha kama utakuwa unaendekeza mambo haya.
Kwahiyo kwa Bill Nenga hakuna pombe za bure ndiyo maana umeifananisha.
Unafanya jambo pale mkono wako unapoishia. Ushajiuliza kwanini wewe hauna pesa kama MO? Ndiyo jinsi maisha yalivyo. Unajikuna unapofikia
Tulikunywa Bia za bure kwa Wiki Mbili hadi tukazikinai achilia mbali Misosi na Mapochopocho.
 
Hii Harusi haijaifikia hata ROBO ya ile ya ALIKIBA.
 
Hii harusi ya leo kali sana acha majungu

Harusi kuwa nzuri sababu sio chakula wala vinywaji. Bali ni maharusi wenyewe jinsi wanavyoendana. Jinsi wavyopendwa na jamii hasa watoto.

Unajua leo kanisani watoto waliokuwa kwenye mafundisho wa kipaimara walitoroka darasani kwao sababu kwenda kuwaona maharusi tu wanavyoingia kanisani na kwenye ibada watoto wakazama wakasahau mafundisho yao
Mabody guard wanasukuma watu why kwanini wasogezwe si waliwaaliaka wao
 
Back
Top Bottom