Mmoja auawa kwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi - Mataa ya Airport

Mmoja auawa kwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi - Mataa ya Airport

Unataka kuniambia UWT ndio weupe kiasi hiki kiasi wakitaka kuuana wenyewe kwa wenyewe mpaka wakasubiriane barabarani?

Tuache utani jamani, mimi naamini kuna kitu kingine na sio UWT, maana naamini wanakili zaidi ya hii, kwanini wasimpumzishe kwa amani tu ana akajifia kimyakimyaa kuliko kuja barabrani na fujo zote hizo.

They sent clear message, a comprehensive package no need for other unnecessary covert!
 
Maarufu kama mbena malumbi kafanya maendeleo sana moro.hakika wengi wataathirika maana alikuwa na wafanyakaz weng ktk investment zake
 
ni gharana kiasi gani utaingia kama ukiamua kuomba askari ili wakusindikize? si zaidi ya elfu hamsini na unakuwa na ulinzi wa uhakika. huu ujinga mwingine wa kuangalia faida tuu bila kutaka matumiziz mazao yake ndo hayo

kama wanakwenda piga dili chafu ulinz hawawez kuomba.
 
Mambo ya kuchukua wake za watu mabaya sana. Hata hivyo serikali iimarishe ulinzi dhidi ya raia wake, maana sheria za kudeal na wagoni zipo.
Nakubaliana nawewe mkuu,hawa jamaa wamezidi kuchukua wake za watu hasa makazini huko wanawatishatisha tu!
 
Mkuu na ww uwezo wako wa kuchangia ndio umefikia hapa? Sasa si bora uwe msomaji tu.

Uwezo wako wakufikiri unapoishia mm ndipo napojazia, kwani s3 mnazitaka? mbona yule mzenji mlivua ubunge? Kwa ccm mbona kawaida?
 
Ofisa mwandamizi wa idara ya Usalama wa Taifa nchini Bwana Silvanus Mzeru ameuwawa na watu wasiojulikana katika mazingira ya kutatanisha. Mauwaji hayo ambayo taarifa zake zimeibua hofu kubwa, yalitokea jana jioni katika mataa ya barabarani ya karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl Julius Nyerere jijini Dar es salaam.

Habari zinasema mara baada ya kufanyika kwa tukio hilo la kinyama wauwaji hao waliondoka na briefcase ya marehemu huyo ambayo haijajulikani ndani yake ilikuwa na vitu gani.
Kwa mujibu wa watu walioshuhudia tukio hilo, kabla ya kuuwawa kwa Mzeru watu wawili waliokuwa kwenye pikipiki walirusha risasi kuelekea katika gari yake.

"Baada ya risasi hizo kurindima, Mzeru aliendesha gari lake kwa kasi na kwenda kugonga magari mengine yaliyokuwa mbele yake na kisha gari lake kutumbukia mtaroni" Alisema mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo.

Mashuhuda hao waliongeza kuwa wauwaji wa Mzeru walimfuata katika mtaro na kuumua kabla ya kuondoka na briefcase iliyokuwa kwenye gari.

Chanzo: Tanzanidaima Toleo namba 3436 Uk 3 la leo Alhamisi, Mei 1 2014.

Mytake:

Kama watu wa usalama wa Taifa wanaweza kuuwawa kinyama kiasi hicho, vipi kuhusu raia wa kawaida?! Kama raia wa kawaida wamekuwa wanapigwa risasi na kuuwa kwa mabomu kwenye mikutano ya vyama vya siasa na waliopaswa kulinda usalama wao, Kumbe haina tofauti na watu wa usalama wa Taifa?! Kama usalama wa taifa huwa wanalalamikiwa kwa kuteka na kutesa kama ilivyosemwa kwa Dr Ulimboka, Nani yuko salama?

Kazi ya usalama wa taifa ni kazi nyeti na wanaofanya hiyo kazi wamejitolea maana wanakuwa na siri nzito za nchi husika kuuawa hutokea sana iwapo wanasiasa wanashindana katika kuwania uongozi inabidi kuwaondoa na kuwaua baadhi wenye siri nzito dhidi yao au wenye mafaili yao. Pia iwapo wana file la kigogo dhidi ya kesi fulani mhusika aliyekusanya habari za kiusalama na kuwa nazo huuawa. Angalizo kuuawa kwa wanausalama wa taifa hakuhusini na kwamba usalama wa raia wa kawaida utakuwaje hiyo ipo hata nchi zilizoendelea kama za Ulaya na Marekani ingawa raia wa nchi hizo wako salama
 
Mhhhh!!! Msalama anauwa ki rahisi hivyo!!!

Haya bana....
 
Back
Top Bottom