Mnadhani kwa huu mpango kabambe wa viongozi wa Yanga utaacha kuleta lawama na makelele kwa watu makini kama Mimi na wengineo?

Mnadhani kwa huu mpango kabambe wa viongozi wa Yanga utaacha kuleta lawama na makelele kwa watu makini kama Mimi na wengineo?

GSM ni mfanya biashara Tena mwenye mafanikiao kabla ya kuja Yanga, Ao wakina Mavunde, Kitenge n.k walipambana ku mshawishi GSM kuja kuwekeza Yanga.
GSM ata Leo akiamua kuiacha Yanga hawezi filisika ila Yanga tutarudi kwenye uhalisia wetu kama Mwanzo.
Wakati Manji ameodoka, Yanga ilikua na Logo yake na Facility zake na hakuna aliye sogea kuisaidi.

Yanga Ina mabilioni ya mashabiki ndani na nje ya Nchi lakini mpaka Sasa waliojiandikisha na kuchukua kadi hawazidi elfu 90.

Wengi wao hawatalipia kadi za uanachama msimu huu 2023/2024 na kufanya mapato ya klabu kupitia wanachama kupungua kutoka bilion Moja na ushee kufikia milioni 600 timu ikiwa imetwaa taji lake la 30.
Iyo milioni 600 ni fedha ya maji kwa wachezaji na first Aid kit ya timu kwa msimu.
GSM anacho faidika ni kutangaza Bland yake kupitia Yanga na wame Target kimataifa zaidi maana kwa hapa ndani wao ni maarufu.
GSM ana wekeza katika Yanga ili wote wafaidike lakini ata asipowekeza Yanga, Bado GSM bland Yao inaweza ku survive bila Yanga, ila Yanga iki achwa pekeyake haitokufa ila ita zimia (collapse) kama kipindi alipo ondoka Manji.
Udhamini wa Sasa ambao ni mkubwa haizidi bilion mbili kwa Mwaka ambao Simba wameingia na Sunderland.

Yanga na Simba wakati wanafanya iyo biashara ya jezi wao wenyewe walikua walikua wakipata 200 milioni ambayo kwa Sasa ni tone tu katika Bajeti zao.
Izo jezi Zina uharamia mwingi mpaka uziuze na kurudisha fedha Yako ndio maana Vunja bei alishindwa.

Wewe una print jez China/ Thailand kwa gharama kubwa na unalipa kodi,
Wahuni wako DAR wamesha print copy tayari na Wana ziuza 5000/= full kit.
Wote tulishuhudia siku za karibuni zilipo kamatwa maelfu ya Jezi haramu kwenye ma godown Chang'ombe DSM .
Kuiendesha klabu sio jambo rahisi kwa apa Nchini.
Ulivyoandika tu kuwa Yanga ina mabilioni ya mashabiki ndani na nnje ya nchi nikaishia hapo kwani nimeng'amua wewe ni baba wa uongo na propaganda kama CCM.
 
Hii nchi hata hatujui tunataka nini! Hivi GSM ananufaika nini ha hii yanga? Mkiachiwa timu yenu wiki tu inawashinda. Manji aliwaachia timu yenu, ilikuwaje? Miaka minne ya msoto
Kwa hyo hata kama mambo wanayaficha ficha na kuyaharibu waachwe kisa wanatoa hela zao?
GSM anatangaza biashara zake pale,GSM anasimamia mapato yote ya yanga pale.anajua kinachotoka na kinachoingia.faida anapata kubwa na hawezi kutuambia.
 
Wabongo ujuaji mwingi, mtu mmoja anajifanya anajua kukosoa ufundishaji, uchezaji, uchumi, n.k. hivi kabla ya ujio wa Manji, Mo na GSM hizi vilabu vilikuwa na hali gani kiuchumi, kimafanikio na kithamani? Tulikuwa tunazidiwa hadi timu za Kenya, Sudani. Leo hii GSM na Mo wamezifanya hizi timu zipande thamani, ubora na mafanikio tele Africa mnaanza majungu na fitina kuwa zinapata faida.

Je mashabiki wanataka pesa au mafanikio? Kwasababu hizo ela ambazo mnazohoji kuwa wanachukua ni matokeo ya hao hao wakina Mo na GSM kuzikuza hizo timu na mwisho kuongeza ushawishi kwa wadhamini ili kufanya wao wasipate hasara kwa kutoa pesa zao mifukoni kuendesha timu. Kabla ya ujio wa hawa watu vilabu vilikuwa vinaingiza sh ngapi kiasi kwamba tuone hivi vilabu vilikuwa na pesa za kutosha?
 
mifukoni kuendesha timu. Kabla ya ujio wa hawa watu vilabu vilikuwa vinaingiza sh ngapi kiasi kwamba tuone hivi vilabu vilikuwa na pesa za kutosha?
unataka kusema hivi vilabu Mo dewji na GSM hawapati faida
 
Mleta mada naomba utuwekee hapa Kadi yako ya Uanachama Ili tukishaiona ndiyo tujadili HOJA yako!
 
unataka kusema hivi vilabu Mo dewji na GSM hawapati faida
Inawezekana kuna wakati wakawa wanapata faida na kuna nyakati wanapata hasara hao ni wafanyabiashara. Hao wanaendesha mambo yote kwenye taasisi inayohusu Simba na Yanga hivyo gharama za matumizi ikizidi mapato ni hasara. Ila ikitokea matumizi yamezidi mapato hiyo ni hasara. Tukumbuke kuwa sisi mashabiki hatutaki kusikia mchezaji anadai mshahara au timu imeshindwa kusafiri au kushindikana jambo fulani sababu ya pesa bali tunahitaji kila kitu kiende. Hivyo ni wajibu wa hawa akina GSM na Mo kukopa au kufanya chochote kile ili ipatikane pesa mambo yaende.
 
Inawezekana kuna wakati wakawa wanapata faida na kuna nyakati wanapata hasara hao ni . Hao wanaendesha mambo yote kwenye taasisi inayohusu Simba na Yanga hivyo gharama za matumizi ikizidi mapato ni hasara. Ila ikitokea matumizi yamezidi mapato hiyo ni hasara. Tukumbuke kuwa sisi mashabiki hatutaki kusikia mchezaji anadai mshahara au timu imeshindwa kusafiri au kushindikana jambo fulani sababu ya pesa bali tunahitaji kila kitu kiende. Hivyo ni wajibu wa hawa akina GSM na Mo kukopa au kufanya chochote kile ili ipatikane pesa mambo yaende.
mkuu unaongelea hisia na siyo uhalisia kabisa
 
mkuu unaongelea hisia na siyo uhalisia kabisa
Wewe ndio unaongelea hisia sio uhalisia. Unataka ulazimishe kuwa kila siku wanapata faida. Kwenye hili mimi nitakuuliza swali je unafahamu mapato halisi ya hizi timu? Je unafahamu kiwango halisi cha matumizi ya hizi timu? Ili upate uhalisia lazima uwe na data halisi.
 
Back
Top Bottom