Mnaodhani Hayati Magufuli aliokota Dodo chini ya mnazi, mnajidanganya alijiandaa kuwa Rais miaka 20 kabla

Mnaodhani Hayati Magufuli aliokota Dodo chini ya mnazi, mnajidanganya alijiandaa kuwa Rais miaka 20 kabla

mdukuzi

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2014
Posts
20,925
Reaction score
51,688
Naweza sema ni mzee Ruksa, Mkapa na mama Samia ndio waliokota dodo chini ya mnazi, Nyerere, Kikwete na Magufuli waliutafuta urais kwa mbinu zote chafu na safi.

Leo tumuangalia Rais Magufuli, Pompeo wa bongo alivyousaka urais kwa mbinu za chini kwa chini.

Hapo mwanzo kulikuwa na jimbo moja likiitwa Biharamulo mkoani Kagera, John Pombe aligombea na mtu anaitwa Kabuye, yule mzee alimpa wakati mgumu sana Magufuli, wengine hawajui kuwa Magufuli aliwahi kuangukia pua kwenye ubunge alivyogombea kwa mara ya kwanza,

Watu wa Biharamulo ambao wengi ni kutoka kabila la Abasubi hawakumpenda John walimuita Mnyamahanga kwa maana ya wakuja.

John akaomba mizimu yake jimbo likagawanywa , Biharamulo Mashariki na Magharibi, akakimbilia Mashariki kwenye wanyamahanga wengi.

Huko akapambana kiume na wapinzani wake kibabe mpaka wengine kukimbia jimbo.

Mwaka 2006 akafanikisha kuundwa kwa wilaya ya Chato na jimbo la Chato.

Baadae akapambana Chato ikatoka Biharamulo Kagera ikaingia mkoa wa Geita mwaka 2012, huo ulikuwa ushindi mkubwa sana kwa Magufuli, unajua sababu.

Chato kuwa mkoa wa Kagera ingemuharibia sana kisiasa, watu hudhani Kagera yote ni ya Wahaya na Wahaya hawapendwi nchii hii kubali kataa, hawaaminiki kupewa madaraka makubwa.

Nikutajie sasa makabila yanayopatikana wilaya ya Chato. **** Warundi wengi sana kutoka Burundi kuna Waha, Wasumbwa, Wasubi, Wazinza, Warongo, Wahaya ,Wasukuma na watu wa Musoma. Kila mtu anaona hapa ni kwake na wazee wengi hapa wanaongea hizo lugha zote, ndivyo ilivokuwa kwa Magufuli, yeye aliamua kujiita Msukuma ila hakuwa Msukuma, ilikuwa ni sababu za kisiasa tu.

Mpaka wa Chato sasa ukaambaa kutoka Mganza, Bwanga, Buseresere, Buziku, Buzirayombo nk hizo kata mtu unaamua tu kujiita kabila lolote kati ya hayo makabila niliyotaja.

Huu ulikuwa ni mpango mkubwa sana ulihitaji mchakato wa miaka 20 akazaliwa John mpya kabila Msukuma ,kwenye kampeni ya urais 2020 akafungia kampeni Mwanza akahutubia kwa kisukuma akazoa kura za wasukuma wote hata wa Bariadi na Shinyanga. Ingekuwaje angehutubia kwa lugha ya Kirundi au Kizinza lugha alizozimudu vizuri, au angehutubia kwa kihaya, bila shaka asingepata hizo kura za kanda ya ziwa, kura za wasukuma ambao ni wengi .

Mbinu ya pili aliyotumia ni kutaka kuonekana ni msomi mzuri kwa kutafuta PhD ili kujenga trust kwa watu kuwa yupo vizuri kitaaluma. Magu hakuwa kilaza darasani ila hakuwa kipanga, ile PhD ina ukakasi jinsi ilivyopatikana lakini zote ilikuwa ni maadalizi ya kugombea Urais.

Mkakati wa tatu ilikuwa ni kujifanya yeye ni masikini kumbe alikuwani tajiri mkubwa sana huwezi kuwa wizara ya ujenzi ukafa masikini, Kilometa moja ya lami ni zaidi ya bilioni 1.5 amesimamia kilometa nyingi sana zilizojengwa chini yake. Hii mbinu hata Kikwete aliitumia sana kujifanya masikini kumbe ni mabilionea, ujue Watanzania wengi hawawapendi matajiri hudhani wao ndio sababu ya wao kuwa masikini.kwa hiyo aliigiza kuwa yeye ni mnyonge na masikini kumbe uongo lengo ni kuteka akili za masikini ambao ndio wengi na aliwapata aswaa

Itaendelea.....
 
Uongozi hapatikani kwa kujiandaa mzee.

Wapo waliojiandaa na majina yao tunayajua.

Uongozi ni kalama na kipawa ambacho super natural power decided (Mungu/Yesu) huamua nabi apewe nani asipewe.

Ila hii haimaanishi usigombee su usijiandae kama unaweza fanya.

Sasa Rais wetu alikuwa katulia zake home Kikatiba tukamuita sasa anakula nchi hadi 2030 hiyo

Sasa hapo ni utake usitake imeshakuwa hivyo tulia maisha yaendelee
 
Naweza sema ni mzee Ruksa,Mkapa na mama Samia ndio waliokota dodo chini ya mnazi,Nyerere,Kikwete na Magufuli waliutafuta urais kwa mbinu zote chafu na safi.
Hebu tueleze na ule mradi wake Canada, magari yake ya usafirishaji Rwanda na mradi wa Msumbiji.
Fedha za kujaza chumba kizima nyumbani kwake Chato, kweli alijitayarisha ku loot!
 
Uongozi hapatikani kwa kujiandaa mzee
Wapo waliojiandaa na majina yao tunayajua
Uongozi ni kalama na kipawa ambacho super natural power decided (Mungu/Yesu) huamua nabi apewe nani asipewe
Ila hii haimaanishi usigombee su usijiandae kama unaweza fanya
Sasa Rais wetu alikuwa katulia zake home Kikatiba tukamuita sasa anakula nchi hadi 2030 hiyo
Sasa hapo ni utake usitake imeshakuwa hivyo tulia maisha yaendelee
Kikwete na Jpm walijiandaa nakubaluana na wewe kuwa unaweza kujiandaa akaangukua pua,na usijiandae ukaokota dodo
 
Naweza sema ni mzee Ruksa, Mkapa na mama Samia ndio waliokota dodo chini ya mnazi, Nyerere, Kikwete na Magufuli waliutafuta urais kwa mbinu zote chafu na safi.

Leo tumuangalia Rais Magufuli, Pompeo wa bongo alivyousaka urais kwa mbinu za chini kwa chini.

Hapo mwanzo kulikuwa na jimbo moja likiitwa Biharamulo mkoani Kagera, John Pombe aligombea na mtu anaitwa Kabuye, yule mzee alimpa wakati mgumu sana Magufuli, wengine hawajui kuwa Magufuli aliwahi kuangukia pua kwenye ubunge alivyogombea kwa mara ya kwanza,

Watu wa Biharamulo ambao wengi ni kutoka kabila la Abasubi hawakumpenda John walimuita Mnyamahanga kwa maana ya wakuja.

John akaomba mizimu yake jimbo likagawanywa , Biharamulo Mashariki na Magharibi, akakimbilia Mashariki kwenye wanyamahanga wengi.

Huko akapambana kiume na wapinzani wake kibabe mpaka wengine kukimbia jimbo.

Mwaka 2006 akafanikisha kuundwa kwa wilaya ya Chato na jimbo la Chato.

Baadae akapambana Chato ikatoka Biharamulo Kagera ikaingia mkoa wa Geita mwaka 2012, huo ulikuwa ushindi mkubwa sana kwa Magufuli, unajua sababu.

Chato kuwa mkoa wa Kagera ingemuharibia sana kisiasa, watu hudhani Kagera yote ni ya Wahaya na Wahaya hawapendwi nchii hii kubali kataa, hawaaminiki kupewa madaraka makubwa.

Nikutajie sasa makabila yanayopatikana wilaya ya Chato. **** Warundi wengi sana kutoka Burundi kuna Waha, Wasumbwa, Wasubi, Wazinza, Warongo, Wahaya ,Wasukuma na watu wa Musoma. Kila mtu anaona hapa ni kwake na wazee wengi hapa wanaongea hizo lugha zote, ndivyo ilivokuwa kwa Magufuli, yeye aliamua kujiita Msukuma ila hakuwa Msukuma, ilikuwa ni sababu za kisiasa tu.

Mpaka wa Chato sasa ukaambaa kutoka Mganza, Bwanga, Buseresere, Buziku, Buzirayombo nk hizo kata mtu unaamua tu kujiita kabila lolote kati ya hayo makabila niliyotaja.

Huu ulikuwa ni mpango mkubwa sana ulihitaji mchakato wa miaka 20 akazaliwa John mpya kabila Msukuma ,kwenye kampeni ya urais 2020 akafungia kampeni Mwanza akahutubia kwa kisukuma akazoa kura za wasukuma wote hata wa Bariadi na Shinyanga. Ingekuwaje angehutubia kwa lugha ya Kirundi au Kizinza lugha alizozimudu vizuri, au angehutubia kwa kihaya, bila shaka asingepata hizo kura za kanda ya ziwa, kura za wasukuma ambao ni wengi .

Mbinu ya pili aliyotumia ni kutaka kuonekana ni msomi mzuri kwa kutafuta PhD ili kujenga trust kwa watu kuwa yupo vizuri kitaaluma. Magu hakuwa kilaza darasani ila hakuwa kipanga, ile PhD ina ukakasi jinsi ilivyopatikana lakini zote ilikuwa ni maadalizi ya kugombea Urais.

Mkakati wa tatu ilikuwa ni kujifanya yeye ni masikini kumbe alikuwani tajiri mkubwa sana huwezi kuwa wizara ya ujenzi ukafa masikini, Kilometa moja ya lami ni zaidi ya bilioni 1.5 amesimamia kilometa nyingi sana zilizojengwa chini yake. Hii mbinu hata Kikwete aliitumia sana kujifanya masikini kumbe ni mabilionea, ujue Watanzania wengi hawawapendi matajiri hudhani wao ndio sababu ya wao kuwa masikini.kwa hiyo aliigiza kuwa yeye ni mnyonge na masikini kumbe uongo lengo ni kuteka akili za masikini ambao ndio wengi

Itaendelea.....
Ujue binadamu siku zote anapanga mambo yake lakini na Mungu anapanga yake ! Na ndio yatakayokua !!
 
Ujue binadamu siku zote anapanga mambo yake lakini na Mungu anapanga yake ! Na ndio yatakayokua !!
We lala usingizi sema Mungu anapanga,fortune goes to the brave ones
Omba Mungu huku ukichukua hatua utafanikiwa.
Kuandika maombi ya kazi au kuchukua fomu ya kugombea cheo,kuomba tenda ndio hatua hizo.nafasi za kuteuliwa bila kuomba zipo chache sana
 
Uongo mkubwa sana huu ulioandika hapa.
Uongozi hapatikani kwa kujiandaa mzee
Wapo waliojiandaa na majina yao tunayajua
Uongozi ni kalama na kipawa ambacho super natural power decided (Mungu/Yesu) huamua nabi apewe nani asipewe
Ila hii haimaanishi usigombee su usijiandae kama unaweza fanya
Sasa Rais wetu alikuwa katulia zake home Kikatiba tukamuita sasa anakula nchi hadi 2030 hiyo
Sasa hapo ni utake usitake imeshakuwa hivyo tulia maisha yaendelee
 
Uchambuzi umejitosheleza kabisa , Hayati JPM alijipanga haswaa japo alikuwa na mtihani mzito dhidi ya watoto wa mujini MEMBE, LOWASSA , KIKWETE nk , nguzo yake ilikuwa hayati MKAPA tu,
pia bila ugomvi baina ya Mh Kikwete na Lowassa ingekuwa tabu sana kutoboa.
 
Uongozi hapatikani kwa kujiandaa mzee
Wapo waliojiandaa na majina yao tunayajua
Uongozi ni kalama na kipawa ambacho super natural power decided (Mungu/Yesu) huamua nabi apewe nani asipewe
Ila hii haimaanishi usigombee su usijiandae kama unaweza fanya
Sasa Rais wetu alikuwa katulia zake home Kikatiba tukamuita sasa anakula nchi hadi 2030 hiyo
Sasa hapo ni utake usitake imeshakuwa hivyo tulia maisha yaendelee
Uko serious kweli? Ina maana Yesu ndio ameamua Mama Samia awe Rais? Rais Xi Jinping wa China alipewa na Yesu? Ebu acha ushamba ndugu!
 
Aiseh!sasa huyo jamaa Ndio TAYARI kaenda KWA Baba mwenyezi!sasa kwanini kumuandika!?

Rudi andika kuhusu mafanikio ya umeme na maji KWA awamu ya sita!!

Jinsi awamu hii inavopambana na UFISADI na UBADHIRIFU!

Acha kuandika marehemu andika waliopo sasa

Niandike HATA Mimi nilie hai jinsi ninavoweza kuivusha nchi nikishika hatamu!!
 
Aiseh!sasa huyo jamaa Ndio TAYARI kaenda KWA Baba mwenyezi!sasa kwanini kumuandika!?

Rudi andika kuhusu mafanikio ya umeme na maji KWA awamu ya sita!!

Jinsi awamu hii inavopambana na UFISADI na UBADHIRIFU!

Acha kuandika marehemu andika waliopo sasa

Niandike HATA Mimi nilie hai jinsi ninavoweza kuivusha nchi nikishika hatamu!!
Yesu amekufa miaka 2000 iliyopita ila bado biblia zinachapishwa sana ,na ndio kitabu kinaongoza kwa mauzo.
Shetani ana miska mingi sana ulimwenguni ila hatukomi kusoma habari zake .ungewajuaje hitler,stalin,musollin,iddi amini bila maandishi
 
Back
Top Bottom