Mnaojenga nyumba, kuweni makini na watu mnaowaomba wawalindie nyumba zenu

Mnaojenga nyumba, kuweni makini na watu mnaowaomba wawalindie nyumba zenu

Simbamteme

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2011
Posts
804
Reaction score
2,131
Wasalaam,

Naomba tu kutoa wito kwa wale wenzangu na mimi tunaojidunduliza ili kujenga nyumba za kuishi na familia zetu kuwa MAKINI sana na WATU tunaowaweka wawe walinzi wa nyumba zetu. Kuna tukio lilitokea hapa kitaani likaniacha Mimi na baadhi ya majirani tulioshuhudia tukio hilo kubaki midomo wazi

TUKIO LENYEWE:
Hapa ninapoishi nipo tokea Mwaka 1999 nikiwa mdogo sana..kuna nyumba kama ya 5 hivi kutoka hapa ninapokaa kuanzia mwaka huo 1999 ilikuwa imejengwa ila haikuwa imemalizika ndani madirisha na milango vilikwepo

Tokea mwaka 1999 hiyo nyumba ilikuwa hivyo hadi mwaka 2005 hivi kuendelea, mwenye nyumba akaizunguishia ukuta (ndani ilikuwa vilevile)

Ilikaa hvyo kwa miaka mingi kidogo then ikaanza kukarabatiwa na kufanyiwa finishing kali ikapendeza kweli

Sasa mwezi kama mmoja hivi uliopita tulisikia vurumati ndani ya hiyo nyumba, watu kutukanana, kugombana kwa sauti kali, ikabidi tujisogeze kujua nini shida

Ndipo yule jamaa aliekuwa anafoka kutuambia kuwa ile nyumba ni yake na huyo tuliemdhania kwamba anamiliki ile nyumba aliwekwa na huyo jamaa kama mlinzi tu

Ila baada tu ya kumuweka huyo jamaa kama mlinzi ALISAHAU kabisa kuhusu ile nyumba na hakuwahi kukumbuka kama ana ile nyumba mpaka alipobahatika kwenda kuombewa huko kwenye makanisa ya walokole (though alienda kwa shida nyingine).

Dunia ina mambo mengi sana, TUWENI MAKINI JAMANI
 
Kuna bro wangu ingawa scenario yake ni tofauti kidogo, yeye yupo nje alijenga nyumba yake Makongo halafu akaweka mlinzi kwa miaka kadhaa amlindie yule mlinzi. Baadaye bro alipotaka kuweka mpangaji jamaa akagoma akidai nyumba ni yake hawezi kutoka au alipwe ilikuwa issue nenda mpaka mahakamani huko ndiyo kushindwa akatolewa.
 
Unajua watu wengi hawafahamu kuwa wachawi wapo mjini mfano angalia nyumba nyingi ukianza kujenga ikafikia sehemu ya finishing ukaweka Mmasai mlinzi au Mmakonde na wengine ujue nyumba hiyo huwezi kuimalizia itakaa hivyo hivyo mda mrefu utakuwa umeisahau kabisa.

Mfano mimi nina nyumba buguruni barabara kubwa nina fremu 4 za maduka zipo tupu niliwahi kumpangisha mdada mmoja fremu mmoja. Na zingine nikawa sijapangisha kwa sababu nilikuwa naishi nje ya nchi ila kila 3 month nakuja Tanzania huyu mdada alipanga kwa miaka 4 lakini ajabu kila watu wakija kutaka fremu nilikuwa nakataa kupangisha moyo hautaki kabisa mdada huyu akapata fremu nyumba ya jirani akahama lakini mpaka leo sijapangisha zaidi ya miaka 10 fremu zote 4 na watu wananiijia kunibembeleza kupanga moyo unakataa mtaa wangu huu umechangamka sana maduka majirani wananishangaa sana kwa nini sipangishi na mpaka sasa nina shida ya pesa kulipa school fees ya mwanangu form 5.

Napata tabu kupata pesa na fremu ninazo na watu wanataka kupanga kila fremu laki 250 lakini nakataa naomba mniombee kila anaesoma maana kazi niliacha mda mrefu sana baada ya kuumia na umri pia.mimi najijua kuwa huyo mdada kanifanyia maana kila akiniona anatabasamu nakuniuliza hujapangisha tu au nirudi mimi
 
Unajua watu wengi hawafahamu kuwa wachawi wapo mjini mfano angalia nyumba nyingi ukianza kujenga ikafikia sehemu ya finishing ukaweka mmasai mlinzi au mmakonde na wengine ujue nyumba hiyo huwezi kuimalizia itakaa hivyo hivyo mda mrefu utakuwa umeisahau kabisa...
Wewe huna haja ya kuombewa. Acha kulialia kama mtoto mdogo. Ondoka katika usingizi mzito ulionao, nenda kapangishe hizo fremu.
 
Unajua watu wengi hawafahamu kuwa wachawi wapo mjini mfano angalia nyumba nyingi ukianza kujenga ikafikia sehemu ya finishing ukaweka mmasai mlinzi au mmakonde na wengine ujue nyumba hiyo huwezi kuimalizia itakaa hivyo hivyo mda mrefu utakuwa umeisahau kabisa..
Umendaa shule lakini akili yako haijaenda shule, hakuna uchawi wala nini huo ni ujinga wako tu na wala usimsingizie huyo dada unapata dhambi bure. Nyie ndio wale mnaoua vikongwe kwa imani za kishirikina kama hutaki kupangizwa ni ujinga wako.
 
Kwahiyo huyo jamaa miaka yote hiyo alikuwa akiishi wapi!

Hapo kuna watu wamekalia picha, wivu tu!
 
Back
Top Bottom