Mnaoondoa mabampa ya Plastiki kwenye gari na kuweka ya Chuma au Ngao mnajitafutia kifo cha kujitakia!

Mnaoondoa mabampa ya Plastiki kwenye gari na kuweka ya Chuma au Ngao mnajitafutia kifo cha kujitakia!

Farolito

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2018
Posts
12,001
Reaction score
27,175
Wakuu,

Kumekuwa na tabia ya wamiliki wa magari hasa magari binafsi kutoa mabampa(bumpers) ya mbele au nyuma na kuweka ya chuma wakiamini kwamba ndio gari itakuwa imara na Salama zaidi kama itapata ajali ya kugongana uso kwa uso au wakati mwingine wanaweka Ngao ya Chuma mbele wakiamini gari itakuwa ngumu na Salama kama itagonga mti au kitu kigumu lakini wanajidanganya,iko hivi;

Katika ajali,gari isiyovunjika au kukatika itakuwa ni majanga kwa abiria waliopo ndani.

Magari ya zama hizi yametengenezwa kuvunjika na kukatika vipande mbele na nyuma ili kupunguza nguvu ya mgongano(impact) kwa abiria waliopo ndani.

Hivyo gari zimetengenezwa katika mfumo wa 'crumple zones'(maeneo ya kuvunjikia) na hizi zipo mbele na nyuma na inaanzia pale ambapo bumpers za plastic zinaanzia,kwa mbele inaanzia kwenye bumper mpaka inapoishia injini,na nyuma pia inaanzia kwenye bumper mpaka inapoishia buti ya mzigo.

Pia bodi ya gari za sasa zimeungwa kwa vipande vya vyuma ambavyo hivi inapotokea impact huvunjika au kuchomoka kwa nje ili kunyonya(crumple) ile nguvu ya mgongano tofauti na gari za zamani ambazo bodi lilikuwa linaungwa na chuma linalounganisha gari nzima.

Kwahio bumpers zimewekwa laini ili gari inapogongana zivunjike au kupasuka na kuruhusu ile force iendelee kubomoa hizi crumple zones na wakati huohuo katika kuharibiwa ndio inayonya na kupunguza force kumfikia abiria ndani,kifupi hizo Bampa ni kama godoro linamzuia mtu aliyeanguka kutoka juu ya bati ambapo godoro ndio litabeba ile force aliyonayo muangukaji na hivyo kuzuia madhara kwake.

Kwahio unapoweka bumper la chuma au Ngao ni kwamba unazuia mchakato huu kufanyika na hivyo ile force ya mgongano moja kwa moja itakufikia wewe na kukuua.

Hii iliwekwa ili kuzuia kinetic energy kwa namna salama(Energy is force by distance) kwa hio ukiongeza distance unapunguza force.

Kwahio kunapotokea mgongano zile crumple zones zitapokea ile impact ya ajali na kuisafirisha katika maelfu ya viajali vidogo vidogo ili kupunguza ile nguvu ya mgongano mkuu kukufikia wewe uliyeko ndani kwa wakati mmoja.

Kwahio kila kipande cha bumper kilichopasuka au kila bati linalopinda jua limenyofoa ile nguvu ya ajali iliyokuwa ikufikie wewe,tofauti na hapo ile force ingekukuta wewe kama ilivyo.

Kanuni ya Fizikia inasema kwamba kama unaendesha kwa spidi ya 50 mph na ajali ikasababisha gari isimame ghafla,abiria aliyeko ndani ataendelea kusafiri kwa spidi ileile ya 50 mph.

Sasa hapa utaona jinsi ambavyo kama umeweka machuma ambavyo ni magumu ile force itakubamiza mbele kwa spidi gani kama uko 100 Kph au 120 kph,hapo ndio ule msemo wa utumbo kuchanganyika na maini utapokamilika au ubongo kupasuka kama ulifunga mkanda,na kama hukufunguka mkanda fikiria utaenda kutupwa kilomita ngapi kupitia kioo cha mbele kabla ya kufa.

Kwahio nashauri haya marekebisho ya kuweka chuma mbele muache,waliotengeza gari walipima ni namna gani gari itaumia ili kukulinda wewe uliyeko ndani ila wewe unataka uilinde gari isiumie bila kujali usalama wako.

Kama huamini fuatilia ajali za magari ya STK,STL nk, hasa za uso kwa uso uone ni wangapi huwa wanatoka salama,nyingi zimewekwa vyuma mbele.

Picha za maelezo zimeambatanishwa.

Asante.
images%20(17).jpg
images%20(18).jpg
images%20(19).jpg
IMG_20230506_070849.jpg
IMG_20230506_070941.jpg
 
Wakuu,

Kumekuwa na tabia ya wamiliki wa magari hasa magari binafsi kutoa mabampa(bumpers) ya mbele au nyuma na kuweka ya chuma wakiamini kwamba ndio gari itakuwa imara na Salama zaidi kama itapata ajali ya kugongana uso kwa uso au wakati mwingine wanaweka Ngao ya Chuma mbele wakiamini gari itakuwa ngumu na Salama kama itagonga mti au kitu kigumu lakini wanajidanganya,iko hivi;

Katika ajali,gari isiyovunjika au kukatika itakuwa ni majanga kwa abiria waliopo ndani.

Magari ya zama hizi yametengenezwa kuvunjika na kukatika vipande mbele na nyuma ili kupunguza nguvu ya mgongano(impact) kwa abiria waliopo ndani.

Hivyo gari zimetengenezwa katika mfumo wa 'crumple zones'(maeneo ya kuvunjikia) na hizi zipo mbele na nyuma na inaanzia pale ambapo bumpers za plastic zinaanzia,kwa mbele inaanzia kwenye bumper mpaka inapoishia injini,na nyuma pia inaanzia kwenye bumper mpaka inapoishia buti ya mzigo.

Pia bodi ya gari za sasa zimeungwa kwa vipande vya vyuma ambavyo hivi inapotokea impact huvunjika au kuchomoka kwa nje ili kunyonya(crumple) ile nguvu ya mgongano tofauti na gari za zamani ambazo bodi lilikuwa linaungwa na chuma linalounganisha gari nzima.

Kwahio bumpers zimewekwa laini ili gari inapogongana zivunjike au kupasuka na kuruhusu ile force iendelee kubomoa hizi crumple zones na wakati huohuo katika kuharibiwa ndio inayonya na kupunguza force kumfikia abiria ndani,kifupi hizo Bampa ni kama godoro linamzuia mtu aliyeanguka kutoka juu ya bati ambapo godoro ndio litabeba ile force aliyonayo muangukaji na hivyo kuzuia madhara kwake.

Kwahio unapoweka bumper la chuma au Ngao ni kwamba unazuia mchakato huu kufanyika na hivyo ile force ya mgongano moja kwa moja itakufikia wewe na kukuua.

Hii iliwekwa ili kuzuia kinetic energy kwa namna salama(Energy is force by distance) kwa hio ukiongeza distance unapunguza force.

Kwahio kunapotokea mgongano zile crumple zones zitapokea ile impact ya ajali na kuisafirisha katika maelfu ya viajali vidogo vidogo ili kupunguza ile nguvu ya mgongano mkuu kukufikia wewe uliyeko ndani kwa wakati mmoja.

Kwahio kila kipande cha bumper kilichopasuka au kila bati linalopinda jua limenyofoa ile nguvu ya ajali iliyokuwa ikufikie wewe,tofauti na hapo ile force ingekukuta wewe kama ilivyo.

Kanuni ya Fizikia inasema kwamba kama unaendesha kwa spidi ya 50 mph na ajali ikasababisha gari isimame ghafla,abiria aliyeko ndani ataendelea kusafiri kwa spidi ileile ya 50 mph.

Sasa hapa utaona jinsi ambavyo kama umeweka machuma ambavyo ni magumu ile force itakubamiza mbele kwa spidi gani kama uko 100 au 120,hapo ndio ule msemo wa utumbo kuchanganyika na maini utapokamilika au ubongo kupasuka kama ulifunga mkanda,na kama hukufunguka mkanda fikiria utaenda kutupwa kilomita ngapi kupitia kioo cha mbele kabla ya kufa.

Kwahio nashauri haya marekebisho ya kuweka chuma mbele muache,waliotengeza gari walipima ni namna gani gari itaumia ili kukulinda wewe uliyeko ndani ila wewe unataka uilinde gari isiumie bila kujali usalama wako.

Kama huamini fuatilia ajali za magari ya STK,STL nk, hasa za uso kwa uso uone ni wangapi huwa wanatoka salama,nyingi zimewekwa vyuma mbele.

Picha za maelezo zimeambatanishwa.

Asante.View attachment 2611618View attachment 2611619View attachment 2611620View attachment 2611621View attachment 2611622
Watakaokuelewa wachache lakini ndio ukweli.
 
Ni kweli kabisa
Ni kweli uliyoelezea, lakini hii kanuni inafanya kazi kwenye mazingira ya speed ndogo. Ndiyo maana siku zote tunaambiwa ''speed kali inaua''. Ukiwa kwenye mwendo mkali, na uko kwenye gari ndogo kwa mfano, uvaane na lori, lile lori litakusanya vi-crumple zones vyako vyote pamoja na wewe na kukusagasaga. Nakuunga mkono, ila nazidi kusisitiza tuendeshe magari kwa mwendo wa kawaida.
 
Safi sana mkuu,
Wengine wanaweka machuma kupambana na Boda, guta, Bajaj daladal na misuguano kwenye foleni... hii imekaaje.

Ila Toyota sio gari kwenye ajal ukilinganisha na mzung... yani Toyota inasambaratika in pices.
 
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂 109 mandolin
Hili tulikuwa nalo home miaka ya 94 mpaka early 2000s. Brake na clutch unakanyaga mara tatu halafu kila siku inaisha brake fluid kama huna unachukua sabuni ya mche unaiweka kwenye maji ikiwa uji uji ukoroga lile rojo unaweka kitu kinatambaa tu. Hakuna services za sijui 3000kms. Oil unaongeza kila mara kwa sababu inavuja kila siku so lazima ipungue sio kuongeza eti imeisha kms. Siku ikipiga starter unaiona mpya maana mara nyingi ni kusukumwa likastuliwa. Ila lilikuwa linakula mzigo balaa likishindwa panda mlima kwa forward linapanda kwa reverse. Landrover 109 noma
 
Back
Top Bottom