Mnaosujudu Israel, ni kipi hasa kinachofanya mlione ni taifa lenye watu wenye akili zaidi duniani?

Tangantika

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2018
Posts
5,586
Reaction score
7,087
Waisraeli wamerusha satellite mpya kwa dhumuni la ujasusi hasa kuichunguza Iran na teknolojia yao ya Mabomu ya Nyuklia.

Ni vipi waihofia Iran huku ninyi mnaowasujudu mnaamini kuwa wana akili sana kuliko mtu yoyote duniani. Kwanini wasiunde vifaa vya kufanya hayo mabomu ya Iran yawe maji ya kunywa?

Mnaosujudu Waisraeli kuwa wana akili sana, mbona sio nchi inaoongoza kuwa na akili zaidi katika top ten countries. Siyo nchi inayoongoza kuwa na smartest people on earth. Sio nchi inayoongoza kuwa na teknolojia mpya duniani.

Sio nchi inayoongoza kuwa na wanafunzi werevu zaidi duniani. Sio nchi inayoongoza kwa research papers duniani.

Sio nchi inayoleta teknolojia mpya zinazoshangaza dunia. Mfano Kompyuta, gari, treni za mwendokasi, ndege, mitandao. Vyote vimeanzia Ulaya na Marekani ndio Israel.

Akili yao ni ya ajabu sana. Mbona sioni kipya walichonacho ambacho Wazungu, Wamarekani hawana? Ninyi mnawapima vipi hizo akili nyingi zilizobarikiwa?
 
Mkuu, sijajua tatizo hapa ni nini?Wa Irani ni Waajemi kama walivyo wapalestina hawa ni maadui wa kihistoria. Kuhusu uwezo wa kiakili wa Waisrael hawana tofauti na wewe ila uwezo wao huo mdogo wanautumia kikamilifu kuhakikisha wana survive kama taifa.

Israel haina magenius ila wa self determination ya hali ya juu ambayo inafanya wahangaike kuhakikisha kuwa wanaendelea kuwepo.

Kuhusu watu kushabikia Israel, hizo ni matokea ya Propaganda tu ambazo huwa zinakuja kupitia dini na historia sioni tatizo hapo kama ambavyo inaonesha kwamba hata wewe kuna mambo fulani umelishwa dhidi ya Waisrael.

All in all tuwaze ya kwetu kwa sasa.
 
Mkuu AI ni matokea ya kazi za watu wengi sana.Zuckerber akiwa mmoja wao.Hakuna uhusiano kati ya ugunduzi huo na uisrael wake japo anazo akili nyingi.
 
Unajua muasisi wa AI. Nikusaidie..jina lake anaitwa John Mccarthy unajua asili yake.?
Mark asili yake pia Israel
Mkuu sijui kama una elewa. Acha kula propaganda. Tumia akili kuelewa mambo badala ya kusema tu kumeza.Unakuwa unatumika kusambaza propanda bila kujua. Zucker sio myahudi wa asili wala Mccarthy sio myahudi wa asili.

Kama umenielewa hapo basi utatambua kwamba wayahudi wa asili ni wachache sana na hawana utofauti wa kiakili na wewe. Kama unataka kufanya jambo kubwa unaweza. Chukua tu hatua.
 
Itakua nawe ni mmoja ya wasiopenda maendeleo ya Israelities. Kwenye Comments zangu hakuna sehemu nimesema Mccarthy na Zuckerberg ni wayahudi. Nimesema ni waisrael. Ukute hujui tofauti ya wayahudi na israelities
 
AI wanaoongoza no China inafuatia USA
 
AI wanaoongoza no China inafuatia USA
CHNA. In IQ ni wa 3, Kwa smart people ni 1 kwa Research paper ni 1, Ndio nchi yenye 5G.
Kwa uchumi mkubwa duniani ni ya 2. Hao unaowasujudia hata wajawazidi wachina hata Kimoja. Wenye akili sana hakuna wanaoongoza duniani kuliko wasio na akili how come?
 
Mambo yote yanayosomwa katika Biblia yanalihusu taifa hilo la Kiyahudi.

Pasi na shaka unalolifikiria limeanzia hapo na kuisha hapo.
 
Itakua nawe ni mmoja ya wasiopenda maendeleo ya Israelities. Kwenye Comments zangu hakuna sehemu nimesema Mccarthy na Zuckerberg ni wayahudi. Nimesema ni waisrael. Ukute hujui tofauti ya wayahudi na israelities
Dah!!Ngoja niachane na huu mjadala maana naona sasa tunakoelekea siko. Sizungumzii unachosema wewe wala sizungumzii tofauti ya Uyahudi na Uisrael.

Ninachozungumzia hapa ni issue ya kwamba wao wanajua kila kitu, wana akili kuliko kila mtu, Hiyo ni well planned propaganda ambayo binafsi nafikiri haina nafasi katika karne hii ya 21. Hayo mengine nafikiri hayana maana yoyote kwangu binafsi.
 
Nilitaka hii coment, ila umemaliza kila kitu.

Huko Marekani sijui Ulaya, Israeli ndio kila kitu.
 
Sawa ni propaganda lakini je hawana uwezo huo mkubwa.?
Tuweke hapa orodha ya watu wenye asili ya Israel ambao wamefanya makubwa. Au wanaushawishi zaidi duniani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…