Mnaotaka kufanya kazi na wanaojiita Nickshine Media Production kuweni makini sana

Mnaotaka kufanya kazi na wanaojiita Nickshine Media Production kuweni makini sana

Haina neno, tutajadili tuafikiane, shukrani sana kwa kunijibu vizuri
Tunaoffer packages za aina nne.

Kuna Basic, Ordinary, Advanced na Executive the lowest being Basic package and the highest ni Executibe package.

Basic Package inajumuisha:
  • Coverage ya event nzima kwa picha na video.
  • Projector 2 kwa ajili ya live shooting.
  • Albamu itakayokua na picha 160 size ya 5/7.
  • Nakala tatu za DVD.
  • Flash itakayokua na picha na video za tukio.

Kulingana na package kuna vitu vitaongezeka au vitabadilika ila ambacho hakitabadilika ni ubora wa picha na video zako na delivery ya kazi kwa mteja. Two weeks baada ya event tunakukabidhi mzigo wako.
 
Tunaoffer packages za aina nne.

Kuna Basic, Ordinary, Advanced na Executive the lowest being Basic package and the highest ni Executibe package.

Basic Package inajumuisha:
  • Coverage ya event nzima kwa picha na video.
  • Projector 2 kwa ajili ya live shooting.
  • Albamu itakayokua na picha 160 size ya 5/7.
  • Nakala tatu za DVD.
  • Flash itakayokua na picha na video za tukio.

Kulingana na package kuna vitu vitaongezeka au vitabadilika ila ambacho hakitabadilika ni ubora wa picha na video zako na delivery ya kazi kwa mteja. Two weeks baada ya event tunakukabidhi mzigo wako.
Shughuli ni simple, sitahitaji hizo projector, halafu ukitegemea upo dar, nauli kwangu,, naona hatutawezana ila umejitangaza wadau wanakusoma naamini utapata wateja,, kila la heri
 
Wengi nadhani ni shule ndogo na hawana exposure Mimi Kuna wapiga picha was chugga huwatafta na huwa nagharamia wako humble kazi zao nzuri huwa wanaendaga kupiga picha Hadi Nairobi na hawana longolongo hao vijana ila Hawa was Dar hamna kitu
Siyo wote una bahati mbaya umekutana na watu miyeyusho ila kama umewahi kusikia sehemu inaitwa Get Real Training ndipo timu yetu ilikutana tukiwa tunafanya mafunzo ya video production, shooting etc.

Baadhi walienda kwenye tamthilia maarufu ya Siri ya Mtungi na wengine tukasogea kwenye deals za kufanya still picture na shooting. So tunajua tunachofanya.
 
Shughuli ni simple, sitahitaji hizo projector, halafu ukitegemea upo dar, nauli kwangu,, naona hatutawezana ila umejitangaza wadau wanakusoma naamini utapata wateja,, kila la heri
Yea kweli kama ni hivyo itakupa unnecessary costs.
 
Kama wewe upo famous sana kwenye jamii, watumie vendors wenye majina kwasababu wataogopa kukuharibia na watatumia event yako kujitangaza, watakupa best services.

Ila kama wewe ni ngumbaru kama mimi, fanya kazi na ngumbaru wenzako unaowamudu kuwakoromea wakikuharibia kazi. Na wao watahakikisha wanapambana wakupe huduma bora ili uwarecommend wengine waende kwao.

Nimeshakutana na watu wengi wanawapapatikia vendors wenye majina waliangukia pua vibaya sana.

Ni list ndefu sana.
Eti ngumbaru[emoji1787]
 
Hizi Screenshots tunaweza kuprove kwamba ulikuwa unatuma kwa Nicki? Hata kublue Tick haijatick, namba ya Nicki akisoma inablue Tick.

Dada acha kua na spidi zisizo na maana, mimi tangu nachangia huu uzi nmesema kabisa vendor wangu hakua Nick, vendor aliyefanya kazi namimi hata akipitia huu uzi na kuona hizi screenshot ataelewa kuwa ni yeye maana kwangu na kwake kwenye simu zipo!! Na mimi sijataka kumtaja jina kwa sababu hata baada ya kutufanyia ubaya sikua na nia ya kuja kumleta huku kwenye mtandao na huu uzi haujaanzisha kwa ajili yangu, mimi nimechangia kutokana na kilichonikuta.
Alafu pia acha ushamba, namba ikisoma ina blue tick nini?? Mimi nmemute read recepients ingeblue tick kivipi? Kama hujui uliza.
 
Inawezekana huyo mtumaji ndiye mhusika ila anakuja kujifanya naye ni mhanga.

Mitandao hii ni balaa

Mimi sina haja ya kujieleza zaidi ya hapa ila naamini aliyefanya kazi ya shughuli yangu ya harusi akipita hapa ataelewa na naamini pia atabadilika for good. ( narudia tena kwa upande wangu mimi vendor hakua Nickshine).
 
Sina hamu na washona suti vijana wa kibongo, nikipata event yoyote bora ninunue nguo kuliko kwenda shona suti.

Mshona suti ambaye anaustaarabu angalau kwa upande wnagu naona ni Jm na Mtani kwakweli, wanazingatia muda wa kumaliza kazi ya mtu na hata kama pana excuse wanakujulisha, sitaki kukumbuka nilimsindikiza ndg yangu na kwa suti bega kushona suti ya shughuli yake yaliyotukuta tulikoma ni ahadi za njoo kesho njoo keshokutwa ikisindikizwa na kubadilishiwa aina ya kitambaa alichochagua na uzuri alipiga picha wakati anachagua[emoji3525][emoji847] .
 
So namfahamu NICK, aliwahi kufanya Wedding ya Rafiki yangu mwaka huu hapo Dar es Salaam. ALIFANYA KAZI HIYO KWA UBORA NA UAMINIFU
Nilipoona hii post niliamua kumtafuta sikumpata, lakini rafiki yangu ambaye alifanya naye kazi alimpata na kumuuliza kuhusu Uzi huu ulioweka.

Ndugu, uzi wako una kasoro na viashiria kwamba UNATAKA TU KUMCHAFUA NICK KWA SABABU ZAKO. Kasoro hizo ni;

1. Huelezi Nick kakukosea nini haswa. Uko too general husemi ulichofanywa.

2. Umetanguliza kujihami kwingi kwamba huandiki kwa nia mbaya, ilinipa hofu kuona kwamba unaweza kuwa na nia mbaya. Umemaliza pia kwa kusema utaletewa povu, why uletewe povu kweny jambo hilo?

Nicki amejieleza na kuomba wanajamvi wapime mambo yafuatayo:

1. Yeye sio biashara ya mtandaoni ambayo mtu anaweza kupata tabu kuifahamu. YEYE NI KAMPUNI, INA OFISI ZAKE ZIKO SINZA. Hivyo kama kweli una malalamiko kwake, ni rahisi kabisa kumkamata na kufungua kesi. So fara Ofisni kwake hakuna malalamiko ya hivyo unavyosema kwamba eti unashindwa kumpeleka mahakamani.

2. Nicki anahusisaha suala hili na vita za kibiashara kwa sababu YEYE ANAJITANGAZA SANA NA KUTOA HUDUMA KWA BEI NAFUU jambo ambalo washindani wake kwenye biashara linawakera sana. Mnaungana kumpiga vita.

3. Nicki amehusisha hili na TUZO, mnajua wenyewe mambo yenu ya tuzo ambazo mwaka jana Nicki alishinda. Mwaka huu tena yuko Nominated, hivyo kuelekea tuzo hizo mmeanza kuwekeana fitna.

MSICHAFUANE, MWENYE MALALAMIKO YA KWELI TUAMBIE ULIFANYWA NINI, NICKI YUPO OFISNI KWAKE TUELEZE KWA NINI HUJAMKAMATA?

Uzi wako una dalili zote za chuki za kibiashara, umekosa mashiko na ukweli wa hoja. ACHA.
Najiuliza iweje wewe ushindwe kumpata hewaaani huyo Nick ila rafiki yako ampate. Nick tulia.
 
Mshona suti ambaye anaustaarabu angalau kwa upande wnagu naona ni Jm na Mtani kwakweli, wanazingatia muda wa kumaliza kazi ya mtu na hata kama pana excuse wanakujulisha, sitaki kukumbuka nilimsindikiza ndg yangu na kwa suti bega kushona suti ya shughuli yake yaliyotukuta tulikoma ni ahadi za njoo kesho njoo keshokutwa ikisindikizwa na kubadilishiwa aina ya kitambaa alichochagua na uzuri alipiga picha wakati anachagua[emoji3525][emoji847] .

Washona suti wengi janja janja, wanapeleka kazi zao kwa mafundi ambao pia wanafanya kazi za kimtaa
 
Mimi sina haja ya kujieleza zaidi ya hapa ila naamini aliyefanya kazi ya shughuli yangu ya harusi akipita hapa ataelewa na naamini pia atabadilika for good. ( narudia tena kwa upande wangu mimi vendor hakua Nickshine).
Code za lugha yako inakukamatisha vizuri.

Endelea kufunguka
 
Habari za asubuhi wanajamvi

Siandiki waraka huu kuharibu Biashara ya mtu au kwa chuki ila kwa nia njema kuepusha wanajamvi wenzangu kutokewa na yaliyonitokea.Na hata kama itatafsirika vibaya ila wameyataka wenyewe kwa kuharibu siku za watu.

Hawa vijana kwa wasiowafahamu ni wapiga picha za Video na Mnato hasa kwenye sherehe mbalimbali na Maharusi,Wanatumia Media sana kujitangaza sana kuwa ni wabunifu na wameweza kufanya lobying na kuchukua tuzo mbalimbali kitu ambacho kimewajengea kuaminika na kufuatwa na watu wengi sana.

Ila niwatahadharishe wanajamvi na Wengine wenye nia njema msije mkaingia kwenye mkumbo wa hawa wahuni na vijana wa mjini mkaharibiwa shughuli zenu msiamini kabisa kwamba kuna wanadamu wana roho za ajabu na kushindwa kuwa na utu kiasi hicho.

Ninaongea kwa yaliyonikuta mimi binafsi baada ya ukaidi,Niweke wazi nilitahadharishwa lakini nikajenga imani kwa kuangalia namna wanavyojitangaza na kupewa tuzo nikajua ndivyo walivyo,nikawapa siku yangu muhimu kabisa maishani ya kufunga ndoa yangu wanifanyie kazi ya Still picture na Video.

Aisee hawa vijana ni wahuni walichukua hela zangu wakaniharibia siku yangu walivuruga kazi zote pamoja na gharama kubwa walizochaji karibu vitu vingi wanavyoweka kwenye vipeperushi vyao ni utapeli havifanyiki na hivyo vichache wanavyoamua kuvifanya wao kwa matakwa yao huvipati utafuatilia miaka mimi nimeamua kuwaachia lakini nikiwa nimeumia sana.

Changamoto niliyoipata mimi sikuingia nao Mkataba nilikuwa nafanya malipo tu wananipa virisiti vyao vya Vitabu kwasababu ni wakwepa kodi pia nikashindwa hata kuwashtaki ila kwa jinsi walivyoniharibia shughuli yangu ningewapeleka mahakamani kama ningekuwa na Mkataba,Niwashauri wenye shughuli zenu ingieni tu Mkataba wa kisheria na Mavendors.

Kilichoniuma nilikuta watu wengi sana pale Ofisini kwao kila nikienda wanalalamika kufanyiwa vitu tofauti na makubaliano,kushindwa kupatiwa kazi zao,kuharibiwa shughuli zao nk niliumia sana kwasababu na mimi niliambiwa na dada mmoja nje wakati naenda kuwa ni wasumbufu nikakaidi baada ya kuwasikiliza manake wana sound balaa ikala kwangu.

Narudia nimeandika kwa nia njema ya kuzuia wengine wasitapeliwe au yasiwakute yaliyonikuta mimi,sherehe yangu ya harusi ambayo niliipanga kwa gharama kubwa sana na ndiyo siku yangu ya kipekee baada ya hapo ni kifo iliharibiwa na hawa wahuni,na kumbukumbu sina hadi leo kama mnavyojua picha ndiyo kumbukumbu zinazobakia.

Kwa jinsi nilivyoumia sipendi mtu mwingine aumie kama mimi au afanyiwe nilivyofanyiwa nimeona nina wajibu wa kutoka kushare na wenzangu.

Naruhusu povu kwa wenye upeo mdogo na watu wa kuchukulia mambo negative nimeshawasamehe ila wenye kuniona positive hii post itawasaidia.
Mkuu kwani unakimbizwa au unadhani kila mtu anawajua hao watesi wako, unapoleta habari ungetuambiwa wako wapi,ni kipi uliharibiwa na makubaliano yenu yalikuwaje? hii story imekuwa nyepesi sana haina uzito na mwisho tutaona kama ni vita vya kibiashara tu.
 
Back
Top Bottom