Wana ubalozi nchi gani ya nje?!
Umeshawahi kujiuliza impact ya wazanzibari wooote kuhamia Bara au Wabara wooote kuhamia Zanzibar?Hadi leo sijajua, kwamba wazanzibar wanamiliki ardhi ya bara kwa uhuru wote, ila sisi tukienda kule tunafanywa wawekezaji hakuna kumiliki kwa haki sawa kama wao wakija huku. wazanzibar wameajiriwa kwenye serikali huku bara lakini marufuku kuajiri mbara kule kwao. si ujinga huu?
Kama ardhi kule ndogo wahamie huku na wawauzie wabara wenye mitaji wawekeze kule kwa nini wabara wakose fursa kule wakati wao wanafursa huku.Hadi leo sijajua, kwamba wazanzibar wanamiliki ardhi ya bara kwa uhuru wote, ila sisi tukienda kule tunafanywa wawekezaji hakuna kumiliki kwa haki sawa kama wao wakija huku. wazanzibar wameajiriwa kwenye serikali huku bara lakini marufuku kuajiri mbara kule kwao. si ujinga huu?
Misifa tu ilimponzaMuungano wa hovyo kabisa uvunjwe, upo sahihi mkuu
Zanzibar itapataje sehemu kubwa ya bahari wakati kuanzia tanga mpaka mtwara ni km ngapi za coast line ya Tanganyika. Pia umesahau kuna ukingo pia pale mafia island hawana uwezo wa kuendelea kumiliki chini ya mafia ktk ya mafia na znz ni nusu kwa nusuNadhani Tukitengana tutapoteza sehemu kubwa ya eneo la bahari na zanzibar itapaa kiuchumi kupitia marafiki zao waarabu.
In short kujitenga kuna manufaa makubwa sana kwa Zanzibar kukiko Tanganyika.
Mkuu, nikuhakikishie, hili busu la Tanganyika na Zanzibar halitenguliwi ng'o; pamoja na huo unaousema nchi changa.Hong Kong na China wana historia ndefu. Historia ya Tanzania kama taifa ilianza 1964, ni nchi changa. Huwezi kulinganisha China na Tanzania. Kuachana kunawezekana sana kwenye nchi hizi changa, Sudan wameachana na Sudan Kusini. Kule Iraq unaona wale WaKurds wanataka nao kuachana na Iraq waendelee na Kurdistan, Syria vile vile. Tatizo ni kutambulika kimataifa, international legitimacy. Je Zanzibar kama nchi itakubalika kule UN?
Jiografia mbona ipo pia baina ya Tanzania na nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi lakini hakuna muungano? Kwa nini Muungano wa Zanzibar ndiyo muhimu zaidi?Mkuu, nikuhakikishie, hili busu la Tanganyika na Zanzibar halitenguliwi ng'o; pamoja na huo unaousema nchi changa.
Jiografia hii iliyopo kati ya Tanganyika na Zanzibar huwezi kuifumbia macho. Hiyo historia ya waarabu haiwezi kuja huku kuondoa uhakika wa visiwa hivyo kuwa sehemu ya bara.
Waarabu walipokuja hawakutuuliza mahusiano kati yetu tokea enzi na enzi, kwa nini historia hiyo iwe pingamizi la uhusiano wa jadi?
Mkuu Mwanajeshi wa Angani, sky soldier , kwanza asante kujikubali wewe ni mjinga, kutokana na maono mafupi kuwa Zanzibar inatunyonya, hivyo kupatwa na hasira. Uzuri wa kujikubali ujinga, ni ukielimishwa, ujinga utakutoka, hivyo karibu hili darsa langu.Naombeni wenye jicho la ziada mnitoe ujinga maana huu ujinga nilionao ndio unanifanya niwe napatwa na hasira kwa maono mafupi yanayonifanga nione Zanzibar inatunyonya
Si mara moja wala mbili, niliwahi kusisitiza humu, Watanzania waelimishwe historia ya muungano, chanzo halisi ni nini na ni nani. Japo ni kweli waasisi wa muungano wetu huu adhimu ni Nyerere na Karume, lakini kuna chanzo, sababu, na mtu aliyemuanza mwenzake kutaka muungano. Kwanza futa hiyo kauli kuwa Nyerere "alimbembeleza sana Karume kuwe na muungano", ni kauli ya kijinga tuu kwa kutokujua, hivyo Wazanzibari wengi na wasioutakia mema muungano wetu kudhani chanzo ni Nyerere!.Tukubali kwamba wazanzibar "WALITUZIDI AKILI" na wanafaidi mno muungano bila kujijua.
Kwa upeo wangu nimegundua Karume alimzidi akili Nyerere, Alipoona kwamba Nyerere anambembeleza sana kuwe na muungano, Karume akatumia nafasi hii kumbana Nyerere aipe Zanzibar upendeleo kama huu tunaouona ama sivyo hakuna muungano,
Miungano yote duniani ni kama ndoa, kuna give and take, na siku zote kwenye muungano wa the majority na minority, siku zote the minority ndio anafaudu. Zanzibar ni the minority. Ndani ya structure hii ya muungano, Tanzania ni nchi moja, ndani ya nchi moja hii kuna uraia mmoja tuu, uraia wa Tanzania, hivyo kila Mtanzania ni Mtanzania tuu, hakuna Mtanzania Bara wala Mzanzibari, kuna raia mmoja tuu , Mtanzania, hivyo Wazanzibari wote wana haki zote za Utanzania swa na Mtanzania mwingine yoyote ikiwemo kumiliki ardhi, ajira, uongozi na kila kitu, yaani kila Mzanzibari ni Mtanzania mwenye haki zote.Pia akaongezea kipengere kwamba endapo kukiwa na muungano basi Zanzibar iwe kwajili ya Zanzibar lakini Tanganyika ibanwe iwe kwajili ya wote, Kwa lugha nyepesi "changu ni changu ila chako tutagawana" matokeo yake leo Tanganyika tunashuhudia inapigwa nje ndani na wazanzibar,
Hao Wanzanzibari wanaolalamika wananyonywa nao ni wajinga tuu kama Watania wanaolalamika wananyonywa. Muungano wetu ni wa milele!. Hauwezi kufa kwasabu tutaulinda kwa gharama yoyote.haya malalamiko kutoka Zanzibar kwamba wananyonywa yaliwekwa kimkakati ili iwe silaha kwa wazanzibar kuridhika na kujitapa kwamba wametuzidi akili, ingekuwa hivi muungano ungekufa mapema.
Hii pia sii kweli, kwenye muungano wote tunanufaika, ila pia ni ukweli usiopingingika the minority anafaudu zaidi!.lakini pia haya malalamiko yapo kimkakti kuizubaza Tanganyika idhani kwamba Zanzibar ni kama mkoa wake kumbe kiukweli wazanziba ndio wanaonufaika.
Nami nimefaidi .binafsi sijawahi kumsikia mzanzibar akijitambulisha kama mtanzania sijui hii imekaaje. Pili unadhani muungano ukifa mwarabu anaweza kurudi? Una habari huyo mwarabu alokimbilia uingereza kwamba bado anajipa hadhi ya kuwa mtawala wa Zanzibar ?Mkuu Mwanajeshi wa Angani, sky soldier , kwanza asante kujikubali wewe ni mjinga, kutokana na maono mafupi kuwa Zanzibar inatunyonya, hivyo kupatwa na hasira. Uzuri wa kujikubali ujinga, ni ukielimishwa, ujinga utakutoka, hivyo karibu hili darsa langu.
Si mara moja wala mbili, niliwahi kusisitiza humu, Watanzania waelimishwe historia ya muungano, chanzo halisi ni nini na ni nani. Japo ni kweli waasisi wa muungano wetu huu adhimu ni Nyerere na Karume, lakini kuna chanzo, sababu, na mtu aliyemuanza mwenzake kutaka muungano. Kwanza futa hiyo kauli kuwa Nyerere "alimbembeleza sana Karume kuwe na muungano", ni kauli ya kijinga tuu kwa kutokujua, hivyo Wazanzibari wengi na wasioutakia mema muungano wetu kudhani chanzo ni Nyerere!.
Chonzo Halisi cha Muungano ni Karume, Nyerere Akamalizia!.
Baada ya yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yaliyomng'oa Sultani, Sultani alikimbilia Uingereza, na kuomba msaada, zikatumwa meli vita kuja kuadabisha Zanzibar ili kumrejesha Sultani. Karume ndio akavuka maji, kuja Bara, kumuomba Nyerere ulinzi ili Tanganyika iliilinde Zanzibar dhidi ya kipigo cha Mungereza kinachofuata na kumrejesha Sultani!.
Sasa katika kuwaza na kuwazua Tanganyika itaisaidia kuilinda vipi Zanzibar dhidi ya Uingereza?, ndipo Mwalimu akatoa wazo, "tuungane". Karume akakubali hapo hapo na kusema "Tuungane hata leo, wewe rais, mimi makamu". Karume alidhamiria muungano wa nchi moja na alitaka utangazwe kesho yake!. Ni Nyerere alimkatalia, kutokana na Tanganyika kuwa ni li nchi likubwa, tukiungano kuwa nchi moja, itaonekana Tanganyika imeimeza Zanzibar, hivyo ni Nyerere ndio alimkatalia Karume muungano wa nchi moja na kuipatia Zanzibar status ya "the minority" kwenye muungano huu. Hivyo chanzo cha muungano ni Zanzibar, alitaka ulinzi, aliyemuanza mwenzie ni Karume, Nyerere alimalizia!.
Miungano yote duniani ni kama ndoa, kuna give and take, na siku zote kwenye muungano wa the majority na minority, siku zote the minority ndio anafaudu. Zanzibar ni the minority. Ndani ya structure hii ya muungano, Tanzania ni nchi moja, ndani ya nchi moja hii kuna uraia mmoja tuu, uraia wa Tanzania, hivyo kila Mtanzania ni Mtanzania tuu, hakuna Mtanzania Bara wala Mzanzibari, kuna raia mmoja tuu , Mtanzania, hivyo Wazanzibari wote wana haki zote za Utanzania swa na Mtanzania mwingine yoyote ikiwemo kumiliki ardhi, ajira, uongozi na kila kitu, yaani kila Mzanzibari ni Mtanzania mwenye haki zote.
Lakini ndani ya the majority ya Utanzania, kuna the minority ya Uzanzibari, ambao ni special kwajili ya Wazanzibari pekee, hivyo kila Mzanzibari, kwanza ni Mtanzania, kisha ni Mzanzibari, lakini sio kila Mtanzania ni Mzanzibari, Mtanzania ni Mtanzania tuu Wazanzibari wakiwemo, ila Mzanzibari ni Mtanzania ambaye pia ni Mzanzibari, an added advantage!.
Hao Wanzanzibari wanaolalamika wananyonywa nao ni wajinga tuu kama Watania wanaolalamika wananyonywa. Muungano wetu ni wa milele!. Hauwezi kufa kwasabu tutaulinda kwa gharama yoyote.
Hii pia sii kweli, kwenye muungano wote tunanufaika, ila pia ni ukweli usiopingingika the minority anafaudu zaidi!.
Mwisho.
Muungano kama ndoa!.
Hili naomba nisilifafanue lisije likawatia watu hasira, ila siku hizi kuna wanaume wa ajabu, mtu anaoa mke, ana jukumu la kumhudumia, lakini anamuonea wivu eti mke anafaidi kula bure, kulala bure, lakini anasahau zile huduma ambazo zinalipiwa na kugharimikiwa. Ndani ya ndoa nani anafaidi zaidi au kufaudu zaidi?.
P
Huu ujinga mim ndo staki Et security reason , Hao wazanzibar ndo wanatulinda Kuna Kilomita 200 za bahari za kwetu baharini , hata Kama US, China, Russia akitaka kutupiga anashindwa, anaweza kutupiga hata akiwa kwo inshort Muungano ni Nonsense kabisa siku nikiwa raisi ni serikali Tatu au kuvunja Muungano basiTatizo nyie vijan hamuelewi, Nyerere aliona mbali sana for security reasons kwasababu hata leo hii zanzbar wakijitenga hawata survive coz watakua week kijeshi kitendo cha nyerere kuleta muungano ni kutaka ku access eneo kubwa la bahari ya hind
Hio siku ikifika utakuwa ushakufa zamani sana, ni miaka 2000 ijayo, ila kama kweli upo serious unataka kuishuhudia basi anza ule ubaguzi wa kiafrika Kusini dhidi ya wapemba na waunguja , anza Harakati za kuwatimua.binafsi najua hili litaibuka tu kwenye kampeni za uchaguzi 2025, ni madukuduku yamekaa mioyoni mwa wabara miaka mingi, na ukweli ni kwamba pamoja na kwamba wazenji wanalialia kila wakati, kwa jinsi walivyojiwekeza huku bara, muungano ukifa wao watapata hasara na maumivu makubwa kuliko hata sisi. naisubiri sana hiyo siku watembee kwa mguu hadi zanzibar.