Mnyika: Bavicha ngazi zote kuanzia taifa hadi Msingi undeni kamati za kudai Katiba mpya kabla hatujaingia rasmi mitaani!

Mama anachezewa sharubu
 
Nadhani wamemuona ni Mtu Mstaarabu anaweza kuwasikiliza. Hata kama watatumia njia ambazo siyo formal....
 
Udhalimu wa marehemu ndiyo ulioamsha hamasa ya kudai katiba mpya, ili kuzuia viongozi wa aina ya marehemu, kuja kuongoza watu wenye akili timamu.
 
Hao punguani wanaoendeshwa na mihemko, achana nao. Hawajitambui. Ni lini na ni vita gani kiongozi alikaa mstari wa mbele. Kiongozi siku zote jukumu lake kubwa ni kuwaunganusha wananchi kupigania a common interest.
 
Hao punguani wanaoendeshwa na mihemko, achana nao. Hawajitambui. Ni lini na ni vita gani kiongozi alikaa mstari wa mbele. Kiongozi siku zote jukumu lake kubwa ni kuwaunganusha wananchi kupigania a common interest.
Mbona Tundu Lisu pale Kibaha alikaa mstari wa mbele akipambana na mapolisi?!!
 
Samahani mkuu, hivi yale maandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi ya ndugu yetu Lissu ulijitokeza? Na yalifanyikia mitaa ipi vile naomba kukumbushia kidogo.
 

Samahani Mkuu...
Wanataka kudai katiba Mpya au Serikali 3?
Nieleweshe Mkuu
 
Mzee hapa tunafurahisha baraza tu hakuna muandamanaji hapo
 
Kumbe wewe ni mwanaccm huru , barikiwa sana
 
Hilo neno kuingia mitaani lina ukakasi sana sababu mitaani kuna watu kila siku.
 
Hilo neno kuingia mitaani lina ukakasi sana sababu mitaani kuna watu kila siku.

Hiyo itakuwa ni kutoa elimu ya umuhimu wa katiba mpya mtaa kwa mtaa, nyumba Hadi nyumba...

Maandamano ni pale elimu itakapo mfikia kila raia...
 

Kuna ugomvi gani mpaka useme kuna kuvunjwa miguu? Ww ndio wale wajinga msiojua haki zenu, na ndio mnawapa viongozi viburi wanaishia kutumia nguvu kwenye madai halali ya wananchi. Usiwe lofa boss.
 
Mtu makini hawezi kuamini kuwa Tanzani kuna upinzani. Kuna magenge ya wahuni tu na matapeli. Nchi haifanyiwi majaribio. Wanaowatuma kujaribu nguvu za mamlaka zilizowekwa kisheria mtarudi muwape salam zao.
 
Samahani mkuu, hivi yale maandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi ya ndugu yetu Lissu ulijitokeza? Na yalifanyikia mitaa ipi vile naomba kukumbushia kidogo.

Hakuna mtu angeandamana wakati dhalimu alishaagiza watu wauwawe. Watanzania kwa asili yako ni watu wa kumuachia Mungu na huishia kusimanga. Na si kila kitu hutokea mara moja, mambo mengine ni mchakato. Lakini uzuri ni kuwa mbegu ya watu kuandamana imeshapandwa, kama si leo basi haiko mbali. Mfano angalia makondoo wa hapo Eswatini walikuwa ni mateka wa mfalme. Umeona kilichotokea siku mbili hizi? Huko Zimbabwe Mugabe aligeuza watu wote ni mandondocha hakuna aliyekuwa anakohoa. Lete mrejesho wa kipi kilimkuta?

Maandamano kutokufanyika juzi haimaniishi watu waliridhika na kilichofanyika, ila udhubutu ndio bado. Kwa sasa chukulia ule ukatili na uoga ni ushindi, lakini iko siku hutaamini macho yako, utatamani siku zirudi nyuma.
 
Chadema ni failed opposition party.Ila kwa hapa tanzania kina ka unafuu kuliko wengine
 
Mtu makini hawezi kuamini kuwa Tanzani kuna upinzani. Kuna magenge ya wahuni tu na matapeli. Nchi haifanyiwi majaribio. Wanaowatuma kujaribu nguvu za mamlaka zilizowekwa kisheria mtarudi muwape salam zao.
Hata Elbashir alitawala kwa jeuri kama hii hii unayotambia leo. Wapambe wake kama ww walikuwa wanasema nchi yao haifanyiwi majaribio, leo hayuko madarakani bali yuko jela, na nchi inaendeshwa na watu wengine ambao hakuwakabidhi.
 
Nyooooo!!!
Kwa Magu!!

aliwaambia wajaribu kumwaga hata mkojo tu acha damu waone.

Nilipenda utawala wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…