Mnyika: Bavicha ngazi zote kuanzia taifa hadi Msingi undeni kamati za kudai Katiba mpya kabla hatujaingia rasmi mitaani!

Mnyika: Bavicha ngazi zote kuanzia taifa hadi Msingi undeni kamati za kudai Katiba mpya kabla hatujaingia rasmi mitaani!

Katibu mkuu wa Chadema J J Mnyika amevitaka vikao vyote vya kikatiba vya Bavicha kuanzia Taifa hadi Msingi kuandaa kamati za kudai Katiba mpya.

Mnyika amesema ni vema wakajipanga sawasawa kabla ya kuingia rasmi mitaani kushinikiza uundwaji wa katiba mpya.

Nawasalimu kwa jina la JMT!
Mama anachezewa sharubu
 
Hawa watu wanajaribu kupimana ubavu na rais,kuwa fair kwa vyama vya kihuni huni Kama chadema ni kuliangamiza taifa,

Rais Hana budi kubadili mikakati ya kudili na vyama vya kihuni huni Kama hivi ili kuliepusha taifa kuingia kwenye machafuko.

Walikuwa wapi kudai katiba enzi za JPM,why now ,je wamemuona rais ni mtu dhaifu kwao hivyo ni muda muafaka wa kuanzisha chokochoko?

Chadema nawahakikishia kile mnachokitafuta hakika mutakipata muda si mrefu,wait and see.
Nadhani wamemuona ni Mtu Mstaarabu anaweza kuwasikiliza. Hata kama watatumia njia ambazo siyo formal....
 
Hawa watu wanajaribu kupimana ubavu na rais,kuwa fair kwa vyama vya kihuni huni Kama chadema ni kuliangamiza taifa,

Rais Hana budi kubadili mikakati ya kudili na vyama vya kihuni huni Kama hivi ili kuliepusha taifa kuingia kwenye machafuko.

Walikuwa wapi kudai katiba enzi za JPM,why now ,je wamemuona rais ni mtu dhaifu kwao hivyo ni muda muafaka wa kuanzisha chokochoko?

Chadema nawahakikishia kile mnachokitafuta hakika mutakipata muda si mrefu,wait and see.
Udhalimu wa marehemu ndiyo ulioamsha hamasa ya kudai katiba mpya, ili kuzuia viongozi wa aina ya marehemu, kuja kuongoza watu wenye akili timamu.
 
Uko sahihi sana, hata wakati wa vita vya Uganda wananchi walikuwa tayari, je Nyerere alikuwa mstari wa mbele huko vitani? Hawa askari wote wanaokwenda kulinda amani sehemu zenye vita, viongozi wanaosaini hiyo mikataba na wao huwa wanaenda huko kwenye vita wao na familia zao? Kwenye mechi za soka huwa kunakuwa na kocha, je huwa naye anaingia uwanjani kucheza?

Hizi lugha za kijinga ndio hutengenezea uhalali wa viongozi kusigina haki na maslahi ya watu. Ndio maana unaona viongozi wanaoishi hapa Dar wanatembelea maVX ya 400m+, huku wao wakiwa na maji safi ya kuflash mpaka vinyesi, wakati huko vijijini watu wakosa hata kisima cha maji cha 50m tu. Na mleta post unaona umepost kitu cha maana kwelikweli.
Hao punguani wanaoendeshwa na mihemko, achana nao. Hawajitambui. Ni lini na ni vita gani kiongozi alikaa mstari wa mbele. Kiongozi siku zote jukumu lake kubwa ni kuwaunganusha wananchi kupigania a common interest.
 
Hao punguani wanaoendeshwa na mihemko, achana nao. Hawajitambui. Ni lini na ni vita gani kiongozi alikaa mstari wa mbele. Kiongozi siku zote jukumu lake kubwa ni kuwaunganusha wananchi kupigania a common interest.
Mbona Tundu Lisu pale Kibaha alikaa mstari wa mbele akipambana na mapolisi?!!
 
Uko sahihi sana, hata wakati wa vita vya Uganda wananchi walikuwa tayari, je Nyerere alikuwa mstari wa mbele huko vitani? Hawa askari wote wanaokwenda kulinda amani sehemu zenye vita, viongozi wanaosaini hiyo mikataba na wao huwa wanaenda huko kwenye vita wao na familia zao? Kwenye mechi za soka huwa kunakuwa na kocha, je huwa naye anaingia uwanjani kucheza?

Hizi lugha za kijinga ndio hutengenezea uhalali wa viongozi kusigina haki na maslahi ya watu. Ndio maana unaona viongozi wanaoishi hapa Dar wanatembelea maVX ya 400m+, huku wao wakiwa na maji safi ya kuflash mpaka vinyesi, wakati huko vijijini watu wakosa hata kisima cha maji cha 50m tu. Na mleta post unaona umepost kitu cha maana kwelikweli.
Samahani mkuu, hivi yale maandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi ya ndugu yetu Lissu ulijitokeza? Na yalifanyikia mitaa ipi vile naomba kukumbushia kidogo.
 
Katibu mkuu wa Chadema J J Mnyika amevitaka vikao vyote vya kikatiba vya Bavicha kuanzia Taifa hadi Msingi kuandaa kamati za kudai Katiba mpya.

Mnyika amesema ni vema wakajipanga sawasawa kabla ya kuingia rasmi mitaani kushinikiza uundwaji wa katiba mpya.

Nawasalimu kwa jina la JMT!

Samahani Mkuu...
Wanataka kudai katiba Mpya au Serikali 3?
Nieleweshe Mkuu
 
Sawa nenda ukaandamane uvunjwe mguu huku viongozi wa chadema hawana muda na wewe.

Bogus lema alivotoka jela alikuja na nyimbo kuwaimbia watu kwenye viwanja vya samunge Arusha mjini sasa na ww ukivunjwa mguu wakati wazazi wako wanapambana hospitali viongozi wa chadema wanakutungia nyimbo
Mzee hapa tunafurahisha baraza tu hakuna muandamanaji hapo
 
Katibu mkuu wa Chadema J J Mnyika amevitaka vikao vyote vya kikatiba vya Bavicha kuanzia Taifa hadi Msingi kuandaa kamati za kudai Katiba mpya.

Mnyika amesema ni vema wakajipanga sawasawa kabla ya kuingia rasmi mitaani kushinikiza uundwaji wa katiba mpya.

Nawasalimu kwa jina la JMT!
Kumbe wewe ni mwanaccm huru , barikiwa sana
 
Hilo neno kuingia mitaani lina ukakasi sana sababu mitaani kuna watu kila siku.
 
Hilo neno kuingia mitaani lina ukakasi sana sababu mitaani kuna watu kila siku.

Hiyo itakuwa ni kutoa elimu ya umuhimu wa katiba mpya mtaa kwa mtaa, nyumba Hadi nyumba...

Maandamano ni pale elimu itakapo mfikia kila raia...
 
Sawa nenda ukaandamane uvunjwe mguu huku viongozi wa chadema hawana muda na wewe.

Bogus lema alivotoka jela alikuja na nyimbo kuwaimbia watu kwenye viwanja vya samunge Arusha mjini sasa na ww ukivunjwa mguu wakati wazazi wako wanapambana hospitali viongozi wa chadema wanakutungia nyimbo

Kuna ugomvi gani mpaka useme kuna kuvunjwa miguu? Ww ndio wale wajinga msiojua haki zenu, na ndio mnawapa viongozi viburi wanaishia kutumia nguvu kwenye madai halali ya wananchi. Usiwe lofa boss.
 
Mtu makini hawezi kuamini kuwa Tanzani kuna upinzani. Kuna magenge ya wahuni tu na matapeli. Nchi haifanyiwi majaribio. Wanaowatuma kujaribu nguvu za mamlaka zilizowekwa kisheria mtarudi muwape salam zao.
 
Samahani mkuu, hivi yale maandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi ya ndugu yetu Lissu ulijitokeza? Na yalifanyikia mitaa ipi vile naomba kukumbushia kidogo.

Hakuna mtu angeandamana wakati dhalimu alishaagiza watu wauwawe. Watanzania kwa asili yako ni watu wa kumuachia Mungu na huishia kusimanga. Na si kila kitu hutokea mara moja, mambo mengine ni mchakato. Lakini uzuri ni kuwa mbegu ya watu kuandamana imeshapandwa, kama si leo basi haiko mbali. Mfano angalia makondoo wa hapo Eswatini walikuwa ni mateka wa mfalme. Umeona kilichotokea siku mbili hizi? Huko Zimbabwe Mugabe aligeuza watu wote ni mandondocha hakuna aliyekuwa anakohoa. Lete mrejesho wa kipi kilimkuta?

Maandamano kutokufanyika juzi haimaniishi watu waliridhika na kilichofanyika, ila udhubutu ndio bado. Kwa sasa chukulia ule ukatili na uoga ni ushindi, lakini iko siku hutaamini macho yako, utatamani siku zirudi nyuma.
 
Chadema ni failed opposition party.Ila kwa hapa tanzania kina ka unafuu kuliko wengine
 
Mtu makini hawezi kuamini kuwa Tanzani kuna upinzani. Kuna magenge ya wahuni tu na matapeli. Nchi haifanyiwi majaribio. Wanaowatuma kujaribu nguvu za mamlaka zilizowekwa kisheria mtarudi muwape salam zao.
Hata Elbashir alitawala kwa jeuri kama hii hii unayotambia leo. Wapambe wake kama ww walikuwa wanasema nchi yao haifanyiwi majaribio, leo hayuko madarakani bali yuko jela, na nchi inaendeshwa na watu wengine ambao hakuwakabidhi.
 
Kwa taarifa yako hata rais mumjaze mtakavyo hata ikibidi kuifuta cdm, bado katiba mpya itapatikana. Hata angefufuka Magufuli leo hii bado katiba mpya ingepatikana. Na vile alikuwa ameshaangusha uchumi, tena yeye ingepatikana hata kwa machafuko. Hitaji la katiba mpya ni la wakati, halikwepeki kwa hila wala mabavu. Someni alama za nyakati.
Nyooooo!!!
Kwa Magu!!

aliwaambia wajaribu kumwaga hata mkojo tu acha damu waone.

Nilipenda utawala wake.
 
Back
Top Bottom