Pre GE2025 Mnyika: Tumealikwa Kwenye Kikao Cha kupitia Kanuni za uchaguzi wa serikali za mitaa lakini hatujapewa Rasimu, Wanachama tunaomba Ushauri wenu!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Katibu mkuu wa Chadema John Mnyika amesema wamealikwa kwenye kikao Cha kupitia Kanuni za uchaguzi wa serikali za mitaa Lakini hawajapewa rasimu ya Kanuni Ili wazipitie na kikao ni June 15

Viongozi wanaomba ushauri wa wanachama katika Mazingira hayo wafanye nini?

Ayo tv
 
Wawaandikie barua haraka kuomba nakala ya kanuni ili waipitie vinginevyo wa protest, zinatafutwa mbinu za kuwa provoke ili msishiriki uchaguzi ili nyani aachiwe shamba no this time pambanani nao ikibibidi nguvu ya umma itumike km last solution.
 
Huyu si ccm wanasema kasusa kufanya kazi za Chadema, kwani bado yupo?
 
Hapa ndio pale baadhi wanao wapendelea wanaotuendesha kama gari bovu kulingana na watakavyo wao,wawasiliane na waliotoa mwaliko iwapo hawataonyesha nia na utayari wa uwazi wa rasimu husika,yafanyike maamuzi mengine.Taarifa ya mambo yasiyo sawa na upendeleo wa chama twawala,zimfikie Lucas,Tlatla na wengine taifa ni letu sote sharti ujenzi wake uwe jumuishi.
 
Mwaliko ni umekosewa, ni kikao cha kutunga kanuni!.
Ila nijuavyo mimi sheria mpya ya uchaguzi imeifuta sheria ya uchaguzi wa serikali za mitaa, hivyo nawashauri Chadema wahudhurie na kuomba uchaguzi wa serikali za mitaa ufanywe mwakani na usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi kama nilivyo shauri hapa Mabadiliko ya Sheria ya Uchaguzi: Je Tupige Ndege Wawili kwa Jiwe Moja kwa Uchaguzi Serikali za Mitaa/Mkuu, Ufanyike Siku Moja au Tuendeleze Mazoea?

Na hapa Mnaonaje Uchaguzi wa Serikali za Mtaa Ufanywe Siku Moja na Uchaguzi Mkuu na Usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi? Samia Atabarikiwa Sana!

P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…