kusufuria makoko
Member
- Mar 22, 2018
- 77
- 82
Siku ya mashindano ya Miss Mbeya, timu ya Simba ilikuwepo Mbeya kucheza na TZ Prisons, baada ya kumaliza mechi mashabiki wakaenda ukumbini kushuhudia Dream FM wanavyomkabidhi Miss Mbeya zawadi ya pikipiki ya TANHERO, bila shaka walimpelekea habari MO naye akaamua afuate nyayo za Dream FM na TANHEROWachezaji wa Mikia wapo kapu Moja na Miss Mbeya
Yaani bodaboda kweli?? Kweli wahindi ni matapeli tu!!Na Bakari Chiijumba,
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Timu ya SimbaSC , Mo Dewji amesema baada ya Kocha Mkuu wa Klabu hiyo,Patrick Aussems kutimiza malengo yaliyowekwa na Klabu,tayari bodi imepanga kukaa naye na kumuongezea mkataba mpya ili aendelee kuifundisha Simba SC.
Kuhusu ahadi ya Milioni 5 kwa kila mchezaji baada ya ubingwa, Mo Dewji amesema hakutoa ahadi hiyo bali alisema atatoa zawadi ya Pikipiki(Boxer) kwa kila mchezaji na tayari amewapa ili kuinua vipato vyao,MO amesema wakiweka watu wa kuziendesha zitawaingizia kipato.
Dewji amesema ameshaongea na viongozi wa klabu ya DC United ya Marekani na kuwaomba wakafanye maandalizi ya msimu ujao huko pia wacheze nao na timu nyingine za LMS au kwenda nchini Ureno ili wakacheze na timu za huko.
Katika hatua nyingine MO ameipongeza Klabu ya Yanga kwa kuongeza ushindani kwenye Ligi.
"Naipongeza Yanga SC kwa kuleta ushindani mkubwa kwenye Ligi yetu na nichukue fursa hii kuwapongeza viongozi wapya wa Yanga SC na niwaombee wajipange ili waweze kufanikiwa, najua msimu ujao utakuwa mgumu sana"amesema Mo na kuongeza;
''Kwenye usajili tupo makini sana,leo tunapata ripoti ya kocha juu ya wachezaji wa nyumbani anaowataka,pia katika wachezaji 10 wa kigeni mpaka leo usiku kocha atatuambia anabaki na nani na nani waondoke..Simba itakuwa kwenye soko la kushindana na timu kama Mazembe na Al Ahly"
''Katika kusajili, kuna wachezaji wengine tutawatoa kwa mkopo lengo ni kutengeneza timu yenye ushindani zaidi na tutajitahidi usajili wetu uende sawa na vilabu vikubwa Afrika ili tukafanye vizuri kwenye Ligi ya Mabingwa''View attachment 1104709
5m na bajaji ipi kubwa?Inamaana aliyesikia milioni 5 alisikia vibaya?
pikipiki boxer5m na bajaji ipi kubwa?
Hongera kwao, bodaboda moja kwa wachezaji zaidi ya Ishirini ni kiasi kikubwa sana cha fedha ukilinganisha na Faida iliyopatikana kutokana na ubingwa huo,,, pia ikumbukwe hiyo sio Mshahara ila ni Zawadi
5m na bajaji ipi kubwa?
Asante Mkuu kwa kuliweka sawaWachezaji 30 ×2,330,000=69,000,000
Mil 69 imebaki Mil 11 tu sawa na hela za ubingwa .
Mo kajitahidi.
Yanga wamepewa nini tofauti na futari?Walifika robo finali hivyo CAF imewalipa dola 650,000.Kashindwa hata kutoa Dola 200,000 kuwagawia wachezaji ? TATIZO UTAJIRI WA KURITHI. MHINDI BAHILI.
Yanga mlichukua ubingwa mkawapa zawadi gani wachezaji wenu?...Wachezaji wa Mikia wapo kapu Moja na Miss Mbeya
Bodaboda fc
Walipewa futari na pepsi big.Boxer mnaidharau! wakati wachezaji wa yanga hawana hata phoenix bomba mbili
Hata kama mkuu.. wanaozodoa wamewahi kupewa nini tofauti na wali maharage..Nadhani hizo boda boda hazihusiani na robo fainali itakua maalumu kwa ajili ya ubingwa wa tpl
Yanga wanaona ni ndogo wakati wao kuipata mpaka bakuli lipite nchi nzimaPesa haiokotwi. Simba imemuingizia SH ngapi mpaka agawe 5M.
Manji amewaachia nini yanga tofati na Akilimali?..Vitu vingine hadi nimeona aibu mimi kwa mtu mkubwa kama mo
"bodaboda kweli waongeze vipato vyao"
Ngassa, Boban, Makapu, Kindoki ndio mlitaka wawape ubingwa?m5 itamkata maana hela nyingi zimetumika kutafuta ubingwa ambao zawad yake haifiki hata robo.