Mo Dewji amshauri Kocha Omog aachie ngazi, Simba yavunja naye Mkataba

Mo Dewji amshauri Kocha Omog aachie ngazi, Simba yavunja naye Mkataba

Suala ni timu zetu kuendeshwa na viongozi ambao wanaacha majukumu yao ya kiutawala na kuingilia masuala ya kiufundi.
Viongozi wamekuwa makocha, madaktari, mawakala, maskauti n.k.
Kwa hali hiyo, hata aje Guardiola, Van Gaal au Mourinho atapata shida sana kufanya kazi na kupata mafanikio.
 
Manara alisema huyo ndio kocha bora KBS ktk ligi yetu ambae amewahi kuwa kocha kwenye kombe LA dunia na pia kushinda ubingwa ktk mashindano ya Caf.
Lkn Leo hii ndio amekuwa kocha mbovu KBS ktk ligi.
manara anaongea kwa mihemko sana yule
 
Naomba simba imuweke pembeni na Haji Manara, anachokifanya simba sioni kama Ndiyo kazi ya idara ya habari kile
 
Bora timu akabiziwe mzawa tu,Omog alikuwa alikuwa hajui kuwatumia vizuri wachezaji
 
Jibu ni rahisi.
Simba hawampi kocha yeyote nafasi ya kusajili na kupanga kikosi chake uwanjani. Viongozi wanadhani wanajua zaidi.
Ugonjwa huu haupo tena Yanga na matokeo yake tutayaona.
Sasa wataajiri mwingine na yatakuwa yale yale. Hii ni neema kwa Yanga.
 
Kocha anafukuzwa kwa tweet. Hahaha.
Poor african football.
 
omog anakariri wachezaji ana tabia ya kusugulisha benchi wachezaji wazuri mfano Mo ibrahim angalia alivyodidimiza kipaji cha Manyika afadhali wamemtoa mapema pia mbinu yake kubwa ni ulinzi
Manyika ni kipa Wa kiwango cha kawaida sana sema anapaishwa na media na jina la babake basi
 
Wa kufukuzwa simba ni Niyonzima na Okwi, hata akija Guardiola, kama kocha analetewa wachezaji na uongozi wakati yeye hawataki, vikombe tusahau.
 
Inawezekana Omog akawa in tatizo Simba, lakini nnachokiona Mimi tofauti sana.
Kama washabiki tumeamua kumtwisha zigo la ' Mavi ' kocha tu.
Mosi, Nafikiri ulifanyika usajili wa majina tu pale Simba kuliko kuangalia uhalisia. Mfano, unamuachaje Janvier Besala Bokungu kwaajili ya Ally Shomari au mchezaji ' majeruhi ' Kapombe?
Pili, wachezaji was Simba naona wanaamini kuwa wao ni ' wakubwa ' kuliko timu. Sioni timu ikiwa na spirit ya ushindi uwanjani, kifupi wachezaji ' hawajitumi ' kabisa. Most of them ni mizigo tu.
Faida ya kuwa na wachezaji wanaoitwa ' wazoefu ' ni ipi kama wanashindwa kusoma mbinu za timu ndogo kama ile ya Jana?
Ni ujinga na uwendawazimu kuendelea kumtupia lawama kocha pekee.
Nafikiri ' reform ' inahitajika hata kwa wachezaji wa Simba ambao ' tunaaminishwa ' eti wa mabilioni ya pesa.
Nawasilisha..!
Point mkuu nimependa wazo lako
 
View attachment 657658

Naungana na Mo Dewji,huyu kocha hawezi kuwa na kipya tena
---------

Baada ya SAA kadhaa kupita..

Klabu ya Simba na Kocha wake Mkuu Joseph Omog wameamua kwa pamoja kuvunja mkataba baina yao kwa makubaliano maalum yanayozingatia maslahi ya pande zote mbili

> Uongozi wa Simba SC umesema unamshukuru kocha Omog na kumtakia kila la kheri kwenye maisha yake nje ya Simba..
Baada ya kufungwa na grw thimbwaaaa
 
Back
Top Bottom