Mo dewji: Nimepoteza billion 41 ndani ya Simba

Mbona hakubali wakaguzi wa hesabu wakague timu watujie na ukweli wa faida asiyotaja ya matangazo dhidi ya hela aliyoweka .
 
Huyu ni takataka sana ..gsm anaweza hata asile wiki nzima ili yanga ile ,,
Tajiri anayeongoza timu yake pasipo kupiga ni mmoja tu hapa TZ naye ni Bhakresa.

Hawa kina MO na GSM ni vijana wa mjini wenye malengo yao kwa hizo timu pinzani.

Waasisi wa zile timu mbili za kariakoo walisimamia zaidi makundi ya wacheza mdundiko, lakini walipokuja hawa vijana wa mjini (sio Kariakoo) wakaanzisha mtindo nipe nikupe na ndio unaoziongoza hizo timu.

Kwa kuwatoa ushamba tu wale wajinga mnaomjadili MO niwape hii siri kwamba "MO & GSM ni pipa na mfuniko" .

Karaghabaho 😂😂
 
Kwa hiyo ndiyo kusema zile bilioni 20 ni sehemu ya hizo bilioni 40 alizopata hasara, au!!!
 
Mudi anawatesa sana MAKOLO!kila wakikaribia kuingia nusu final anakuja na misemo ya kuwavuruga!!
 
Ni bora gsm kuliko dewji huwezi kubali ila mda utaongea
 
Yanga haiendeshwi kwa hisa kama simba
Gsm hajanunua hisa zozote Yanga
 
Kwamba yupo tayari kufilisika kisa Simba
Si ndo hapo??
Hii ni trick ya kishamba sana,, kwamba kila simba inapata kitu flani (kizuri au kibaya), ye anajitokeza na kutangaza pesa alizowekeza. Anafanya hivi kwa maelngo mawili tu kwa maoni yangu.

1. Lengo la kwanza ni kutafuta kutukuzwa aonekane amejitolea sana na anastahili pongezi na si lawama.

Mifano ni mingi hapa nitatoa michache, mwaka 2020, Simba ilipofungwa na Mtibwa kwenye fainali ya mapinduzi cup, aliingia twitter akatangaza pesa alizotumia kusajili na kulipa mishahara kisha akajiuzulu then kesho yake wakamlamba miguu akaahirisha kujiuzulu, huku akiwa na uhakika kwamba hatopata lawama kwa ie failure ya mapinduzi.

Mwanzoni mwa msimu huu. ilivyoonekana kwamba Simba imesajili wachezaji wengi wabovu yeye alitokea tena kwenye mtandao wa X (twitter) akasema mara hii ametoa B 3 so mtu asiseme Mo hajatoa hela. Lengo ni kujiweka pembeni kutokana na lawama za kusajili wachezaji magalasa wa bei chee.

2. Lengo la pili ni anatengeneza mazingira asiulizwe faida anayoipata kwa uwekezaji wake hapo Simba. Ndo maana mara zote amekua hodari wa kutangaza hasara anayoipata ili ionekane hafaidiki. Lakini swali la kujiuliza ni inakuaje mfanyabiashara aliyefanikiwa kama yeye aendelee kuikumbatia biashara inayompa hasara kama aliyoitangaza kwa miaka 5 mfululizo bila kuiacha? Hadi hapo alipo, ameziacha biashara ngapi ambazo aliona zinampa hasara? Kwanini Simba impe hasara na aendelee kuing'ang'ania?
Pia kama anakubali hasara labda kutokana na mapenzi yake kwa simba, kwanini haishi kulalamika kwenye media kuhusu hasara anayopata. Si apate hasara kimyakimya tu coz anatimiza mapenzi yake kwa klabu anayoipenda?
Mbona tangu alipoiacha mwaka 2003 hadi mabadiliko yalipofanyika 2017 timu ilikua inaendeshwa kwa pesa za HansPope na mzee Hanspope hakuwahi kwenda kulalamika hasara kwenye media yoyote nchini?
Huyu jamaa anatuchukuliaje sisi watz?
 
Huyu ni Mpuuzi haununui Team ili utengeneze Pesa; Faina unayopata sio monetary bali brand na promotion ya Image yako...

Kama alidhani anaweka Tshs 20 ili iwe 200/= nadhani hakufanya due diligence... Na hii kauli ya kupoteza ni mbaya sana hakuna anachopata kwa kutoa hio Kauli zaidi ya kujijengea maadui (Angesema ametumia / ameweka na sio Kupoteza)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…