Mohamed Said ''Mzungu wa Unga,'' 2007 Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere

Mohamed Said ''Mzungu wa Unga,'' 2007 Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere

sasa naanza amini jamaa liposema religion is opium of the people...... ni kama mzee wetu umepoteza imani na nchi yako kabisa unaanza elekea radicalism..unanikumbusha jamaa yangu tulisoma naye shule ya msingi aliishia mpiga vibao raisi mstahafu sasa hivi amekua kama amerukwa hivi...angalizo www.mohammed.com sio website na wala hakuna kitu..na swala la kusachiwa mbona hata raisi mstahafu alishawahi sema watanzania walikua wanabeba sana madawa hadi naye alisimamishwa kiwanja cha ndege ughaibuni..nadhani swala hapo ni eneo ulilotokea kipindi hicho kama tehran ndipo madawa ya kulevya yalikua yanasambazwa sana na haina haja kuituhumu serikali..nisamehe mzee wangu kama nimekukosea heshima..ni mawazi =o ya upeo wangu mdogo tu
Cmoney,
Hii ni nchi huru na kila mtu ana uhuru wa mawazo yake.
Ikiwa wewe unaamini dini ni kasumba nani wa kukukataza?

Unaweza kuwa kitu chochote unachopenda huvunji sheria.
 
Mohamed Said,
Kwa hotuba hiyo ambayo umetubandikia na kwa wanaoelewa hali ya mambo nchini Tanzania nachelea kusema ulikuwa unamwaga sumu labda bado unaendelea kumwaga sumu kwa umma wa watanzania (waislam na wasio waislam). Tupe ushahidi kanisa kutaka kuua uislam, tupe ushahidi kwamba Waisalam nchini Tanzania ni wengi kuliko makundi mengine, tupe ushahidi pia kwamba vita vya majimaji vilipiganishwa na waislam pekee, tupe ushahidi kwamba uhuru wa Tanzania ulipiganiwa na waislam pekee na kuukabidhi kwa wakristo. Mohamed, kwa uongo huo ulistahili kubanwa na hata hivo nashangaa ni kwa nini uliachiwa huru hufai kukaa ndani ya jamii.

Nikuunge mkono kwa hili, Amerika ni mchonganishi na anachokiangalia ni maslahi yake tu. Amerika amefanikiwa kukuaminisha wewe kuwa nchini Tanzania kanisa ni adui wa uislam (you're very wrong). Kwa hali hiyo, ndio maana unapita na unataka kupita dunia nzima kutangaza uongo kwamba waislam wa Tanzania wanadhulumiwa haki zao na ni daraja la pili katika nchi ambayo wao wameiletea uhuru. Wahausa wa Nigeria walipigwa na butwaa baada ya kusikia mada yako hata mimi ningeshangaa yaani kundi Fulani limwage damu kasha matunda ya damu zao yakabidhiwe kwa kundi linguine kasha kundi kabidhiwa lianze dhuluma dhidi yao hii inasikitisha sana na kama ni sumu kweli ulimwaga. Boko Haramu kule Nigeria ilipata nguvu kupitia wamwaga sumu kama wewe. Na mashaka kama wewe haufungamani na wale magaidi wa Mkuranga na Amboni Tanga.

Nakushauri, tangaza ukweli bila kushawishiwa na makundi yaliyo nje ya mipaka ya Tanzania na uwe mwakilishi mzuri kwa nchi yako. Wanaofahamu ukweli hotuba yako haikuwa kitu kingine bali kueneza chuki kati ya makundi mawili kama ulivyosema (waislam na wakristo)
Fugwe,
Haya mbona tushsyajadili sana hapa jamvini?
Fungua post za nyuma.
 
Mpaka hapo sina haja ya kuendelea kusoma kwsb jamaa limeishaingiza masuala ya udini kwahyo story yake abakie nayo tu
Chalabizo,
Hakuna anekulazimisha kunisoma.

Binafsi huwa nasoma vile ninavyovipenda sasa ikiwa wewe hupendi
maandishi yangu wala hakuna ugomvi.

Hulazimishwi.
 
Mzee Mohamed Said nawewe unashutumu mno ukristo. Ukisoma hadithi yako utazani nchi hii iko vitani na waislam wanauwawa. Kuwa na kiasi mzee. Mikasa ya kukamatwa kwa hila inawakuta wengi tu.

Baada ya kusema hayo nakupa pole ni usumbufu mkubwa......ungerusha hata ngumi umtandike asifa mmoja puani waone hutaki mchezo.
Mwelewa,
Ndugu yangu unalikuza jambo bure.
 
Mohamed Said mzee wetu unayeishi kwa kueneza sumu😛. Hiyo sensa ya waislamu wengi zaid imetoka wapi? Kiashiria rahisi ni bungeni ambako wewe umesema kumetawaliwa na kanisa, kama nyie ni wengi kwanini hamjachagua wabunge wengi waislamu? Kwanini kampeni yako isianzie kuhamasisha waislam wachague wenzao badala ya kuwafundisha kuwachukia wakristo?
Sooth...
Unalirahisisha jambo hili.

Unaweza kupata majibu yako kwa kumsoma Bergen, Sivalon na Njozi.
Kila kitu huja na sababu zake.
 
Eddy,
Soma niliyomwandikia rafiki yangu mmoja anetaka kujua habari zangu za unga:

Wakati huo sasa ni usiku wa manane na nishapeleka SMS kwa sahib yangu mmoja bingwa wa mambo ya mtandao wa kompyuta kumjulisha kuwa nimekamatwa uwanja wa ndege kwa tuhuma za uongo za kuvusha mihadarati na yeye ile kuipata tu ule ujumbe wangu akaifahamisha dunia kuwa nimekamatwa uwanja wa ndege nikitokea mkutanoni Iran na nimebambikiziwa tuhuma za kuingiza nchini mihadarati. Waliponitia mbaroni tu walinionya kuhusu kutumia simu yangu ya mkononi lakini bahati nzuri hawakuninya’ganya. Aliyenipa onyo hili alikuwa mkuu wa kituo cha polisi cha uwanja wa ndege. Huyu rafiki yangu akawa kanisaidia sana maana hadi kumekucha wapenzi wangu wote ndani na nje ya nchi pamoja na vyombo vya habari vinavyonifahamu walikuwa na taarifa za kukamatwa kwangu. (Kwa kipindi takriban miaka ishirini nyuma kwa nyakati fofauti nimekuwa nifanya mahojiano na radio zote muhimu kama, BBC, VOA, Sauti ya Ujerumani, Sauti ya Iran nk.).

Kilichotokea Chuo Kikuu Cha Ibadan ni hiki: Unajua ile paper yangu ilibadili mwelekeo wa ule mkutano na mimi
nilikuwa kati ya wazungumzaji wa mwisho.

Waamerika ingawa wanajifanya wanajua lakini si kuwa kila kitu kiko
hadhir kwao.

Naamini walishtuka sana nilipowaambia kuwa Waislam wa Tanzania
hawana ugomvi na USA wao wana matatizo yao ya ndani na utawala
ulioko madarakani.

Walishtuka nilipowaambia kuwa Waislam wa Tanzania wangependa
kuwe na mjadala wa wazi kujadili matatizo yote wanayowakabili kama
elimu na fursa zingine.

Bahati mbaya Sheria ya Ugaidi imesababisha viongozi wao kukamatwa
na taasisi zao kufungwa kwa uonevu tu.

Sasa pale Chuo Kikuu Cha Ibadan kitabu cha Sykes kimekuwa kikisomeshwa
toka 2003 na rafiki yangu Oleduso huyu kijana ni ''political scientist,'' wa
haja na ndiye aliyenialika.

Tulifahamiana Kampala mwaka wa 2003 katika mkutano.

Wanafunzi na waalimu wakawa wanaijua hali ilivyo Tanzania na hii ndiyo
sababu ya wao kusema Sheria ya Ugaidi haiwezi kupitishwa Nigeria kwani
huko ni kutangaza vita na Waislam. Walikuwa tayari washaona athari yake
kwa Tanzania.

Waamerika wakawa kwa njia moja nimewavurugia mipango yao.
Yaliyofuatia hapo sasa ni historia.

Haya yameshapita na naamini ipo faida imepatikana katika kuandika na kusema maneno yale mbele ya Wamarekani siku ile pale Ibadan kwani 2011 nilialikwa Marekani na hao hao Waamerika na nikafanya mihadhara miwili Chuo Kikuu Cha iowa, Iowa City na Northwestern University, Evanston Chicago. Waliniambia kuwa nimewasaidia sana kujua historia ya Tanzania. Alhamdulilah. Hivi tunavyozungumza sasa kuna jopo linaongozwa na Prof. Shivji linaandika upya historia ya TANU na historia ya uhuru wa Tanganyika kupitia maisha ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Nimefanya mahojiano na jopo hili mara tatu na nimewapa picha na nyaraka za wazee wetu.

zANheiH8lxo1CMBnRgffqHWPtjrAGffz_Cb3A24Mi4XAraJQtc9uayUAReib2Ut_JWareMWQauVeV-a6_CmyFMJGyGHn214X7Pa0aeyioXIVabzDZ_u3JqtfZT6HOHsylrSd9lEtsjJkxZckOopynK5eew8-CjuabfMwaI_2e8dIGuOj9__6JW9KXCacOsfFGM7sRYqJ1GhkbYOSMxgcu2XFmPArnSLzrVQ2fUQtflVh6k4JSGhd3ZB_QO9v7HMEhtoWKhYZiisZJZngLsz0YU8VLUfVSeWO7JDKrmU6-t1O6fgytxHgD6bQpGgdgRGc16mWQEFU_CJy0t48c7TaxnPGDXh-Tvc7Wx-eLFMPDweSuQdfyx0FDQzRw15u4cL1E7TpCeX0cDfBLhw4BkCsu8AWg2kZq8Ib784NEyYZXeYu_xcA_UfQani9e6R33KoOo-_e8xlGtJ1ClzQpHLwW-8T324w9n55mkxG5ujP7fn_AjVI9swJr9E3hplmIx_85vAjEQjdxVAzhgM6ySmWEjaFa8EnUAvFVe_73vHLCvHcX5TqiTlYeSz7-YLiareiV-I-G13K_G2T7OI2iiMhBfc6jSFtQCyMiQr2lq6GkWQlU5FrnHERV=w800-h534-no

Prof. Shivji, Prof. Saida Othman na Mwandishi
Saida.Othman
Mke wa.Marehem Prof Haroub Othman?
 
Ukizaliwa muislamu kitu cha kwanza kabla ya nguzo nyingine kujifunza ni kwamba WAISLAMU WANAONEWA na wakristo haswa Wakatoliki wanapendelewa baada ya hapo ni ruksa kujifunza mengine usishangae sehemu zote wao wanalialia tu toka uhuru mpaka sasa ila hii imani wanayo tu wenyewe na wanapandikizana wenyewe.
Raisi wetu akiwa mkristo watalia kua hawapendi lakini hata akiwa muislamu watalia tena anawatenga ndugu zake kinachokatisha tamaa kwa hakika kuna waislamu wengi wenye elimu tena ya kutosha wapo wabobezi kibao ila na wao wanalia tu yaani ukisikia na kusoma visa vyao inabidi ucheke maana hata kuwaonea huruma haifai wanaweza kulia tena kwa nini tunawaonea huruma.
 
Ukizaliwa muislamu kitu cha kwanza kabla ya nguzo nyingine kujifunza ni kwamba WAISLAMU WANAONEWA na wakristo haswa Wakatoliki wanapendelewa baada ya hapo ni ruksa kujifunza mengine usishangae sehemu zote wao wanalialia tu toka uhuru mpaka sasa ila hii imani wanayo tu wenyewe na wanapandikizana wenyewe.
Raisi wetu akiwa mkristo watalia kua hawapendi lakini hata akiwa muislamu watalia tena anawatenga ndugu zake kinachokatisha tamaa kwa hakika kuna waislamu wengi wenye elimu tena ya kutosha wapo wabobezi kibao ila na wao wanalia tu yaani ukisikia na kusoma visa vyao inabidi ucheke maana hata kuwaonea huruma haifai wanaweza kulia tena kwa nini tunawaonea huruma.
McDonald Jr,
Hiyo kauli yako ni lugha ambayo ishazoeleka.
Wala mimi huwa hainikeri kiasi cha kutaka nami nitoe kejeli mfano wa hizi zako.

Huwa natoa rejea na kuwaomba wasome na kisha warejee jamvini waseme
walichoona katika hizo rejea.

Hajapata kurudi mtu.
Wote ndiyo unakuwa mwisho wao.

Nami kwa utaratibu na uungwana nakupa rejea hizi usome na urejee hapa
jamvini ueleza ulichoona:

Religion and Development, P van Bergen 1981
Kanisa Katoliki na Siasa ya Tanzania Bara 1953 Hadi 1985, John Sivalon 1992
Mwembecha Killings and the Political Future of Tanzania, Hamza Mustafa Njozi, 2002

Kitabu cha Njozi serikali ilikipiga marufuku.
Lakini pia ikiwa utapenda unaweza ukasoma:
The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924-1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika, Mohamed Said 1998.

Kwa kawaida huwa hamna subira na wala hamtaki kusoma hizo rejea sasa
sielewi kwa nini, ni kwa uvivu wa kusoma au kwa kuwa ile dhana ya kuwa,
''unajua'' huna jipya la kujifunza.

Nakusihi usiwe katika kundi hilo.
Najua hapo una kurasa takriban 500 za kusoma lakini soma yapo mengi utajifunza.
 
Namfaham huyu mama kama nguli wa uandishi wa.vitabu na pia mhadhiri.
Mumewe alinifundisha ila yeye hakunifundisha
Saida Othuman-Yahya
Mkoroshokigoli,
Hata mimi Prof. Haroub Othman kanisomesha.

Prof. Haroub kwa kunieleza mwenyewe alipata mstuko mkubwa
aliposoma kitabu cha Sykes na kukuta mafungamano yaliyokuwapo
baina ya Abdul Sykes na Nyerere kabla ya kuunda TANU 1954.

Kwa miaka yote hakupata kujua kuwa TANU ilikuwa, ''brain child'' ya
Abdul Sykes.

Alikwenda hadi kwa Mwalimu Nyerere kumuomba na yeye aeleze vipi
TANU iliasisiwa.

Haya yote kanieleza mwenyewe tumesimama nje ya Msikiti wa Ibadhi 1998.

Ni kisa kirefu.
 
Mkoroshokigoli,
Hata mimi Prof. Haroub Othman kanisomesha.

Prof. Haroub kwa kunieleza mwenyewe alipata mstuko mkubwa
aliposoma kitabu cha Sykes na kukuta mafungamano yaliyokuwapo
baina ya Abdul Sykes na Nyerere kabla ya kuunda TANU 1954.

Kwa miaka yote hakupata kujua kuwa TANU ilikuwa, ''brain child'' ya
Abdul Sykes.

Alikwenda hadi kwa Mwalimu Nyerere kumuomba na yeye aeleze vipi
TANU iliasisiwa.

Haya yote kanieleza mwenyewe tumesimama nje ya Msikiti wa Ibadhi 1998.

Ni kisa kirefu.
Mashallah.
 
Sooth...
Unalirahisisha jambo hili.

Unaweza kupata majibu yako kwa kumsoma Bergen, Sivalon na Njozi.
Kila kitu huja na sababu zake.
Nimekisoma kitabu cha Njozi ambaye amewanukuu hao waandishi wengine na 'bahati nzuri' nilikisoma kwa moyo mkunjufu. Hakuna kitu kibaya kama tetesi, mtu mzima na msomi kama wewe sio vizuri ukaamua mambo kwa kutumia tetesi. Mfano mdogo tu, hizi takwimu za waislamu wengi unazitoa wapi wakati NBS haijawahi kuwa na dodoso linalouliza dini kwa takribani miaka 40? Tumuamini nani kati yako wewe na CIA wanaosema wakristo ndio wengi Tanzania? Mimi binafsi sikuamini wewe wala CIA, nitaamini kazi itakayofanywa na NBS.

Lakini pia kama tunataka kupata picha ya wapi wengi twaweza kutumia uzoefu wa mikoa yetu. Mikoa ya 'Pwani' ndiko kuna waislamu wengi. Mikoa hiyo ni DSM, Pwani, Tanga, Lindi, Mtwara, Kigoma, Tabora, Singida, na mikoa ya Zanzibar. Napata wasiwasi kuamini kuwa kwa mikoa hii tu waislamu ni wengi zaidi. Kuna hoja ambazo hazijaenda shule kama waislamu kuwa na wake wengi kuna nako kumechangia kuongeza idadi ya waislamu. Hoja hii haina msingi maana kuwa na wake wengi sio kuwa na watoto wengi. Msingi wa kuwa na wake wengi ni tamaa ya ngono, sio tamaa ya watoto. Pia, ninafahamu watu wengi ambao wana mke mmoja lakini wanazaa watoto 8 au zaidi. Hivyo hakuna uhusiano kati ya kuwa na wake wengi na kuwa na watoto wengi ukichukulia kuna 'single mothers' wengi mtaani.
 
Mambo yalianza wakati sasa narudi Dar es Salaam na ndege ya Emirates iliyokuwa inatua usiku. Inaelekea maofisa wa pasi pale uwanjani walikuwa na taarifa zangu mapema na walikuwa wakinisubiri kwa hamu kubwa kwani nilipotoa pasi yangu kwa afisa wa pasi hapo ndipo shughuli za kunishughulikia zilipoaanza.

Mimi sikuwa na hili wala lile. Nikawa namuona yule dada aliyekuwa kwenye kile kizimba akikukurika na pasi yangu akiitia katika mashine na kuitoa mara kadhaa. Fikra iliyonijia kwa haraka ilikuwa mashine ni mbovu na harakati zile zilikuwa ni kurekebisha mitambo.

Kumbe sivyo wahusika nadhani walikuwa wanahakikisha kuwa mimi ndiyo huyo waliokuwa wakimwinda na kumsubiri na sasa kapatikana, kaingia mwenyewe kwenye mtego na kanasa. Yule afisa wa pasi akanambia nikae pembeni natakiwa kwa mahojiano na watu wa usalama.

Hofu haikuwa imeniingia kwa kuwa nilikuwa natambua kuwa harakati dhidi ya ugaidi zilikuwa zimepamba moto na labda nilitakiwa kwa mahojiano mafupi kutaka kujua nyendo zangu. Sikujua wala kutarajia kuwa mshtuko mkubwa ulikuwa unanisubiri.

Nilichukuliwa hadi kwenye chumba kimoja na hapo niliwakuta maofisa wa usalama watatu wakanikaribisha kwa taadhima kisha wakanambia kuwa niko chini ya ulinzi kwa kuwa zimewafikia taarifa zangu kuwa mimi nasafirisha mihadarati. Mpaka hapa sikuwa na hofu bado ilinijia picha kuwa yawezekana wamefananisha majina.

Niliwaambia huenda Mohamed Said muuza madawa ya kulevya siyo mimi niliye mbele yao. Wakaniambia kwa kujiamini kabisa kuwa taarifa zao ni madhubuti muuza unga ni mimi na wamekuwa wakinifuatilia siku nyingi. Hapo ndipo walipotoa pasi yangu na kuniomba niitambue kama hiyo pasi ni yangu au la. Niliwajibu kuwa hakika hiyo ndiyo pasi yangu khasa.

Wakaniamuru sasa tutoke twende nikachukue mizigo yangu ili wafanye upekuzi wa mihadarati katika mizigo niliyotokanayo Tehran. Hapo ndipo nilipojuwa kuwa niko katika lindi kubwa la matatizo na ubongo wangu ukaanza kufanya kazi kwa haraka huku nikisoma dua kumuomba Allah ulinzi wake kwani kwa hakika nilijua kama ni njama zimekamilika na leo imefika siku yangu.

Nikajiuliza itakuwaje watakapotoa madawa kwenye mizigo yangu. Nikaanza kufikiri vichwa vya habari vya magazeti yatakavyopambwa na habari zangu. Ikanijia yakini kuwa watu wa usalama wameniwekea madawa ya kulevya katika mizigo yangu ili waniangamize na maadui zangu wapumzike na shari yangu.

Nilimgeukia yule ofisa mkuu aliyekuwa ananihoji nikamwambia kuwa sitokubali kugusa mizigo yangu bila kuwapo mashahidi isijekuwa mizigo yangu ishawekewa hayo madawa ya kulevya kwani nilikotoka Tehran mizigo ilikuwa imekaguliwa na ilikuwa salama.

Hoja yangu kubwa kwao ilikuwa kupata uhakika kutoka kwao kuwa wananijua vizuri kiasi cha kuthibitisha kuwa kweli mie ni msafirishaji wa madawa ya kulevya. Jibu nililopewa ni kuwa wao wanafanya kazi kutokana na taarifa zilizowafikia. Wakasema, “Sisi tunazo taarifa zako kamili kuwa wewe ni msafirisha madawa ya kulevya.”

Nikawauliza,“Baada ya kupata taarifa hizo zangu nyie mmechunguza kutafuta ukweli?” Wakasema, “Ndiyo maana leo tumekukamata.” Nikawaambia, “Si kweli kama kwa sababu mie nafahamika Dar es Salaam takriban kwingi maana ndio nilikozaliwa na kukulia. Hapo Kariakoo ukiwaambia watu kuwa Mohamed ni “Mzungu wa Unga” kila mtu atacheka maana huo kwao ndugu zangu ni mzaha mbaya.”

Walitaka kujua nilkwenda kufanya nini Iran. Niliwaambia nilialikwa na serikali ya huko kuhudhuria mkutano. Wakataka kujua vipi nilipata mwaliko. Nikawajibu kuwa hilo swali sina jibu labda waiulize serikali ya Iran. Nikawaeleza kuwa mbona siku zote napita hapo uwanjani nikenda sehemu tofauti duniani kwa mialiko na kutoa mada sijakamatwa kimezidi nini katika hii safari ya Iran?

Niliwaeleza kuwa miezi michache iliyopita nilikuwa Chuo Kikuu Cha Ibadan kwa mwaliko tena mkutano umefadhiliwa na serikali ya Marekani na wamenipa na tiketi toka Dar es Salaam hadi Lagos na kuniweka hoteli na kunilipa fedha.

“Mbona hamkunikamata wakati ule?” Nikafungua mlango mwingine nikawaambia, “Nakuapieni nyie msingethubutu kumkamata Mkristo anaetoka Vatican mkutanoni. Lakini kwa kuwa mie ni Muislam sina wa kunitetea. Nchi hii nani atakuuliza kwa kumnyanyasa Muislam?” Walishtuka na wakawa wanyonge sana wakasema si kweli kuwa naponzwa na dini yangu.

Baada ya kukurukakara nyingi na mabishano makubwa kuhusu mie kukubali kufanyiwa upekuzi wa mizigo yangu alikuja binti mmoja katika wao na yeye akanihakikishia kuwa wao ni serikali na sio wahuni. Hawathubutu kuniwekea dawa katika mizigo yangu hivyo akanisihi sana kwa upole nikubali ili wajitoe wasiwasi na wataniachia endapo hakuna kitu.

Niliomba apatikane shahidi wa kushuhudia mizigo yangu kabla ya kufanyiwa upekuzi lakini hakuna mtu aliyekubali kuchukua dhima ile katika maofisa waliokuwa kazini pale uwanja wa ndege usiku ule. Upekuzi ukafanyika hadi mwilini. Hakuna kitu. Wakanipela katika choo maalum cha kutolea madawa kwa njia ya haja kubwa.

Nikakataa kujisaidia pale. Ilikuwa ndio mara yangu ya kwanza kuona choo kama kile. Choo chenyewe ni cha aluminium. Tofauti na vyoo vya pale ambavyo siku zote ni vichafu, hiki kilikuwa kisafi sana kiasi mtu unaweza hata kutengewa chakula na akala bila ya kuhisi kinyaa.

Nilitegemea wataweka ahadi yao kuwa ikiwa hawatakuta madawa ya kulevya katika mizigo yangu watanirejeshea uhuru wangu wataniachia niende nyumbani. Haikuwa hivyo. Wakanirudisha ofisini kwao. Sasa wakaacha madawa ya kulevya wakahamia katika vitabu na “audio cassette” nilizokuwa nimepewa kama zawadi kule Tehran wakaniluliza kwa nini naingiza vitu vile khasa kanda za Khomeni na vitabu vyake nchini. Nikawauliza, “Kwani kanda na vitabu vya Khomeni haviruhusiwi kuingizwa Tanzania?
Umejaa Chuki Za kidini Haitakusaidia. Mbona Zanzibar ni sehemu ya Tanzania hakuna kiongozi mkiristo hujawai kusikia wakristo wakilalamika? Acha ubaguzi
Mambo yalianza wakati sasa narudi Dar es Salaam na ndege ya Emirates iliyokuwa inatua usiku. Inaelekea maofisa wa pasi pale uwanjani walikuwa na taarifa zangu mapema na walikuwa wakinisubiri kwa hamu kubwa kwani nilipotoa pasi yangu kwa afisa wa pasi hapo ndipo shughuli za kunishughulikia zilipoaanza.

Mimi sikuwa na hili wala lile. Nikawa namuona yule dada aliyekuwa kwenye kile kizimba akikukurika na pasi yangu akiitia katika mashine na kuitoa mara kadhaa. Fikra iliyonijia kwa haraka ilikuwa mashine ni mbovu na harakati zile zilikuwa ni kurekebisha mitambo.

Kumbe sivyo wahusika nadhani walikuwa wanahakikisha kuwa mimi ndiyo huyo waliokuwa wakimwinda na kumsubiri na sasa kapatikana, kaingia mwenyewe kwenye mtego na kanasa. Yule afisa wa pasi akanambia nikae pembeni natakiwa kwa mahojiano na watu wa usalama.

Hofu haikuwa imeniingia kwa kuwa nilikuwa natambua kuwa harakati dhidi ya ugaidi zilikuwa zimepamba moto na labda nilitakiwa kwa mahojiano mafupi kutaka kujua nyendo zangu. Sikujua wala kutarajia kuwa mshtuko mkubwa ulikuwa unanisubiri.

Nilichukuliwa hadi kwenye chumba kimoja na hapo niliwakuta maofisa wa usalama watatu wakanikaribisha kwa taadhima kisha wakanambia kuwa niko chini ya ulinzi kwa kuwa zimewafikia taarifa zangu kuwa mimi nasafirisha mihadarati. Mpaka hapa sikuwa na hofu bado ilinijia picha kuwa yawezekana wamefananisha majina.

Niliwaambia huenda Mohamed Said muuza madawa ya kulevya siyo mimi niliye mbele yao. Wakaniambia kwa kujiamini kabisa kuwa taarifa zao ni madhubuti muuza unga ni mimi na wamekuwa wakinifuatilia siku nyingi. Hapo ndipo walipotoa pasi yangu na kuniomba niitambue kama hiyo pasi ni yangu au la. Niliwajibu kuwa hakika hiyo ndiyo pasi yangu khasa.

Wakaniamuru sasa tutoke twende nikachukue mizigo yangu ili wafanye upekuzi wa mihadarati katika mizigo niliyotokanayo Tehran. Hapo ndipo nilipojuwa kuwa niko katika lindi kubwa la matatizo na ubongo wangu ukaanza kufanya kazi kwa haraka huku nikisoma dua kumuomba Allah ulinzi wake kwani kwa hakika nilijua kama ni njama zimekamilika na leo imefika siku yangu.

Nikajiuliza itakuwaje watakapotoa madawa kwenye mizigo yangu. Nikaanza kufikiri vichwa vya habari vya magazeti yatakavyopambwa na habari zangu. Ikanijia yakini kuwa watu wa usalama wameniwekea madawa ya kulevya katika mizigo yangu ili waniangamize na maadui zangu wapumzike na shari yangu.

Nilimgeukia yule ofisa mkuu aliyekuwa ananihoji nikamwambia kuwa sitokubali kugusa mizigo yangu bila kuwapo mashahidi isijekuwa mizigo yangu ishawekewa hayo madawa ya kulevya kwani nilikotoka Tehran mizigo ilikuwa imekaguliwa na ilikuwa salama.

Hoja yangu kubwa kwao ilikuwa kupata uhakika kutoka kwao kuwa wananijua vizuri kiasi cha kuthibitisha kuwa kweli mie ni msafirishaji wa madawa ya kulevya. Jibu nililopewa ni kuwa wao wanafanya kazi kutokana na taarifa zilizowafikia. Wakasema, “Sisi tunazo taarifa zako kamili kuwa wewe ni msafirisha madawa ya kulevya.”

Nikawauliza,“Baada ya kupata taarifa hizo zangu nyie mmechunguza kutafuta ukweli?” Wakasema, “Ndiyo maana leo tumekukamata.” Nikawaambia, “Si kweli kama kwa sababu mie nafahamika Dar es Salaam takriban kwingi maana ndio nilikozaliwa na kukulia. Hapo Kariakoo ukiwaambia watu kuwa Mohamed ni “Mzungu wa Unga” kila mtu atacheka maana huo kwao ndugu zangu ni mzaha mbaya.”

Walitaka kujua nilkwenda kufanya nini Iran. Niliwaambia nilialikwa na serikali ya huko kuhudhuria mkutano. Wakataka kujua vipi nilipata mwaliko. Nikawajibu kuwa hilo swali sina jibu labda waiulize serikali ya Iran. Nikawaeleza kuwa mbona siku zote napita hapo uwanjani nikenda sehemu tofauti duniani kwa mialiko na kutoa mada sijakamatwa kimezidi nini katika hii safari ya Iran?

Niliwaeleza kuwa miezi michache iliyopita nilikuwa Chuo Kikuu Cha Ibadan kwa mwaliko tena mkutano umefadhiliwa na serikali ya Marekani na wamenipa na tiketi toka Dar es Salaam hadi Lagos na kuniweka hoteli na kunilipa fedha.

“Mbona hamkunikamata wakati ule?” Nikafungua mlango mwingine nikawaambia, “Nakuapieni nyie msingethubutu kumkamata Mkristo anaetoka Vatican mkutanoni. Lakini kwa kuwa mie ni Muislam sina wa kunitetea. Nchi hii nani atakuuliza kwa kumnyanyasa Muislam?” Walishtuka na wakawa wanyonge sana wakasema si kweli kuwa naponzwa na dini yangu.

Baada ya kukurukakara nyingi na mabishano makubwa kuhusu mie kukubali kufanyiwa upekuzi wa mizigo yangu alikuja binti mmoja katika wao na yeye akanihakikishia kuwa wao ni serikali na sio wahuni. Hawathubutu kuniwekea dawa katika mizigo yangu hivyo akanisihi sana kwa upole nikubali ili wajitoe wasiwasi na wataniachia endapo hakuna kitu.

Niliomba apatikane shahidi wa kushuhudia mizigo yangu kabla ya kufanyiwa upekuzi lakini hakuna mtu aliyekubali kuchukua dhima ile katika maofisa waliokuwa kazini pale uwanja wa ndege usiku ule. Upekuzi ukafanyika hadi mwilini. Hakuna kitu. Wakanipela katika choo maalum cha kutolea madawa kwa njia ya haja kubwa.

Nikakataa kujisaidia pale. Ilikuwa ndio mara yangu ya kwanza kuona choo kama kile. Choo chenyewe ni cha aluminium. Tofauti na vyoo vya pale ambavyo siku zote ni vichafu, hiki kilikuwa kisafi sana kiasi mtu unaweza hata kutengewa chakula na akala bila ya kuhisi kinyaa.

Nilitegemea wataweka ahadi yao kuwa ikiwa hawatakuta madawa ya kulevya katika mizigo yangu watanirejeshea uhuru wangu wataniachia niende nyumbani. Haikuwa hivyo. Wakanirudisha ofisini kwao. Sasa wakaacha madawa ya kulevya wakahamia katika vitabu na “audio cassette” nilizokuwa nimepewa kama zawadi kule Tehran wakaniluliza kwa nini naingiza vitu vile khasa kanda za Khomeni na vitabu vyake nchini. Nikawauliza, “Kwani kanda na vitabu vya Khomeni haviruhusiwi kuingizwa Tanzania?
 
Nimekisoma kitabu cha Njozi ambaye amewanukuu hao waandishi wengine na 'bahati nzuri' nilikisoma kwa moyo mkunjufu. Hakuna kitu kibaya kama tetesi, mtu mzima na msomi kama wewe sio vizuri ukaamua mambo kwa kutumia tetesi. Mfano mdogo tu, hizi takwimu za waislamu wengi unazitoa wapi wakati NBS haijawahi kuwa na dodoso linalouliza dini kwa takribani miaka 40? Tumuamini nani kati yako wewe na CIA wanaosema wakristo ndio wengi Tanzania? Mimi binafsi sikuamini wewe wala CIA, nitaamini kazi itakayofanywa na NBS.

Lakini pia kama tunataka kupata picha ya wapi wengi twaweza kutumia uzoefu wa mikoa yetu. Mikoa ya 'Pwani' ndiko kuna waislamu wengi. Mikoa hiyo ni DSM, Pwani, Tanga, Lindi, Mtwara, Kigoma, Tabora, Singida, na mikoa ya Zanzibar. Napata wasiwasi kuamini kuwa kwa mikoa hii tu waislamu ni wengi zaidi. Kuna hoja ambazo hazijaenda shule kama waislamu kuwa na wake wengi kuna nako kumechangia kuongeza idadi ya waislamu. Hoja hii haina msingi maana kuwa na wake wengi sio kuwa na watoto wengi. Msingi wa kuwa na wake wengi ni tamaa ya ngono, sio tamaa ya watoto. Pia, ninafahamu watu wengi ambao wana mke mmoja lakini wanazaa watoto 8 au zaidi. Hivyo hakuna uhusiano kati ya kuwa na wake wengi na kuwa na watoto wengi ukichukulia kuna 'single mothers' wengi mtaani.
Sooth,
Swali la, ''religious distribution,'' ni swali nyeti sana Tanzania.

Huwa sipendi kulijadili ila panapo budi na nia khasa ni kuonyesha hali halisi ya
siassa nchini petu.

Katika kitabu cha Sykes (1998) niliandika maneno hayo hapo chini:
About two-thirds of East African Muslims reside in Tanzania[1] which is the most populous of the East African countries, i.e. Kenya, Uganda and Tanzania. This includes Zanzibar-a predominantly Muslim country with a 99% Muslim population and once the centre of Islamic learning in East and Central Africa. According to the 1957 population census, Muslims outnumbered Christians at a ratio of three to two. This, at that time, meant that Tanzania was a leading Muslim nation South of the Sahara. But in the first post-independence census of 1967 the total figures for Tanzania Mainland were 32% Christian, 30% Muslim and 37% local belief. These figures show Pagans as a leading majority in Tanzania. The 1967 census has not been able to show the reasons for the sudden decrease of Muslim population nor the growth of animists amidst believers in the span of the last ten years.

This was the last population census showing religious distribution. It is widely believed that the figures for the 1967 census were doctored for political reasons to show that Muslims were trailing behind Christians in numerical strength. There is evidence that the government in 1970, having realised that Muslims were a majority in Tanzania, directed the Statistical Department to destroy all the 1967 census results. [2]

Unfortunately power sharing in the political system in Tanzania is very much skewed against Muslims, although it is known that the stability of any nation depends on proper balancing of these facts. Different sources provide different Muslim-Christian religious distribution figures. These conflicting figures are as a result of sensitivity of the issue. Among African countries with sizable population of Muslims and Christians, like Tanzania and Nigeria,[3] the inquiry as to which faith commands a leading majority, is a source of potential conflict and controversy. Tanzania is of no exception. D.B. Barret[4]gives figures which show Muslims as a minority in Tanzania. The Muslim population is purported to be 26%, Christian 45%, local belief 28%. Tanzania National Demographic Survey figures for 1973 put Muslims in Tanzania slightly above Christians at 40%, Christians 38.9% and local belief 21.1%. But according to Africa South of The Sahara, [5] Muslims in Tanzania are a leading majority at 60%. This figure has remained constant in all its publications since 1982. Since research by Tanzanian Muslims on Islam is scant or almost non-existent, the issue of Muslim population has yet to be tackled from an Islamic point of view. [6]

[1] August H. Nimtz Jr, Islam and Politics in East Africa, University of Miannapolis, 1980, p.11.
[2] See Family Mirror, Second Issue, November, 1994, p. 6.
[3] Ali A. Mazrui, ‘African Islam and Competititive Religion: Between Revivalism and Expansion’, in Third World Quarterly Vol. 10. No. 2 April, 1988, pp. 499-518.
[4] D.B.Barret, Frontier Situations for Evangelisation in Africa ,Nairobi, 1976.
[5] Africa South of The Sahara, Europa Publication, London, No. 20, 1991, p. 1027.
[6]The only conclusive Muslim research is by Dar es Salaam University Muslim Trustee (DUMT), see 'The Position of Muslims and Islam in Tanzania', in Al Haq International (Karachi) September/October1992.

Sooth,
Sasa tuje kwenye takwimu za CIA.
Niko Chuo Kikuu Cha Iowa, Iowa City US nimemaliza kufanya mhadhara wangu na sasa ni zamu
ya mimi kuulizwa maswali.

Hawa jamaa ni hodari na maswali yao yote nimeyajibu kadri nilivyoweza lakini kuna kitu kimoja
nahisi hawakipendi sana katika, ''presentation,'' yangu ambayo kwao juu ya ujanja wao Wamarekani
hawakuwa wanakijua.

Nacho ni, ''the Islamic movement in the struggle for peoples emancipation in Tanganyika,'' hii inawapa
shida lakini vipi watamtoa Abdul Sykes na baba yake katika African Association (1929) na Al Jamiatul
Islamiyya (1933) na TANU (1950)?

Vyama hivi viwili ndivyo msingi wa kuasisiwa kwa TANU 1954 na takriban viongozi wake
walikuwa Waislam.

Historia wanayoijua wao ni ile rasmi ya Nyerere kuasisi TANU 1954.

Zimebaki kama dakika tano tunamaliza ndipo wakaja na hizi tawimu za CIA kuwa Wakrsto ni wengi
Tanzania.

Hili swali liliwekwa mwisho kwa makusudi ili linishinde kwa hiyo nishuke pale ulingoni kichwa chini.
Nilisimama kwa sekunde chache swali limenishtua.

Nilijua takwimu zangu hazitafua dafu mbele ya takwimu za CIA.
Niliomba dua Allah anisitiri nisiadhirike mbele ya hawa Wazungu.

Naam jibu lilikuja hapo hapo.
Jibu ambalo hata siku moja halikupata kunipitikia katika fikra zangu.

Nilianza kwa mimi kuwauliza wao swali kuwa katika historia ya dunia kuna nchi yoyote ambayo
raia ''minority,'' walishika silaha kupambana na ukoloni?

Nikaendelea kuwaeleza kuwa kuhusu Vita Vya Maji Maji na mashujaa wake akina Sultani Abdul
Rauf Songea Mbano
na vipi historia hii inavyo hujumiwa ili kuufuta Uislam katika ukombozi wa
Tanganyika na katika Vita Vya Maji Maji dhidi ya ukoloni wa Wajerumani.

Nikaendelea nikawaambia waisome historia ya African Association na TANU na waangalie nani
walikuwa mstari wa mbele katika siasa za utaifa na siasa za kupigania uhuru.

Nikawaambia Waislam ndiyo waasisi wa harakati zote hizo kwa kuwa wao ndiyo walikuwa, ''majority,''
katika Tanganyika.

Nikamaliza kwa kuwauliza inawezekana vipi, ''minority,'' wawaongoze, ''majority,'' katika haya yote?
Je ingewezekana kwa India harakati za uhuru zitawaliwe na Waislam ambao ni, ''minority'' ukiwalinganisha na Wahindu?

Nikahitimisha kwa kusema kuwa siku zote Waislam hawajapata kuwa pungugu si katika Tanganyika wala Tanzania.

Ukumbi ulikuwa kimyaaa.
Ungeangusha sindano ungesikia mlio wake.

Nilishuka ulingoni kichwa nimekiweka chini si kwa aibu ya kushindwa ila kwa shukrani kwa muumba
wangu.

Katika ukumbi ule kulikuwa na vijana sasa maprofesa ambao walipata kuja Tanga kunihoji kuhusu
historia ya Tanzania wakati wanafanya Ph D lakini sasa nikiwaangalia wamekuwa watu wazima.

Wakati ule walikuwa bado watoto vijana wadogo.

Hapo hapo nikaombwa kwenda kufanya mhadhara kama ule Northwestern University, Evanston Chicago.

Hawa Northwestern University ndiyo mabingwa wa African History ulimwengu mzima.
Nilkwenda na nikafanya mhadhara katika ukumbi wa Eduardo Mondlane.

Hivi ndivyo nilivyoumaliza ubishi wa takwimu za CIA na wingi wa Waislam Tanzania.
 
Umejaa Chuki Za kidini Haitakusaidia. Mbona Zanzibar ni sehemu ya Tanzania hakuna kiongozi mkiristo hujawai kusikia wakristo wakilalamika? Acha ubaguzi
Frey,
Unataka Zanzibar wawepo viongozi Wakristo.
Labda nikuulize swali.

Katika historia ya Zanzibar ya kudai uhuru ulipata kusikia kama kulikuwa
na kiongozi Mkristo akipigania uhuru wa Zanzibar?

Sasa wapi atapatikana huyo kiongozi Mkristo hii leo?

Ndiyo maana Maalim Faiza hukuulizeni watu mfano wa wewe hivi nyie mmesoma
kweli?
 
Back
Top Bottom