Mohamed Said ''Mzungu wa Unga,'' 2007 Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere

Mohamed Said ''Mzungu wa Unga,'' 2007 Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere

Prince...nimekueleza lazima kwanza ufahamu kwa nini iliundwa BAKWATA ndipo utakuwa katika hali ya kufanya mjadala wa maana.

Ikiwa hujui jana yako kamwe hutoijua leo yako.

Historia ni mwalimu mzuri wa kufundisha na kukuelewesha kwa nini leo uko hivi ulivyo.

Ingekuwa bora ukaachana na ulalamishi ukafanya ya muhimu kwa sasa kusaidia hao unaona wanaonewa. Wanachohitaji ni elimu. Elimu ndiyo inayowafanya wawe wachache katika nyadhifa za juu. Tunazungumzia watu wanaogomea sensa ya taifa. Watu wanaogomea kuchukua vitambulisho vya taifa. Na wanakatazwa na mashehe wasio na elimu ya shule. Watu ambao wakiwa masikini wanaamini Mungu kawapangia wawe masikini.

Mtikila alikuwa anakamatwa. Gwajima kalala central. Ingekuwa Gwajima ni shehe ungesema waislamu wanaonewa. Halafu unatoa mifano ya kusadikika. Mapdri hawatakaa wafanye mikutano ya vurugu iliyofanywa na mashehe wa Zanzibar. Na wakifanya hivyo na wao watakamatwa.
 
Prince...hili ndilo tatizo kubwa anaetakiwa kuwakabili Waislam wakajadili hayo usemayo wako kimya kwa kuwa wanaujua ukweli na ushahidi uliopo mikononi kwa Waislam.

Kwao hili ni jambo zito na linawatisha sana na ndiyo kisa cha kukipiga marufuku kitabu cha Njozi maana ushahidi wote uko mle.

Wahimize wahusika wakuu wafungue mjadala tuyazungumze matatizo haya.

Wewe si mzungumzaji wa haya kwani wenyewe wapo.
 
Sheikh Said tatizo la waislamu ni masheikh. Masheikh wengi hawakusoma shule na hawana kazi. Chochote cha maendeleo wasichokijua mashehe hawa wanakiharamisha. Utakuta shehe hana kazi na ana wake wanne wasio na kazi. Mwisho wa siku ni ubabaishaji na kula mali za waislamu.

Wewe uliebahatika kusoma shule na ukatembea na kuiona dunia unajukumu kidini na dhima kubwa mbele ya Mungu kuwaelimisha waislamu.

Tafuta mashehe wenzio waliosoma shule mchukue uongozi BAKWATA ili muweze kutoa muongozo halali bila ya kuonekana ni wachochezi au wavurugaji wa amani.

Wafundisheni waislamu waache kucheza kibati watumie benki. Waelimisheni si kila interest ya benki ni riba au haramu. Waislamu watambue tofauti ya interest na usury. Wafundishe waislamu inflation. Aliyokopa shilingi 100 mwaka 1980 akilipa 100 leo atakuwa kafanya dhuluma. Lakini aliyekopa kilo ya mchele mwaka 1980 akilipa kilo ya mchele leo atakuwa kalipa haki. Waislamu waelimishwe kuwa na bima. Wewe mwanahistoria ungefundisha historia yenye tija. Wafundishe waislamu kuwa bima ilianzishwa na wafanyabiashara wa kiislamu waliokuwa wakipakia mizigo kwenye majahazi. Wakajiuliza jahazi likizama watapataje fidia ya mali zao.

Waelimishe waislamu kuwa mwanamke mahali pake si jikoni. Kila siku kuna mashehe hotuba zao zinarushwa kwenye mitandao. Wanafundisha upumbavu mpaka jinsi ya kumtekenya mke.

Kuna mashehe walikataza watu kuhesabiwa. Kuna mashehe wanakataza watu kupiga kura. Ni juu yako sheikh Said kama kweli una nia ya kutetea waislamu kupambana na hawa mashehe ubwabwa wanaopoteza dira ya maendeleo kwa waislamu. Hiyo hofu yako ya waislamu kuonewa itatimia zaidi waislamu wakigoma kugombea uongozi na wakigoma kupiga kura halafu nchi ikamatwe na upande wa pili kikamilifu. Tanzania itakuwa kama Zambia.

TV zipo za dini na za dunia. Anzisha kipindi na jina la kipindi nakupa “Uislamu na Maendeleo” uwaelimishe waislamu ya kufanya huko tunakokwenda.

Topiki ni nyingi sana za kufundisha. Wakristo hawana tatizo hili kwa sababu wachungaji wamesoma shule.

Historia ya Abdulwahid Sykes na Nyerere sasa tena basi. Yamepita hayo sheikh wangu.
 
Prince...
Waislam walishachukua uongozi wa BAKWATA 1981 na wakaweka mipango madhubuti ya elimu kwa kuzibadilisha shule zao Kinondoni, Kibohehe na nyinginezo kuwa seminari.

Kwa mara ya kwanza shule hizi zilitoa Div. 1.

Hiki ni kisa kirefu kinachoshabihiana na mkasa wa East African Muslim Welfare Society (EAMWS).

Kwa ufupi amri ilitoka juu kuwa hizo shule zifutwe kuwa seminari na uongozi mpya ulioingia madarakani uondolewe.

Haikuishia hapo uongozi huu ambao ulikuwa wa vijana waliomaliza Chuo Kikuu wapigwe marufuku kuongoza taasisi yoyote ya Kiislam.
 
Prince...
Waislam walishachukua uongozi wa BAKWATA 1981 na wakaweka mipango madhubuti ya elimu kwa kuzibadilisha shule zao Kinondoni, Kibohehe na nyinginezo kuwa seminari.

Kwa mara ya kwanza shule hizi zilitoa Div. 1.

Hiki ni kisa kirefu kinachoshabihiana na mkasa wa East African Muslim Welfare Society (EAMWS).

Kwa ufupi amri ilitoka juu kuwa hizo shule zifutwe kuwa seminari na uongozi mpya ulioingia madarakani uondolewe.

Haikuishia hapo uongozi huu ambao ulikuwa wa vijana waliomaliza Chuo Kikuu wapigwe marufuku kuongoza taasisi yoyote ya Kiislam.

Mwaka 1981 enzi za marehemu shehe msomi wa chuo kikuu sheikh Muhammad Ali. Sikumbuki kama alitolewa BAKWATA na serikali. Na kwanini mlitaka ziwe seminary wakati seminary za wakristo zilitaifishwa kuwa za serikali.
Mimi si mzuri wa historia. Yaliyopita si ndwele tugange yajayo. Utawala umebadilika hata huko Vatican siku hizi wana Papa asiye taliano. Vaeni jezi mashehe mliosoma shule muokoe uislamu.
 
Busara lazima itangulie jazba popote pale. Mkiwapa mujahidina uongozi hakuna watakacholeta zaidi ya fujo.
 
Mtu...
Njozi katika kitabu chake kaeleza vipi Sheikh Mohamed Ali alivyofukuzwa BAKWATA.
 
Prince...
Huna uwezo wa kujadili haya.
Wahusika wakuu wenyewe wako kimya.
 
Ki usema ukweli hipo hivi wenye MOHAMED SAID MOHAMED wengi sana wapo kwenye list ya wauza madawa ya kulevya na wengi wao ndo wale waarabu koko wapo kwenye kundi la watch list kwenye mitambo na system za uwanja wa ndege na mipakani so yawezekana walivyoingiza passport yako ikamatch jina so uliingizwa kwenye chumba kuhakikiwa kuwa we ni mmoja wapo?
Wenye jina MOHAMED kiukweli hata huku mtaani ni wajanja wajanja fulani hivi(JARIBU KUCHUNGUZA NYENDO ZA WATU WENYE JINA MOHAMED)

Kaka hiyo ni profiling na si vema kuassume hivyo
 
Back
Top Bottom