Mohammed Said na Mapinduzi ya Zanzibar

Mohammed Said na Mapinduzi ya Zanzibar

Mkuu tatizo lako jengine ni kuwa Humuelewi kabisa Karume alikua ni mtu wa aina gani.

Karume alikua ni Dikteta wa kiwango cha Juu sana.

Kassim Hanga alikua ni katika walioongoza mapinduzi ya 1964, na baada ya hapo akatelekezwa na Karume na Nyerere. Walikua na hofu nae kubwa kuwa either angeliweza ku attemp mapinduzi mengine au angelitoa siri za mapinduzi yale.
Hanga anajua alichokifanya ila wapinzani wa SMZ waga hamusemi ukweli
 
Kwahiyo kaka unataka kutuambia hizbu na shamte na waarabu walikua waungwana kuliko babu zetu waliowapindua!!!Na tukuulize kwanini babu zetu waliwapindua sultan na hizbu????

Mkuu Kwani Zanzibar ndio nchi Peke iliyofanyika mapinduzi Afrika? Kwanini Iddi Amini alipindua Uganda? Kwanini Zaire kulifanyika mapinduzi? Burundi je? Seychelles ? Au hufaham kuwa hata Tanganyika Mapinduzi yalifanyika ila hayakufanikiwa baada Serikali ya U.K kuingilia kati.

Mapinduzi ni trend iliyoingia Africa kuanzia miaka ya 50's mwishoni mpaka miaka ya karibuni tu hapa. Hakuna popote pailipokua na sababu za msingi za hayo mapinduzi zaidi ya Tamaa za kisiasa tu.
 
Kaka Mohammed Said,

Kwanza nakuamkia.

Pili, khutba zako kwenye social media zinaendelea kuwapotosha watu kuhusu mapinduzi matukufu ya Zanzibar ya mwaka 1964. Bila ya mapinduzi haya wengi wetu visiwani leo tungelikuwa wakwezi au wateka maji.

Mapinduzi ya Zanzibar hayakumpinduwa Mzanzibari kama unavyosema wewe. Natumai unafahamu vizuri vipi waarabu kutoka Oman walifika kuitawala Zanzibar.

Wa-Omani waliichukuwa Zanzibar kwa nguvu kinyume na matakwa ya Wazanzibari wenyewe baada ya kumshinda mreno, sasa na wao kwanini wasiondoshwe kwa nguvu? Ni kweli kuwa Wa-Omani walimfukuza mreno kutoka Zanzibar, lakini baada ya Wa-Omani kuwarejeshea utawala wao Wazanzibari, walijifanya wao wafalme wa visiwa hivi.

Kwahivyo, kupinduliwa kwa Wa-Omani katika mwaka 1964 ilikuwa ni muendelezo wa events ambazo wao wenyewe Wa-Omani walizianzisha. Wa-Omani walivivamia visiwa vya Zanzibar kwa nguvu na wakajifanya wafalme na kwahivyo kwa wenyeji wa kizanzibari kutafuta msaada 1964 kutoka kwa wamakonde wa Tanga (kama unavyoeleza) ili kuwaondoa wavamizi visiwani mwao hayafanyi mapinduzi ya Zanzibar kuwa sio halali.

Tanzania tuliwasaidia wapigania uhuru kutoka Msumbiji, South Africa, Zimbabwe, etc. je, ushindi wao sio halali leo kwasababu walisaidiwa na watu kutoka nje? Kumwita jirani yako kuja kukusaidia kumtoa alievamia nyumba yako ni kosa?

Kama Wa-Omani walikuwa wenye nia njema, basi baada ya kumuondosha mreno visiwani wangeliwarejeshea wenyewe Wazanzibari utawala wao na sio wao Wa-Omani kujifanya wafalme kwa nguvu zao.

Eti unasema mfalme wa Zanzibar hata siku moja hajamuuwa muafrika hata mmoja. Are you in your proper senses Sir? Umesahau waafrika walivyokuwa wakikandamizwa kielimu visiwani? Muafrika gani alikuwa akipata nafasi ya kuingia secondary school? Hao akina Jumbe na Ali Hassan Mwinyi sio ilikuwa ni fluke tu? Kumuuwa mtu kwani ni lazima umtie kisu au kumnyonga kwa kamba?

Leo tunamshukuru Mola kwenye familia yetu tuna PhD moja, Masters 2, bachelors karibu zitakuwa 3 kwani mmoja yupo mwaka watatu akielekea kwenye graduation yake. Hivyo chini ya huyo Sultani wako asieuwa watu tungelifikia level hii? Inasikitisha mtu kama wewe mwenye kufahamu mambo kutoa mifano isiyokuwa na maana.
Nakushauri uisome historia ya Mapinduzi ya Zanzibar kutoka katika vyanzo sahihi.
 
Hanga ndie alieongoza mapinduzi, Hilo ndio lilikua kosa lake kuu, Kila alieshiriki kiundani kuandaa yale mapinduzi aliuwawa, kwa ajili ya kupoteza ushahidi.
Hayo maoni yako au utafiti wa kikachero na source zake ni zipi???
 
Mkuu Kwani Zanzibar ndio nchi Peke iliyofanyika mapinduzi Afrika? Kwanini Iddi Amini alipindua Uganda? Kwanini Zaire kulifanyika mapinduzi? Burundi je? Seychelles ? Au hufaham kuwa hata Tanganyika Mapinduzi yalifanyika ila hayakufanikiwa baada Serikali ya U.K kuingilia kati.

Mapinduzi ni trend iliyoingia Africa kuanzia miaka ya 50's mwishoni mpaka miaka ya karibuni tu hapa. Hakuna popote pailipokua na sababu za msingi za hayo mapinduzi zaidi ya Tamaa za kisiasa tu.
Kwahiyo babu zetu walikua hawanyanyasiki na waarabu na vizazi vyao vya machotara wsliowafanya wabantu kua raia wa tabaka la chini???Ni tamaa za kisiasa tu sababu sultan na hizbu walikua wema kwa wabantu kaka?????Tujuze kidogo mema ya sultani kaka???
 
mkuu mbona mpaka vitabu vipo, tatizo lako umekua obsessed na propaganda uchwara za CCM.
Kaka hivyo vitabu aliandika nani?????Na huyo mwandishi lengo lake ni nini????Au vile vitabu vya mzee wangu said mohamed!!!!!Na mkuu kwahiyo tuamini kila kitu kinachoandikwa kwenye vitabu tusihoji kaka????
 
Kaka hivyo vitabu aliandika nani?????Na huyo mwandishi lengo lake ni nini????Au vile vitabu vya mzee wangu said mohamed!!!!!Na mkuu kwahiyo tuamini kila kitu kinachoandikwa kwenye vitabu tusihoji kaka????

nahicho unachokiamini wewe unahisi kimetoka wapi? kama si masimulizi kutoka kwa watu wa upande fulani. Unachotakiwa ni kupitia historia za pande zote huku ukiwa na fikra huru na ndipo utakapoona akili inafunguka kuona ukweli.
 
Kwahiyo babu zetu walikua hawanyanyasiki na waarabu na vizazi vyao vya machotara wsliowafanya wabantu kua raia wa tabaka la chini???Ni tamaa za kisiasa tu sababu sultan na hizbu walikua wema kwa wabantu kaka?????Tujuze kidogo mema ya sultani kaka???

hiyo ni mada nyengine kabisa mkuu. Waarabu waliishi Zanzibar na Maeneo ya Pwani na wazee wakiafrika waliokua wakiishi maeneo hayo kwanini waliwapenda waarabu? kwanini wamekua ndio role models wao na mpaka dini yao wakaifuata? mtu mmbaya kupindukia anakuaje na influence kwenye jamii kiasi hicho? Kuanzia mavazi, dini, chakula, Ustaarbu. Mbona hatuoni hilo kwa wareno na wajerumani katika influence katika jamii?
Sisemi waarabu kama walikua ni watu watukufu ili napinga hizo propaganda uchwara za kuwachafua kupindukia tulizolishwa.

Unapoambiwa changanya na zako.
 
nahicho unachokiamini wewe unahisi kimetoka wapi? kama si masimulizi kutoka kwa watu wa upande fulani. Unachotakiwa ni kupitia historia za pande zote huku ukiwa na fikra huru na ndipo utakapoona akili inafunguka kuona ukweli.
Upo sahii lakini tatizo la baadhi ya watu hasa waarabu na machotara wenye nasaba za kiarabu na wafuasi wa hizbu na maswaiba wao wa kibantu wanapondea upande mmoja tu SMZ hasa kwenye vitabu vyao!!!Mimi siamini upande wowote kishabiki ila katika hili dhulma ya walowezi wa kiarabu na wakoloni dhidi ya wabantu wa zanzbar ipo wazi toka karne na karne
 
hiyo ni mada nyengine kabisa mkuu. Waarabu waliishi Zanzibar na Maeneo ya Pwani na wazee wakiafrika waliokua wakiishi maeneo hayo kwanini waliwapenda waarabu? kwanini wamekua ndio role models wao na mpaka dini yao wakaifuata? mtu mmbaya kupindukia anakuaje na influence kwenye jamii kiasi hicho? Kuanzia mavazi, dini, chakula, Ustaarbu. Mbona hatuoni hilo kwa wareno na wajerumani katika influence katika jamii?
Sisemi waarabu kama walikua ni watu watukufu ili napinga hizo propaganda uchwara za kuwachafua kupindukia tulizolishwa.

Unapoambiwa changanya na zako.
Wewe umejuaje wazee wetu wa pwani waliwapenda waarabu kuamini katika uidlamu nakuchukua tamaduni za kiarabu ndio kumekuhakikishia kua babu zetu wsbantu wa pwani waliwapenda waarabu kaka???
 
hiyo ni mada nyengine kabisa mkuu. Waarabu waliishi Zanzibar na Maeneo ya Pwani na wazee wakiafrika waliokua wakiishi maeneo hayo kwanini waliwapenda waarabu? kwanini wamekua ndio role models wao na mpaka dini yao wakaifuata? mtu mmbaya kupindukia anakuaje na influence kwenye jamii kiasi hicho? Kuanzia mavazi, dini, chakula, Ustaarbu. Mbona hatuoni hilo kwa wareno na wajerumani katika influence katika jamii?
Sisemi waarabu kama walikua ni watu watukufu ili napinga hizo propaganda uchwara za kuwachafua kupindukia tulizolishwa.

Unapoambiwa changanya na zako.
Hakuna propaganda waarabu walowezi hawakuwahi kuwapenda wabantu!!!Wao walikua daraja la juu na wabantu watwana na vijakazi kwenye nyanja nyingi tu kaka
 
nahicho unachokiamini wewe unahisi kimetoka wapi? kama si masimulizi kutoka kwa watu wa upande fulani. Unachotakiwa ni kupitia historia za pande zote huku ukiwa na fikra huru na ndipo utakapoona akili inafunguka kuona ukweli.
Mimi msomi siamini katika vitabu bali nachimba historia kisomi!!!!Na sio dhambi kusema mabaya ya walowezi wa kiarabu unguja na pemba kaka
 
Upo sahii lakini tatizo la baadhi ya watu hasa waarabu na machotara wenye nasaba za kiarabu na wafuasi wa hizbu na maswaiba wao wa kibantu wanapondea upande mmoja tu SMZ hasa kwenye vitabu vyao!!!Mimi siamini upande wowote kishabiki ila katika hili dhulma ya walowezi wa kiarabu na wakoloni dhidi ya wabantu wa zanzbar ipo wazi toka karne na karne

ipo wazi kwa njia gani?
 
Hakuna propaganda waarabu walowezi hawakuwahi kuwapenda wabantu!!!Wao walikua daraja la juu na wabantu watwana na vijakazi kwenye nyanja nyingi tu kaka
Wewe umejuaje wazee wetu wa pwani waliwapenda waarabu kuamini katika uidlamu nakuchukua tamaduni za kiarabu ndio kumekuhakikishia kua babu zetu wsbantu wa pwani waliwapenda waarabu kaka???

Ili tujue kama wana wapenda tunahitaji ushahidi gani? kuzipenda na kujinasibihisha na mila zao hayo je sio mapenzi?
 
Back
Top Bottom