Mohammed Said na Mapinduzi ya Zanzibar

Mohammed Said na Mapinduzi ya Zanzibar

Kaka Mohammed Said,

Kwanza nakuamkia.

Pili, khutba zako kwenye social media zinaendelea kuwapotosha watu kuhusu mapinduzi matukufu ya Zanzibar ya mwaka 1964. Bila ya mapinduzi haya wengi wetu visiwani leo tungelikuwa wakwezi au wateka maji.

Mapinduzi ya Zanzibar hayakumpinduwa Mzanzibari kama unavyosema wewe. Natumai unafahamu vizuri vipi waarabu kutoka Oman walifika kuitawala Zanzibar.

Wa-Omani waliichukuwa Zanzibar kwa nguvu kinyume na matakwa ya Wazanzibari wenyewe baada ya kumshinda mreno, sasa na wao kwanini wasiondoshwe kwa nguvu? Ni kweli kuwa Wa-Omani walimfukuza mreno kutoka Zanzibar, lakini baada ya Wa-Omani kuwarejeshea utawala wao Wazanzibari, walijifanya wao wafalme wa visiwa hivi.

Kwahivyo, kupinduliwa kwa Wa-Omani katika mwaka 1964 ilikuwa ni muendelezo wa events ambazo wao wenyewe Wa-Omani walizianzisha. Wa-Omani walivivamia visiwa vya Zanzibar kwa nguvu na wakajifanya wafalme na kwahivyo kwa wenyeji wa kizanzibari kutafuta msaada 1964 kutoka kwa wamakonde wa Tanga (kama unavyoeleza) ili kuwaondoa wavamizi visiwani mwao hayafanyi mapinduzi ya Zanzibar kuwa sio halali.

Tanzania tuliwasaidia wapigania uhuru kutoka Msumbiji, South Africa, Zimbabwe, etc. je, ushindi wao sio halali leo kwasababu walisaidiwa na watu kutoka nje? Kumwita jirani yako kuja kukusaidia kumtoa alievamia nyumba yako ni kosa?

Kama Wa-Omani walikuwa wenye nia njema, basi baada ya kumuondosha mreno visiwani wangeliwarejeshea wenyewe Wazanzibari utawala wao na sio wao Wa-Omani kujifanya wafalme kwa nguvu zao.

Eti unasema mfalme wa Zanzibar hata siku moja hajamuuwa muafrika hata mmoja. Are you in your proper senses Sir? Umesahau waafrika walivyokuwa wakikandamizwa kielimu visiwani? Muafrika gani alikuwa akipata nafasi ya kuingia secondary school? Hao akina Jumbe na Ali Hassan Mwinyi sio ilikuwa ni fluke tu? Kumuuwa mtu kwani ni lazima umtie kisu au kumnyonga kwa kamba?

Leo tunamshukuru Mola kwenye familia yetu tuna PhD moja, Masters 2, bachelors karibu zitakuwa 3 kwani mmoja yupo mwaka watatu akielekea kwenye graduation yake. Hivyo chini ya huyo Sultani wako asieuwa watu tungelifikia level hii? Inasikitisha mtu kama wewe mwenye kufahamu mambo kutoa mifano isiyokuwa na maana.
Umechanganya Usultani na Ukoloni, hivi ni vitu viwili tofauti. Usultani ndio ulokomboa Zanzibar dhidi ya wareno ambao ni makatili na ni Wazanzibari wenyewe walomuomba Sultan Said aje kuwaondoa Wareno.

Baadae Zanzibar ikawa chini ya Sultan ndipo ukoloni ulipokuja na kuifanya Zanzibar kuwa protectorate, yaani Waengereza ndio waliokua na nguvu Zanzibar na wao ndio walioleta ubaguzi na hayo madhila unayosema.
 
Hujajibu kitu unarukaruka tu . Wewe unayejitia ulikuwepo jibu swali
Wewe msomi mwenzangu toka mwanzo nimekuambia kua una chuki binafsi na SMZ na una mahaba na sultani wa walowezi wa kiarabu na kizazi chao cha machotara ndio maana unasema hujui chochote kuhusu wakati wa sultani!!!Sasa mimi nitakujibu nini wakatiki historia ya nyuma huijui umsbaki na mahaba tu ya kisaikolojia na kiimani!!!Msomi mwenzangu unategemea kweli tutajadiliana kinagaubaga
 
Umechanganya Usultani na Ukoloni, hivi ni vitu viwili tofauti. Usultani ndio ulokomboa Zanzibar dhidi ya wareno ambao ni makatili na ni Wazanzibari wenyewe walomuomba Sultan Said aje kuwaondoa Wareno.

Baadae Zanzibar ikawa chini ya Sultan ndipo ukoloni ulipokuja na kuifanya Zanzibar kuwa protectorate, yaani Waengereza ndio waliokua na nguvu Zanzibar na wao ndio walioleta ubaguzi na hayo madhila unayosema.
Ebu tupe source za uhakika msomi mwenzetu!!!Vipi wale walowezi na wafanyabiashara wa kiarabu waliomba msaada wa waraabu wenzao kuwaondoa wareno unguja na mombasa na ilikua mwaka gani na seyyid alikuja unguja mwaka gani??????Pili kwa wabantu asilia ambao hawakua machotara vipi waarabu walowezi wa zanzbar na seyid said walikua wanawapa haki sawa kama wao kwa kuanzia kumiliki mali na kuoleana na kumiliki aridhi na kutokuwa wajakazi,watumwa na wapagazi????
 
Umechanganya Usultani na Ukoloni, hivi ni vitu viwili tofauti. Usultani ndio ulokomboa Zanzibar dhidi ya wareno ambao ni makatili na ni Wazanzibari wenyewe walomuomba Sultan Said aje kuwaondoa Wareno.

Baadae Zanzibar ikawa chini ya Sultan ndipo ukoloni ulipokuja na kuifanya Zanzibar kuwa protectorate, yaani Waengereza ndio waliokua na nguvu Zanzibar na wao ndio walioleta ubaguzi na hayo madhila unayosema.
Kwahiyo walowezi wa kiarabu hawakua makatili na wabaguzi!!!!Ebu acha siasa acha udini acha ushabiki bali nijibu kama msomi mwenzangu mwenye weledi
 
Kwani hizi lugha Za bara hazina mseto na machotara wa kiarabu. Au bara hakujawahi kuishi waarabu ?Kumbe nimekuelewa huna kitu ukijuacho zaidi ya ubishi usio mashiko.
Msomi mwenzangu umeshawahi kusikia kibangu bangu,kinyambo,kihaya,kiha,kikinga,kinyalua,kiruga ruga,kichazi,kikwere,kiseta,kizaramo,kipugua,kiluo,kilingala and ect......kina nasaba za kiarabu?????Kaka tunazungumzia lugha hatuzungumzii watu kuoleana na kuzaa machotara!!!Swali lako lilikua kuhusu kimvita,kingazija ,kipemba and ect......!!!!Au umesahau swali lako msomi mwenzangu???
 
Wewe msomi mwenzangu toka mwanzo nimekuambia kua una chuki binafsi na SMZ na una mahaba na sultani wa walowezi wa kiarabu na kizazi chao cha machotara ndio maana unasema hujui chochote kuhusu wakati wa sultani!!!Sasa mimi nitakujibu nini wakatiki historia ya nyuma huijui umsbaki na mahaba tu ya kisaikolojia na kiimani!!!Msomi mwenzangu unategemea kweli tutajadiliana kinagaubaga
Tumekusikia unavyonilisha maneno kinywani mwangu , Sasa jibu swali uliloulizwa
 
Msomi mwenzangu umeshawahi kusikia kibangu bangu,kinyambo,kihaya,kiha,kikinga,kinyalua,kiruga ruga,kichazi,kikwere,kiseta,kizaramo,kipugua,kiluo,kilingala and ect......kina nasaba za kiarabu?????Kaka tunazungumzia lugha hatuzungumzii watu kuoleana na kuzaa machotara!!!Swali lako lilikua kuhusu kimvita,kingazija ,kipemba and ect......!!!!Au umesahau swali lako msomi mwenzangu???
Yaani hizo lugha hazina hata neno la kiarabu ,Hongera sana
 
Tanja mzanzibari mmoja aliyeuwawa kwa kupinga serikali? Au kunajisiwa au kuchukuliwa Mali yake
Sasa huo utoto msomi!!!!Basi sawa sultani seyid na watoto wake na wajukuu wake walikua watu wema sana kwa wabantu wa zanzbar ila akina karume walikua na wivu na wauaji ndio maana wakawapindua walowezi wa kiarabu upo sahii kaka!!!!
 
Nani aliyemweka Nyerere madarakani baada ya kupinduliwa na wanajeshi waafrika? Au nao walikuwa walowezi wa kiarabu?Unafikiri Mzungu hukufanyia Bure tu ?
Kaka mrengo wako unajulikana ndio maana unaona tu ya walowezi wa kizungu ila ya walowezi wa kiarabu huyaoni sababu una mahaba nao kaka!!
 
Wakati wa Sultani sikupatapo kuona mtu kauliwa au kupigwa na majeshi au mapolisi. Sultani hatujasikia kanunua meli mtumba pesa zikaibiwa. Hatujasikia mtu aliiba mkungu wa ndizi au shina la muhogo kwa njaa, hatukusikia mtu kunajisiwa kwa sababu ya kuwa chama pinzani wala majeshi au polisi kutesa watu au watu kukimbia nchi
Sultani yupi kaka au unawazungumzia masultani hawa hawa wa kiarabu wenye asili ya omani!!!!Haupo serious kaka na haujui historia unaleta ushabiki wa kidini na kisiasa!!!Sasa wasomi hatujadili au kutazama mambo hivyo kaka
 
Sultani yupi kaka au unawazungumzia masultani hawa hawa wa kiarabu wenye asili ya omani!!!!Haupo serious kaka na haujui historia unaleta ushabiki wa kidini na kisiasa!!!Sasa wasomi hatujadili au kutazama mambo hivyo kaka

Tumekusikia sasa wewe unayeijua historia jibu swali . Kwani tunaongelea Sultani yupi ?? kama wewe uko serous ,
 
Kaka mrengo wako unajulikana ndio maana unaona tu ya walowezi wa kizungu ila ya walowezi wa kiarabu huyaoni sababu una mahaba nao kaka!!
Kwani mrengo wako haujulikani ?? Nimekuuliza taja nani Sultani Jemshid alimchukulia mali yake au kumuuwa kwa kujiunga na ASP au kunajisiwa familia yake au kununua meli ya mtumba au kujijengea majumba ya kifahari
 
Wewe una mapenzi na kanisa na walowezi na machotara wa kizungu
Kanisa na misikiti walileta wao wageni akina sultani na wadachi wa ulaya nitakuaje na mapenzi na watu walionyanyasa babu zangu unguja pemba na tanganyika bara kaka????
 
Mimi msomi nina mapenzi na ubantu sema nyie ndugu zangu na wabantu wenzangu mmekua brain washed!!!Sina mapenzi na wazungu,waarabu,wahindi,wayahudi,wachina na dini zao pia!!!!

Kama una mapenzi na ubantu jee wale waliompindua Nyerere mbona huwaungi mkono ??
 
Ebu tupe source za uhakika msomi mwenzetu!!!Vipi wale walowezi na wafanyabiashara wa kiarabu waliomba msaada wa waraabu wenzao kuwaondoa wareno unguja na mombasa na ilikua mwaka gani na seyyid alikuja unguja mwaka gani??????Pili kwa wabantu asilia ambao hawakua machotara vipi waarabu walowezi wa zanzbar na seyid said walikua wanawapa haki sawa kama wao kwa kuanzia kumiliki mali na kuoleana na kumiliki aridhi na kutokuwa wajakazi,watumwa na wapagazi????
Unajua nyie mnachanganya mambo. Hizo ni propaganda za waliopindua kujastify mapinduzi. Lakini ukae ukijua Sultan hakua na nguvu Zanzibar na iliopinduliwa ilikua ni serekali iliochaguliwa kidemokrasia chini ya Waziri Mkuu Shamte ambae alikua ni muafrika sio muarabu. Halafu hao waarabu mnasema makatili mliweza vipi kuwapindua bila upinzani wowote,
 
Back
Top Bottom