Mombasa: Kondakta wa basi la shule mbaroni kwa kudaiwa kumbaka mtoto wa miaka 5

Mombasa: Kondakta wa basi la shule mbaroni kwa kudaiwa kumbaka mtoto wa miaka 5

Sam Gidori

Senior Member
Joined
Sep 7, 2020
Posts
165
Reaction score
417
Polisi katika Mji wa Mombasa nchini Kenya wanamshikilia kondakta wa Basi la Shule kwa madai ya kumbaka mwanafunzi mwenye umri wa miaka mitano alipokuwa akimpeleka nyumbani kutoka shule.

Mwanafunzi huyo wa Shule ya Msingi Maryjoy mjini humo alikuwa akirudishwa nyumbani, na anadaiwa kubaki peke yake kwenye basi baada ya wenzake wote kuwa wameshushwa majumbani mwao, ndipo Kondakta huyo alipotumia mwanya huo kumwingilia kingono hapo Mei 18.

“Tulimwandaa kama kawaida asubuhi, na aliporudi alipokelewa na mfanyakazi wetu ambaye aligundua kasoro katika mwendo wake,” amesema Baba wa mtoto huyo.

Baada ya ripoti ya Hospitali kuthibitisha kuingiliwa kimwili kwa mtoto huyo, mtuhumiwa anashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Miembeni akisubiri kupandishwa kizimbani.

Uongozi wa Shule umesema hauelewi namna tukio hilo lilivyotokea, ikidai basi liliondoka shuleni likiwa na wanafunzi 28 na waalimu 6 wa kike. Umedai kuwa haiwezekani mwanafunzi huyo kubaki peke yake kwenye basi wakati kulikuwa na wenzake waliotakiwa kushushwa majumbani baada yake.

Mzazi wa mtoto amewasihi wazazi kuwakagua watoto wao wanapotoka shule.

Chanzo: Nation
 
Yaani dada wa kazi ndo anagundua mtoto kabakwa rip all mothers
 
Five years? Asee huo ni ukatili wa kinyama. Hivi mtu kweli timamu anaweza kufanya huo unyama? 💔
 
Yaani dada wa kazi ndo anagundua mtoto kabakwa rip all mothers
Soma habari vizuri acha mihemko. Dada ndie aliempokea aliporejea kutoka shule na kugundua kuwa hayupo sawa kutokana na mwendo wake.

Pili kama mama ana shughuli zake na wakati mtoto akirejea kutoka shule hayupo ni nani wakumpokea?
 
Huyo kifungo cha maisha ndo kinamsubiri tu. Asahau inje,dadeq. Huyu jamaa na Alshabab, hakuna tofauti... 🤬
 
Soma habari vizuri acha mihemko. Dada ndie aliempokea aliporejea kutoka shule na kugundua kuwa hayupo sawa kutokana na mwendo wake.

Pili kama mama ana shughuli zake na wakati mtoto akirejea kutoka shule hayupo ni nani wakumpokea?
Kwann huyo dogo asiseme kwamba alibakwa akaamua kukaa kimya
Soma habari vizuri acha mihemko. Dada ndie aliempokea aliporejea kutoka shule na kugundua kuwa hayupo sawa kutokana na mwendo wake.

Pili kama mama ana shughuli zake na wakati mtoto akirejea kutoka shule hayupo ni nani wakumpokea?
 
Majirani mnasikitisha sana.

Mji wa Mombasa ulivyojaa wanawake vile mnawaacha mnaenda kufanya vitendo vya aibu.
 
Soma habari vizuri acha mihemko. Dada ndie aliempokea aliporejea kutoka shule na kugundua kuwa hayupo sawa kutokana na mwendo wake.

Pili kama mama ana shughuli zake na wakati mtoto akirejea kutoka shule hayupo ni nani wakumpokea?
Wewe ndo hujasoma vizuri huyu mtoto alibakwa jion akitoka shule kesho yake dada anapomuandaa kwenda shule anapomsindikiza akagundua mwendo umebadilika ndo akagundua kuwa mtoto alibakwa ina maana usiku mzima mama hakugundua kuwa mwanae kabakwa wamama tengeni muda wa kukaa na watoto wenu ubize does not give you an excuse mama mzembe.

Kama hamna muda wa kula mnazaa watoto wa nn bure kabisa.
 
Wewe ndo hujasoma vizuri huyu mtoto alibakwa jion akitoka shule kesho yake dada anapomuandaa kwenda shule anapomsindikiza akagundua mwendo umebadilika ndo akagundua kuwa mtoto alibakwa ina maana usiku mzima mama hakugundua kuwa mwanae kabakwa wamama tengeni muda wa kukaa na watoto wenu ubize does not give you an excuse mama mzembe.

Kama hamna muda wa kula mnazaa watoto wa nn bure kabisa.
Una akili kweli? Unajua kusoma kweli? Na je kama unajua kusoma unaelewa unachosoma kweli?

“Tulimwandaa kama kawaida asubuhi, na aliporudi alipokelewa na mfanyakazi wetu ambaye aligundua kasoro katika mwendo wake,” amesema Baba wa mtoto huyo.

UBONGO WAKO MZITO SANA.
 
Back
Top Bottom