Monitoring thread: John Pombe Magufuli katika Awamu ya Nne

Monitoring thread: John Pombe Magufuli katika Awamu ya Nne

it seems Magufuli ni mtu mwoga sana. Yaani muuaji akutishie kwa kukuandikia sms. Ni kitu ambacho hakiwezekani. hao sio wauaji walikuwa wanataka kumtisha tu!
 
Firstlady1, na Wengine

Mmenena. Bahati mbaya sana Watu hawamjui Pombe kwa undani. Ni mtu wa visasi na muonevu. Binafsi wakati akiwa Waziri wa Ujenzi (wakati wa awamu ya tatu) aliniweka ndani pale Central Police kwa siku saba bila dhamana toka tarehe 15/09/2005 mpaka tarehe 22/09/2005 akidai kuwa nimemtishia kumuua. Alituma askari wasiopungua wanne (wakiwa na SMG) kuja kunichukua nyumbani kwangu, wakati huo, pale Kijitonyama Kisiwani.

Mkuu Sabi Pole sana,

Hilo na jambo moja wapo ambalo huyu Magufuli analo..........ni baadhi ya mapungufu yake.........
 
Mkuu Sabi Pole sana,

Hilo na jambo moja wapo ambalo huyu Magufuli analo..........ni baadhi ya mapungufu yake.........

Yah!! ni kweli ila kitu kina uzuri wake na mabaya(mapungufu) yake vilevile,if mazuri yakiwa mengi kuliko mabaya is ok,but if mabaya ni mengi kuliko mazuri,then it is very bad!!!
 
Yah!! ni kweli ila kitu kina uzuri wake na mabaya(mapungufu) yake vilevile,if mazuri yakiwa mengi kuliko mabaya is ok,but if mabaya ni mengi kuliko mazuri,then it is very bad!!!

Ila ni muhimu sana kuangalia aina ya mapungufu ambayo mtu anayo. Pamoja na unyama wa kutisha alionifanyia, binafsi namuonea sana huruma. Pamoja na urafiki wetu wa zaidi ya miaka 15 hawezi kupokea simu yangu. Tuombe MUNGU akiupata huo Urais asije akawafanyia Watanzania wengine mambo ya namna hiyo.
 
Firstlady1, na Wengine

Mmenena. Bahati mbaya sana Watu hawamjui Pombe kwa undani. Ni mtu wa visasi na muonevu. Binafsi wakati akiwa Waziri wa Ujenzi (wakati wa awamu ya tatu) aliniweka ndani pale Central Police kwa siku saba bila dhamana toka tarehe 15/09/2005 mpaka tarehe 22/09/2005 akidai kuwa nimemtishia kumuua. Alituma askari wasiopungua wanne (wakiwa na SMG) kuja kunichukua nyumbani kwangu, wakati huo, pale Kijitonyama Kisiwani.

Hicho ni kitu cha kawaida, we kukaa ndani tu siku saba unaona tatizo? hayo ndiyo mambo tunayotaka rais afanye, siyo acheke cheke tu na marafiki na wanafiki, na wewe hujaeleza siri yako, nafikiri ungefungwa tu hadi sasa maana yake ulimfanyia kosa ndiyo maana ukakamatwa na kama ulionewa kwa nini usimchukulie hatua za kisheria? nafikiri 7 days wasn't enough for you.

Huyu kijana ni mchapakazi mzuri sana, tatazo CCM NEC hawawezi kumpitisha na hana chance yoyote kuwa rais wa tanzania sasa kumwongelea hapa ni kupoteza muda tu, mtaendelea na JK wenu awamu inayokuja na msitegemee changes zaidi, mbali ya maumlivu mengine ya miaka 5 ijayo hadi mtakapaotia akili. " I call it Kifungo cha miaka 5 na kazi ngumu"

We have a long way to go comrades.....
 
Wakuu, tujaribu kuupitia utendaji wa Magufuli katika awamu ya nne na kwa kuanzia naanza na makala hii kutoka gazeti la Tanzania Daima


JANA vyombo vya habari nchini vimechapisha taarifa za ajabu. Taarifa hizi zinasema Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, John Pombe Magufuli, ametishiwa kuuawa na waandishi wa habari.

Waandishi anaowatuhumu ni Mhariri Mtendaji wa Habari Corporation, John Bwire, Mhariri wa Rai, Muhingo Rweyemamu na mwandishi wa Rai, Neophitius Kyaruzi. Ametoa taarifa polisi Dodoma Julai, mwaka huu na kupewa RB namba DO/IR/3085/2006.

Katika mashitaka yake, anasema wahariri hao na mwandishi huyo wamemtishia kwa kutumia SMS kuwa watamuua.

Wao katika utetezi wanasema waliwasiliana naye kupata ufafanuzi juu ya taarifa za barabara ya Usagara hadi Geita, zilizoonyesha kuwa kuna mahali hakutenda kwa usahihi, hali iliyoitia serikali hasara.

Magufuli ni waziri aliyepata heshima kweli katika utawala wa Awamu ya Tatu. Aliaminika kutokana na utoaji wa takwimu zilizowavutia wananchi kuona yu kiongozi makini mwenye kustahili heshima, kwani aliwatumikia wananchi kwa mujibu wa matakwa yao. Alipata kusema ametishiwa maisha katika awamu iliyopita na akapewa ulinzi.

Hata hivyo, kitendo cha Magufuli sasa kudai waandishi wa habari wanataka kumuua, sisi kimetutia wasiwasi. Kimetutia wasiwasi, na Magufuli kwa wadhifa wa ofisi ya umma anayoishikilia tunapaswa kumjadili na kuhoji, amekuwaje hadi anapata fikra na kutenda maajabu kama haya?

Magufuli amekuwa waziri wa kwanza duniani au pengine kiongozi anayepaswa kuingizwa kwenye vitabu vya historia kuthubutu, kudai na kutamka kuwa waandishi wanataka kumuua. Haijapata kutokea duniani mwandishi akataka kumuua kiongozi yeyote.

Waandishi ndio huuawa mara nyingi na takwimu na kumbukumbu zilizo katika fikra zetu sahihi zinaonyesha kuwa mwandishi hawezi kabisa hata kufikiri kumuua mtu, bali wao ndio wamekuwa wakiwindwa.

Hatuwezi kumhukumu moja kwa moja, lakini magazeti yameeleza walichofanya wahariri hao na kauli ya Magufuli na uamuzi wake.

Sisi tunapendekeza uchunguzi wa kesi hii usiishie kwenye kuchunguza SMS, Magufuli na waandishi tajwa, wote wafanyiwe uchunguzi wa akili pia, kuthibitisha kama wanao uwezo na wanaendelea kufanya kazi kwa matarajio ya jamii na taaluma wanazozitumikia; uandishi na siasa.

Bila hivyo, hatudhani kama tutapata jibu sahihi. Inawezekana kama waandishi hawa wemefikia hatua ya kumwinda waziri wamuue, basi wachunguzwe huenda wana matatizo ya akili. Wakibainika waondolewe katika kazi hii kabla hawajaliteketeza taifa, lakini pia Magufuli naye apimwe akili. Ikithibitika kuwa hajatishiwa, ametunga na ana akili timamu, aadhibiwe kwa mujibu wa sheria.

Source: Tanzania Daima
Kwendeni zenu kwani waandishi wa Bongo si wavuta bangi tu? kuna kitu wasichoweza? kama wameshanunuliwa na fisadis watashindwa nini kununua kesi? hii ni dhahiri wanataka kumchafua magufuru washaona JF inamzimikia sasa kilichobaki ni kumuharibia credibility yake! wanataka ku-put his pant on fire!!!! na watashindwa for sure!
 
Waandishi anaowatuhumu ni Mhariri Mtendaji wa Habari Corporation, John Bwire, Mhariri wa Rai, Muhingo Rweyemamu na mwandishi wa Rai, Neophitius Kyaruzi. Ametoa taarifa polisi Dodoma Julai, mwaka huu na kupewa RB namba DO/IR/3085/2006.

Kama kweli hao ndio waandishi walio tajwa hapo ntashangaaa sana kwanza wote wametokea kanda ya ziwa na kama wanachuki ya namna hiyo sijui au kama kuan mtu anataka kuwapambanisha hao watu wa kanda ya ziwa sijui au kuna mkono wa mtu ????
 
Hicho ni kitu cha kawaida, we kukaa ndani tu siku saba unaona tatizo? hayo ndiyo mambo tunayotaka rais afanye, siyo acheke cheke tu na marafiki na wanafiki, na wewe hujaeleza siri yako, nafikiri ungefungwa tu hadi sasa maana yake ulimfanyia kosa ndiyo maana ukakamatwa na kama ulionewa kwa nini usimchukulie hatua za kisheria? nafikiri 7 days wasn't enough for you.

Huyu kijana ni mchapakazi mzuri sana, tatazo CCM NEC hawawezi kumpitisha na hana chance yoyote kuwa rais wa tanzania sasa kumwongelea hapa ni kupoteza muda tu, mtaendelea na JK wenu awamu inayokuja na msitegemee changes zaidi, mbali ya maumlivu mengine ya miaka 5 ijayo hadi mtakapaotia akili. " I call it Kifungo cha miaka 5 na kazi ngumu"

We have a long way to go comrades.....

Tuombe MUNGU
 
Wakuu, tujaribu kuupitia utendaji wa Magufuli katika awamu ya nne na kwa kuanzia naanza na makala hii kutoka gazeti la Tanzania Daima


JANA vyombo vya habari nchini vimechapisha taarifa za ajabu. Taarifa hizi zinasema Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, John Pombe Magufuli, ametishiwa kuuawa na waandishi wa habari.

Waandishi anaowatuhumu ni Mhariri Mtendaji wa Habari Corporation, John Bwire, Mhariri wa Rai, Muhingo Rweyemamu na mwandishi wa Rai, Neophitius Kyaruzi. Ametoa taarifa polisi Dodoma Julai, mwaka huu na kupewa RB namba DO/IR/3085/2006.

Katika mashitaka yake, anasema wahariri hao na mwandishi huyo wamemtishia kwa kutumia SMS kuwa watamuua.

Wao katika utetezi wanasema waliwasiliana naye kupata ufafanuzi juu ya taarifa za barabara ya Usagara hadi Geita, zilizoonyesha kuwa kuna mahali hakutenda kwa usahihi, hali iliyoitia serikali hasara.

Magufuli ni waziri aliyepata heshima kweli katika utawala wa Awamu ya Tatu. Aliaminika kutokana na utoaji wa takwimu zilizowavutia wananchi kuona yu kiongozi makini mwenye kustahili heshima, kwani aliwatumikia wananchi kwa mujibu wa matakwa yao. Alipata kusema ametishiwa maisha katika awamu iliyopita na akapewa ulinzi.

Hata hivyo, kitendo cha Magufuli sasa kudai waandishi wa habari wanataka kumuua, sisi kimetutia wasiwasi. Kimetutia wasiwasi, na Magufuli kwa wadhifa wa ofisi ya umma anayoishikilia tunapaswa kumjadili na kuhoji, amekuwaje hadi anapata fikra na kutenda maajabu kama haya?

Magufuli amekuwa waziri wa kwanza duniani au pengine kiongozi anayepaswa kuingizwa kwenye vitabu vya historia kuthubutu, kudai na kutamka kuwa waandishi wanataka kumuua. Haijapata kutokea duniani mwandishi akataka kumuua kiongozi yeyote.

Waandishi ndio huuawa mara nyingi na takwimu na kumbukumbu zilizo katika fikra zetu sahihi zinaonyesha kuwa mwandishi hawezi kabisa hata kufikiri kumuua mtu, bali wao ndio wamekuwa wakiwindwa.

Hatuwezi kumhukumu moja kwa moja, lakini magazeti yameeleza walichofanya wahariri hao na kauli ya Magufuli na uamuzi wake.

Sisi tunapendekeza uchunguzi wa kesi hii usiishie kwenye kuchunguza SMS, Magufuli na waandishi tajwa, wote wafanyiwe uchunguzi wa akili pia, kuthibitisha kama wanao uwezo na wanaendelea kufanya kazi kwa matarajio ya jamii na taaluma wanazozitumikia; uandishi na siasa.

Bila hivyo, hatudhani kama tutapata jibu sahihi. Inawezekana kama waandishi hawa wemefikia hatua ya kumwinda waziri wamuue, basi wachunguzwe huenda wana matatizo ya akili. Wakibainika waondolewe katika kazi hii kabla hawajaliteketeza taifa, lakini pia Magufuli naye apimwe akili. Ikithibitika kuwa hajatishiwa, ametunga na ana akili timamu, aadhibiwe kwa mujibu wa sheria.

Source: Tanzania Daima
Mbona hakumhoji wakati spika ambaye tayari anaulinzi lakini aliomba kuimarishwa kwa ulinzi kutokana na taarifa za mitandao na magazeti tu. Usione ya ajabu ya musa tu bali kuna firauni vilevile
 
haya magazeti unayoyataja ni ya nani? Tupe jina la mwenyewe nasi tutajuwa pumba na mchele.
Msisumbuke bure ni ya rost zizi, sasa cha ajabu ni nini? Hivi rost anaweza kupikwa chungu kimoja na mwana wa Tanganyika?
Wanaanza kampeni ya kumchafua naye hachafuki ngo,Record yake inamsemea.
 
pombe nampenda ni mcchapakazi mzuri ila mara ingine anafanya kazi kwa jazba na chuki,matokeo yake analiingizia hasara taifa,kuna maamuzi mengi aliyoyafanya wakati ni waziri wa mawasiliano na uhukuzi yalileta hasara kwa taifa,ikabidi serikali ilipe fidia kubwa baada ya kushindwa mahakamani,
 
pombe nampenda ni mcchapakazi mzuri ila mara ingine anafanya kazi kwa jazba na chuki,matokeo yake analiingizia hasara taifa,kuna maamuzi mengi aliyoyafanya wakati ni waziri wa mawasiliano na uhukuzi yalileta hasara kwa taifa,ikabidi serikali ilipe fidia kubwa baada ya kushindwa mahakamani,

Aksante kwa Taarifa ya habari.

u-presidaa hata uweza, zungumzia uwaziri mkuu...

Tukupe wewe u-presidaa
 
watu wengi hawajui upande wa pili wa shilingi wa huyu mheshimiwa.anapenda kuabudiwa sana na usipofanya hivyo unakuwa adui yake mkubwa.kwa asiyeamini aulize wizara yake ya sasa au wizara na taasisi zilizo chini ya wizara ya miundombinu k. tcaa,tanroads watakwambia
 
Aksante kwa Taarifa ya habari.



Tukupe wewe u-presidaa

Jamaa sio mtu mwenye maono.....yeye ni mtu wa fasta fasta tu....hana vision...hana uwezo wa kuchambua mambo!
Kwa maoni yangu, hata viatu vya uwaziri kwake ni vikubwa!
Anaweza kuwa mfuatiliaji sana (ana uwezo mkubwa wa kukariri), ila hamna uwezo wa kuchambua mambo, hana uwezo kujenga sera.......

Urais (hata uwaziri) ni zaidi ya kuwa mfuatiliaji...apaswa kuwa mtu mwenye maono, aone mbali, ajenge sera na ajenga taasisi ya kutekeleza aonayo!
 
Back
Top Bottom