Montero Agrees to US$27 Million Settlement from Tanzania

Endeleeni kumsukumia jumba bovu Mwendazake ili wajanja waendelee kutupiga kisawasawa !

Kweli walisemaga Akili ni mali !
Bado kesi zingine ziko ngapi ??!
Mpaka ajue kumbe alikuwa hajui 😳🙄 !
 
Uhitaji Google kukusaidia unahitaji kujifunza terms za mkataba. Hizo ndio ukivunja unashitakiwa, mahala gani depends mmkataba husika unasemaje.

Unapo sign ‘bilateral treaty’ hiyo ni implied term ya mkataba hata kama sio written on the actual contract; breach watu wanaweza tumia kama inaruhusu kufungua madai nje ya nchi.

Eco-village wametumia Sweden-Tanzania bilateral treaty kukamata hiyo ndege.

Shida yenu kuongelea mambo ambayo hamna abc nayo mnatumia common sense; badala ya discipline knowledge. Ndio maana Lissu anawachota, take it from Lissu hajui mambo ya contract law. Sasa we jichuze siku umpeleke mahakamani uone kama atashinda kesi.

Uwezi kujiandikia vitu tu kutoka kichwani kwako based on common sense rationale, ni lazima ujifunze hata foundation knowledge ya discipline husika.

Umekazana na MIGA kisa Lissu kakwambia tu, leta ushahidi huna. Mimi sijiandikii kama wewe, ila nina abc za contract law in general na nimeandika hayo mambo ya uwekezaji.

Wewe unabisha tu kutumia akili zako mwenyewe lakini huna elementary knowledge ya maswala ya mikataba.

Ndio shida yenu you think you can argue on common sense only kwenye kila kitu.
 
Hayo si makusanyo ya mwezi mmoja tu TRA. Yanalipika hayo.
 
Iwe MIGA au isiwe MIGA haibadilishi cho chote, tutaendelea kuchapwa mboko tu na hao wazungu. Kichekesho gani hiki?
Ni kwa sababu wanapeleka watu wasio na uwezo kutetea hizo kesi.

Sakata DPW wanasheria wengi wa Tanzania walishindwa kuelewa ‘IGA’ ni kitu gani, maswala ya mikataba wanasheria wa Tanzania wanapwaya sana.
 
Ni kwa sababu wanapeleka watu wasio na uwezo kutetea hizo kesi.

Sakata DPW wanasheria wengi wa Tanzania walishindwa kuelewa ‘IGA’ ni kitu gani, maswala ya mikataba wanasheria wa Tanzania wanapwaya sana.
Acha uongo mkataba wowote una-mambo ya kuangali ya msingi
  1. Unaangali kodi
  2. Unaangalia vitu vitakavyosababisha mkataba kuvunjwa
  3. Unaangalia mda wa mkataba
  4. Mwekezaji asipotimiza wajibu wake anafanyiwa nini
  5. Kesi zako na mwekezaji mtatumia mahakama za nchi ipi na sheria zipi
Haya nayo tena ni-magumu ayo ya iga na mengine ni mbwembwe tu
 
Wewe umesoma finance na mba mambo ya contract law umesoma wapi
Lissu alishawapambania wananchi bure dhidi ya mgodi wa north mara na alishinda kesi

Wewe unayejua ni kesi ipi ambayo umeipiganja wananchi na ukashinda
 
Chukua huu ushauri utakusaidia kwenye debates, soma kwanza kuhusu topic husika kabla ya kupotezea watu muda.

Unajiandikia tu upuuzi na kuchosha watu, halafu kwenye kichwa chako unadhani umeandika vitu vya maana.

Mkataba una aspects tano:
Offer/acceptance
Consideration
Capacity
Privity
Intention to form legal relation.

Acha kuandika mambo ya kuchosha watu na kutaka wajibu ujinga wako. Kama basics tu hujui utaelewa aina ya terms za mkataba.
 
Hivyo ulivyotaja havina-tofauti na nilivyoandika ni kwamba umetumia tu kingereza

Kuandika mkatana ni art hakuna sheria inasema iwe hivi ila kuna mambo ya msingi lazima yawepo

Tatizo lako umekariri mambo ya darasani ambayo ni tofauti na dunia yaani unachukulia mambo ya academic exercise na mikataba ya kibiashara

Mkataba hauna aspect tano zinaweza zikawa hata 10 kulingana na anayetaka kuandika
Acha kukariri na kutishia watu

Mkataba wa nchi lazima uwe na mambo ya fuatayo
Kodi
Namna ya kuuvunja
Majuku ya kila muhusika kwenye mkataba

Hayo ni mambo machache ambayo yanatakiwa yawepo achana na hizo academic exercise.
 
Utakuwa una shida kichwani sio bure kwa huo un’gan’ganizi wako.

Unataka nijadili mambo ya PSA/Concession agreements wakati hata elementary knowledge ya contract law huna.

Nilishakubaliana na wewe Magufuli ndio kaleta yote haya, bado tu ujaridhika.

Unaandika mambo hata nikikuuliza hiyo ni sehemu ya clause gani uwezi jibu kwa sababu hujui your stabilisation clause to your dispute resolution let alone terms implied by national laws before a breach is persued.

Mimi sijiandikii upuuzi kama wewe nimewasikiliza hao wanasheria kwenye kesi ya Indiana hawana uwezo kabisa hakuna sehemu wamezungumzia issue za performance ya mwekezaji.

Na wewe ndio poyoyo unaendika ujinga mtupu hujui lolote zaidi ya kulałama tu Magufuli ndio kasababisha.

Sio kwamba sitaki tujadiliane kuelimishana ni afya; shida ni kwamba wewe hata abc huna sasa kukueleza hadi upate concept tu ya mkataba dah huo muda sina kwakweli.
 
Tatizo lako umekariri maisha
Kuandika mkataba ni art ingekua kuandika mikataba nikama unavyotaka kuaminisha watu basi mikataba yote ingekua mizuri huku dunia sababu watu wangefuata formula wewe unayoisemea

Ila bahati mbaya tukija mikataba ya kibiashara ya mabilion inahitaji art kubwa sana kuiandika sababu kila mtu/kampuni inajaribu kuvutia kwake

Mfano Tanzania tuliingia mkataba na makampuni ya madini kule kanda ya ziwa ila ni zaidi ya miaka 20 kanda ya ziwa kuna umaskini wa kutisha inamaa kuna mambo ya msingi kwenye mkataba hatukuyazingatia mfano
  1. Kodi mpaka sahivi uchanguaji wa ile migodi kwenye kodi ni mdogo sana hili ni tatizo kubwa sana lililopo kwenye ule mkataba na yale makampuni ya madini
  2. Ile migodi zaidi ya miaka 20 bila hata kujenga smelter hili ni tatizo kubwa la kimkataba ingekua baada ya mda flani labda miaka 5 wajenge smelter ili wasiwe wanapelekea makinikia nje na kujenga smelter ni ela ya kawaida
Hayo mambo mawili kwenye mkata na wale wakina barrick, north mara na wengineo hayakuwepo ndo maana ile migodi haina mchango wa maana kwenye nchi yaani wanazidiwa mpaka na wachimbaji wadogo kwenye kulipa kodi we unaona ni sawa

Wewe balaa ujikite na mambo ya msingi ya mkataba mara umejikita na consideration, capacity na mambo mengine ambayo hayana msaada kwa nchi huku ukiacha maswala ya kodi ambayo ndo ya muhimu kupita maelezo
 
Dogo embu tafuta sinema ya kichina YouTube utoe stress uone sterling anavyo watangwa bad guys, kung fu mpaka hewani.

Huko kwenye mikataba unalazimisha tu hivi kuna commercial agreement isiyo na consideration kweli au unadhani hawa walioweka frameworks ni mataahira wewe peke yako ndio unajua.

Chukua ushauri wa awali soma kwanza abc za maswala husika kabla ya kujadili mambo, hili ni tatizo Tanzania unakuta mtu anabishia kitu ambacho hana uelewa nacho kabisa, kama wewe.

👋
 
Wewe ndiye uliye mjinga mara 1,000,000 maana kwanza ni wazi hujui hata maana ya MIGA...

Kukutoa ujinga tu ni kuwa:

MIGA - Multilateral Investment Guarantee Agency

Formed
: On 12 April 1988

Membership
: 182 countries, Tanzania inclusive

Executive Vice President:
Hiroshi Matano

Parent organization
: World Bank Group

Website
: MIGA.org

In short:
MIGA was established in 1988 as an investment insurance facility to encourage confident investment in developing countries. MIGA is owned and governed by its 182 member states countries worlwide, but has its own executive leadership and staff which carry out its daily operations. Its shareholders are member governments that provide paid-in capital and have the right to vote on its matters. It insures long-term debt and equity investments as well as other assets and contracts with long-term periods. The agency is assessed by the World Bank's Independent Evaluation Group each year.

Vipi kuhusu ICSID?
Masikini nyie machawa wa mama na CCM wa akili na ufahamu hata hamjui kuwa International Centre for Settlement of Investment Disputes [ICSID] - Mahakama ya migogoro ya kimataifa ya kibiashara na uwekezaji ambako huwa mnapelekwa na kuchinjwa kwa sababu ya ujinga wa viongozi wa CCM ni mkono wa MIGA/WB na IMF na Multilateral Financial Institutions zote duniani zinazotoa fedha kama mikopo kwa ajili uwekezaji wa kimataifa....

Kwa ufahamu na uelewa, CCM wote ni wajinga tu....

Kamwe wewe na chawa wenzako hamwezi kujilinganisha na Tundu Lissu kiasi cha kumtukana kwa sababu ya ujinga wenu tu..

Mwenzio mwingine mjinga asiye na akili kabisa yupo humu anaotwa Etwege
 
Wewe ndiye uliye mjinga mara 1,000,000 maana hujui hata maana ya MIGA...

Masikini wa akili na ufahamu wewe unashindwa kuelewa kuwa ICSID ambako mnapelekwa na kuchinjwa ni mkono wa MIGA...

Kukutoa ujinga tu ni kuwa:
Ungekuwa Unafahamu tofauti ya litigation na ADR usingeandika huo upuuzi maana hujui hata ICSID ni chombo cha aina gani kisheria.

Pili unadhani watu wanaweza kukufungulia kesi ya madai tu kama hizo terms sio expressed kwenye contract clauses au mwekezaji nchi yake ina BIT na host nation.

Ili ushitakiwe nje ya nchi hayo mambo lazima either yapo expressed kwenye stabilisation clause ya mkataba husika au watatumia BIT (hiyo term implied by law) kwenye mkataba.

Vinginevyo ukurupuki tu na kuifungulia nchi kesi ya madai popote unapojisikia kama huna BIT wala expressed ADR processes kwenye stabilisation clause hiyo arbitration itakutimua tu.

Ni hivi acheni kukadhania arguments wakati abc za topic husika hamna na kuleta hoja za kutoka vichwani mwenu au za kuambiwa na Lissu.
 
Wakati umefika kwa serikali kuajiri mawakaili toka nje ya nchi. Unakuta jitu linajiita wakili msomi kumbe hata kujieleza au kuitetea nchi hawezi ila akirudi Bongo Kiingereza kiiiingi kama wanafunzi wa UDSM ila hawajuwi lolote. Hii elimu ya kukariri kwa kweli inatulostisha watanzania sana, yaani tunakariri hata namna ya kuishi?
 
Ungekuwa Unafahamu tofauti ya litigation na ADR usingeandika huo upuuzi maana hujui hata ICSID ni chombo cha aina gani kisheria.
The issue in question is Tundu Lissu vs MIGA. Ukasema hajui lolote na tunaomsikiliza hatunazo, au siyo?

Sasa nikuulize: Wewe kwa maelezo yako haya unadhani unazo ngapi kichwani mwako against him?

Unaleta mambo ya litigation & ADR. Tell us how are they related to MIGA & ICSID? Kisha eleza ujinga wa Tundu Lissu uko wapi. Acha kukwepa hoja, simama kwenye hoja ulioianzisha mwenyewe....
Pili unadhani watu wanaweza kukufungulia kesi ya madai tu kama hizo terms sio expressed kwenye contract clauses au mwekezaji nchi yake ina BIT na host nation.
Unaelewa maana ya MIGA & ICSID (their objectives & how they work?). Na unaelewa kuwa Tanzania ni mwanachama hizi multilateral Organizations ambazo ziko chini ya WB...?

After all kwenye hii hoja, hueleweki unazungumzia nini. Maana kama ni kesi za madai Tanzania ina kesi nyingi tu za madai dhidi ya makampuni ya kimataifa ambayo kwa makusudi na ujinga tu wa viongozi wa CCM wali breach mikataba waliyoingia..
Ili ushitakiwe nje ya nchi hayo mambo lazima either yapo expressed kwenye stabilisation clause ya mkataba husika au watatumia BIT (hiyo term implied by law) kwenye mkataba.
Still hueleweki...

Unatumia neno "ili ushitakiwe" wakati nchi yako ndiyo hiyo imeshitakiwa kwa kesi lukuki za madai kwa sbb ya kukiuka mikataba...?

Unajua hueleweki unatetea nini wewe..???
Vinginevyo ukurupuki tu na kuifungulia nchi kesi ya madai popote unapojisikia kama huna BIT wala expressed ADR processes kwenye stabilisation clause hiyo arbitration itakutimua tu.
Ingekuwa ni mwalimu wako na unaandika insha ya namna hii ningekulima 0%. Maana sioni mantiki ya unachoelezea hapa na kutetea...

By the way unaelewa MIGA na ICSID ni kitu gani? Unajua ni kwanini Tanzania imeshitakiwa ICSID na kukutwa na hatia na hivyo kulazimika kulipa mamilioni ya dola kwa kukiuka mikataba ya kimataifa ya wawekezaji...?
Ni hivi acheni kukadhania arguments wakati abc za topic husika hamna na kuleta hoja za kutoka vichwani mwenu au za kuambiwa na Lissu.
ABC za topic ipi ambayo mimi sina lakini wewe unazo...?

The intial topic was about Tundu Lissu na MIGA na ICSID kwa hoja yako kuwa, sisi ni wajinga kwa kuwa tunamsikiliza Tundu Lissu na hoja yake ya MIGA/ICSID...

Lakini the facts which are on the table ni kuwa Tanzania inashitakiwa ICSID kwa sababu sisi (Tanzania) ni member wa MIGA - Multilateral Investment Guarantee Agency na ni member wa - International Centre for Settlement of Investment Disputes [ICSID] which is the evidence kuwa kuna the breach of terms of contracts among the two contractual parties na hivyo lazima mwende kwenye arbitration...

Sasa nakuliza: Kweli au siyo kweli? Nani anapuyanga kwenye mjadala huu? Bila shaka ni wewe. Angalia vizuri na utagundua kuwa hujui kuwa hujui...!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…