Montero Agrees to US$27 Million Settlement from Tanzania

Montero Agrees to US$27 Million Settlement from Tanzania

Kukuuliza haina maana kuwa sijui isipokuwa ni kupata uhakika iwapo wewe unayeyaandika haya mambo unayajua kweli au la...

Nimepata uhakika huo, kwamba, una argue mambo usiyoyajua vyema...

Unaelewa maana ya hayo niliyoya bold..?

"Host Government" inam - host nani...?

"Stabilization clause" ni kitu gani ndugu Mayor Quimby? Mbona unashindwa kutumia ufahamu wako kumwaga ujuzi wako?

Nilikuuliza pia kuwa, how these "stabilization clauses" work and haw they have prevented the nation/country to be sent to ICSID for the breach of these bilateral agreements & contracts...?

Bi - lateral Investment Treaty - simply means ni mkataba wa kimataifa kati ya pande mbili. ..

Mfano, yaweza kuwa kampuni toka nchi/taifa fulani vs serikali ya Tanzania labda kwa shughuli ya uchimbaji wa madini wa kampuni hiyo ndani ya Tanzania...

Mkataba utakaosainiwa na pande hizi mbili utakuwa categorized kama "bilateral treaty" na taasisi zinazolinda uwekezaji wa kimataifa zina sehemu ya kuhusika kwake..

Na infact, wawekezaji wa kimataifa wanakuja nchini kwetu (Tanganyika) kuwekeza kwa sababu wanajua kuwa nchi yetu ni mwanachama wa taasisi za kimataifa za kulinda wawekezaji kama MIGA na ICSIDs...

Na mkiiingia kwenye migogoro ya kimkataba, mtakutana huko ICSID ili kusuluhishwa...

Wewe unasemaje mpaka hapo..?
Acha kaka unajidhiilisha BIT sio kwa specific contracts ni general kwa wawekezaji wote wa nchi husika. Kwa sehemu kubwa na yenyewe ni stabilisation clause.

Sasa hivi mimi mwenyewe naanza kukuhurumia kumbe kilaza hivi.
 
Wanatubamiza bila huruma. Hii ni kampuni ya nne ambazo tatu wameshafikia makubaliano na wameanza kulipwa:
1)Winshear Gold Corp - US$ 30 million
2)Ntaka Hill - US$ 90 million
3)Montero - US$ 27 million
4) Aqua Power na Catalysis Capita. Hii imefungu kesi tarehe 9th October kudai US$ 500 million. Ina shareholders Wakenya.
Hv kesi gani na waekezaji tumewahi kushinda?! Na hatuachi kuwakaribisha wanaoitwa "wawekezaji wa nje" ati waje kuwekeza, kwamba Tz ina maliasili zenye "...fursa tele za kutuletea maendleo ..."Au ni wanaosaini mikataba hawana utaalamu au weledi?! Madeni yamezidi xaxa ...dah!
 
My simple question ndugu Mayor Quimby ambalo hulijibu ni hili👇🏻👇🏻:

Ni kwa vipi hayo yote yameshindwa kuzuia Tanzania kutoshitakiwa huko kwenye mahakama za usuluhuhishi wa migogoro ya kibiashara na uwekezaji wa kimataifa...?

Okay. Let's assume kuwa, hivyo ndivyo ilivyo. Sasa shida iko wapi pamoja na yooote haya unayoeleza...?

Maana unaeleza ooh iko hivi, mara ooh kuna "stabilization clause", mara oooh kuna "bilateral treaty" na blaah blaah zingine kibao lakini wakati huohuo kama nchi tunaliwa na kupigwa kila siku kupitia mikataba hii ya kimataifa. Shida ni nini? Jikite hapo...!!!

Unadhani Tundu Lissu ni nuisance tu kweli pale aliposhauri namna njema ya ku - deal na mambo hayo? Really?

In my opinion:

Toka mwanzo nimekuambia, ukiwa honest, tunaweza kuelewana kirahisi sana juu ya mambo haya....

Tatizo lako ni kuwa, unaji - complicate mwenyewe kwa kuibua mambo magumu unayoshindwa kuyaeleza kwa lugha rahisi, straight na inayoeleweka...

Kwa heri, alfajiri njema..
Mimi sio nakwambia hadithi nimeandika hizo academic reports kwa miaka kama sita za vilaza.

Bado kwenye masomo yangu ni mandatory kuelewa aspects za contract, tort na business law.

Sasa usidhani najiongelea tu kama wewe na mwenzako Lissu. Mpaka sasa kwenye hoja żako kwa level yangu ujavuka hata elementary level, ili tuelekee kwenye maswala ya breach and other nitty gritties

Kadri unavyozidi kuandika ndio unavyoonyesha uwezo wako mdogo.

Anyway your wish is granted, kwangu muda wa kulała. 👋
 
Je
Ni kwa sababu wanapeleka watu wasio na uwezo kutetea hizo kesi.

Sakata DPW wanasheria wengi wa Tanzania walishindwa kuelewa ‘IGA’ ni kitu gani, maswala ya mikataba wanasheria wa Tanzania wanapwaya sana.
wewe Mtanzania mwenzetu kwanini huisaidii Nchi yako pendwa iepukane na hili jinamizi la kushindwa shindwa kesi kila mara ???!
Au wenye kuhusika na hizi deals hawataki kushirikisha watu werevu wenye uelewa mpana wa mambo ya mikataba ???!!!

Nimesoma arguments zako nyingi humu jf zinadai kwamba wanaopelekwa kwenda kusimama upande wa Government katika hizo kesi hawajui kabisa masuala ya mikataba ya kimataifa ndio maana kila kesi tunagaragazwa na mapesa mengi yanakwenda !

Je hapa kuna kiini macho gani kinachoendelea ??!
Kwanini watu kama nyinyi msipewe hizo kazi za utetezi au za ushauri ???!
Au na nyinyi ni watu wa kulalamika tu bila kuwa tayari kukomesha hali Hiyo ??!
Hii inaumiza sana eti kila kesi tunashindwa !!
Je hii itakuwa hivi mpaka lini ???!!
 
Wanatubamiza bila huruma. Hii ni kampuni ya nne ambazo tatu wameshafikia makubaliano na wameanza kulipwa:
1)Winshear Gold Corp - US$ 30 million
2)Ntaka Hill - US$ 90 million
3)Montero - US$ 27 million
4) Aqua Power na Catalysis Capita. Hii imefungu kesi tarehe 9th October kudai US$ 500 million. Ina shareholders Wakenya.
Hiyo namba 4 ni utakatishaji hela mkubwa sana unafanyika towards election period. Ifuatilie utarudi hapa.
 
Tatizo lako umekariri maisha
Kuandika mkataba ni art ingekua kuandika mikataba nikama unavyotaka kuaminisha watu basi mikataba yote ingekua mizuri huku dunia sababu watu wangefuata formula wewe unayoisemea

Ila bahati mbaya tukija mikataba ya kibiashara ya mabilion inahitaji art kubwa sana kuiandika sababu kila mtu/kampuni inajaribu kuvutia kwake

Mfano Tanzania tuliingia mkataba na makampuni ya madini kule kanda ya ziwa ila ni zaidi ya miaka 20 kanda ya ziwa kuna umaskini wa kutisha inamaa kuna mambo ya msingi kwenye mkataba hatukuyazingatia mfano
  1. Kodi mpaka sahivi uchanguaji wa ile migodi kwenye kodi ni mdogo sana hili ni tatizo kubwa sana lililopo kwenye ule mkataba na yale makampuni ya madini
  2. Ile migodi zaidi ya miaka 20 bila hata kujenga smelter hili ni tatizo kubwa la kimkataba ingekua baada ya mda flani labda miaka 5 wajenge smelter ili wasiwe wanapelekea makinikia nje na kujenga smelter ni ela ya kawaida
Hayo mambo mawili kwenye mkata na wale wakina barrick, north mara na wengineo hayakuwepo ndo maana ile migodi haina mchango wa maana kwenye nchi yaani wanazidiwa mpaka na wachimbaji wadogo kwenye kulipa kodi we unaona ni sawa

Wewe balaa ujikite na mambo ya msingi ya mkataba mara umejikita na consideration, capacity na mambo mengine ambayo hayana msaada kwa nchi huku ukiacha maswala ya kodi ambayo ndo ya muhimu kupita maelezo
Una jiabisha asee.
 
Wanatubamiza bila huruma. Hii ni kampuni ya nne ambazo tatu wameshafikia makubaliano na wameanza kulipwa:
1)Winshear Gold Corp - US$ 30 million
2)Ntaka Hill - US$ 90 million
3)Montero - US$ 27 million
4) Aqua Power na Catalysis Capita. Hii imefungu kesi tarehe 9th October kudai US$ 500 million. Ina shareholders Wakenya.
Wanapiga pesa za bure bure tu,
Utapeli mtupu.
 
Alisema kitu gani wewe, upeleke watu wasio na uwezo wa kutetea kesi rahisi halafu umlaumu Magufuli.

Yaani una kibali cha mining toka 2008 bado unafanya exploration mpaka 2018, maana yake huna hiyo hela ya uwekezaji tu zaidi kukalia ardhi.
Kwa nini serikali ya mnawapa wanaoitwa wawekezaji vibali vya aina hii na mikataba ya hovyo hivyo ya hasara kwa taifa?? FaizaFoxy ChoiceVariable chiembe kipara kipya
 
Si ndio maana mnashindwa kesi kila siku, umewahi kuona kesi ya dispute imepelekwa huko MIGA toka uzaliwe au hata umewai sikia ‘claimant’ anataja neno MIGA kama source of breach.

Akili za Lissu kuna wasaa zinamtosha yeye na wafuasi huko CDM.
ICSID ndio hao hao MIGA wewe kilaza.
 
Ilitakiwa warudishiwe Leseni zao kisha wapewe muda waanze kazi na hawaruhusiwi uzia mtu, wakishindwa warudishe kwa mmiliki ambaye ni GoT
 
Una jiabisha asee.
Ndio najiaibisha
Ila ni ukweli kwamba kanda ya ziwa kuna migodi mikubwa ila ni miaka zaidi ya ishirini kuna umaskini wa kutisha

Wazungu kwenye mikataba wanataka mfocus kwenye mambo ambayo hayana maana yeyote
Mambo kama kodi hawataki mfocus nayo sababu hayo ndo yana-manufaa
 
Serikali ina haki ya ku-terminate mikataba ambayo performance airidhishi iwe kupitia sheria au maelezo.

Shida ni wanasheria, usikariri breach zipo tofauti depend on severity kama ni conditional breach, hiyo ni ya termination ya mkataba. Uwezi kukalia ardhi uliyopewa kwa kuwekeza 10 years ujafanya kitu cha maana halafu warranty or lesser breach.
Mlifungua shauri kokote? Kwani mliweka limit of exploration au retention licence? Au mnajiamulia tu kuwa miaka 10 ni mingi na unaenda tu kufuta leseni?

Mambo ya kisheria yanahitaji umakini maana technicalities tu zinaweza kukulipisha faini ya mabilioni
 
Mlifungua shauri kokote? Kwani mliweka limit of exploration au retention licence? Au mnajiamulia tu kuwa miaka 10 ni mingi na unaenda tu kufuta leseni?

Mambo ya kisheria yanahitaji umakini maana technicalities tu zinaweza kukulipisha faini ya mabilioni
Yaani magufuli alikua anatumia hisia kuvunja mikataba alafu huyo mjuaji anayejiita bingwa wa mikataba ana-mtetea
 
Back
Top Bottom