Morogoro: Hospitali yaikataa bili ya maji "hatujatumia maji ya milioni 1.8

Morogoro: Hospitali yaikataa bili ya maji "hatujatumia maji ya milioni 1.8

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Mbunge wa Jimbo la Ulanga, Salim Alaudin Hasham amemtaka Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Ulanga kuangalia miundombinu ya maji katika hospitali ili kurekebisha maeneo yenye mivujo ya maji.

Salim amesema hayo baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika hospitali hiyo na kuoneshwa bili ya maji yenye gharama ya milioni moja na laki nane (M 1.8) kwa mwezi Oktoba jambo ambalo Mbunge huyo hakukubaliana nalo.

Mbunge Salim amesema haiwezekani kuwe na bili yenye gharama kubwa kiasi hicho wakati hata maji hayatoki katika hospitali hiyo ambapo mwezi Septemba bili ilikuwa laki nane (800,000) na mwezi Agosti bili ilikuwa milioni moja na laki nne (M 1.4) ambapo ndani ya miezi mitatu wamepelekewa bili ya zaidi ya Tsh. Milioni nne.

Aidha, Mbunge Salim ameshauri kisima cha pampu cha maji kilichochimbwa katika hospitali hiyo kifufuliwe ili kitumike kusambaza maji katika hospitali hiyo ili kuepusha gharama zisizokuwa za lazima.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Ulanga, Stephano Liwemba amesema bili wanazopewa kutoka idara ya maji haziendani na maji wanayotumia kwa kuwa maji baadhi ya wodi hazifikiwi na na maji.

Liwemba ameeleza kuwa wastani wa matumizi ya maji katika hospitali hiyo kwa mwezi ni laki sita hivyo ameshangazwa na bili zenye ghalama kubwa wanazopewa.

Chanzo: Wasafi FM
 
Huku ni kujipiga ngumi kichwani. Si eti eeh? Hawa Tanesco, hawa. I mean idara ya maji 🙂 Hela tamu, ila kuboresha miundombinu ya maji ni sheeidaa.
 
Mbunge wa Jimbo la Ulanga, Salim Alaudin Hasham amemtaka Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Ulanga kuangalia miundombinu ya maji katika hospitali ili kurekebisha maeneo yenye mivujo ya maji...
Kwa taasisi kama hospitali ni bili ya kawaida sana.

Kama umelaza wastani wa wagojwa 200 kwa mwezi mmoja kila mgonjwa akatumia 5000 tu ni 1M.

Bado usafi wa mawodi kila siku kudeki,wagonjwa wa nje ambao nina uhakika ni zaidi ya 6000 kwa mwezi na watumishi wote wanaoweza kufikia idadi ya 300 au zaidi,kwa nini bili ya maji isifike 1.8M?

Tuacheni siasa kwenye mambo ya msingi
 
Kwa taasisi kama hospitali ni bili ya kawaida sana.
Kama umelaza wastani wa wagojwa 200 kwa mwezi mmoja kila mgonjwa akatumia 5000 tu ni 1M
Bado usafi wa mawodi kila siku kudeki,wagonjwa wa nje ambao nina uhakika ni zaidi ya 6000 kwa mwezi na watumishi wote wanaoweza kufikia idadi ya 300 au zaidi,kwa nini bili ya maji isifike 1.8M?

Tuacheni siasa kwenye mambo ya msingi
Hizi "assumptions" zako na "estimates" kiboko.
 
Back
Top Bottom