DOKEZO Morogoro: Kuharibika kwa daraja la miti la milioni 31

DOKEZO Morogoro: Kuharibika kwa daraja la miti la milioni 31

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Pax Vobiscum

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
450
Reaction score
757
IMG_20221230_054250.jpg


Kwanza tunashukuru Serikali kwa kutuletea daraja la muda kwa wakazi wa kata ya Mngeta, limetusaidia Sana katika kuepukana na adha ya mto Mngeta hasa hasa Tatizo la Mamba.

Hivi karibuni kulifanyika ukabati wa korongo linalojulikana Kama "Madandoni" ktk ukarabati huo wajengaji waliinua tuta kubwa na kufukia makaravati matatu ambayo husaidia kupitisha maji toka upande mmoja kwenda mwingine.

Juzi kuamkia Jana yametokea mafuriko makubwa yaliyoleta madhara makubwa Sana;

1) kuvunjika kwa lile daraja
Hii inanesabishwa na maji kushindwa kupata njia sahihi ya kupita baada ya makaravati matatu Yale kufukiwa hivyo kumpelekea kutafuta njia mbadala na pia kubeba magogo makubwa Hadi kuvunja nguzo za daraja.

2) Kuharibika kwa korongo la Madandoni
Hii imesababishwa na uzembe wa mafundi waliojenga lile tuta kubwa, maji yapojaa yakakosa njia yakaoasua barabara kwenye yale Yale makaravati yake matatu ya Asili,

3) mafuriko mashambani
Kwa kawaida mwezi 12 huwa hauna mafuriko lakini kutokana na uzembe wa wahandisi imepelekea kuleta mafuriko mashambani, watu walishapanda mpunga hivyo wamepata hasara kubwa Sana.

4) kukatika kwa mawasiliano ya miundombinu
Barabara hii inahudumia maelfu wa watu vijiji vingi Sana Mgudeni, Isago, mkangawalo, Ilole, Itongowa, Mngeta, mchombe, Lukolongo n.k kote hutumia daraja hili, kwa Sasa Hali Ni mbaya na Ni ngumu kupitika.

MAOMBI
~ Tunaomba Serikali itusaidie kwa haraka Sana kutatua hii changamoto.

~ Mkuu wa wilaya hatuna (wilaya ya Mlimba), tuna mkurugenzi tu, mbunge Kunambi, Diwani, ofisi ya Tarura, Ofisi ya Waziri mkuu (kitengo Cha maafa) n.k tunaomba msaada wenu haraka ili kutusaidia kupata ufumbuzi wa daraja na lile korongo la Madandoni.

~ Tunaelekea msimu wa mvua kubwa na masika wananchi tutataabika Sana, Mto Mngeta mamba wengi Sana kwa Sasa Ni hatari kubwa iko mbele yetu.

~ Tunaomba Sana hatua za haraka zifanyike kutusaidia wananchi.

Ushauri
~ Tunaomba Serikali isaidie kusimamia mazingira vizuri, watu wanalima Hadi mtoni hii inapelekea kina Cha mto kupungua na kusababisha mafuriko.

Walau watu wangeacha kulima mita 20 Hadi 30 tu nje ya mita 60 zile za sheria ya mazingira ya 2004.

Naambatanisha picha.


IMG_20221229_182836_9.jpg


IMG_20221229_183746_9.jpg

Hii ni picha ya lile korongo linalojulikana Kama Madandoni baada ya kuharibika.

Update
Leo asubuhi daraja limekatika loteee katikati, hakuna mawasiliano kabisa!
IMG_20221230_064222_1.jpg
 
hii nchi ni ngumu sana kuiongoza na kufikia mafanikio tuyawazayoo
 
Kwanza tunashukuru Serikali kwa kutuletea daraja la muda kwa wakazi wa kata ya Mngeta, limetusaidia Sana katika kuepukana na adha ya mto Mngeta hasa hasa Tatizo la Mamba,

Hivi karibuni kulifanyika ukabati wa korongo linalojulikana Kama "Madandoni" ktk ukarabati huo wajengaji waliinua tuta kubwa na kufukia makaravati matatu ambayo husaidia kupitisha maji toka upande mmoja kwenda mwingine,

Juzi kuamkia Jana yametokea mafuriko makubwa yaliyoleta madhara makubwa Sana,
1) kuvunjika kwa lile daraja
Hii inanesabishwa na maji kushindwa kupata njia sahihi ya kupita baada ya makaravati matatu Yale kufukiwa hivyo kumpelekea kutafuta njia mbadala na pia kubeba magogo makubwa Hadi kuvunja nguzo za daraja,
2) Kuharibika kwa korongo la Madandoni
Hii imesababishwa na uzembe wa mafundi waliojenga lile tuta kubwa , maji yapojaa yakakosa njia yakaoasua barabara kwenye yale Yale makaravati yake matatu ya Asili,
3) mafuriko mashambani
Kwa kawaida mwezi 12 huwa hauna mafuriko lakini kutokana na uzembe wa wahandisi imepelekea kuleta mafuriko mashambani, watu walishapanda mpunga hivyo wamepata hasara kubwa Sana,
4) kukatika kwa mawasiliano ya miundombinu
Barabara hii inahudumia maelfu wa watu vijiji vingi Sana Mgudeni, Isago, mkangawalo, Ilole, Itongowa, Mngeta, mchombe, Lukolongo n.k kote hutumia daraja hili, kwa Sasa Hali Ni mbaya na Ni ngumu kupitika,

MAOMBI,
Tunaomba Serikali itusaidie kwa haraka Sana kutatua hii changamoto,

Mkuu wa wilaya hatuna( wilaya ya Mlimba), tuna mkurugenzi tu, mbunge Kunambi, Diwani, ofisi ya Tarura, Ofisi ya Waziri mkuu( kitengo Cha maafa) n.k tunaomba msaada wenu haraka ili kutusaidia kupata ufumbuzi wa daraja na lile korongo la Madandoni,

Tunaelekea msimu wa mvua kubwa na masika wananchi tutataabika Sana , Mto Mngeta mamba wengi Sana kwa Sasa Ni hatari kubwa iko mbele yetu,

Tunaomba Sana hatua za haraka zifanyike kutusaidia wananchi ,

Ushauri,
Tunaomba Serikali isaidie kusimamia mazingira vizuri, watu wanalima Hadi mtoni hii inapelekea kina Cha mto kupungua na kusababisha mafuriko ,

Walau watu wangeacha kulima mita 20 Hadi 30 tu nje ya mita 60 zile za sheria ya mazingira ya 2004,

Naambatanisha picha,

View attachment 2462992View attachment 2462993View attachment 2462995View attachment 2462994View attachment 2462996View attachment 2462997
Force Akaunti oyeeee!
Aitwe PM Majaliwa hapo na TAKUKURU!
 
Juzi kuamkia Jana yametokea mafuriko makubwa yaliyoleta madhara makubwa Sana,
1) kuvunjika kwa lile daraja
Hii inanesabishwa na maji kushindwa kupata njia sahihi ya kupita baada ya makaravati matatu Yale kufukiwa hivyo kumpelekea kutafuta njia mbadala na pia kubeba magogo makubwa Hadi kuvunja nguzo za daraja,
2) Kuharibika kwa korongo la Madandoni
Hii imesababishwa na uzembe wa mafundi waliojenga lile tuta kubwa , maji yapojaa yakakosa njia yakaoasua barabara kwenye yale Yale makaravati yake matatu ya Asili,
3) mafuriko mashambani
Kwa kawaida mwezi 12 huwa hauna mafuriko lakini kutokana na uzembe wa wahandisi imepelekea kuleta mafuriko mashambani, watu walishapanda mpunga hivyo wamepata hasara kubwa Sana,
4) kukatika kwa mawasiliano ya miundombinu
Barabara hii inahudumia maelfu wa watu vijiji vingi Sana Mgudeni, Isago, mkangawalo, Ilole, Itongowa, Mngeta, mchombe, Lukolongo n.k kote hutumia daraja hili, kwa Sasa Hali Ni mbaya na Ni ngumu kupitika,
Wahusika wangeswekwa ndani
 
Morogoro hamjawahi kupata viongozi wanaowasaidia kwa dhati ndio maana mnakila kitu lakini maendeleo yenu mko nyuma, anzia wabunge, wakuu wa wilaya, na DED, na kadhalika wengi wakata viuno na mipasho na sio watendaji
Sahihi kabisa
Mito yote mikubwa inapita Morogoro na mingine inaanzia Morogoro, lakini watu wake wanashida ya maji kuzidi wanaoishi jangwani
 
Nimecheka sana,anyway kuna mdau humu bwana Lucas mwashambwa
Atamfikishia ujumbe bi mkubwa,waje hapo washugulikie hilo tatizo chap

Ova
huyo mwashambwa punga wa kumsifia samia kila siku analeta nyuzi mara SAMIA KAWAVUSHA WATANZANIA VIZURI MWAKA 2022, mara VIJANA WAKO NA MAMA SAMIA hapo kuna akili au matope.
 
Back
Top Bottom