Saint Anne
JF-Expert Member
- Aug 19, 2018
- 76,039
- 230,142
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Update!!
Leo asubuhi daraja limekatika loteee katikati,
Hakuna mawasiliano kabisaView attachment 2463009View attachment 2463010View attachment 2463011
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Update!!
Leo asubuhi daraja limekatika loteee katikati,
Hakuna mawasiliano kabisaView attachment 2463009View attachment 2463010View attachment 2463011
Na majambaziChama cha Majizi
Wasalimie nyandila huko [emoji1]Update!!
Leo asubuhi daraja limekatika loteee katikati,
Hakuna mawasiliano kabisaView attachment 2463009View attachment 2463010View attachment 2463011
Usiwasema hao watu kuwa wamedanganywa ...Ccm imedanganya kila mtuHilo Daraja halina Thamani ya mil 30 ,
Wananchi wa huko mmedanganywa Sana.
Poleni sana.View attachment 2463055
Kwanza tunashukuru Serikali kwa kutuletea daraja la muda kwa wakazi wa kata ya Mngeta, limetusaidia Sana katika kuepukana na adha ya mto Mngeta hasa hasa Tatizo la Mamba.
Hivi karibuni kulifanyika ukabati wa korongo linalojulikana Kama "Madandoni" ktk ukarabati huo wajengaji waliinua tuta kubwa na kufukia makaravati matatu ambayo husaidia kupitisha maji toka upande mmoja kwenda mwingine.
Juzi kuamkia Jana yametokea mafuriko makubwa yaliyoleta madhara makubwa Sana;
1) kuvunjika kwa lile daraja
Hii inanesabishwa na maji kushindwa kupata njia sahihi ya kupita baada ya makaravati matatu Yale kufukiwa hivyo kumpelekea kutafuta njia mbadala na pia kubeba magogo makubwa Hadi kuvunja nguzo za daraja.
2) Kuharibika kwa korongo la Madandoni
Hii imesababishwa na uzembe wa mafundi waliojenga lile tuta kubwa, maji yapojaa yakakosa njia yakaoasua barabara kwenye yale Yale makaravati yake matatu ya Asili,
3) mafuriko mashambani
Kwa kawaida mwezi 12 huwa hauna mafuriko lakini kutokana na uzembe wa wahandisi imepelekea kuleta mafuriko mashambani, watu walishapanda mpunga hivyo wamepata hasara kubwa Sana.
4) kukatika kwa mawasiliano ya miundombinu
Barabara hii inahudumia maelfu wa watu vijiji vingi Sana Mgudeni, Isago, mkangawalo, Ilole, Itongowa, Mngeta, mchombe, Lukolongo n.k kote hutumia daraja hili, kwa Sasa Hali Ni mbaya na Ni ngumu kupitika.
MAOMBI
~ Tunaomba Serikali itusaidie kwa haraka Sana kutatua hii changamoto.
~ Mkuu wa wilaya hatuna (wilaya ya Mlimba), tuna mkurugenzi tu, mbunge Kunambi, Diwani, ofisi ya Tarura, Ofisi ya Waziri mkuu (kitengo Cha maafa) n.k tunaomba msaada wenu haraka ili kutusaidia kupata ufumbuzi wa daraja na lile korongo la Madandoni.
~ Tunaelekea msimu wa mvua kubwa na masika wananchi tutataabika Sana, Mto Mngeta mamba wengi Sana kwa Sasa Ni hatari kubwa iko mbele yetu.
~ Tunaomba Sana hatua za haraka zifanyike kutusaidia wananchi.
Ushauri
~ Tunaomba Serikali isaidie kusimamia mazingira vizuri, watu wanalima Hadi mtoni hii inapelekea kina Cha mto kupungua na kusababisha mafuriko.
Walau watu wangeacha kulima mita 20 Hadi 30 tu nje ya mita 60 zile za sheria ya mazingira ya 2004.
Naambatanisha picha.
View attachment 2463059
View attachment 2462997
View attachment 2463051
Hii ni picha ya lile korongo linalojulikana Kama Madandoni baada ya kuharibika.
Update
Leo asubuhi daraja limekatika loteee katikati, hakuna mawasiliano kabisa!
View attachment 2463056
Babu Tale yuko Morogoro Kusini! Mbali kabisa kutoka hayo maeneo ya Mlimba, Mngeta, Chita, Mbingu, nk. Mbunge wa hilo eneo alikuwa ni kijana wa magu anayeitwa Godwin Kunambi. Aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma enzi za utawala wa awamu ya 5.Viongozi wao ni akina babu tale
Hili lipo mngeta ifakara na nyandila ipo mgeta mvomeroWasalimie nyandila huko [emoji1]
Ova
Wilaya ya Moro mjini ndo wilaya inao ongoza kwa maendeleo kuliko wilaya zote tzMorogoro hamjawahi kupata viongozi wanaowasaidia kwa dhati ndio maana mnakila kitu lakini maendeleo yenu mko nyuma, anzia wabunge, wakuu wa wilaya, na DED, na kadhalika wengi wakata viuno na mipasho na sio watendaji
kaka mshana, nikumbuke kule Pm, mdogo wako bado sina maishaNa majambazi
Mkuu huku Ni mngeta[emoji1], Nyandila IPO mgeta unapitia mlali, mzumbe, Ila huku unapita IfakaraWasalimie nyandila huko [emoji1]
Ova
Inasikitisha Sana mkuu, huku kuanzia mbunge wote sifuri tu, CCM Ni janga kubwaHayo maeneo nayafahamu fika! nimeishi huko kwa miaka mingi. Kiufupi serikali ya ccm imewekeza sana kwenye siasa, kuliko kwenye mambo ya msingi.
Wilaya za Kilombero, Ulanga na Malinyi zina umuhimu mkubwa sana kwa uchumi wa nchi yetu! Lakini linapokuja suala la miundombinu ya barabara, hali ni mbaya kupitiliza.
Hayo maeneo yanazalisha sana mpunga, miwa, ndizi! kuna samaki wa mto Kilombero, nk. Lakini barabara zake ni mbovu mpaka basi.
Hizo Wilaya tatu zinafanana sana na Wilaya za Mufindi na Kilolo Mkoani Iringa. Nako mambo ni hayo hayo. Kuna uzalishaji mkubwa wa mazao yatokanayo na miti, pamoja na chai! Lakini barabara zake hazipitiki wakati wa masika.
Cha kujiuliza; hii serikali haina pesa za kujenga barabara za lami kwenye haya maeneo muhimu kwa uchumi wa nchi? Hivi hawaoni wakijenga barabara kwenye hayo maeneo, bidhaa muhimu kama chakula, mbao, nk. Zitawafikia walaji kwa gharama nafuu?
Hizo hela mnazochezea kununulia magari ya kifahari, kwa nini msijenge barabara za uhakika ili kuwaondolea wananchi hizi kero za miaka nenda?
Asantee Sana kwa ufafanuzi wako, karibu Sana wilaya ya MlimbaHili lipo mngeta ifakara na nyandila ipo mgeta mvomero
Nyandila pazuri sana green mwaka mzima