Morogoro: Mfungwa aliyetoka gerezani kwa msamaha wa Rais adaiwa kufanya mauaji

Morogoro: Mfungwa aliyetoka gerezani kwa msamaha wa Rais adaiwa kufanya mauaji

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro linamshikilia mmoja wa wafungwa ambao waliachiwa huru kwa msamaha wa Rais mnamo Mei Mosi, 2022, Nestory Elias (62) kwa tuhuma za mauaji.

Elias anadaiwa kumuua Mwajuma Sadru (75), Mkazi wa Mtaa wa Bong'ola kutokana na mgogoro wa kugombania eneo la biashara ambalo mtuhumiwa alikuwa akilitumia kwa ajili ya biashara ya kuchoma mihogo.

Marehemu alimtaka Elias aondoke eneo hilo, mtuhumiwa akamtishia kumuua Mwajuma ambaye alienda kutoa taarifa Serikali za Mtaa, wakati viongozi wakijiandaa kushughulikia tukio hilo ndipo Elias akafanya mauaji hayo.

Chanzo: Azam TV
 
Hao wanaotoa watu jela kwa msamaha huwa hawaangalii tabia ya mtu?
 
Serikali ifanye uchunguzi Bong'ola ni sehemu iliyopimwa na viwanja ni expensive sana. Kwanini wagombee eneo hadi mauajii?
 
Serikali ifanye uchunguzi Bong'ola ni sehemu iliyopimwa na viwanja ni expensive sana. Kwanini wagombee eneo hadi mauajii?
Eneo walilogombea sio la kujenga, ni barabarani tu kwaajili ya kuweka jiko la kuchomea mihogo na mahindi
 
Urasimu wa viongozi at its best. Eti wakali wakijiandaa kushughulikia jambo Hilo, nyoko kabisa

Hao viongozi nao wakamatwe waunganishwe na huyo mzee kwenye kesi ya mauaji
Njaa za viongozii naongezea Kenge kabisa.
 
Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro linamshikilia mmoja wa wafungwa ambao waliachiwa huru kwa msamaha wa Rais mnamo Mei Mosi, 2022, Nestory Elias (62) kwa tuhuma za mauaji.

Elias anadaiwa kumuua Mwajuma Sadru (75), Mkazi wa Mtaa wa Bong'ola kutokana na mgogoro wa kugombania eneo la biashara ambalo mtuhumiwa alikuwa akilitumia kwa ajili ya biashara ya kuchoma mihogo.

Marehemu alimtaka Elias aondoke eneo hilo, mtuhumiwa akamtishia kumuua Mwajuma ambaye alienda kutoa taarifa Serikali za Mtaa, wakati viongozi wakijiandaa kushughulikia tukio hilo ndipo Elias akafanya mauaji hayo.

Chanzo: Azam TV
Kifo kingezuilika endapo ofisi ya mtaa wamgetoa barua marehemu aende kuripoti tishio polisi
 
Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro linamshikilia mmoja wa wafungwa ambao waliachiwa huru kwa msamaha wa Rais mnamo Mei Mosi, 2022, Nestory Elias (62) kwa tuhuma za mauaji.

Elias anadaiwa kumuua Mwajuma Sadru (75), Mkazi wa Mtaa wa Bong'ola kutokana na mgogoro wa kugombania eneo la biashara ambalo mtuhumiwa alikuwa akilitumia kwa ajili ya biashara ya kuchoma mihogo.

Marehemu alimtaka Elias aondoke eneo hilo, mtuhumiwa akamtishia kumuua Mwajuma ambaye alienda kutoa taarifa Serikali za Mtaa, wakati viongozi wakijiandaa kushughulikia tukio hilo ndipo Elias akafanya mauaji hayo.

Chanzo: Azam TV
Tangu nione sijazaliwa
 
Back
Top Bottom