Morogoro: Mpiga debe amuua mpiga debe mwenzake wakigombea abiria stendi ya Msamvu

Morogoro: Mpiga debe amuua mpiga debe mwenzake wakigombea abiria stendi ya Msamvu

Idugunde

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2020
Posts
6,404
Reaction score
6,969
Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro linamshikilia mpigadebe wa mabasi ya Abood Abdilah Yassin (32) mkazi wa Kihonda Manispaa ya Morogoro kwa tuhuma za kumuua mpiga debe mwenzake wakati wakigombea abiria kwenye stendi kuu ya mabasi Msamvu.

---
Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linamshikilia Abdilah Yassin mkazi wa Kihonda Manispaa ya Morogoro mpigadebe wa basi la Abood katika kituo kikuu cha mabasi cha Msamvu mkoani Morogoro kwa kusababisha mauaji kwa kumchoma kisu mpigadebe mwenzie wa basi la BM Tazani Mndeme mkazi wa Mwembesongo wakigombea abiria.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi (SACP) Fortunatus Musilimu amethibitisha kutokea kwa tukio hilo leo Machi 28 mwaka huu majira ya saa 12 asubuhi katika stendi hiyo.

Amesema katika ugomvi huo wa kugombea abiria Abdilah Yassin ambaye anafahamika zaidi kwa jina la "HAJIMONGA BONGE" alimchoma kisu kifuani upande wa kushoto Tazani Mndeme ambapo alikimbizwa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro na kufariki wakati akipatiwa matibabu hospitalini hapo.

Source: WasafiDigital

msanvu.JPG
 
Inna lillah wainah illahi rajiun. Inasikitisha sana hii taarifa yaani unatoa uhai wa mwenzako kisa hela tu,Ewe mungu baba tupe maarifa yaliyo mema kichwani mwetu
 
Lete kapucha tuone basi jinsi mpiga debe anavyo muuwa mwenzake!!!
 
Shangaa wewe, eti mtu umetoka zako nyumban unaenda kupanda gari ya kwenda mwanza afu kuna mtu anatokea hapo katikati anaseema amekuleta!
😄😆😅🤣😂😃😀
Yaani Anasema Watu Wangu Hawa Hapa Kama Hamjui Lolote
Wapiga Debe Wanajua Kufanyizia Vibaya Abiria
Jeshi La Police Lipo Msamvu Hapo Hapo

Kuna Wahuni Wapo CBE DODOMA Yaani Lile Eneo Kama Wamelinunua Wanatishia Wenye Magari, Abiria
Lazima Wakatie Chochote!!! Tanzania Mahovyo Hovyo Hajaishi
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linamshikilia Abdilah Yassin mkazi wa Kihonda Manispaa ya Morogoro mpigadebe wa basi la Abood katika kituo kikuu cha mabasi cha Msamvu mkoani Morogoro kwa kusababisha mauaji kwa kumchoma kisu mpigadebe mwenzie wa basi la BM Tazani Mndeme mkazi wa Mwembesongo wakigombea abiria.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi (SACP) Fortunatus Musilimu amethibitisha kutokea kwa tukio hilo leo Machi 28 mwaka huu majira ya saa 12 asubuhi katika stendi hiyo.

Amesema katika ugomvi huo wa kugombea abiria Abdilah Yassin ambaye anafahamika zaidi kwa jina la "HAJIMONGA BONGE" alimchoma kisu kifuani upande wa kushoto Tazani Mndeme ambapo alikimbizwa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro na kufariki wakati akipatiwa matibabu hospitalini hapo.

Source: WasafiDigital
 
Back
Top Bottom