Morogoro: Msanii Emmanuel Elibariki 'Nay wa Mitego', akamatwa na Polisi

Hao wenzetu hawakusubiri tu halafu wakajikuta wameyafikia hayo maendeleo. Maendeleo pamoja na mambo mengine ni transformation, yaani kubadilisha fikra zetu na namna ya kutazama mambo, na siyo kukaa tu na kusubiri maendeleo yaje. Daima ni jukumu la raia kubadili mtazamo wa watawala na siyo watawala kubadilisha mtazamo wa raia. Vinginevyo watawala watapenda daima status quo maana ndiyo inayolinda masilahi yao.

Kinachokatisha tamaa hapa kwetu bado tunadhani watawala wana haki ya kulinda hali ibaki hivi hivi ili waendelee kupiga maisha tukidhani ifikapo 2050 kutakucha tu tujikute maendeleo yako mlangoni. Hiyo ni kujinyonga wenyewe na kamwe mabadiliko hayatakuja kwa mtindo huo. Ee Mungu tusaidie watz tujitambue.
 
Ngoja niuchune kwanza maana nisije nyea ndoo mie. Ila kiukweli kabisa WAPOO.....!!!!!
 
Huyu mtafuta kiki wacha ale na wakwao
 
Nchi ya ajabu hii
Wanaacha Ku deal na major issues
Wanaangaika na vitu vya kijinga
Ney hana kosa
Freedom of Speech
 
Kaiba mvomero ndo maana katoka moro twn wamemrudisha mvomero
Yeah! Nadhani kakamatwa kwa jambo tofauti kabisa na sisi tunajadili kitu tofauti hapa. Kwa nini apelekwe Mvomelo na siyo Dar alikofanyia uhalifu (kama ni huo wa wimbo wake). Kwani aliurekodia Mvomelao?
 
Hii serkali bado haijatambua kosa kubwa inalolifanya la kuwafanya watu kuonekana mashujaa (heros ) au kuwataftia kiki.
Kwa mfano, hivi sasa ni ukweli usiopingika kuwa ushindi wa kishindo wa Lissu ilibustiwa na ile hali ya kuwekewa vikwazo na serkal.

Nape leo anaonekana shujaa tu baada ya kuoneshewa bustola na askari aliyetumwa kumzuia asiongee na waandishi wa habari.

Leo lema naye hivyo hivyo. Anaonekana kama mandela wa Tanzania, baada yakufanyiwa figisufigisu za kumuweka gerezani takriban miez mitano.

Jana Mange kimambe kaweza fikisha one million followers sababu ya kupata umaarufu baada yà kushikilia kidedea vyeti vya Makonda. Yani hivi sasa followers wa mange wanaongezeka kwa 2k followers kwa siku huku followers wa makonda wakipungua kwa kasi.

Leo sasa Ney wa mitego inasemekana Tyar yupo mikononi mwa Polisi. Na sababu hasa itakuwa ni wimbo alioutoa juzi. ( jina sijafahamu unaitwaje ila kuna sehemu wanaitikia " wapo")

Siku ya leo habari za Ney kukamatwa zinaenea mitandaoni na vyombo vya habari vyote. Kesho ni front page magazetini. Na kila atakayepata hii habari lazima autafte huu wimbo ausikilize ili ajue Mantic ya uo wimbo kupelekea kukamatwa kwa Ney.

Kuja kufika kesho. Huu wimbo utakuwa ukipigwa kila mtaa. Hata wa kule kijijini kolomije mpka sasa watakuwa wamesha upata.

Serikali ingekaa kimya na kuupuuza huu wimbo basi hata wanaousikiliza wangeupuuza. Sasa kitakachotokea hivi sasa ni kila mtu atausikiliza ili ahoji ni kwa nini Ney akamatwe?

Nakumbuka kuna kipindi Nikk mbishi alitoa wimbo akimsifu kikwete. Cjui basata au TCRA wakamuita na kuufungia. Mi binafsi nilikuwa sijausikiliza maana si fani wake. Ila niliutafta nikausikiliza ili nijue kilichoimbwa mpaka ukafungiwa.

Katika hii dunia ya Utandawazi na Technology. Serikali inajisumbua kucontrol kila kitu wanachotaka wananchi wao wasikie au waambiwe. Yani hapa serkal IMECHEMSHA.

Walifanikiwa nini Pale walivyopiga marufuku wimbo wa Viva Roma 2015?

Serikali iconcentrate na Mambo ya kimaendeleo sio personality. VIWANDA HAVIJENGWI KWA KUMKAMATA NEY BHNA.

Kodi zetu Mnatumia ovyo hamtaki tuseme. Kama hamtaki kusemwa mstep down wapo ambao wapotyar kuongoza nchi na kukubali kukosolewa na Wananchi wao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…