Morogoro ndio mkoa uliotoa vipaji vingi Tanzania kuliko mikoa mingine.

Morogoro ndio mkoa uliotoa vipaji vingi Tanzania kuliko mikoa mingine.

Linapokuja suala la burudani hususani muziki, Kigoma iko sayari ya 7 kutoka sayari ya Tanzania.

Tangu huko nyuma kuna wasanii wengi nguli kama akina Bichuka n.k, hivyo vyovyote utakavyo linganisha, Kigoma hailinganishwi na mkoa wowote.

Ni sawa uilinganishe Mbeya na mkoa wowote kwenye masuala ya Ukristo(uimbaji wa Gospel, idadi ya nyumba za ibada n.k), hapo unakuwa unajilisha upepo maana ina watu ngulii haswaa kibao ambao mikoa mingine hawapo.
Mbeya inaongoza kwa dini at the same time pia sifa yake nyengine inasifika kwa uchawi, ubaguzi na unafki

Hii sijui tuuitaje [emoji16]
 
Ni mkoa mzuri sana na wenye vipaji lukuki lakini naungana na MINOCYCLINE hapo juu kwa hoja alizotoa maana ni ukweli mtupu,japokuwa vipaji ni kweli vipo aisee maana tukiangalia nyanja hizi tunapata jibu...

1.Kisoka...
Ukiachana na timu za Dar Morogoro inafuatia kuwa na timu nyingu zilizowahi kutwaa taji la ligi kuu nazo ni Mtibwa Sugar na Mseto ukiachana na Tukuyu stars ya Mbeya hakuna mkoa uliowah kufanya hivyo hapa Tz..na kuna timu ilikuwa inaitwa reli "kiboko ya vigogo" Simba na Yanga zilikuwa hazitoki zikicheza na timu hii

Morogoro ni nyumba ya vipaji vya soka tangu zamani Kina Mohamed Msomali,Malota Soma,Zamoyoni Mogella,Charles Boniface Mkwasa(alilelewa na dada yake mtaa wa karume Morogoro tangu akiwa kijana mdogo) na wengineo magwiji wa zamani,kwa sasa wapo kina Mkude kibabage,Dickson Job,Aishi Manula,Kelvin wa Genk,Shomari Kapombe,Kibwana Shomari n.k
2.Ngumi
Hakuna asiyejua kwamba ukitoa Dar Moro ina ufalme wake katika ngumi Francis Cheka,Cosmas Cheka,Twaha Kiduku,Mandonga na wengine kibao wanatoka Moro
3.Muziki
Zamani watu dansi walikuwa wanalifuata Moro kutoka dar kuja kuwaona Cuban Marimba ya Salum abdallah na baadae Juma Kilaza na Moro Jazz ya Mbaraka Mwishehe,,Wasanii wa Moro kwa sasa ni Rich Mavoco,Jay Melody,Belle 9,Dayna,Conboi,Tundaman na wengineo hata Salam, Babu Tale wanatokea Moro

Mwandishi wa comment hii aliishi Moro kuanzia 1982-1993
Upo .tanga coastal union pamoja zote na African sports washawahi chukua ligi kuu
 
Naongelea Moro ya zamani kaka miaka ya 90 kushuka chini.Maendeleo yalitakiwa yaanzie tangu zamani enzi za Shan Cinema,Mango Club n.k zamani ilikuwa wandewa wanaishi pale mjini ukitaka kuwekeza ni lazima watoe idhini wao kama hawakutaki huwezi kuishi utafanyiwa figisu sana kwao ni heri mwarabu au mhindi kuliko mchaga anayetaa kuwekeza Moro,Morogoro ilitakiwa iwe ya pili baada ya Dar sema majungu,fitna,uchawi umepinza mkoa Tanzania kuna viwanda vitanovya sukari viwili vinatoka Moro vikiwakilisha viwamda vingi vilivyokuwepo Moro enzi hizo kina Canvas,Moproco,21 century vilikufa bila sababu ya msingi..kwa sasa naona Moro inachipua sana wawekezaji wamekuwa wengi tofaut na zamani
Naskitika sahivi vibaka na waizi wamekuwa wengi wenye kufanya vitendo viovu hasa mitaa ya Chamwino , Misufini, vibandani , mafiga
 
Mkoa wa morogoro ndio tunu ya sanaa, burudani na michezo. Huo mkoa umetoa vipaji adhimu na adimu sana na ndio tegemeo kubwa kwa taifa kwenye kuzalisha burudani na michezo.

Hapo Morogoro wametoka akina Albert Mangwea, mbaraka mwinshehe, twaha kiduku, francis Cheka, shomari kapombe n.k.

Huwezi kwa sasa Tanzania kuulinganisha mkoa wa morogoro kwenye burudani na michezo na mkoa wowote ule hata kigoma bado ipo mbali na itasubiri kwa morogoro

Haya ndio mambo WaTanzania hii tuliyonayo na ndio maana hakuna kuelimika ni ushabiki ushabiki hata bungeni ni hayo hayo! Hakuna kinachojiri utakuta vijana kijiweni wanamshabikia mfungaji wa magoli hadi ngumu zinatoka Kwa ubishi!
Mmemsikiza Mbunge Musukuma na kiswanglishi yake. Na ndio maana hii CCM ni janga la Taifa hili.
 
wanafanana na wakwere?
Wakwere, wazaramo na wadoe hawa ni kama vile jamii moja iliyogawanyika kutokana na historia fulani huko nyuma.
Ni kama vile wachaga kuna wamarangu, wakibosho, wamachame nk. Ila wote ni jamii 1 ya kichaga.
 
Unawajua ras wa nyika?
Screenshot_20220925-124448.png
 
Back
Top Bottom